Waziri Ummy: Nakataza Michango Mashuleni, asiyekuwa na Sare za Shule acha asome

===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
Huyu Mama afikiriwe nafasi za Juu hapo baadae,
 
Tujitafakari haya mambo eti tupo uchumi wa kati. Ukweli usemwe uzazi wa mpango kuwapotosha watu elimu bure, huduma afya zimeboreshwa mfyatuane!!!
 
Watoto wa ummy wanasoma international wenzao wanaambiwa msivae sare vaeni yeboyebo nchi hii bado tupo Karne 15
 
===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
Ahsante,Waziri wetu,Ahsante Rais wetu kwa kuteletea Waziri,anayejuwa matatizo ya wananchi.
 
Mambo ya ajabu sana kwa kuharibu utaratibu uliowekwa. Mwanafunzi lazima aende akiwa ndani ya uniform.

Kuwaruhusu kwenda bila uniform ni presence mbaya sana, siku tutawaruhusu waingie darasani hata kama hawana daftari.
Ikiwa wewe una uwezo kumbuka wapo wasio na uwezo.Ikifika mwisho wa mwaka,kuna kulipia kodi ya pango la nyumba,watoto wakuwanunulia uniform sio mmoja,wapo wa ndugu na jamaa waliofiwa na wazazi wao.Sikukuu za mwisho wa mwaka.Wapo wenye wagonjwa,nk,wengine wanamsubiria michango ya ndugu na jamaa.
 
Mojawapo ya jambo linaloleta nidhamu mashuleni ya hali ya juu ni wanafunzi kulazimika kuvaa sale za shule zilizo nadhifu. Hili ni jambo ambalo linakubalika kwa wazazi/walezi na hata kwa uongozi wa shule husika.

Sasa kama mzazi amepewa unafuu wa kutokulipa ada, sasa huruma nyingine ya kijinga inaingia hata katika masuala muhimu ya kinidhamu. Hivi serikali inafikiria kuwa ili kumkomboa mtu maskini ni kwa kumsaidia kuishi kwake katika fikra za kifukara!?
Wamepewa mda wajipange.
 
===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
Hela za tozo zingenunua uniform,
Kwan madarasa yanajegwa kwa hela ya corona.
 
Binadamu Kila kitu kwake shida! Wangezuiliwa mngelaumu! Wameruhusiwa kwenda kwa muda bila uniform pia mnalaumu! Hakika duniani sio sehemu salama kwa watendao mema!!!
Umesema kweli tupu,watoto wengi wanashindwa kusoma kutokana na mahitaji ya shule,miongoni mwa hayo mahitaji ni sare za shule.Inasikitisha nilihudhuria kikao cha shule fulani,mtoto anavyaa sueta juu ya shati la shule siku zote,kumbe shati mgongoni ,mgongo wote uko wazi, limepasuka,walimu walipomuuliza,ndio akajieleza.
 
Ahsante Waziri,unajuwa matatizo ya unaowaongoza,Mungu akubariki sana.Rais wetu aliyekuteua wewe,alijuwa wazi uko vizuri.
 
Huo uhuru wakianza kuutumia vizuri ndipo itafahamika kama wamesaidia au wameharibu.
Walau uniform zinasaidia hususan upande wa nidham wanapokuwa nje ya viunga vya shule.
 
Sare ya shule huondoa matabaka shuleni, hapo moja kwa moja itaonekana asiye na sare ni maskini wa kutupwa.

Uniform si jambo la kupuuza.

Tunarudi enzi za mwalimu Nyerere.
 
Mambo ya ajabu sana kwa kuharibu utaratibu uliowekwa. Mwanafunzi lazima aende akiwa ndani ya uniform.

Kuwaruhusu kwenda bila uniform ni presence mbaya sana, siku tutawaruhusu waingie darasani hata kama hawana daftari.
Uwelewa mbaya,ukiangalia shule za private mwanafunzi anafika shuleni Hana uniform anaenda darasani mpaka itakapokuwa tayari Sasa ubaya upo wapi wa wazazi kupewa muda huku mtoto akiendelea na masomo?
Tuache kufikiria negative kila kijacho
 
Lengo la uniform ni mwanafunzi anapotoroka au akipata matatizo mtaani watu wanajua waanzie wapi; ni utambulisho wa mwanafunzi.

Ndio maana kwa wale waliosoma boarding ilikuwa tukitoroka shule kitu cha kwanza ni kuvua mashati yatakayo tutambulisha tumetoka shule gani au kutovaa uniform kabisa.

Huyu mama mweupe sijapata kuona halafu sijui kwanini wanapenda kumpa wizara kubwa na ngumu; it’s beyond me.
 
Lengo la uniform ni mwanafunzi anapotoroka au akipata matatizo mtaani watu wanajua waanzie wapi; ni utambulisho wa mwanafunzi.

Ndio maana kwa wale waliosoma boarding tukitoroka shule kitu cha kwanza ni kuvua mashati yatakayo tutambulisha tumetoka shule gani au kutovaa uniform kabisa.

Huyu mama mweupe sijapata kuona halafu sijui kwanini wanapenda kumpa wizara kubwa na ngumu; it’s beyond me.
Kwahiyo watoto we unafikiria Kuna mtoto akidondoka kipindi hiki Cha likizo hawatasaidiwa kisa Hana uniform?
 
Nakumbuka form one headmaster alisema hatambui uniform nje ya shule lazima tutoe hela tupimishwe shuleni,tulitoa hela baadaye wanaume tumeletewa suruali nyeusi za mtumba
 
Back
Top Bottom