Weekend Story! Ugly Benny! (Get Rich Or Die Trying)

Weekend Story! Ugly Benny! (Get Rich Or Die Trying)

Muddy akiwa Makongo, akashauriwa na Luteni Kanali Kipingu kuwa mpira bongo hauna hela sanaaa, sababu umri anao mkononi bora aingie kwenye mbio za umbali mrefu maana alishindaga mataji mengi ya mbio kwenye Umitashunta na Umiseta. Akampa tu live mashindano yako mengi, na ufadhili ni mwingi mnooo, anaweza faidika kimaisha haraka mnooo kuliko kupoteza mda kwenye mpira. Muddy akawa amekubali, akaachana na mpira kabisaaa akaanza kutrain mbio.

Na Makongo ilisifika kwa michezo, akapewa mwalimu wake wa michezo kabisaa wa kumtrain, amabpo ratiba yake ya wiki ilijumuisha kuamka saa 10 usiku mara 5 kwa wiki, kukimbia mita 7000 na kuhudhuria masomo darasani, na mwisho wa wiki kushiriki mbio mbali mbali za kitaifa. Muddy was committed, very comitted mpaka mwalimu wake akamwambia utafika mbali Muddy maana katika kufanya kwako vitu unaweka moyo woteeee.

In no time Muddy akaanza kushinda mbio za hapa nchini, za mashule, na Luteni akaona amekwivaaa. Akamsukumia mbio za Amsterdam. Muddy kama kawaida hakufanya ajizi, akachukua medali ya dhahabu. Ofcourse kanali alijua Muddy ni mzuri ila sio wa kushinda dhahabu fasta kiasi hikooo. Akazidi kumuamini. Katika hizo mbio za Amsterdam Muddy alilipwa $ 8000 kama zawadi, na allowance zingine akapata kama $$$ 10,000. Alivorudi Bongo akanunua gari yake ya kwanza Toyota Mark 2 Grande. Basi shule wadada wote wazurii Muddy, Muddy. Sio kwa gari lile kwenda nalo shule.

Akiwa canteen siku moja kaja msichana akampa kikaratasi. Wapambe wake wako kina nini kina nini? Muddy ushachukua chiu wa bureeee. Muddy ushachukua chiu wa bureee. Muddy akawaambia tulizeni ball, msitake kunipanda kichwani. Baadae kwa mda wake akakisoma kile kikaratasi kumbe namba ya simu, imeandikwa nitafute, Shufaaa. Muddy akasema kuku kaingia bandani. Akampigia Shufaa, niambie mrembo! Shufaa anajichekesha chekesha tu, akamwambia tunaweza onana weekend hii labda, pale Mwenge, Utajiju guest house saa 5 flani. Shufaa yuko haina shida kabisaaaa. Muddy akawa kajiandaa kula mambo. Akawaambia wenzie hivi mtaamini huyu Shufaa wa form 4, kanitakaaa?

Wenzie wakamwambia tunaamini kwani si mwanamke, na mwanamke yeyote lazima aliwe. Muddy saa 5 weekend kajiandaa kabisaaa kwa mechi kali, hakukimbia siku hio wala nini, ili kutunza staminaaa. Kanyoa kabisaa, anajua anaenda kumla Shufaa, afu akifikiria katamuuu, kanavoonekana anadata kabisaaaa. Akawa anawaza akimzingua takuwa kamchefuaaaa. Mara asitokeee si balaaa, hilo. Akajipa moyo, akasogea maeneo ya tukio. Akamnunuliazawadi kabisaa maana kumla mtu bure si hulka yake wala nini. Kufika pale hajakaa sanaa, Shufaa huyu hapa, akajua ashakula mzigooo.

Wakaingia guest fresh kabisaaa, akampa zawadi yake ya cheni na hereni za silver, alizinunuaga Amsterdam akawa kakosa wa kumpa, so alikuwa nazo tu. Akamuuliza utakula nini, Shufaa yupo chips kuku, akanunua na soda. Shufaa kala weee pale, kashiba ndiii. Muddy sasa anaanza kumsogeza waanze mambo, Shufaa natia nipo Mp! Muddy akamuuliza nini? Nipo MP! Muddy akamuuliza sasa hapa tumekuja kufanya nini labda? kwanini hukusema mda wote? Shufaa yupo nilitaka tu tuongeee siji nini. Muddy huyo kaamsha kamwacha mule ndani kachimba zake.

