Waziri wa zamani, Chadiel Mgonja afariki

Ngono kwa viongozi na WATANZANIA kwa jumla ni tabia na desturi yetu. Wapo akina Rashidi, NNauye, Nelson Mkisi, Mzee Mengi, Msekwa, Mahita, Anna Abdallah, JK, Malecela, ....Orodha ni ndefu.
Mnakumbuka Brother Ditto aliwajibu nini Waandishi waliokuwa wameshupalia vitendo vyake vya ngono?
 
Nimekusikia Mkuu "Naomba maneno yangu yasichochee kukosa Heshima dhidi ya Wazee wetu" kama maneno yangu kuhusu Totoz yanaondoa staha,usiyatilie maanani.....sote kwa pamoja tuungane na familia ya Marehemu kuelekeza sala zetu huko.

- Mkuu Mwawado, tupo pamoja hapa, na besides wote tuko njiani kuelekea kwenye hukumu ya haki na mwenye uamuzi wa mwisho ni Munyazi Mungu na sio anybody else,

- mapungufu ya kimaisha wote tunayo hata viongozi, ya totos sidhani hata kama huu uwanja utatosha tukianza kujichambua kabla ya viongozi mbona itakuwa aibu!.

Mungu amlaze pema marehemu Mgonja.
 
Ngono kwa viongozi na WATANZANIA kwa jumla ni tabia na desturi yetu. Wapo akina Rashidi, NNauye, Nelson Mkisi, Mzee Mengi, Msekwa, Mahita, Anna Abdallah, JK, Malecela, ....Orodha ni ndefu.
Mnakumbuka Brother Ditto aliwajibu nini Waandishi waliokuwa wameshupalia vitendo vyake vya ngono?

Wildcard,
Huyo Mkisi nilimsikia sana sifa zake nikiwa JKT. Alikuwa anatesa sana kambi atakayolala, kuanzia Maafande hadi watoto wa kike wa watu. Nilisikia kituko kimoja kuwa alidai ale nyama ya mbuzi ya kuchoma. Wakamtafutia mbuzi na kumletea nyama tayari. Akauliza kama mbuzi alioshwa, wakasema ndiyo. Akauliza tena, "siyo nyama ila mbuzi kabla ya kuchinjwa". Hapo ilibidi kwenda kutafuta mbuzi mwingine, tena usiku kwenye kijiji cha jirani. Hapo akija kulala kama kawaida ni lazima alale na totoz. Mkisi nasikia akaja kumpa mimba binti mmoja service woman. Kwa woga wa kugunduliwa maovu yake, akatafutwa kijana arithi mimba kwa kuowa kabisa mtoto. Huyu akaja kupanda kwa kasi sana ki-cheo kwa kumuokoa mzee. Mwisho akaja kuwa mkuu wa kambi ya JKT Mlale (Afande MTONO). Anyway, waliopitia huko watakuwa na story zaidi.

Mahita, mhhh I LOVE THIS GUY. Huyu bwana alipoandikwa kuwa alizaa na house girl wake, wala sikuamini. Ila nashukuru waandishi wa habari kwa kumtafuta kijana na kumuweka gazetini. Nakumbuka siku hizo nilikuwa nimepata cd ya Msondo ya HURUMA KWA WAGONJWA. Humo ndani kuna wimbo wanaimba "mtu mzima ovyo .......... ohh ohhh, mtoto sura yako.." Nilipokaona kale katoto wanakodai ka-Mahita, nilicheka siku nzima. Kitoto Kimahita kabisaaaa na jamaa bado anakataa. Heri walau angelidai wa mdogo wake au hata wa DADA YAKE (Cloning??) Ila jamaa kusema si wake na HAMTAMBUI wakati kwenye gazeti tunaona KIMAHITA kitoto, wala hai-ingii akilini. Jamaa yani anatembeza ubabe hata kwa ka-house girl? Heri Mrema aligomagoma na mwisho akakubali.

Mengi yule si MWANA SIASA. Hakuja kupiga magoti tumchague. Awe na ufuska wake huko, hiyo ni aibu yake na familia yake. Ila hawa wanasiasa na watu wanaotesa kwa kutumia kodi zatu, wee andika.
 
Pole kwa familia ya Mzee Mgonja na watu wote wa Same.....Waungwana tujaribu kumstahi Mzee kidogo kwenye kipindi hichi kigumu cha Maombolezo,mambo mengine si wakati wake huu.....Kumuangalia Mgonja nje ya ofisi ya Uwaziri/Ubunge wake ni kutomtendea haki,Viongozi wengi ugonjwa wa Totos ni kama sifa ya kazi....tukianza kuwaangalia kwa upande huo hakuna atakayepona!!!

Pengine imefika wakati wa kuwaangalia kwa upande huo! Kama hakuna atakayepona, basi, so be it! Hatuwezi kuendekeza tabia hizi kwa kisingizio kuwa wengi wanafanya na ni mila zetu. Maisha ya binti zetu ni lazima yaanze kuwa na thamani kuliko reputation ya wanaowaharibu.

Amandla...........
 
Wildcard,
Huyo Mkisi nilimsikia sana sifa zake nikiwa JKT. Alikuwa anatesa sana kambi atakayolala, kuanzia Maafande hadi watoto wa kike wa watu. Nilisikia kituko kimoja kuwa alidai ale nyama ya mbuzi ya kuchoma. Wakamtafutia mbuzi na kumletea nyama tayari. Akauliza kama mbuzi alioshwa, wakasema ndiyo. Akauliza tena, "siyo nyama ila mbuzi kabla ya kuchinjwa". Hapo ilibidi kwenda kutafuta mbuzi mwingine, tena usiku kwenye kijiji cha jirani. Hapo akija kulala kama kawaida ni lazima alale na totoz. Mkisi nasikia akaja kumpa mimba binti mmoja service woman. Kwa woga wa kugunduliwa maovu yake, akatafutwa kijana arithi mimba kwa kuowa kabisa mtoto. Huyu akaja kupanda kwa kasi sana ki-cheo kwa kumuokoa mzee. Mwisho akaja kuwa mkuu wa kambi ya JKT Mlale (Afande MTONO). Anyway, waliopitia huko watakuwa na story zaidi.

Mahita, mhhh I LOVE THIS GUY. Huyu bwana alipoandikwa kuwa alizaa na house girl wake, wala sikuamini. Ila nashukuru waandishi wa habari kwa kumtafuta kijana na kumuweka gazetini. Nakumbuka siku hizo nilikuwa nimepata cd ya Msondo ya HURUMA KWA WAGONJWA. Humo ndani kuna wimbo wanaimba "mtu mzima ovyo .......... ohh ohhh, mtoto sura yako.." Nilipokaona kale katoto wanakodai ka-Mahita, nilicheka siku nzima. Kitoto Kimahita kabisaaaa na jamaa bado anakataa. Heri walau angelidai wa mdogo wake au hata wa DADA YAKE (Cloning??) Ila jamaa kusema si wake na HAMTAMBUI wakati kwenye gazeti tunaona KIMAHITA kitoto, wala hai-ingii akilini. Jamaa yani anatembeza ubabe hata kwa ka-house girl? Heri Mrema aligomagoma na mwisho akakubali.

