Waziri wa zamani, Chadiel Mgonja afariki

ooooooooooooohh that great br polen sana huyu mzee nilikuwa simjui nimemjulisha mzee wangu jana akataahamaki kama anamtoamtu b***ra!!!kweli?amewapa pole sana mungu aangalie rehema zake asiangalie makosa yake!!!!!
endelaa necha mekuoko!!!
 
Michael na familia yote poleni sana kwa msiba mkubwa uliowapata wa kuondokewa na Baba yenu mpendwa. Namuomba Mwenyezi Mungu awape subira na faraja katika kipindi hiki kigumu kwenu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi~AMEN.
 
..hilo la uhamasishaji ilikuwa moja ya sifa yake nzuri.......

- Viongozi wengi au karibu wote wa enzi zile walikuwa waadilifu sana, sawa walikuwa na matatizo madogo madogo ya kinamama, lakini in ther big picture walikuwa imara sana kuliko wa sasa, hawakuwa mafisadi, huyu naye naamini kuwa alikuwa kiongozi safi.
 
..huyu bwana hakuwa fisadi lakini kwa zupu bwana we...,!..alikuwa akienda mikoani hafikii hotelini bali anaandaliwa malazi na ma head mistress...wa shule husika...,sasa nasikia kuna siku alienda singida headmostress alikuwa thabita siwale....akamwandalia kila kitu alafu akamletea na binti ..du mzee kuangalia binti akakuta ni binti yake]


PHILEMONI,
Haya si maneno yakusema wakat huu wa majonzi.
 
wana JF hatujawa fair kabisa ..wiki iliyopita amefariki ABEL K.MWANGA..hatujatoa rambi rambi zetu kama sikosei..moja ya wazee waadilifu kabisa ..amefariki kisukari kama huyu mzee mgonja na wote walikuwa wanabembeleza angalau wakatibiwe INDIA lakini serikali nafikiri ilishawasahau...nashangaa sana kwanini KAWAWA hawatetei old guards wenzake..maana hawa kina kikwete nao walikuwa vijana wadogo miaka hiyo...ambaye angeweza kuwasemea vema hawa pale waanaposahaulika ni KAWAWA...au MWINYI.....LAKINI hasa kawawa ambaye siku hizi kila siku yupo london anatibiwa hata kikohozi ....wakati mawaziri wenzake wa zamani wanakosa hata dola 2,000 za kuwafanyia check up hapo appolo ,india angalau mara moja kwa miaka 5....yeye kwa mwaka anaenda mara 6 london..tena nahisi yule bi mdogo ana abuse hiyo nafasi ya mzee..kwa ku fake mumewe anaumwa wakati hata MOI pangemfaa.....miaka yote mbona alikuwa anatibiwa MOI au INDIA,CHINA kabla hajamuowa....mbona hakufa?
 
- Viongozi wengi au karibu wote wa enzi zile walikuwa waadilifu sana, sawa walikuwa na matatizo madogo madogo ya kinamama, lakini in ther big picture walikuwa imara sana kuliko wa sasa, hawakuwa mafisadi, huyu naye naamini kuwa alikuwa kiongozi safi.

Hivi kupenda waschana tena wanafunzi ukiwa waziri wao- je haya ni matatizo madogo? Uadilifu uko wapi?

RIP Mgonja!
 
Pole kwa familia ya Mzee Mgonja na watu wote wa Same.....Waungwana tujaribu kumstahi Mzee kidogo kwenye kipindi hichi kigumu cha Maombolezo,mambo mengine si wakati wake huu.....Kumuangalia Mgonja nje ya ofisi ya Uwaziri/Ubunge wake ni kutomtendea haki,Viongozi wengi ugonjwa wa Totos ni kama sifa ya kazi....tukianza kuwaangalia kwa upande huo hakuna atakayepona!!!
 
FMes,
Si ndiyo huyu ulisema alichukua mke wa kipenzi chetu Patrick Balisidya? Na kama hiyo haitoshi, akasababisha na jamaa kukosa vyombo vya kupigia mziki wake na huo ndiyo ukawa mwisho wake? Lohh, sasa sijui atamwambia nini Balisya wakikutana huko. Na vile vitoto vya watu alivyovichezea au kuviharibia maisha kabisa.
Wakati wa Nyerere kulikuwa nako kuna madudu yake. Ila sema Mawaziri walikuwa wana muogopa sana Nyerere na hivyo KUTIMIZA WAJIBU WAO. Rais anapokuwa BOMU hadi watoto wa shule ya msingi wanamdharau, yeye mwenyewe kwenda kuchukua watoto wa secondary kama kwa mfano Jangwani, inafanya hata watu wake wa chini waache kumheshimu. Hili kwa JKN halikuwepo. Ila linalonisumbua ni hili la viongozi kuandaliwa vitoto vya watu. Nilishalisikia kwa mkuu mmoja wa JKT ila nimesahau jina ila kama sikosei ni huyo kabla ya Makame. Huyu na yeye nasikia alikuwa akifika anadai aletewe Kuruta wa kulala naye. Kumbe walikuwa wengi? Waanikeni hapa ili wajukuu wao waone Babu alikuwa wa aina gani.
Sijui niseme RIP au nisiseme? Wakristo wanasema KILA MTU ATAUCHUKUA MZIGO WAKE MWENYEWE. Hivyo, namwachia Mungu mwenyewe kuamua.
 
Mchukia Ufisadi,

Hawa wazee nao walikuwa na ufisadi wao, kwa mfano Mgonja ilikuwa kazi yake kuchukua wasichana kwenye hizo shule za secondary. Alikuwa hana tofauti na yule Mkisi wa JKT.

Miaka hiyo watu walikuwa na uzalendo wa kulitumikia taifa ukiachia matatizo yao madogo madogo.

Wakuu heshima mbele, Mbona tunaishushia hadhi baraza
Huo uvulana ndio mila zetu
Jee tushushe mafaili ya fuatayo
1. mwalimu
2. Lowasa
3 muungwana
4. Rostam Aziz
5. Freeman Mbowe
6. Lau Masha
7. David Mattaka
Na wengineo wengi tuu
Mbona wengine ni mafisadi wa vyote
Tumuombee kwa mungu amlaze pema peponi mzee wetu na alifanya kazi kwa moyo hili halina mjadala na ni mfano wa kuigwa
 
....Waungwana tujaribu kumstahi Mzee kidogo kwenye kipindi hichi kigumu cha Maombolezo,mambo mengine si wakati wake huu.....Kumuangalia Mgonja nje ya ofisi ya Uwaziri/Ubunge wake ni kutomtendea haki,Viongozi wengi ugonjwa wa Totos ni kama sifa ya kazi....tukianza kuwaangalia kwa upande huo hakuna atakayepona!!!

Mwawado ndugu,

Unatuasa huu si wakati wa kujadili mambo ambayo sio ya kumstahi marehemu lakini na wewe unaanza kutupa ka mhadhara kuteteatetea tabia ya "totos," eti ni nje ya ofisi, na kwamba ni wengi wanayafanya.

Sasa ndugu, labda ungechagua aidha kusimamia huu utamaduni wa kubakiza staha katika kipindi hiki kigumu au uwe tayari kwa yatakayojiri baada ya wewe kufungulia malango ya mdahalo wa uhalali na uharamu wa ukahaba na ufuska wa Wazee wa jamii, mawaziri au wananchi, wa hai na wafu.

Marehemu Chadiel Mgonja shukurani kwa mchango wako wa toka siku za uchanga wa Taifa letu.
 
Mwawado ndugu,

Unatuasa huu si wakati wa kujadili mambo ambayo sio ya kumstahi marehemu lakini na wewe unaanza kutupa ka mhadhara kuteteatetea tabia ya "totos," eti ni nje ya ofisi, na kwamba ni wengi wanayafanya.

Sasa ndugu, labda ungechagua aidha kusimamia huu utamaduni wa kubakiza staha katika kipindi hiki kigumu au uwe tayari kwa yatakayojiri baada ya wewe kufungulia malango ya mdahalo wa uhalali na uharamu wa ukahaba na ufuska wa Wazee wa jamii, mawaziri au wananchi, wa hai na wafu.

Marehemu Chadiel Mgonja shukurani kwa mchango wako wa toka siku za uchanga wa Taifa letu.

Nimekusikia Mkuu "Naomba maneno yangu yasichochee kukosa Heshima dhidi ya Wazee wetu" kama maneno yangu kuhusu Totoz yanaondoa staha,usiyatilie maanani.....sote kwa pamoja tuungane na familia ya Marehemu kuelekeza sala zetu huko.
 
Marehemu Mgonja na Marehemu Eliufoo ndio waliopanua ELIMU mkoani Kilimanjaro kiasi kwamba tuna wasomi wengi kutoka mkoa huo pekee. Kama huo ulikuwa ni ukabila labda "tuwalaumu" kwa hilo. Poleni wafiwa.
 
Marehemu Mgonja na Marehemu Eliufoo ndio waliopanua ELIMU mkoani Kilimanjaro kiasi kwamba tuna wasomi wengi kutoka mkoa huo pekee. Kama huo ulikuwa ni ukabila labda "tuwalaumu" kwa hilo. Poleni wafiwa.

Good Charity always starts at home. Sio ukabila, some people just seem to understand the concept more than others...
 
Philemon Mikael umesema maneno ya kweli tena ya uhakika sana,Kipindi mgonja alikuwa waziri na Mkuu wa Mkoa wa Tabora mie nilikuwa mwanafunzi katika ile shule ya ma-Boyz (TS) Nilimshuhudia mheshimiwa huyo akienda visiting shule ya Wasichana (TG)siyo kama mzazi au ndugu wa mwanafunzi bali kama mshikaji wa mwanafunzi.Tuliyajua yote hayo kwani wale walikuwa mademu zetu,Sasa mzee anapokuja na 110 yenye bendera nyie wavaa magwanda mnakuwa hamna nafasi ya visiting kwa siku hiyo.Si hayo tu Marehemu aliwahi kuteuliwa kushika nafasi ya u-RC.Mwalimu alipogutuka akmwita haraka na kutengua uteuzi ule.Nina uhakika kwamba enzi zile Azimio la Arusha lilishika hatamu,Lakini ufisadi wa ngono ulikuwepo sana,Kwani halikuwa sharti mojawapo katika yale yaliyowabana Viongozi.
Zaidi ya hayo Marehemu Chediel Mgonja hakuna jambo aliloweza kusaidia hata kijijini kwao.Ndo maana hana kumbukumbu yoyote zaidi ya kuendekeza ngono katika jamii.
Ahera ni kwa wote lakini nako kuna peponi na motoni si kazi yetu kumpangia mwenyezi Mungu kwmba huyu na huyu aende wapi.Bali kila mmoja kwa matendo yake atapata kile anachositahili mbele ya haki.

Je viongozi wa sasa si zaidi yake Marehemu Mgonja aloyafanya?
 
RIP Chadiel!......Lakini mhhhh!....alipokuwa waziri wa elimu alipendelea sana mkoa wake kwa kuwapeleka secondary kuliko mikoa mingine achilia mbali ya totos
 
Philemon Mikael umesema maneno ya kweli tena ya uhakika sana,Kipindi mgonja alikuwa waziri na Mkuu wa Mkoa wa Tabora mie nilikuwa mwanafunzi katika ile shule ya ma-Boyz (TS) Nilimshuhudia mheshimiwa huyo akienda visiting shule ya Wasichana (TG)siyo kama mzazi au ndugu wa mwanafunzi bali kama mshikaji wa mwanafunzi.Tuliyajua yote hayo kwani wale walikuwa mademu zetu,Sasa mzee anapokuja na 110 yenye bendera nyie wavaa magwanda mnakuwa hamna nafasi ya visiting kwa siku hiyo.Si hayo tu Marehemu aliwahi kuteuliwa kushika nafasi ya u-RC.Mwalimu alipogutuka akmwita haraka na kutengua uteuzi ule.Nina uhakika kwamba enzi zile Azimio la Arusha lilishika hatamu,Lakini ufisadi wa ngono ulikuwepo sana,Kwani halikuwa sharti mojawapo katika yale yaliyowabana Viongozi.
Zaidi ya hayo Marehemu Chediel Mgonja hakuna jambo aliloweza kusaidia hata kijijini kwao.Ndo maana hana kumbukumbu yoyote zaidi ya kuendekeza ngono katika jamii.
Ahera ni kwa wote lakini nako kuna peponi na motoni si kazi yetu kumpangia mwenyezi Mungu kwmba huyu na huyu aende wapi.Bali kila mmoja kwa matendo yake atapata kile anachositahili mbele ya haki.

Je viongozi wa sasa si zaidi yake Marehemu Mgonja aloyafanya?

Hilo la ngono mbona ni kawaida ya wapare wote!
 
Mwawado ndugu,

Unatuasa huu si wakati wa kujadili mambo ambayo sio ya kumstahi marehemu lakini na wewe unaanza kutupa ka mhadhara kuteteatetea tabia ya "totos," eti ni nje ya ofisi, na kwamba ni wengi wanayafanya.

Sasa ndugu, labda ungechagua aidha kusimamia huu utamaduni wa kubakiza staha katika kipindi hiki kigumu au uwe tayari kwa yatakayojiri baada ya wewe kufungulia malango ya mdahalo wa uhalali na uharamu wa ukahaba na ufuska wa Wazee wa jamii, mawaziri au wananchi, wa hai na wafu.

Marehemu Chadiel Mgonja shukurani kwa mchango wako wa toka siku za uchanga wa Taifa letu.

Matamko kama haya ndiyo yanayofanya nisione taabu kukuita bosi wangu! Uovu huu wa ukahaba na ufuska ( mara nyingi ni ubakaji maana wako wanaotembea na watoto walio chini ya umri unaowaruhusu kujiamulia) wa wale ambao wanadai wapewe heshima na jamii ni lazima ukemewe kwa sauti ya juu. Athari yake kwa jamii ni sawa sawa na hiyo inayosababishwa na hao tunaowaita mafisadi!
 
Back
Top Bottom