Waziri Ummy: Nakataza Michango Mashuleni, asiyekuwa na Sare za Shule acha asome

Lengo la uniform ni mwanafunzi anapotoroka au akipata matatizo mtaani watu wanajua waanzie wapi; ni utambulisho wa mwanafunzi.

Ndio maana kwa wale waliosoma boarding ilikuwa tukitoroka shule kitu cha kwanza ni kuvua mashati yatakayo tutambulisha tumetoka shule gani au kutovaa uniform kabisa.

Huyu mama mweupe sijapata kuona halafu sijui kwanini wanapenda kumpa wizara kubwa na ngumu; it’s beyond me.
Unadhani leo kwenye hizi shule hiyo maana ya uniform bado ni ile ile ya miaka hiyo?

Leo lengo kubwa ni pesa tu, mfano mzazi unaweza kupata uniform kwa gharama kidogo huku mtaani, lakini shule inataka ikuuzie yenyewe tena bei kubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unadhani leo kwenye hizi shule hiyo maana ya uniform bado ni ile ile ya miaka hiyo?

Leo lengo kubwa ni pesa tu, mfano mzazi unaweza kupata uniform kwa gharama kidogo huku mtaani, lakini shule inataka ikuuzie yenyewe tena bei kubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Logic nadhani ipo kwenye nembo ndio utapata shule.

Afadhali ya huko waulize diaspora wanaoishi UK wakwambie kwao huko nembo ya shule inawekwa kwenye masweta, halafu unakuta ni duka moja au mawili tu kwenye jimbo ndio yenye kibali cha kuuza.

Shule zikifunguliwa wanafunzi wapya wanaojiunga na hizo taasisi unakuta wazazi wamepanga mstari mrefu huo mbele ya duka karibu week nzima na bei yake ni masweta 3/4 hayo hayo dukani bila ya nembo.

Swala la uniform especially kwa Africa sio la mzaha, watoto wakifanya vurugu huko mtaani watu wanajua waende wapi.

Zama zetu kwenye adhabu ilikuwa bora utoroke ukamatwe ulivaa uniform. Lakini ukamatwe ujavaa uniform utajuta adhabu yake.

Uniform ni muhimu sana hasa kwa boarding schools.
 
Ni kwa form One tu mkuu
Ikiwa wewe una uwezo kumbuka wapo wasio na uwezo.Ikifika mwisho wa mwaka,kuna kulipia kodi ya pango la nyumba,watoto wakuwanunulia uniform sio mmoja,wapo wa ndugu na jamaa waliofiwa na wazazi wao.Sikukuu za mwisho wa mwaka.Wapo wenye wagonjwa,nk,wengine wanamsubiria michango ya ndugu na jamaa.
Tuna lea ujinga kesho watasema hawana madaftari, haya mambo ndiyo yanayo shusha hadhi ya elimu haya .
 
Uwelewa mbaya,ukiangalia shule za private mwanafunzi anafika shuleni Hana uniform anaenda darasani mpaka itakapokuwa tayari Sasa ubaya upo wapi wa wazazi kupewa muda huku mtoto akiendelea na masomo?
Tuache kufikiria negative kila kijacho
Kifupi tuna lea ujinga sare za shule zinasababu waache kingiza siasa kesho watasema hawana viatu na madaftari wazazi wanafunzwa uzembe
 
"Kama Katiba ingeruhusu Mhe Samia Suluhu Hassan hakupashwa kuwa Rais wa mihula miwuli pekee,

Huyu Mama walau kwa Uchache angestahili miaka walau 15 "
 
===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
Kaziiendelee dada Ummy,
 
===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
Kaziiendelee
 
Sare ni nyenzo muhimu katika kutawala nidhamu ya watoto.

Pia kuhakikisha wanapata upendeleo unaostahili na kuepusha unyanyasaji dhidi yao.

Sare sio suala la kukurupuka. Ni nyenzo ya kisaikolojia inayotumika kwenye taasisi zote zenye kushughulika na idadi kubwa au hata ndogo ya watu ambapo nidhamu ya hali juu sana ni takwa muhimu.

Lakini pia ni utambulisho ambao unaweka wazi kwa jamii yote namna ya kushughulika na mhusika kama akipata tatizo au akiwa na mwenendo tofauti na unaotarajiwa na hali yake inayotambulishwa na sare alizovaa.

Sare kwa wanafunzi haina mbadala na wala haipaswi kuwa na exemption.
 
Kwani waziri wa Elimu anasemaje yeye?


Malimu anafundisha watoto wasio na UNIFORM. Huku anaonyesha, Huku ana Mimba. .HATAREE.
 
Back
Top Bottom