ALianza na wahuni wenzie kumi, akawa ana hubiri kivivu tu, wanaimba mapambio, wana rap humo humo injili. Mara ikafika watu 100 wiki ya kwanza, Wiki ya pili wakazidi kujaa, akapata wazo awe anakusanya sadaka. Akakusanya akapata hela nyingi. Akazidi kuiboresha dini yake ya Bryani, anatumia biblia kutapeli sadaka. Akisimama pale mbele wala hajiandai, maneno yamajia tu, na vifungu vinamjia tu kichwani naturally, anaona amen za kutoshaaa kwa sanaaa. Kujipatia sadka akawa anaombea ufaulu wa masomo, matatizo ya wazazi, matatizo ya kifamilia, uchumi wa wazazi. Dini ikawa kubwaa ikahamia hall.