Mengi yule si MWANA SIASA. Hakuja kupiga magoti tumchague. Awe na ufuska wake huko, hiyo ni aibu yake na familia yake. Ila hawa wanasiasa na watu wanaotesa kwa kutumia kodi zatu, wee andika.

hahhaha

umenichekesha sana!

sijamuona huyo mtoto wa mahita..ila napata picha,kilivyokaa kaa..hahhahahahhah...eti mkaona..KIMAHITA KITOTO hahhahhahahahahah
 
jamii forums,

kuna mambo mengi yanasemwa hapa na mengine siyo ya kweli au si mahali pake. suala la mapungufu binafsi ya Marehemu Chedieli Mgonja hayafai kuibuliwa sasa hivi wakati ameshakata roho. sioni umuhimu wa kushindana kumkandamiza kwa madhambi aliyoyafanya kana kwamba amependekezwa awe mtakatifu, au kuna nafasi kubwa zaidi ya hizo alizopata kushika anapigania.

kama tuna nia ya dhati ya kujadili madhambi ya viongozi wetu, na haswa mambo ya chupi na vinena basi tuanze na wale walioko hai. tena wengine wanatunzwa kwa kodi zetu wananchi. kama tunataka kujadili mpaka wale waliokwisha kata roho basi tusibakishe mtu hapa iletwe orodha yao wajadiliwe bila kujali dini, kabila,rangi, na hata mchango wao kwa taifa.

kuna masuala mengine ambayo ni uongo wa waziwazi. kwa mfano kuna hoja kwamba Chedieli Mgonja hakufanya jambo lolote la maana na ndiyo maana hakuna anayemkumbuka. tena mchangiaji aliyesoma Tabora Boyz anadai hata hakusaidia kijijini kwao Vudee.

naomba wana jamii forums tujielimishe kidogo kuhusu historia na siasa. kati ya viongozi walioweza kuwahamasisha wananchi wao kujitolea kufanya shughuli za maendeleo Chedieli Yohane Mgonja ni mmoja wao. nawaomba mfuatilie shughuli za kuchimba barabara za milimani ktk wilaya ya Pare ndiyo mtaweza kumjua marehemu na utendaji wake.

katika ziara zake ktk wilaya ya Pare Baba wa Taifa alishangazwa na kuvutiwa sana na juhudi za wananchi na kiongozi[Mgonja] wao ktk uchimbaji wa barabara. katika moja ya ziara hizo Mwalimu alitamka "Wapare ni Wachina wa Tanzania."

mchangiaji mwingine amedai Mgonja na Eliufoo walipendelea wananchi wa Kilimanjaro ktk masuala ya elimu. habari hizi siyo za kweli. Eliufoo alikuwa waziri wa elimu kwa kipindi kisichozidi miaka miwili.

kwa upande wa Mgonja na jimbo la Pare(sasa hivi Same + Mwanga) lilibahatika kuwa na pilot project kwa elimu ya watu wazima wakati wa mkoloni. pia mwamko wa elimu umekuwepo ktk maeneo ya Upare tangu kabla ya uhuru.

wakati wa mkoloni Wapare walianzisha chama chao kilichoitwa Pare association. moja ya malengo ya chama hicho ilikuwa kampeni ya kujifunza kusoma na kuandika. hiyo ilikuwa ni miaka ya 1950. Tanzania nzima imekuja kuanzisha kampeni ya elimu/UPE miaka 20 baadaye-- mwaka 1977.

katika masuala ya elimu wananchi wa Pare tutamkumbuka Chedieli kwa kuhamasisha ujenzi wa shule za msingi ktk kila kata. hiyo ilikuwa ni utekelezaji wa ilani za Tanu na CCM kwamba wananchi wapeleke watoto shule. kama wabunge wa wilaya nyingine nchini hawakuhamasisha au walisubiri serikali siyo haki kumlaumu Chedieli Mgonja.

kabla ya wachangiaji hawajadai kwamba Mgonja alipendelea wilaya yake kwa hili au lile, kitu ambacho ni kutudhalilisha, naomba tujaribu kujifunza kidogo historia ya hao tunaowadhalilisha.