Shufaa kampigia kampigia kila akipiga anaambiwa hio namba haipatikani. Akamfata Muddy kamkazia kama hamjuiii. Si kwa kula kuku wake bureee. Mara Muddy akapta mtoto wa kishua Patricia, Muddy kwanza alisita kuwa nae, maana ana mambo mengi kama unga wa ngano, ila akasema no sweat, ngoja tu nimle maana keshanielewa nifanyeje sasa. Patricia hakuwa mbanaji, tena kwao wazazi mara nyingi hawakuwepo mda mwingine akawa anamla kwao humo humo. Akitoka anagongana na kaka zake nao wanatoka na mademu, wanasalimiana tu, tu vipi? Anajibu poa! Wanamwambia fresh. Imetoka hiooo. Mara wamchimbe biti akimzingua mdogo wao wanae. Tatizo Pat alikuwa mtoto sanaaa. Ana vimambo vya kitoto toto akaachana nae.

Akaja kukutana na binti wa kiarabu anaitwa Sultana. Muddy kwanza hakutaka kumchafua huyu binti maana anawajua waarabu hawawezi kumkubalia amuoe huyu Sultana wakati yeye Muddy japo kachanganya kwa mbali ila bado kwao mtwana tu. Ila Sultana pozi zake ndo zilimtega Muddy, kwanza rangi ya Mtume ile ilimchanganya vibayaa, afu mambo yake yale ya shungi masaa 24. Hakuwai kuiona nywele yake. Akajiambia ngoja nimfanye rafiki. Huku na huku shetani kamuingia akasema ngoja nimle ila nitamuoa. Akamjaribu Sultana wakutane Mwenge guest yake ile ile Utajiju. Sultana aka kataa katu katu. Muddy akachange flani hivi, sasa Sultana ile kutaka kumridhisha Muddy akakubali. Muddy kama kawaida kaomba mchezo, Sultana akamuuliza utanioa, mara 100, Muddy akasema ndio nitakuoa usiwe na wasi wasi. Sultana anwambia ujue sisi warabu lazim tuolewe bikira, Muddy anampooza mimi ndo mumeo wasi wasi wako nini? Ukimaliza form 4, nakuoa nakusomesha mwenyeweee.

Mmmmmmmhhhh! Sultana kaingia kingi, akatoa mchezo kwa Muddy. Muddy akamkuta bikira bwanaaa. Weeeee! Hio shurba akasema atakuwa anawafanyia sensa kabisaa, maana sio kwa shurba ileee. Kangatwaaa, kakabwa, raha yenyewe hajaionaaa. Yeye bikra hataki tenaaa. Na kazi ya kummalizia Sultana akawaachia wengine. Alivotoka tu ppale, Sultana akajua tabembelezwa au vipi, Kauzu Muddy akawa haeleweki. Sasa Sultana kanasa, maana bikra ndo hana tenaaa, na bibi zake wale wa kiarabu watamtandikia shuka nyeupeee, siku ya harusi itakuwa kimbembe. Akawa anaona hana jinsi zaidi ya kumbembeleza Muddy.

Muddy bandiduuuu, sazingine Sultana akimfata anamkuta na demu mwingine anasimama pembeni mpaka wamalize kuongea, ndo na yeye aongee. Au akipiga simu anaambiwa kuna demu namkaza huku sio kupiga piga simu, anamwambia basi ukimaliza kumkaza ni beep. Cha moto alikiona Sultana. Sema Muddy akiamka vizuri siku zingine anakuwa mkarimu kweli kwake. Kifupi Sultana alikuwa nyavuni. Ila mvumilivu hula mbivu, kuna safari alienda Swiss kwenye mbio akapewa ofa ya kwenda na familia yake mmoja akaenda na Sultna. Mara amwambie Sultana mwanamke wa maisha yake yupo Arusha ambae ni Irene. Sultana anasema tu sawaaaa.

Walivorudi Sultana kakatiwa ya kushuka JKN, Muddy aakaend akushuka KIA, wakala bata na Irene refuuu kama wiki ndo akarudi bongo na Sultana alikuwa anajua kabisaaa.

ITAENDELEA KESHO SAA 7.
 
Ohw jaman sultana ni nini kujiumiza moyo bure si umuache tu uyo muddy uje kwangu mtoto wa kiarabu......
 
Benny akawaza tu, mda mrefu sanaa umepita, kama ni ishu ya Irene ishapita it is about time aanze upya kutongoza mademu, sio kuzubaa, zubaaa tu. Ila swala lake la ubaya nalo likawa linamtatizaaa sanaaa. Manake mara nyingi hata akijiongeza kuwachekea mademu hawamchekei wala nini, wanampotezea. Hata club mara nyingi amekuwa akienda club, akijiongeza ku dance na wale mademu wakali wakali wanamkimbia. Hiko nako kikawa kikwazo. Ila maadamu sahivi shingi 2, 3 hazimpigi chenga akaona bora tu afanye manuvaaaa mengine.

