Wazito PPF wachota ‘vijisenti’

Status
Not open for further replies.
Jamani nimechunguza hizi habari za ufisadi wa PPF nikagundua kuwa hao wajumbe wanaotajwa kulipwa mamilioni sio kweli. Kwanza bodi haijamaliza muda wake wala hakuna wajumbe walioondoka. Tuangalie waleta habari wasije wakasabisha mtandao wetu ukashatakiwa na hatimaye kufungiwa.
Mhh, hakuna hata mjumbe mmoja aliyelipwa. Habari za aina hii ni hatari mno.

Semsekwa.

Tunaomba ukae kando na uchawi wako. Waachie wenye uchungu na nchi wasonge mbele.
 
Jamani, sitoshangaa hii habari ikafa kama anavyotaka kuiua Semsekwa. Sitaki kuingia undani wa hii habari kama ni sahihi ama la maana PPF baada ya kuandikwa mara kibao na gazeti la RAIA MWEMA, walibadili mapigo kwa kuwachukua wahariri wote na kwenda nao kula kuku kule Bagamoyo na sasa hutaona tena habari ya PPF. Mtindo huu ndio umetumika na NSSF, TICS na EWURA wamewafisadi wahariri kwa kuwakirimu weekend Bagamoyo ama Zanzibar na baadaye kuwapa matangazo. Huwezi kuona tena gazeti linaandika kuhusu PPF, NSSF ama EWURA wala TICS. Hii ni hatari sana kwa maslahi ya nchi yetu na watu wake.

https://www.jamiiforums.com/archive/index.php/t-13104.html
http://www.raiamwema.co.tz/08/05/21/5.php
https://www.jamiiforums.com/archive/index.php/t-13582.html
 
PPF ni moja ya mifuko ya mafao ya uzeeni ambayo imelalamikiwa sana juu ya malipo duni kwa wanachama wao ikilinganishwa na mifuko mingine.

Habari tuliyonyaka inaonyesha kwamba wajumbe wa Bodi iliyomaliza muda wake kipindi kilichopita ilipitisha na kujilipa milioni 200 kwa kila mjumbe. Hiyo ikiwa eti ni shukrani kwa kazi nzuri waliyofanya.

Nimepiga mahesabu yangu kwa idadi ya wajumbe wa bodi ambao walikuwepo, ambao ni wanane mbali na staff wengine wa pembeni:
1. Gray Mgonja
2. Prof Bertha Koda
3. Monica Mbega
4. Elvis Musiba
5. Ramadhan Khijah
6. Dr Kassim Kapalata
7. William Erio
8. Samwel Lwakatare

inaonyesha zaidi ya bilioni iliondoka.

Je, hii ni halali? Wanacahama wa PPF wengine huishia milioni 20 baada ya kuchangia hata kwa miaka 25. hawa wajumbe wanajilipa milioni 200 kila mtu kwa kukaa ktk vikao vya bodi kipindi kisichofikia hata miaka 5!! Na tena nasikia hao hao tena wamependekezwa kurudi ndani ya Bodi.

Heb

Jamani naomba mnisaidie, huyu niliyem-bold. Ndiye huyu, O-level na A-level alisoma Lutheran Junior Seminary Morogoro au huyu ni mwingine??
 
Originally Posted by MchunguZI View Post
PPF ni moja ya mifuko ya mafao ya uzeeni ambayo imelalamikiwa sana juu ya malipo duni kwa wanachama wao ikilinganishwa na mifuko mingine.

Habari tuliyonyaka inaonyesha kwamba wajumbe wa Bodi iliyomaliza muda wake kipindi kilichopita ilipitisha na kujilipa milioni 200 kwa kila mjumbe. Hiyo ikiwa eti ni shukrani kwa kazi nzuri waliyofanya.