kuna suala lingine la kihistoria ktk wilaya ya Pare ambalo lazima lifahamike ili kuwaelewa wananchi wake. wananchi wa Pare walipoona wenzao wa Uchagani na Meru wanapiga kasi ktk maendeleo waliiomba serikali ya mkoloni iwatoze kodi ya maendeleo. mbinu za mkoloni ktk kukusanya kodi hiyo na matumizi yake zilizua mgomo wa wilaya nzima ya Pare uliojulikana kama mbiru.

halafu kuna suala la Mwalimu kutengua uteuzi wa Mgonja kama mkuu wa mkoa. Mwalimu alifanya hivyo baada ya kubaini kwamba Mahakama ilitoa hukumu ya kumfungia Chedieli Mgonja asishiriki siasa kwa miaka 10.

masuala ya kesi ya uchaguzi ya Mgonja ni mapana mno. lakini kwa kifupi baada ya kesi hiyo Mgonja alipata wasaa wa kuzungumza na Mwalimu na kujitetea. pia kulikuwa na ujumbe wa wazee wa Same waliokwenda kumuona Mwalimu na kuzungumza naye kuhusu mgogoro ya kisiasa ya wilaya Pare/Same na kesi ya uchaguzi ya Chedieli Mgonja.

baada ya mazungumzo yake na Mgonja na wazee kwa niaba ya wananchi wa Same Mwalimu aliona kwamba hakuwa na makosa yoyote. Mwalimu alibadilisha uamuzi wake baada ya kukumbushwa kwamba hukumu ya mahakama pia ilimfungia Mgonja asishiriki siasa miaka 10.

sina uhakika kama Mwalimu kwa kutumia madaraka yake alifupisha adhabu ya Chedieli Mgonja. katika uchaguzi wa mwaka 1990 wananchi wa Same walimrudisha bungeni kipenzi chao Chedieli Yohane Mgonja 'kaghembe.'
 
jamii forums,

kuna mambo mengi yanasemwa hapa na mengine siyo ya kweli au si mahali pake. suala la mapungufu binafsi ya Marehemu Chedieli Mgonja hayafai kuibuliwa sasa hivi wakati ameshakata roho. sioni umuhimu wa kushindana kumkandamiza kwa madhambi aliyoyafanya kana kwamba amependekezwa awe mtakatifu, au kuna nafasi kubwa zaidi ya hizo alizopata kushika anapigania.

kama tuna nia ya dhati ya kujadili madhambi ya viongozi wetu, na haswa mambo ya chupi na vinena basi tuanze na wale walioko hai. tena wengine wanatunzwa kwa kodi zetu wananchi. kama tunataka kujadili mpaka wale waliokwisha kata roho basi tusibakishe mtu hapa iletwe orodha yao wajadiliwe bila kujali dini, kabila,rangi, na hata mchango wao kwa taifa........................................................................................................................................................

Eti "mapungufu binafsi"!

Unasema waliokufa tusiwajadili. Lakini unatoa utetezi mreeeefu wa aliyoyafanya Mgonja. Ila hili la "ch*pi na vin*n*" unataka ku-foreclose mdahalo.

Hayo yoooote ya kuanzisha pilot project za Elimu ya Watu wazima, ya kuanzisha Pare Association of Mwanga and Same, kuanzisha UPE, na kutekeleza Ilani ya TANU, sijui kashinda kesi ya uchaguzi (kama hii ni sifa), sijui kuchimba barabara na Nyerere kusema "Wapare ni Wachina wa Tanzania (sijui hii ni sifa au ni nini), yooote hayo hayasemi lolote kuhusu ufisadi wa ngono.

Halafu hayo ya dini na kabila na rangi yanahusiana vipi na tuhuma za ufisadi wa ngono hapa?

Tetea hili: unajua au hujui, unabisha unakubali hoja kwamba Mgonja alikuwa fisadi wa "ch*pi na vin*n*?
 