Mtaani anapoishi kulikuwa na binti mapepe sanaa, anaitwa mwaija mahips. Mtoto alikuwa kiboko ya mtaa, anafatwa na watu wenye magari makubwa makubwaaaa. Benny yeye hana gari hapo. Akaamua kujitosa kwa mwaija, na akasema kama Mwaija akieleweka basi atamuoa kabisaaaa. Siku hio hana hili wala lile, akamkuta Mwaija dukani. Akamsalimia, Mambo Mwaija! Kimyaaaaa! Mwaija akajifanya kama hamsikiii vile. Benny roho ikamuuma ila akaamua tu kumkomoa Mwaijaaa si kwa ubandidu ule. Akamwambia mwenye duka, Mwaija akija hapa uwe unampa anachokitaka, sawaaa. Mimi nitalipa. Mwaija akashutukaaa. Akamuangalia Benny, Hivi unaitwaga nani vileee? Benny akamwambia naitwa Ben. Mwaija akaanza kujibalaguza, hivi Ben unakaaga wapi vile? Ben akamwambia nakaa hapo nyuma karibu nyumbaniii.

Mwaija akaanza kujibalaguza, nitakujaaaa. Siku ingine nitakujaaaa. Mwaija akamwambia mwenye duka amfungie viti vya 10,000 kwenye hio bill ya Ben. Akaondoka. Alivoondoka mwenye duka akamwambia Ben wewe unamuhonga nini huyu maji mara moja? Kila mtu ashajipigia hapa mtaani. Usimpe hata kumi, yule dawa yake unampa maneno tu unamlaaa mbona. Wapo wa kuhongwa ila sio yule. Mi kesho akija namtimuaaa. Lipia tu hio 10,000 afu basi. Kama unataka mtoto wa kuhonga mimi nitakuunganishia Sara yule mtoto wa mjeda. Atleast yule kidogo mgumuuuu ndo inabidi ujiongeze huyu Mwaija huyu hamna kituuuu. Benny akabakia anshangaa na kuchukua pointers kwa ma pro. Muuza duka ambae anaitwa Alex akamwambia Benn uwe unakuja maskani pale, mida ya saa 4 usiku kuna noga kichizi. Utawajua warembo wote wa mtaa huu.

Benny akatoka kuingia kwake, hajafika anasikia mtu anamuita, Ben! Kugeuka Mwaija huyu hapa, keshavua lile dera, kavaa tight. Akaitika, Naaaam! Ndo unakaaga huku. Ben akajibu ndio. Basi Mwaija akawa anamsindikiza. Kufika kwa Ben akawakuta wapangaji wake, Mmmoja akamsalimia Mambo Mwaija. Akajifanyahajasikia wala hamjui. Akaingia ndani na Ben, Ben akajua tu yule mpangaji wake kashemla Mwaija, aksema sio kesi, hainaga makombo. Kufika ndani, Mwaija yupo kwako kuzuriii, Ben. Ben akakumbuka wosia wa kutumia sanaaaa. Akamsoundisha Mwaija, natafuta mke mwenzio. Mwaija akapagawa. Kweli Ben? Ben yupo, serious nakwambia Mwaija. Mwaija akaanza kukaa, kihasara hasara na kumrembulia macho. Ben akaamua kumsogelea. Mwaija akatoa ushirikianooo. Ben akala mzigooo kiulainiii. Akajisemea kumbe wepesi tu hawaaaaaa subiriiii. Mda wa kuondoka akamtoa na elfu 5. Mwaija meno yote nje, ndo keshapata buzi tayariiii.

Saa 4 akaenda kijiweni, hapo kijiweni ni pub, wanjaa vijana kucheza pool table na kunywa viroba na bia. Akamkuta Alex, akamkaribisha. Ben akawaagizia Bia wote, yeye akaagiza soda. Wakamshangaaaa, ila bia wakazinywa. Alex anamwambia mwanangu soda utatuletea nyuki, namna gani. Wakamkazia mpaka kaagiza Bia. Akawa anainywa kwa tabu maana chungu sanaaa. Ila akaona inamchangamsha. Alex akawasimulia eti Ben kamuhonga Mwaija! Khaaaaaaaaa! Wakacheka woteee. Ben kujikosha akadai baada ya kumpiga lile ofa akamkuta kona, akaenda nae kwake akala mzigo. Washkaji wapo hapo sawa sio kutoa 10,000 bure. Ben hakuwaambia kama alimpa na 5000 ya ziada tena baada ya kumla. Akaamua hio ibaki siri yake.