Nimepiga mahesabu yangu kwa idadi ya wajumbe wa bodi ambao walikuwepo, ambao ni wanane mbali na staff wengine wa pembeni:
1. Gray Mgonja
2. Prof Bertha Koda
3. Monica Mbega
4. Elvis Musiba
5. Ramadhan Khijah
6. Dr Kassim Kapalata
7. William Erio
8. Samwel Lwakatare

inaonyesha zaidi ya bilioni iliondoka.

Je, hii ni halali? Wanacahama wa PPF wengine huishia milioni 20 baada ya kuchangia hata kwa miaka 25. hawa wajumbe wanajilipa milioni 200 kila mtu kwa kukaa ktk vikao vya bodi kipindi kisichofikia hata miaka 5!! Na tena nasikia hao hao tena wamependekezwa kurudi ndani ya Bodi.

Mchunguzi rudi utupe data, maana naona kama kuna 'USINGIZI'
 
BabaDesi, Pole sana; hizo ndio sheria za mafao ya PPF kama zinavyoelezwa ktk PPF Act, No. 14 ya 1978 na marekebisho yake ya 2001.

Lakini, scenario kama yako ilisababisha kurekebishwa kwa kifungu cha 26 na 44 cha sheria ya 1978 hapo mwaka 2001. Kama unadhani huitaji kusubiri kama inavyosema sheria ya PPF basi unalazimika kujitoa kwenye mfuko huo ambapo utarudishiwa michango yako yote na ile ya Mwajiri wako:
"44.-(1) Where a member ceases to be benefits employed in circumstances in which he is not eligible for any pension, gratuity or any other benefit under the provisions of this Act, he shall be refunded the amount of his own contributions and that of his employer to the Fund."

Kumbuka, kifungu kinacholazimisha mafao kutolipwa mpaka ufikishe miaka 55 kiliwekwa strategically kumfanya mhusika ambaye atakuwa amehacha/kuhachishwa kazi kabla ya retirement aendelee na mfuko huo pale anapoajiriwa sehemu nyingine. Kwahiyo inabidi uwathibitishie kwamba hujaajiriwa sehemu nyingine na wala hupokei mafao ya aina yoyote kama ilivyoelezwa kwenye marekebisho ya 2001 [9.(d)(b)] ya kifungu cha 26 cha sheria mama ya 1978.

Niishie hapa, wengine pia waweza kukupa ushauri mzuri zaidi na wenye manufaa. Dukuduku muhimu ambalo tunapaswa kuliangalia ni ufinyu wa fao la PPF. Jamani kwa wenye uzoefu tunaomba tusaidiane, fao analopata mstaafu wa PPF ni dogo sana, kuna umuhimu wa kujipanga ili kuomba mabadiliko kwenye hesabu zinazofanywa maana kuna walakini ukilinganisha na fao walipatalo wastaafu wa mifuko mingine.

Weekend njema!

Mkuu JohnShabaan, nashukuru sana kwa ushauri wako. Sasa naweza kusema kuwa angalau nimepata pa kuanzia. Shukrani Zikuendee!:D
 
Jamani nimechunguza hizi habari za ufisadi wa PPF nikagundua kuwa hao wajumbe wanaotajwa kulipwa mamilioni sio kweli. Kwanza bodi haijamaliza muda wake wala hakuna wajumbe walioondoka. Tuangalie waleta habari wasije wakasabisha mtandao wetu ukashatakiwa na hatimaye kufungiwa.
Mhh, hakuna hata mjumbe mmoja aliyelipwa. Habari za aina hii ni hatari mno.

Semsekwa.

Well, Prove it!
 
unarudishiwa na interest au kama ulivyokatwa + mchango wa mwajiri?
Sheria imesema utarudishiwa makato yako + mchango wa mwajiri. Ni wazi kwamba hakutakuwa na suala la interest kwa kuwa wewe ndo unavunja mkataba nao.
 
Jamani naomba mnisaidie, huyu niliyem-bold. Ndiye huyu, O-level na A-level alisoma Lutheran Junior Seminary Morogoro au huyu ni mwingine??[/SIZE]


Elimu sielewi alipatia wapi.