Wanahistoria watakaochunguza jinsi Tanzania ilivyoitambua Jamhuri iliyojitoa kutoka Shirikisho la Nigeria, Jamhuri ya Biafra chini ya Odumegwu Ojukwu, bila ya kujali msimamo wa siku nyingi wa Tanzania wa kuunganisha Afrika kwa kuwa "Afrika ni Moja", watamkumbuka Chadiel Mgonja kama Waziri wa Mambo ya Nje na kiranja machachari wa Nyerere katika kuutetea msimamo huo usioyumkinika.

Ishi vizuri na kazi yako ionekane.
 
Sisi sote ni wa Mwenye-Enzi-Mungu na kwake Yeye-Mungu ni marejeo yetu. Tunamwomba Muumba-wetu aipokee roho ya Marehemu Chediel Mgonja na kuiweka pema peponi. Tunamwomba pia awape nguvu wafiwa ya kuuvumilia msiba huu - Amiin!
 
RIP Mgonja. Nakukumbuka sana ulipokuwa waziri katika nyadhifa mbali mbali katika nchi hii wakati huo ikiwa Tanzania. Ulikuwa waziri wa elimu na mambo yalikuwa yakienda haswa.
Sasa tuko katika nchi ya wadanganyika. Waliosomeshwa nawe bure leo hawasikii kilio cha wanyonge. Wanajali maslahi yao basi.
Sijui itakuwaje wana wa wana wetu.
Mimi nakumbuka nilikuwa sekondari wakati ukiwa waziri wa elimu.

Nakumbuka Waziri wa Elimu, Chediel Mgonja, alipotuhutubia shuleni, Tambaza High School, mwaka wa 1970. Tulimuuliza maswali mengi na alitujibu vizuri sana. Pia shule zetu miaka ile zilikuwa ni nzuri sana pamoja na walimu wetu; kwa mfano mwalimuw wetu mkuu Bori Lilla, ambaye sasa ni marehemu. Alifundisha pia, hakuwa headmaster tu. Na alikuwa ni mtu mwenye akili sana. Alistahili kuwa waziri katika serikali ya Mwalimu.

Yakuti, Msafiri, Chande, na wengineo, mnakumbuka maswali tuliyomuuliza Mgonja siku ile?

Pole sana wafiwa wa Mzee Mgonja na Mzee Lilla.

Rest in peace.
 
Si kipindi cha kusema mabaya ya marehemu sasa. Ni wakati wa kuwapa pole wafiwa na kumkabidhi marehemu kwenye HURUMA ya Mungu.

Hakuna hata mmoja wetu anayefahamu kwa uhakika kwamba mbele ya macho ya Mungu, yeye ni bora kuliko marehemu. Tumwombee na tujiombee.

I request those who would like to talk about the many paedophiles that inhabit, and have inhabited, our corridors of power to do so in another thread.
 
Chedieli Yohane Mgonja.

kuzaliwa 31 December 1934, Vudee Same-Magharibi.

shule ya msingi Vudee, sekondari Ilboru na Tabora.

1959 ---Chuo Kikuu Makerere.

1960 ---Bwana Shauri Tanga.

1961 --- miongoni mwa Watanganyika sita waliotunukiwa zawadi kwa kushiriki ktk shindano la utenzi wa wimbo wa taifa wa Tanganyika.

1961 --- 62 Chuo Kikuu Cambridge UK -- kozi ya utawala na Diplomasia.
wengine katika kozi hiyo ni walioapata kuwa mabalozi George Nhigula,John Malecela, Bernard Mulokozi, Raphael Lukindo, Akili Daniel.

1962 --- Ubalozi wa Tanganyika New York.

1964 --- kuomba kurudi nyumbani kwa nia ya kugombea Ubunge.

1965 --- kupigania ubunge wilaya ya Pare vs Naibu Waziri na katibu mwenezi wa Tanu Elias Kisenge.

1965 --- 67 Mbunge wilaya ya Pare, Waziri wa Maendeleo na Utamaduni. rekodi ya kuwa waziri kijana kuliko wote Tanzania.