Alex akawa anasimulia bwana alimchukua yule mtoto wa skondari, Janet, weeeeeeee! Mjanja hatariiii. Katumia sanaa, amle bureee, zikashindikana kabisaaa. So ikabidi sasa atangaze dau, kamtangazia 10,000 kachomoa. Ikabidi apandishe jokeri. Akamtangazia 50,000. Akagoma kuliwa hapa mtaani madai majungu mengi, ikabidi aingie gharama ya chumba huko Kinondoni. Japo roho ilimuuma akaona sio kesi, akatoa hio gharama ya chumba. Akataka aoneshwe mpunga kwanza hio 50,000. Akamuonesha ATM card kuwa hawezi tembea na cash yote hio, ila wakapatana, wakitoka mguu kwa mguu ATM. Akawa kamuelewa.

Baada ya mchezo, akawa anatafuta namna ya kumchomoka sasa, sio kwa mchezo ule atoe 50,000 yote. Mche huo vepeeee!!!!!!!!!!! Hata 10,000 haifai kwa mchezo ule wa kitoto. Ila Jane yupo smart sanaa, angesema amzime kimafia angzusha timbwili, maana hata kuoga ligomaa, akamwambia kabisaa usiponipa changu naenda home kusema umenibaka, tukienda kupima hospitali huchomoki hapa nakwambia. Fanya tu unipe hio 50,000. Oraaaa. Akawa ashamuweka kwenye 18 zake Jane. Hapo Alex akawa anakuna kichwa amtoke vipi.

Wamefika ATM, Alex kaingia, akachomeka kadi kaomba salio, akatoka akamwambia Jane bwana mashine haifanyi kazi, hamna hela, twende nitakupa siku ingine. Jane akawambia subiri. Yule mtu aliengia nyuma ya Alex ATM akawa katoka sasa, Jane akamuwahi kumuuliza eti mashine haitoi? Akamwambia mimi imetoa fresh tu mbonaaa! Alex akalegezwa na jibu la yule mtu. Akaamua tu kukaa kimya. Jane akamuangalia kwa jicho kali. Ikabidi ajiteteee, sikia Jane labda kadi yangu mbovu ngoja niwapigie. Jane akawa kavuta mdomo ila anasikizia hio simu, akamwambia weka loud speaker.


Akampigia mshikaji wake Mwinyi. Akamuwahi, halooooo, hapo CRDB mbona mnanifanyia hiviiii, kadi yangu haitoi hela wakati hela zipo, mjue mnanikeraaa sanaa, mimi hela zangu na kazi nazo mnajua kama nadaiwa, mpaka naonekana muhuniii, mwanamke wangu kanuna kavuta mdomooo, anataka kunipeleka polisiiii, kwanini lakini. Ikawa ashampa code Miwnyi. Mwinyi akapokea chezo. Karibu CRDB huduma kwa wateja sijui nani mwenzngu? Punguza munkari nipate kukusaidia. Mimi Alex, niko ATM hapa Kinondoni na demu wangu Jane. Nimeweke kadi haitoi helaaaa. Kaingia mtu katoa. Mwinyi akaitikia Ooooooh! Naomba kadi namba yako Bw. Alex. Alex akataja kadi namba yake. Mwinyi si anamjua Alex, akazuga tu, Nakuona huku kwenye simu Mr. Alex Shirima, si ndio, Alex akajibu ndio, Bw. Shirima huku inaonesha account yako ina matatizoooo. Na hutoweza kutoa pesa mwezi wote huuu. Mmmmmh! Jane Akastukaaaa. Alex cheko likwa limembana sio kwa jibu lile la Mwinyi. Akazuga kwanini? mimi nina kazi na hizo hela mjue? Mwinyi akamzaliza tu kwa ufanunuzi zaidi njoo ofisini kuna form unatakiwa ujaze kuhakiki taarifa zako, bila kujaza hio form ziwezi kukusaidia. Kuna kingine Bw. Shirima? Alex akajibu tu hapa. Mwinyi akadakia asante kwa kuchagua CRDB naomba nikutakie mchana mwema. Akakata simu.

Jane akawatukana CRDB matusi ya nguoni njia nzima. Alex akawa kaponea chupu chupu kuchomolewa 50,000 kizembe. Benny akawa kashangaa sanaaa. Sio kwa sanaa zile. Akaona kijiwe kitamfaaa sanaa tatizo lake la mademu.

ITAENDELEA SAA 4 USIKU.
 
Hahahahahaaahahah " mwanangu soda utatuletea nyuki" hhhaahahhaahahh
 
Back
Top Bottom