Waziri Selina Kombani (Katiba na Sheria) na Hatima ya Katiba Mpya

Kwa Tanzania cheo anaweza kupewa mtu yeyote. Sishangai Celina kuwa waziri wa Sheria. Zile enzi za kumweka waziri kwa kufuata taaluma yake ziliondoka na Nyerere. This is Animal Farm my friends. we are the Benjamins and they are Pigs." Ignorance is Strength" - Robert Owen, the Author of Nineteen Eighty Four:

Animal Farm(George Orwell-1884) kabisaa...Kuna mtanzania akiitwa Kawegere Fortunatus aliitafsiri hii kitu kwa kiswahili
 
Sheria nyingi zilizopitishwa na Bunge mwaka huu ni zile ambazo wafadhili walishazidai. Zile ambazo wananchi wanadai serikali haitaki kuzitunga. Siku wafadhili wakisema katiba irekebishwe utaona itatokea mara moja. Jiulize sheria ya NGOs na ile ya Terrorism.

Pengine kuna sababu. Wafadhili wakisema sheria itungwe au iliyopo irekebishwe, wanatoa pesa kufanya hivyo. Kwanza wanachukuliwa maafisa wa serikali, ikiwa ni pamoja na waziri, kutembelea nchi fulani eti kujifunza namna sheria yao ilivyotungwa na inavyofanya kazi. Pili wanatoa pesa za kuendesha seminar mbali mbali hivyo wahusika wanapata ulaji. Tatu wanaleta consultants ambao huja na copy paste ya sheria husika hivyo watendaji wetu wanakuwa hawahitaji kuumiza vichwa vyao. Nne kama sheria hiyo ikishapita, kunakuwepo na msururu wa semina nyingi za kuisambaza.

Katika hali kama hii, ngekuwa wewe ni serikali, ungetekeleza ya wananchi au ya mfadhili?

mkuu, umemaliza kila kitu cha nji hii. na hao watu wanaogaagaa na upwa wa wafadhili wana fedha si mchezo. pekechua vizuri akili kichwani mwako!
 
Celina Kombani deserve to be the first minister to be sacked kwa serikali ya awamu hii

she is totally not fit for that ministry
 
Huyu Celina Kombani, ana CV gani na background yake ni ipi ukiacha mambo ya siasa? maana kimtokacho mtu ndio kilichojaza moyo wake.

Huyu Kombani hana nia ya kuwatumikia watanzania!!
 
Km Raisi ni Kikwete hana uwezo wa kufikiri unafikiri atakua na waziri mwenye positive / constructive thinking and arguments? Never on earth. Fellas, birds of same feathers flock together. She's just one ticking bomb as Kikwete is............ Twalaaaaaaaaaa, twaliwaaaaaaaaaaa....
 
Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani ana maana gani anapowaambia wapiga kura wake (wananchi) kwamba nilikuwa natikisa kibiriti kuhusu Katiba?
 
Alikuwa anatania TUU...

AG: Yalikuwa maoni yangu binafsi.

siMWEMA, kwa nini na yeye tumuamini kuhusu kukataza maandamano labda (i) Alikuwa anatania (ii) Alikuwa anatikisa kiberiti au (iii) Yalikuwa maoni yake binafsi.


Ukiona nchi inakuwa na viongozi waandamizi aina hii basi ujue kuna kasoro kubwa katika mfumo mzima wa utendaji wa serikali.

Yana MWISHO!!
 
Inawezekana na Waziri Ngeleja anatikisa kibiriti kuhusu deni la DOWANS! They are not at all serious.
 
Tatizo letu Watanganyika tunaongozwa na Vilaza na huu mfumo wetu wa Elimu wa Kukalili ndio matokeo yake hayo,Mashuleni,vyuoni kukalili, Ndio Matokeo ya akina Kombani,Werema,Mwama,Jk na mfumo wote wa Ccm kwa Ujumla, Hivi Kiongozi wa Nchi anaongoza kwa kutujaribu? kwa akili zao za kukalili wanaongea kwa umma Upuuzi mtupu, Tunawadharau na Wawajibike.
 
Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani ana maana gani anapowaambia wapiga kura wake (wananchi) kwamba nilikuwa natikisa kibiriti kuhusu Katiba?

Chanzo cha habari ni kipi?

Ila kama ni kweli kasema hivyo basi hawa jamaa wanahitaji 'a crash course in the art of spinning'
 
Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani ana maana gani anapowaambia wapiga kura wake (wananchi) kwamba nilikuwa natikisa kibiriti kuhusu Katiba?

This is ubelievable... sasa hawa watu ni wapi tutajua kwamba wapo serious na wapi wanafanya utani..... You Bring Jokes in Serious Issues.... Hii Nchi Usanii From Top to Bottom.
 
Hawa ndio viongozi tulionao. Vichwani hawana hata chembe ya ubongo ila wamejaza uji............ningetoa neno baya hapa ngoja nimsamehe nisipewe ban JF.
 
Back
Top Bottom