1967 -- 68 Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi ( Mambo ya Nje ). waziri wa kwanza kujiunga na mafunzo ya JKT. baadaye kuendelea na mafunzo ya mgambo. waziri aliyetoa tamko la serikali ya Tanzania kuitambua Jamhuri ya watu wa Biafra.

1968 -- 72 Waziri wa Elimu. mabadiliko makubwa ktk mfumo wetu wa elimu yalifanyika kipindi cha uongozi wake.

1972 -- 75 Mkuu wa Mkoa na Katibu wa Chama Mtwara. ni uteuzi pekee ambao Mwalimu alimjulisha kabla haujatangazwa. ilikuwa ni kipindi cha madaraka mikoani na vita ya ukombozi ya Msumbiji. mkoa wa mtwara kushika nafasi ya pili, ukifuatia dsm, ktk kuchangia vita vya ukombozi.

1977 -- Mkuu wa Mkoa na Katibu wa Chama Tabora.

1977 -- 1980 Waziri wa Utamaduni, Vijana, na Michezo. Tanzania kukataa shinikizo la Marekani kususia michezo ya olympic Moscow. Ujumbe wa Marekani uliletwa na Mohamed Ali.

1980 -- 1982 kushinda Ubunge. Kushinda kesi dhidi yake mahakama Kuu Arusha. Kuvuliwa Ubunge na mahakama ya Rufaa Tanzania.

1984 -- kuteuliwa na Raisi Mkuu wa Mkoa Shinyanga.

1985 -- 95 Mbunge Wilaya ya Same: vs Jonas Manento(85) vs.Dr.Kivurunya Mtera(90).

Chedieli Yohane Mgonja, mbunge wa mwisho wilaya ya Pare(mwanga + same), na mbunge wa mwisho wilaya Same( same mashariki + magharibi )
 
Si kipindi cha kusema mabaya ya marehemu sasa. Ni wakati wa kuwapa pole wafiwa na kumkabidhi marehemu kwenye HURUMA ya Mungu.

Nakuelewa. Fair enough.

Hakuna hata mmoja wetu anayefahamu kwa uhakika kwamba mbele ya macho ya Mungu, yeye ni bora kuliko marehemu. Tumwombee na tujiombee.

False logic. Mantiki ya uongo. Kwanza umeshindwa ku apply the same test uliyotutahadharisha kutojiingiza kwenye mdahalo wa ngono wakati huu, maana unatetea tabia za ngono ngono ukitaka sisi tunaopinga ufuska tukae kimya tu. Au unataka tujibu? Huoni utakuwa umechochea mdahalo huo huo?

Second of all, kama "hakuna mtu anaejua kwa uhakika mbele ya macho ya mungu yeye ni bora kuliko marehemu" kwa hiyo tusiseme kitu, basi nikuulize, kuna mtu ana uhakika kwamba yeye ni bora mbele ya macho ya Mungu katika ufisadi wa malfeasance serikalini? Wewe umewahi kumkosoa kiongozi yeyote yule maishani mwako katika ufisadi wa government malfeasance? Je wewe ni bora zaidi?

I request those who would like to talk about the many paedophiles that inhabit, and have inhabited, our corridors of power to do so in another thread.

Unakosea tena!

Tungeweza kuanzisha thread nyingine katika wakati huu wa majonzi halafu badala ya "Chadiel Mgonja afariki" tukaiita "Ufisadi wa Ngono wa Chadiel Mgonja," huoni hiyo itakuwa ime defeat the purpose?

The issue, the fundamental argument you started out with sio kuchanganya threads, ila ni kwamba muda sio muafaka. Sasa usianze tena kuteteatetea ukahaba, una entertain mdahalo, mdahalo ambao huuwezi maana huutaki, wala usiseme tufungue thread nyingine. Sema muda si muafaka nyamaza!
 
Si kipindi cha kusema mabaya ya marehemu sasa. Ni wakati wa kuwapa pole wafiwa na kumkabidhi marehemu kwenye HURUMA ya Mungu.

Hakuna hata mmoja wetu anayefahamu kwa uhakika kwamba mbele ya macho ya Mungu, yeye ni bora kuliko marehemu. Tumwombee na tujiombee.

I request those who would like to talk about the many paedophiles that inhabit, and have inhabited, our corridors of power to do so in another thread.

Huyu mheshimiwa alipewa dhamana ya kusimamia watoto wetu, nae akaitumia vibaya. Vitendo alivyokuwa akivifanya ni sawasawa na kubaka maana hao mabinti walikuwa hawana maamuzi. Kutokana na vitendo vya viongozi kama hawa na wenzie wakina Mkisi, sehemu zao walizokuwa wakiziongoza zikajenga tabia ya kuona mabinti zetu tuliowapa watuangalilie kuwa ni haki yao kuwatumia watakavyo. Kuanzia walimu wa kawaida, walimu wakuu, maafande wa chini kabisa hadi juu kabisa, wengi wao bila aibu waliwaharibu mabinti za wenzao. Nimeshuhudia katika kambi za JKT watoto wa kujitolea waliomaliza tu darasa la saba walivyokuwa wakichangamkiwa na watu waliokuwa na umri wa babu zao! Nimeona katika shule (hata baada ya marehemu kuondoka katika wizara hiyo) jinsi mabinti wanavyokabidhiwa kwa wageni ili kuwakinga na baridi ya usiku! Hivi katika nyinyi, nani ambae angemsamehe, mtu mzima aliyempa dhamana ya kumuangalia binti yake na badala yake kumharibu? Wangapi mnajiuliza ni maisha ya wasichana wangapi yaliyoharibiwa na hawa tuliowapa dhamana hiyo? Mpaka leo sijasikia hata mmoja wao akiomba msamaha kwa maovu hayo waliyoyafanya. Leo mnataka watu wakae kimya kwa sababu si watoto wenu waliohusika? Hapana, pamoja na majonzi ya wafiwa lakini ni lazima tuseme wazi kuwa matendo kama haya hayana sehemu katika jamii yetu. Pengine, hao wanaoendeleza tabia hiyo wakijua kuwa hatutawasamehe hata wakienda kwenye hukumu watajirudi!
 
Wanahistoria watakaochunguza jinsi Tanzania ilivyoitambua Jamhuri iliyojitoa kutoka Shirikisho la Nigeria, Jamhuri ya Biafra chini ya Odumegwu Ojukwu, bila ya kujali msimamo wa siku nyingi wa Tanzania wa kuunganisha Afrika kwa kuwa "Afrika ni Moja", watamkumbuka Chadiel Mgonja kama Waziri wa Mambo ya Nje na kiranja machachari wa Nyerere katika kuutetea msimamo huo usioyumkinika.

Ishi vizuri na kazi yako ionekane.
Kwa hili la kuitambua Biafra kama kuna lawama zozote anayestahili kuzibeba ni Julius Kambarage Nyerere. Hata kama marehemu Mgonja alikuwa "kiranja machachari" uamuzi huo ulifanywa na Julius Nyerere.
 
Kwa hili la kuitambua Biafra kama kuna lawama zozote anayestahili kuzibeba ni Julius Kambarage Nyerere. Hata kama marehemu Mgonja alikuwa "kiranja machachari" uamuzi huo ulifanywa na Julius Nyerere.

Who was the chief policy adviser at the time? Tunajuaje kwamba yeye sio aliyemshauri Nyerere kuchochea kuvunja muungano wa Nigeria?

Well, unaweza kuwa sahihi Chadiel Mgonja aliburuzwa tu, after all, tunamjua Nyerere wetu, alikuwa ana bulldoze kila mtu na kifimbo cheusi.

Lakini hata kama Mgonja alibururwa bururwa bado tutasema yeye ndio alibeba ujumbe wa nchi.

Collin Power alienda United Nations na vichupa vya ushahidi wa silaha za Iraq. Walipotekeleza siasa ya kuvamia Iraq wakakuta silaha ni hewa Collin alipoteza credibility, na hakusema "nilitumwa na Bush," angeambiwa wewe "roboti"? Hatuwezi kuanza kuchambua ni nani alibeba ujumbe, nani alipelekeshwa ki punda punda kati ya Collin, Diki, Paulo, Donadi, Condi, na George wa Tenet, George wa Bushi, hatujui, hatujali kuanza kuchambua nani alimshawishi nini nani.

Wote walikuwa jikoni, wote walipika siasa ya nje, wakaibeba. Huko jikoni aliyekatishwa vitunguu, aliyechochea kuni, aliyetoa resapi, aliyesongeshwa ugali, wao ndio wanajua.

Kiongozi unaepinga kubururwa bururwa anajiuzulu.
 
Who was the chief policy adviser at the time? Tunajuaje kwamba yeye sio aliyemshauri Nyerere kuchochea kuvunja muungano wa Nigeria?

Well, unaweza kuwa sahihi Chadiel Mgonja aliburuzwa tu, after all, tunamjua Nyerere wetu, alikuwa ana bulldoze kila mtu na kifimbo cheusi.

Lakini hata kama Mgonja alibururwa bururwa bado tutasema yeye ndio alibeba ujumbe wa nchi.

Collin Power alienda United Nations na vichupa vya ushahidi wa silaha za Iraq. Walipotekeleza siasa ya kuvamia Iraq wakakuta silaha ni hewa Collin alipoteza credibility, na hakusema "nilitumwa na Bush," angeambiwa wewe "roboti"? Hatuwezi kuanza kuchambua ni nani alibeba ujumbe, nani alipelekeshwa ki punda punda kati ya Collin, Diki, Paulo, Donadi, Condi, na George wa Tenet, George wa Bushi, hatujui, hatujali kuanza kuchambua nani alimshawishi nini nani.

Wote walikuwa jikoni, wote walipika siasa ya nje, wakaibeba. Huko jikoni aliyekatishwa vitunguu, aliyechochea kuni, aliyetoa resapi, aliyesongeshwa ugali, wao ndio wanajua.

Kiongozi unaepinga kubururwa bururwa anajiuzulu.
Kuhani,
Believe me, uamuzi ulifanywa na Mwalimu Nyerere peke yake. I know this kwa sababu at the time I was staying at Butiku's home. Mwalimu aliamua kuitambua Biafra baada ya juhudi zake kuwapatanisha Ojukwu na Gowon kugonga mwamba--kutokana na jeuri ya Gowon kuwa hawezi kukaa meza moja na junior wake. At the same time people were dying in Eastern Nigeria.
Nimeshalizungumzia suala hili awali katika mojawapo ya threads hapa JF.
And, by the way Watanzania wengi waliunga mkono uamuzi huo.
 
Kuhani,
Believe me, uamuzi ulifanywa na Mwalimu Nyerere peke yake. I know this kwa sababu at the time I was staying at Butiku's home. Mwalimu aliamua kuitambua Biafra baada ya juhudi zake kuwapatanisha Ojukwu na Gowon kugonga mwamba--kutokana na jeuri ya Gowon kuwa hawezi kukaa meza moja na junior wake. At the same time people were dying in Eastern Nigeria.
Nimeshalizungumzia suala hili awali katika mojawapo ya threads hapa JF.
And, by the way Watanzania wengi waliunga mkono uamuzi huo.

Well, Jasusi

Unajuaje Mgonja hakukubaliana na uamuzi wa Nyerere ila alibeba tu ujumbe?
 
Back
Top Bottom