Waziri Ummy: Nakataza Michango Mashuleni, asiyekuwa na Sare za Shule acha asome

Hizi kauli mbona si mpya, tatizo liko wapi?.

Miezi kadhaa nyuma mapema asubuhi nilikutana na Kijana mdogo akiwa amevaa sare za shule ambazo zilikuwa zinasadifu tosha hali ya kiuchumi ya familia anayotokea.

Mtoto yule alikuwa anakwenda kama hataki huku usoni akionekana analia hivyo nikavutika kumuhoji kujua kulikoni...akasema Mama yake amempiga kwa sababu alikuwa anakataa kuondoka nyumbani bila kupewa mia tano ya mchango shuleni ambako nako akifika bila ya hiyo hela Mwalimu husika anamchapa.

Nilimpa mia tano na kumwambia akimbie awahi shuleni, walau akabadilika na kuonesha matumaini.

Hapa unaweza kuona Mtihani anaoupata Mtoto kama huyu wa darasa la kwanza tu ambaye hata kwa kumuangalia inaonesha kabisa kama hata amepata kifungua kinywa ni bahati....hivi kwa nini huyo Mwalimu asivae viatu vya huyu Mtoto?. Mwalimu anapata wapi msukumo wa kumshinikiza Mtoto alete hiyo mia tano kwa kumpiga yeye Mtoto anayepaswa kusubiri apewe pesa na Mzazi?.

Hapo huwa najiuliza Mwalimu anapoamua kumuadhibu Mtoto hivi ni kwamba hatumii akili kumbebesha Mtoto matatizo yasiyomuhusu? tena bila hata kujali hali ya huyo Mtoto mwenyewe.

Je kwa kauli hii ya Waziri itabadilisha nini ambacho hakijawahi kutamkwa kabla?.
 
Hivi hii ni awamu ya sita au ni awamu ya tano lakini rais wa sita ?.Awamu ya tano ilianza mwaka 2020 na itaishia mwezi October mwaka 2025.
 
Da Ummy bana...yaani unakataza michongo shuleni ila chama chenu kinaruhusu michongo mahakamani...kweli jamani ??

Sorry nilijua michongo kumbe michango.
 
===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
Samia Jembe sana
 
Hata hivyo kuna baadhi ya shule kila wiki wanawatoza wazazi 1500 kama ada ya mtihani wa majaribio mtoto asiyetoa hafanyi na hata huu mtihani wa muhula wapili wazazi wametoa pesa kwaajili ya mtihani.
===
Waziri wa TAMISEMI, Mhe Ummy Mwalimu amekemea utozaji wa michango mbalimbali kwa Wanafunzi Shuleni sanjari na vitendo vya baadhi ya Walimu kuwazuia Wanafunzi kuingia Shuleni kwa kukosa sare na mahitaji mengine yanayohitajika Shuleni hapo.

Amesema vitendo hivyo havikubaliki na kwamba Walimu hao wanapaswa kuwa na huruma kwa Wazazi na Walezi wa Watoto hao na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaepuka kuwakwamisha Watoto hao kusoma.

"Walimu wasiweke vikwazo kwa Watoto wanaoanza darasa la kwanza, Katibu Mkuu hakikisha unaandika waraka wa utaratibu, tunataka Shulr zinapofunguliwa January Watoto 90007 wa kidato cha kwanza waanze Shule"

Katika kulisisitiza hilo Waziri Ummy amesema anatafuta Shule mbili au tatu za kutolea mfano endapo zitabainika kutenda kosa hilo na kusisitiza kuwa Wazazi hawapaswi kubebeshwa mzigo kwa kuwa Serikali ilishaweka utaratibu wa elimu bila ada.

"Sitaki kuona Mwanafunzi amerudishwa kwasababu ya michango na kwa hawa wanaonza kidato cha kwanza hata kama hawana sare ya Shule aliyochaguliwa asirudishwe bali apewe muda”Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na Binafsi leo Dar es salaam


View attachment 2045856
 
Hizi kauli mbona si mpya, tatizo liko wapi?.

Miezi kadhaa nyuma mapema asubuhi nilikutana na Kijana mdogo akiwa amevaa sare za shule ambazo zilikuwa zinasadifu tosha hali ya kiuchumi ya familia anayotokea.

Mtoto yule alikuwa anakwenda kama hataki huku usoni akionekana analia hivyo nikavutika kumuhoji kujua kulikoni...akasema Mama yake amempiga kwa sababu alikuwa anakataa kuondoka nyumbani bila kupewa mia tano ya mchango shuleni ambako nako akifika bila ya hiyo hela Mwalimu husika anamchapa.

Nilimpa mia tano na kumwambia akimbie awahi shuleni, walau akabadilika na kuonesha matumaini.

Hapa unaweza kuona Mtihani anaoupata Mtoto kama huyu wa darasa la kwanza tu ambaye hata kwa kumuangalia inaonesha kabisa kama hata amepata kifungua kinywa ni bahati....hivi kwa nini huyo Mwalimu asivae viatu vya huyu Mtoto?. Mwalimu anapata wapi msukumo wa kumshinikiza Mtoto alete hiyo mia tano kwa kumpiga yeye Mtoto anayepaswa kusubiri apewe pesa na Mzazi?.

Hapo huwa najiuliza Mwalimu anapoamua kumuadhibu Mtoto hivi ni kwamba hatumii akili kumbebesha Mtoto matatizo yasiyomuhusu? tena bila hata kujali hali ya huyo Mtoto mwenyewe.

Je kwa kauli hii ya Waziri itabadilisha nini ambacho hakijawahi kutamkwa kabla?.
Umechambua vizuri Sana mkuu
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom