Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,568
Waziri Ummy Mwalimu amezitaka Hospitali za Rufaa kuboresha huduma ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa Muhimbili, Amesema hospitali za kanda, rufani, mikoa na wilaya huwa wanawahamisha wagonjwa wenye matatizo wanayoweza kuyatibu kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Agizo hilo alilitoa baada ya kutembelea MNH jana na kubaini kuwapo kwa mrundikano wa wagonjwa wanaotoka hospitali hizo kwa matatizo ya kawaida.
Akiwa katika kitengo cha dharura, alipokea malalamiko kutoka kwa watoa huduma ya kuwapo kwa mrundikano wa wagonjwa ambao miongoni mwao matatizo yanaweza kutibiwa walipotoka.
“Jambo ambalo limemleta ni la kuelemewa na idadi kubwa ya wagonjwa hapa MNH. Hospitali za wilaya, mkoa, rufani na kanda, nyingi hazitimizi wajibu wake ni lazima zitoe huduma bora ili kuipunguza mzigo Muhimbili, inashangaza kuona hata mgonjwa ambaye hana damu anahamishiwa hapa huu ni uzembe,” alisisitiza Ummy.
Alisema katika kukabiliana na mrundikano wa wagonjwa MNH hasa kitengo cha dharura, wanaandaa mpango mkakati wa kuboresha hospitali hiyo, iliyojengwa zaidi ya miaka 60 iliyopita ili iweze kudumu kwa miaka 50 ijayo.
“Tutaiboresha ili sasa iendane na wakati ulioko, haipendezi kuona wagonjwa wanalala kwenye kona na majengo yamechakaa,” alisema Ummy.
Kadhalika alisema ipo haja ya kuwapo kwa Hospitali ya Kanda ya Dar es Salaam na Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupunguza mzigo wa wagonjwa kwa hospitali hiyo ya taifa.
Ummy pia alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa MHN, Prof. Lowrance Museru, kushughulikia changamoto alizopokea kutoka kwa wagonjwa kama kukaa wodini zaidi ya mwezi kusubiri matibabu.
Alitaja changamoto nyingine ni daktari kupita kwa awamu moja badala ya mbili, lugha mbaya kwa wagonjwa na kukosa huduma stahiki ilhali serikali imewekeza fedha za kutosha kuboresha mazingira na kuweka vifaa tiba vya kisasa.
Akijibu hoja za Ummy, Prof. Museru alisema katika kushughulikia lugha chafu kutoka kwa watumishi, tayari wametoa semina ya huduma kwa wateja kwa watoa huduma wa MNH na Mwananyama na wanaendelea kufanya hivyo.
Prof. Museru alisema wagonjwa wanaokaa muda mrefu bila matibabu, wanakuwa wanaandaliwa kusubiri kufanyiwa upasuaji, na kuahidi kama kuna changamoto nyingine asizozifahamu atazifanyia kazi.
Kuhusu madaktari kupita mara moja, alisema daktari bingwa mmoja anapita mmoja ili kutoa maelekezo ya aina ya matibabu ya kupatiwa na awamu nyingine wanapita madaktari wa kawaida wakiwamo wanafunzi.
Alisema wanakabiliwa na changamoto ya wananchi kukimbilia kueleza kero zao kwenye mitandao ya kijamii, badala ya kutumia njia za kuwaona wahusika.
“Hili ni tatizo waziri, tuna hii shida mgonjwa hawezi kuja kulalamika anaenda kwenye mitandao kuandika na hata tunapotatua changamoto hawezi kurudi kusema alikosea anabaki kimya,” alisema Prof. Museru.
Agizo hilo alilitoa baada ya kutembelea MNH jana na kubaini kuwapo kwa mrundikano wa wagonjwa wanaotoka hospitali hizo kwa matatizo ya kawaida.
Akiwa katika kitengo cha dharura, alipokea malalamiko kutoka kwa watoa huduma ya kuwapo kwa mrundikano wa wagonjwa ambao miongoni mwao matatizo yanaweza kutibiwa walipotoka.
“Jambo ambalo limemleta ni la kuelemewa na idadi kubwa ya wagonjwa hapa MNH. Hospitali za wilaya, mkoa, rufani na kanda, nyingi hazitimizi wajibu wake ni lazima zitoe huduma bora ili kuipunguza mzigo Muhimbili, inashangaza kuona hata mgonjwa ambaye hana damu anahamishiwa hapa huu ni uzembe,” alisisitiza Ummy.
Alisema katika kukabiliana na mrundikano wa wagonjwa MNH hasa kitengo cha dharura, wanaandaa mpango mkakati wa kuboresha hospitali hiyo, iliyojengwa zaidi ya miaka 60 iliyopita ili iweze kudumu kwa miaka 50 ijayo.
“Tutaiboresha ili sasa iendane na wakati ulioko, haipendezi kuona wagonjwa wanalala kwenye kona na majengo yamechakaa,” alisema Ummy.
Kadhalika alisema ipo haja ya kuwapo kwa Hospitali ya Kanda ya Dar es Salaam na Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupunguza mzigo wa wagonjwa kwa hospitali hiyo ya taifa.
Ummy pia alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa MHN, Prof. Lowrance Museru, kushughulikia changamoto alizopokea kutoka kwa wagonjwa kama kukaa wodini zaidi ya mwezi kusubiri matibabu.
Alitaja changamoto nyingine ni daktari kupita kwa awamu moja badala ya mbili, lugha mbaya kwa wagonjwa na kukosa huduma stahiki ilhali serikali imewekeza fedha za kutosha kuboresha mazingira na kuweka vifaa tiba vya kisasa.
Akijibu hoja za Ummy, Prof. Museru alisema katika kushughulikia lugha chafu kutoka kwa watumishi, tayari wametoa semina ya huduma kwa wateja kwa watoa huduma wa MNH na Mwananyama na wanaendelea kufanya hivyo.
Prof. Museru alisema wagonjwa wanaokaa muda mrefu bila matibabu, wanakuwa wanaandaliwa kusubiri kufanyiwa upasuaji, na kuahidi kama kuna changamoto nyingine asizozifahamu atazifanyia kazi.
Kuhusu madaktari kupita mara moja, alisema daktari bingwa mmoja anapita mmoja ili kutoa maelekezo ya aina ya matibabu ya kupatiwa na awamu nyingine wanapita madaktari wa kawaida wakiwamo wanafunzi.
Alisema wanakabiliwa na changamoto ya wananchi kukimbilia kueleza kero zao kwenye mitandao ya kijamii, badala ya kutumia njia za kuwaona wahusika.
“Hili ni tatizo waziri, tuna hii shida mgonjwa hawezi kuja kulalamika anaenda kwenye mitandao kuandika na hata tunapotatua changamoto hawezi kurudi kusema alikosea anabaki kimya,” alisema Prof. Museru.