Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni upo 'serious' kweli katika Kupambana na Ajali za Barabarani nchini Tanzania?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,551
108,885
Yaani Waziri Masauni umeshakiri Mwenyewe kuwa Wamiliki wa Mabasi ya Mikoani kwa Makusudi wameondoa 'Spidi Gavana' katika Mabasi ya hali inayopelekea Madereva Wao kwenda Mwendo Kasi na Kusababisha Maafa (Ajali) zinazoua Watanzania na kuwapa Ulemavu wa kudumu halafu Wewe unawapa 'Ultimatum' ya miezi Sita (6) Kurejesha hizo 'Spidi Gavana' badala ya kuwapa Siku Saba (7) tu zijazo.

Kwahiyo Waziri Masauni kwa Lugha nyepesi hapa ni kama vile Umeshatoa ruhusa ya Watanzania Kuuwawa (Kuuliwa) na Madereva wa Mabasi ya Mikoani kwa Miezi Sita (6) ijayo na baada ya hapo ndipo mtawaonea Huruma kwa kuanza Kuwajali kwa Ustawi wao wawapo Safarini.

Hivi nyie Mawaziri baadhi yenu Vichwani mwenu (hasa Kiakili) mpo sawa sawa kweli au labda mnahitaji Tiba ya haraka Hospitali za Mirembe (Dodoma) na Lutindi (Tanga) kutokana na Kauli zenu na Maamuzi yenu yasiyovumilika kutokana na kuwa ni ya 'Kiudhaifu' zaidi?

Kuna Waziri Mwenzako wa Maji Jumaa Aweso nae Wiki Mbili nyuma alimsifia kweli kweli Boss Mkuu wa DAWASA Cyprian Luhemeja mbele ya Rais Samia huko Chalinze huku akimnadi kuwa ndiyo Mfanyakazi Bora wa mwaka na Jana tu katika Ripoti ya CAG Taasisi yake imekutwa na 'Madudu' ya 'Ubadhirifu' ya karibia Tsh Milioni 800 kwa Kuwadhulumu Watanzania hasa katika Usomaji Hewa wa Mita zao za Maji huko Majumbani mwao.

Waziri Masauni labda nikuambie tu Wewe pamoja na Boss wako Mkuu na Watendaji Wenzako (hasa Mawaziri) kuwa Watanzania tunajitahidi mno Kumsahau Hayati Rais Dkt. Magufuli, ila kwa huu Upuuzi wenu, Maamuzi yenu na Utendaji wenu wa hovyo hovyo ndiyo mnatufanya Watanzania (akina GENTAMYCINE) kila mara tuwe si tunamkumbuka bali pia tumlilie sana Rais Hayati Dkt. Magufuli kutokana na Utendaji wake uliokuwa ni wa Kutukuka na wa Kishujaa zaidi.

Haya Madereva wa Mabasi ya Mikoani na Wamiliki wa Mabasi ya Mikoani jitahidini sasa mtuue kwa Ajali za Mwendo Kasi kwani tayari Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni ameshawapeni ruhusa ya Miezi Sita (6) na hata wale ambao bado Mabasi yenu yana Spidi Gavana mlizofunga mnaweza sasa mkazing'oa tu ili mtuue kwa Mwendo Kasi ndani ya Miezi Sita (6) ijayo na baada ya hapo (mkishashiba Damu zetu na Viungo vyetu) mtazirejesha kama mlivyoagizwa na Waziri.

Halafu akina GENTAMYCINE na Watanzania wengine baadhi wanaojua Kufikiri na Kuona mbali (kwa Kubarikiwa na Mwenyezi Mungu) wakiwakosoa kwa nia ya Kuwajenga na kuwapeni Fursa ya Kujitathmini mnatuchukia, mnatuona ni Wapinzani, tunatumwa na Mabeberu, tuna Chuki Binafsi nanyi na mpaka mnatamani tupotee tu kabisa duniani.

Kwa wale mnaopenda kujua Maamuzi haya ya 'Kipuuzi' ya Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni nimeyasikia wapi ni kwamba nimeyasikia hivi punde tu kutoka katika Kipindi kizuri cha Nipashe kutoka Radio One ambapo Mtangazaji wa Zamu leo ( Alhamisi ) alikuwa ni Mtangazaji Mahiri na Makini Maulid Kambaya.
 
Tuwe wawazi, uwepo WA Askari wengi barabarani kumeongeza Rushwa na stress Kwa watumiaji WA barabara hence ongezeko la ajali Kwa madereva kuendesha wakiwa na mawazo mengi, ni muhimu wanasaikologia wakaingilia kati!! Pia ajali nyingi zilizotokea hazihusishi sana mwendokasi, hivyo wasihusishe sana Askari na mitochi Yao kuongeza wigo WA rushwa
 
Ushauri wangu warekebishe miundo mbinu yaani barabara ziwe nzuri ziendane na aina ya Magari yaliyopo sokoni ili watu watembee haya mambo ya ajali kiasi kikubwa miundo mbinu inachangia
 
Mleta mada acha ujuaji usio na kichwa wala miguu Spidi gavana Madukani hazipo mlitaka Waziri atoe agizo lisilotekelezeka? Spidi gavana ni special order haiko full time Madukani kama nyanya gengeni .Kuagiza nje ya nchi ni process inachukua muda wenye mabasi hawatengenezi hizo spidi gavana Wafanyabiashara ndio huagiza wakiridhika kuwa soko lipo

Pili kuna gharama hazitolewi bure.Huwezi kumwambia kesho ufunge hiyo pesa unampa wewe huyo mwenye basi?
 
Ushauri wangu warekebishe miundo mbinu yaani barabara ziwe nzuri ziendane na aina ya Magari yaliyopo sokoni ili watu watembee haya mambo ya ajali kiasi kikubwa miundo mbinu inachangia
Wengi hawajui mambo ya magari
Ukinunua gari jipya mfano basi unapewa warrants na guarantee .Kuweka modification mfano spidi gavana inaingilia mfumo original wa gari wa spidi hapo unakuwa umeiondia gari yako kwenye guarantee. Kampuni iliyokuuzia haitawajibika tena

Kinachotakiwa ni tu miundombinu iwe.mizuri na madereva Wazuri na magari kuwa hali nzuri
 
Mleta mada acha ujuaji usio na kichwa wala miguu Spidi gavana Madukani hazipo mlitaka Waziri atoe agizo lisilotekelezeka? Spidi gavana ni special order haiko full time Madukani kama nyanya gengeni .Kuagiza nje ya nchi ni process inachukua muda wenye mabasi hawatengenezi hizo spidi gavana Wafanyabiashara ndio huagiza wakiridhika kuwa soko lipo

Pili kuna gharama hazitolewi bure.Huwezi kumwambia kesho ufunge hiyo pesa unampa wewe huyo mwenye basi?
Mpuuzi sana wewe kwann walizitoa na kwann wasiweze kurudisha? Kubali kaka ako ameponyokwa fikira

Ajari haina macho mtetee leo lakini hujui kesho yako
 

Hamad Masauni kwao ni visiwani, huku bara hata mkaisha wote hana hasara.​

Tangu lini waziri wa mambo ya ndani akatoka visiwani kama hii sio shida imeingia Tanganyika?​

Rais mstaafu Mwinyi alishakuwa Waziri wa mambo ya ndani
 
Mpuuzi sana wewe kwann walizitoa na kwann wasiweze kurudisha? Kubali kaka ako ameponyokwa fikira

Ajari haina macho mtetee leo lakini hujui kesho yako
Ukiambiwa uzitoe spidi gavana unaenda kuzitunza stoo? au unatupilia mbali huko.? Waliambiwa hazitakiwi toeni unadhani waliweka jumba la makumbusho museum wakiota kuwa iko siku Serikali itazihitaji tena? Walitupa baada ya kuambiwa hazitakiwi

Inabidi kuagiza upya
 

Hamad Masauni kwao ni visiwani, huku bara hata mkaisha wote hana hasara.​

Tangu lini waziri wa mambo ya ndani akatoka visiwani kama hii sio shida imeingia Tanganyika?​

Hiyo Wizara kwa miaka mingi inaongozwa na watz wa Kisiwani
 
Na Mpumbavu yoyote kama Yeye kamwe hawezi Kusikiliza Redio, ila Kipaumbele chake kikubwa awapo JamiiForums ni Kuhangaika na GENTAMYCINE ambaye naendelea Kueleweka vyema na Mtu Makini kama Wewe, lakini Kwake kutokana na Upumbavu wake wa Kurithishwa sieleweki na kamwe hatokuja Kunielewa.
Tuyaache hyo mkuu . On a serious note.

Nataka kumleta Mkojani aje Kupiga show huko Bunda kijijini unapoishi wewe. Ni ukumbi Gani hapo Bunda kijijini ambao utafaa kutumika?

With much thanks in advance
 
Tuwe wawazi, uwepo WA Askari wengi barabarani kumeongeza Rushwa na stress Kwa watumiaji WA barabara hence ongezeko la ajali Kwa madereva kuendesha wakiwa na mawazo mengi, ni muhimu wanasaikologia wakaingilia kati!! Pia ajali nyingi zilizotokea hazihusishi sana mwendokasi, hivyo wasihusishe sana Askari na mitochi Yao kuongeza wigo WA rushwa
Kama unafuata sheria na utaratibu stress inatoka wapi?
 
Taarifa zikikosewa huna zinaleta madhara ya uelewa kwa jamii nzima,. Sina shida na kukosewa kwa taarifa , hofu yangu ni kuwa taarifa zinapokosewa na mtu ambaye ana dhamana kubwa kama waziri

Mabasi kwa sasa hayafhibitiwi mwendo na speed governor, bali kuna speed monitor , na watchdog wa speed hizo ni Latra!,
Kwa wasioelewa speed monitor ni Gps module with unique transponder in it , kwa maana ya kuwa module hii inajieleza ilipo ,mwendo inaotembea pamoja na muda .basi zote kwa sasa ni lazima kwa sheria za latra kuwa na module hii.,Latra wao kama watchdog, wanastaff ambao kazinyao ni kufanya monitoring ya kila gps module iliyo active, which means kila basi unayoiona barabarani muda wote inaonekana pia kwenye dashboard za latra kwa muda huo.

Yeyote anayesema wamiliki wa mabasi wameondoa vidhibiti mwendo , hana taarifa sahihi au ana lengo la kufanya truth derailment.

Basi zinakimbia na kupata ajali kwa sababu ya Rushwa , watu wana access na Latra hasa watu wa speed monitoring.
 
Mpuuzi sana wewe kwann walizitoa na kwann wasiweze kurudisha? Kubali kaka ako ameponyokwa fikira

Ajari haina macho mtetee leo lakini hujui kesho yako
Huwa nafurahi Werevu wachache hapa JamiiForums mkijitokeza Kuwaelimisha Wapumbavu wengi kama huyo hapa Jamvini. Mimi nilishamdharau Kitambo sana ila hapa namsanifu tu bila lenyewe kujua.

Cc: YEHODAYA
 
Back
Top Bottom