23 February 2024
SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha baba mzazi wa waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, mbunge wz jimbo la Kikwajuni Mh. Hamad Yusuf Masauni kilichotokea leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Rais Dk. Mwinyi amesema atamkumbuka Mzee Masauni Yusuf Masauni kwa mchango wake wa maendeleo ya Zanzibar kwa nyadhifa mbalimbali za utumishi na uongozi serikalini alizotumikia enzi za uhai wake.
Rais Dk. Mwinyi anatoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki na watanzania kwa ujumla.
Source : Mkurugenzi Idara ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu. SMZ tarehe 23 February 2024
Masauni Yusuf Masauni aliwahi kuhudumu kama mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC miaka ya uchaguzi wa mwaka 2005 na pia mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Uhamiaji Zanzibar
Picha maktaba : Mzee Masauni Yusuf Masauni
SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha baba mzazi wa waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, mbunge wz jimbo la Kikwajuni Mh. Hamad Yusuf Masauni kilichotokea leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Rais Dk. Mwinyi amesema atamkumbuka Mzee Masauni Yusuf Masauni kwa mchango wake wa maendeleo ya Zanzibar kwa nyadhifa mbalimbali za utumishi na uongozi serikalini alizotumikia enzi za uhai wake.
Rais Dk. Mwinyi anatoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki na watanzania kwa ujumla.
Source : Mkurugenzi Idara ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu. SMZ tarehe 23 February 2024
Masauni Yusuf Masauni aliwahi kuhudumu kama mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC miaka ya uchaguzi wa mwaka 2005 na pia mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Uhamiaji Zanzibar
Picha maktaba : Mzee Masauni Yusuf Masauni