Bali ni: - mke wa kimbopa mmoja wa Iringa;
- Mbunge, Iringa Mjini;
- RC Ruvuma;
- Formerly, Naibu Waziri - Fedha (akatoka kwa ki-kashfa)
 
Kwa nini habari kama hizi zisipigwe kwenye magazeti halafu wenyewe wakawa na burden of proof? Tukiwa na tabia ya kudai data ili mtoa taarifa aweze kutoa tutaweza kuzuia taarifa kutoka. taarifa zingine zinatakiwa zichokozwe kama hivi ili ziweze kutoka. lakinin mtoa taarifa natakiwa awe mkweli asije kuzusha mambo tu, ikidhihirika ni mzushi next time asiaminike.

magazeti please!!!
 
Mama Mdogo,
Ni amini Usiamini, I had to ask twice, Ni kweli! Ni kweli! the answer was Yes! Yes! 200 mil NOT 20 or 2 mil. Ni mia mbili!

Naifanyia kazi kutafuta doc. husika ili nizimwage JF.

Kuna mtu pale Chuo chetu Kikuu -UD alalama kwamba those wajumbe wa bodi wamekuwa kama kamati ya Olympic. hawatoki ili kulinda siri za bodi. na somehow, PPF management inawazawadia some sort of ufisadi, ili ku-maintain secrecy.

Particularly was complaining on the behaviour of Prof. Koda ambaye she don't care. Hana tena utetezi wa wanachama walio elimu ya juu bali ni mwanachama anayendeleza ufisadi.


subirini

Haraka ilikuwa ya nini kama habari yenyewe haina uthibitisho? Tafiti kwanza ndio umwage jamvini.
 
PPF ni moja ya mifuko ya mafao ya uzeeni ambayo imelalamikiwa sana juu ya malipo duni kwa wanachama wao ikilinganishwa na mifuko mingine.

Habari tuliyonyaka inaonyesha kwamba wajumbe wa Bodi iliyomaliza muda wake kipindi kilichopita ilipitisha na kujilipa milioni 200 kwa kila mjumbe. Hiyo ikiwa eti ni shukrani kwa kazi nzuri waliyofanya.

Nimepiga mahesabu yangu kwa idadi ya wajumbe wa bodi ambao walikuwepo, ambao ni wanane mbali na staff wengine wa pembeni:
1. Gray Mgonja
2. Prof Bertha Koda
3. Monica Mbega
4. Elvis Musiba
5. Ramadhan Khijah
6. Dr Kassim Kapalata
7. William Erio
8. Samwel Lwakatare

inaonyesha zaidi ya bilioni iliondoka.

Je, hii ni halali? Wanacahama wa PPF wengine huishia milioni 20 baada ya kuchangia hata kwa miaka 25. hawa wajumbe wanajilipa milioni 200 kila mtu kwa kukaa ktk vikao vya bodi kipindi kisichofikia hata miaka 5!! Na tena nasikia hao hao tena wamependekezwa kurudi ndani ya Bodi.

Heb

Mil. 200! Unbelievable! Jamaa wana-make bingo namna hii.....kweli haka kajamhuri kameoza!
 
Jamani huu ufisadi uliotapakaa kila mahali ni hatari. La msingi hapa kujua chanzo chake, kwanini watu hawaogopi??????????? Bila shaka kila mmoja jibu analo; mfano mzuri tu; kama baba yako nyumbani ni mwizi! Je wewe mtoto ukiiba kwa jirani atakugombeza???????????????????? Shina la mbuyu likinawiri hali kadhalika na matawi lazima yanawiri!!!!!!shina likififia na matawi hufifia pia. "ukiukata mbuyu matawi hunyauka"!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! katiba mpya ndio suluhisho la yote!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
wenyewe watadai kuwa ni haki yao halafu nyie mtaambiwa mnashinda online kuwapiga vita na kuwafanyia majungu
 
Jamani nchi yetu sio masikini kabisa; ila viongozi wetu ndio wenye roho masikini!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom