Waziri Mulugo aumbuliwa na Sugu

Waziri Mulugo aumbuliwa na Sugu

MBUNGE wa Mbeya Mjini,
Joseph Mbilinyi (CHADEMA),
amemuumbua Naibu
Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi, Philip
Mulugo, akidai hatishwi na
kauli zake kwani ana
elimu ya kuungaunga
akiwa ametumia jina la
mtu mwingine.
Kauli ya Mbilinyi maarufu
kama Sugu, inakuja siku
chache tangu Mulugo
atangaze kuwa Chama Cha
Mapinduzi (CCM),
kitayarejesha majimbo
yaliyoko mikononi mwa
CHADEMA mkoani Mbeya,
likiwemo la Mbeya Mjini.
Akizungumza jana kwa
simu na Tanzania Daima,
Mbilinyi alisema
anamshangaa Mulugo kwa
kauli hiyo wakati akiwa na
hali mbaya kisiasa jimboni
kwake Songwe, kiasi cha
walimu kulalamika kukosa
hata chaki shuleni.
“Mimi Mulugo hanitishi
hata kidogo maana
mambo yake yote ni ya
kuungaunga, kuanzia
elimu yake hadi siasa
jimboni. Huyu nimesoma
naye Sekondari ya Mbeya
Day nikiwa namtangulia,
na jina lake alikuwa
akiitwa Amim si hili la
Philip Mulugo,” alisema.
Mbilinyi aliongeza kuwa
amefanya ziara jimboni
kwa Mulugo na kuelezwa
matatizo mengi
yanayowakabili wapiga
kura wake, na kwamba
alishangazwa na hatua ya
kuona walimu
wakilalamika kukosa chaki
wakati mbunge wao ni
naibu waziri wa elimu.
“Haya mambo hatuyasemi
kwa sababu ya
kuwachukia CCM, bali
wanatuletea wenyewe
malalamiko wakitaka
tuwasaidie kusema. Sasa
Mulugo kashindwa kwake
anakuja Mbeya Mjini
kujitapa kuwa
wataning’oa,” alisema.
Aliongeza kuwa, kutokana
na ubabaishaji wa Mulugo,
kuanzia sasa ataanza
kumuita jina lake halali la
Amim ili watu wafahamu
kuwa hata kweli elimu
aliunga licha ya kuteuliwa
kuwa naibu waziri.
“Kila mtu anakuwa na
ndoto, haikataliwi, hata
yeye alipotoka hadi kuwa
Naibu Waziri wa Elimu ni
ndoto pia, hakutegemea
kutokana na kusoma kwa
kuungaunga kwa kutumia
jina na cheti cha mtu,
hakuwa na uwezo,”
alisema.
Mbilinyi alifafanua kuwa
Mulugo amemchokoza
mwenyewe na kumtaka
atambue kuwa yeye si wa
kuchezea wala chama
chake cha CHADEMA, na
kwamba chama hicho
chini yake au mtu
mwingine kuliacha Jimbo
la Mbeya Mjini ni baada ya
miaka 25 ijayo.
Alisema kutokana na
kupendwa na watu na
kuwapa changamoto
katika halmashauri licha
ya kwamba CCM wana
madiwani 22 na CHADEMA
14, anaamini kabisa kwa
sasa atajipanga kugombea
umeya badala ya ubunge.
“Yaani Mulugo
amechemsha, hakuna
namna ya kumtoa Sugu
wala chama chake, na sasa
itafika wakati nitakuwa
meya, tena pale ndio
wamechemsha kabisa
kumweka mwenyekiti
asiyekubalika, na sasa
wakifanya mikutano yao
hawapati watu.
“Mulugo ndiyo maana
hata historia ya nchi haijui
kwa kuwa elimu yake
yenyewe ina utata, aanze
kuchunguzwa,
mtaniambia kafanya
jambo la ajabu sana,
mwenzake alifaulu, lakini
kutokana na kutokuwa na
uwezo wa kuendelea na
shule yeye akanunua jina
lake,” alisema.
Mbilinyi alisema kama
Mulugo anahitaji
kuendelea na siasa, basi
aende Mbeya Mjini ili
wamfundishe jinsi ya
kuishi na watu jimboni
kwake na kujua kero zao.
Hata hivyo, Mulugo
alipotafutwa kufafanua
madai hayo, alikwepa
kulisemea sakata la
kutumia jina lingine
wakati akisoma sekondari,
akisema kuna vitu ni stori,
lakini fitina hizo za kisiasa
ni majungu ya mtu na
mtu.
Aliongeza kuwa, Mbilinyi
aliwahi kwenda jimboni
kwake Songwe na kusema
madai hayo pamoja na
kumtukana, lakini
wananchi walimzomea
wakisema wao ndio
wanamfahamu mbunge
wao kuanzia elimu ya
msingi mpaka shahada.
“Matusi yale yalisababisha
vurugu mpaka CHADEMA
wakapata kura 19 dhidi ya
kura 365 za CCM.
Nilichokisema kwenye
mkutano wa Mbeya ni
jambo la kawaida kwa
mwanasiasa yeyote aliye
makini, tena mjumbe wa
NEC.
“Nilisema majimbo yote
ya CHADEMA Mkoa wa
Mbeya tutayarudisha. Sasa
kwani mbona wao kila
siku wanasema
watachukua majimbo yote
ya Mkoa wa Mbeya?”
alisema Mulugo kupitia
ujumbe mfupi wa sms.

mh mulugo elezea kuhusu Jina na cheti chako basi??
 
Mulugo hajawahi kuw aheadmaster. Alikuwa school manager wa Southern Highlands Secondary shule iliyokuwa inaongozwa na wahindi. Hata mkuu wa shule alikuwa mhindi. Mulugo alikuwa akisimamia ukusanyaji wa ada za watoto.

Haiko wazi kwangu n ini kilitokea baadaye akaanza kujiita mmiliki wa shule wakati taarifa zisizorasmi zinasema aliwafanyia mbaya sana wale wenye shule.

Nadhani katika kuboresha cv sasa kaeajibandika Headmaster ili angalau asomeke kitaaluma zaidi!

Mulugo ana udanganyifu mwingi lakini hata uwezo hana. Hata anaposema jambo la kawaida utaona kabisa kwamba sasa ngumbaru inanena.i

Huwezi kukosa reference ya class-mates ama walokusomesha ukategemea wapiga kura ambao wala hukusoma nao wala hawakukufundisha kwamba watetee elimu yako hadi chuo! Kwani alikuwa anapeleka matokeo yake na taarifa zake za maendeleo kwenye serikali za vijiji? MIaka minane ya degree hawakuchoka? Kwanza wangefahamu wasingmchagua.

JK ni Janga la Tanzania. Nahisi jk anatoa vyeo kwa watu kama Mlugo Amini kwa ajili ya kutimiza mashart ya waganga wa kienyeji. La sivyo kama binadamu, angekuwa anapata japo chembe ya huruma kwa walipa kodi na wananchi wa TZ kwa ujumla.
 
Elimu ya Tanzania magumashi, Matokeo ya wanafunzi magumashi, waziri wa elimu nae elimu yake magumashi, kila kitu kwenye elimu ni magumashi! Tunaelekea wapi watanzania! Kila kitu kwenye elimu ni feki kama bidhaa za kichina! Ushauri wangu turudi enzi za papa Ben Mkapa! Tubinafisishe hii Wizara ya Elimu au mnasemaje?
 
MEMBER OF PARLIAMENT CV

[TABLE="class: cms_table"]
[TR]
[TH="colspan: 3, align: left"]GENERAL[/TH]
[/TR]
[TR]
[TD]Salutation[/TD]
[TD]Honourable[/TD]
[TD="width: 42%"]Member picture
1645.jpg
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]First Name:[/TD]
[TD]Philipo[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Middle Name:[/TD]
[TD]Augustino[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Last Name:[/TD]
[TD]Mulugo[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 20%"]Member Type:[/TD]
[TD="width: 38%"]Constituency Member[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Constituent:[/TD]
[TD]Songwe[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Political Party:[/TD]
[TD]CCM[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Office Location:[/TD]
[TD]P.O. Box 9121, Dar Es Salaam[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Office Phone:[/TD]
[TD]+255 754 315 922/+255 784 315 922[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Ext.:[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Office Fax:[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Office E-mail:[/TD]
[TD]pmulugo@parliament.go.tz[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Member Status:[/TD]
[TD]Current Member[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Date of Birth[/TD]
[TD]27 January 1972[/TD]
[/TR]
[/TABLE]





[TABLE="class: cms_table"]
[TR]
[TH="width: 35%"]School Name/Location[/TH]
[TH="width: 27%"]Course/Degree/Award[/TH]
[TH="width: 15%"]Start Date[/TH]
[TH="width: 13%"]End Date[/TH]
[TH="width: 10%"]Level[/TH]
[/TR]
[TR]
[TD]Rukwa Primary School, Chunga[/TD]
[TD]Primary Education[/TD]
[TD]1982[/TD]
[TD]1989[/TD]
[TD]PRIMARY[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Mbeya Secondary School[/TD]
[TD]O-Level Education[/TD]
[TD]1990[/TD]
[TD]1993[/TD]
[TD]SECONDARY[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Songea Boys' High School[/TD]
[TD]A-Level Education[/TD]
[TD]1994[/TD]
[TD]1996[/TD]
[TD]HIGH SCHOOL[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Open University of Tanzania[/TD]
[TD]BA (Economics Education )[/TD]
[TD]2002[/TD]
[TD]2008[/TD]
[TD]GRADUATE[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


 
MASIKIN ammim kwa nini kuchokoza makamnda wakati unajijua udhaifu.....wakati mwingine jitahidi kuficha adhaifu wako kwa kutoropoka ovyo. uliyataka mwenyewe
 
Nguvu ya Sugu na Mlugo mkoani Mbeya ni sawa na kutumia kijiko kujazia maji kwenye Pipa. Mlugo Songwe anaabudiwa kama Mungu. Hata kabla hajawa Mbunge. Suala hapo ni busara tu. Sugu yeye CV YAKE YA SHULE IKOJE?

Tatizo siyo CV tatizo ni kununua jina!aaaaa Amimuuuuu
 
huyu amini alituletea aibu kubwa sana south africa! Yan kiukweli jamaa ni kilaza yana hata hajui tanzania ni muungano wa nchi gani akakurupuka na zimbabwe halafu bado wajinga wanamtetea huyu kilaza mwenzao
 
Si Amim ni Hamimu Agustino ndiyo jina lake kabla ya kulirejea jina lake la awali la Philipo Mulugo. Nachotaka kusema hapa na ninarudia alichokisema Mh.Sugu kinaweza kuwa sahihi lakini ikumbukwe tu kwa sisi tuliosoma miaka mingi iliyopita watu walikuwa wanakariri shule ili eventually wafaulu na kuchaguliwa katika shule za serikali! Inawezekana Hamimu Agustino akawa mmoja wa hao waliofanya hivyo lakini sitaki kuamini kama alinunua nafasi ya mtu aliyekuwa amefaulu tayari badala yake naamini kwamba alitumia jina la mmoja wa watu walioacha shule kwasababu mbali mbali ikiwemo hata kufa na kulitumia kama lake na hatimaye akafaulu kwenda Mbeya Day.

Jambo moja muhimu ni kwamba Hamimu anapaswa kuwa makini sana katika namna anavyoendesha siasa zake bila hivyo mambo yake mengi yataanikwa na watu wasiomtakia mema na hivyo kumharibia kabisa nafasi yake kisiasa na kijamii.
 
Nimesoma ujumbe wa naibu waziri wa elimu kupitia gazeti la Tanzania Daima. Kuwa atahakikisha anarejesha majimbo yaliyo mikononi mwa CDM kwenda ccm. Swali kwa mulugo Je utafanya nini kuinua kiwango cha alama za ufaulu s/msingi mlizoshusha hadi 70? Yaani wewe la maana na vipaumbele vyako ni majimbo.Pole sana.
Mkuu hawa mawaziri wa Mhe JK wengi ni vihiyo wamechaguliwa kwa vile ni party cadres, sio watendeji bali ni wanasiasa. Ndio maana tunasema katiba mpya ieleze wazi wazi kuwa waziri sio mwanasiasa wala mbunge, uwaziri watu watangaziwe nafasi waombe kazi kulingana na professional yake. Katiba isiruhusu watu wasio wajuzi wapewe kazi zinazohitaji ujuzi, kusudi tupate watendaji bora kwenye nyanja husika!!!!

 
Amin Mulugo kumbe sio Philip Mulugo.

Kazi tunayo.
 
hapa mukulo ajitokeze na kusema aliosoma nao kama kweli toka dalasa la kwanza hadi la saba alitumia jina hili au kweli amebadilisha ukubwani na kweli alisoma mbeya day?
 
Ndio sababu kiwango cha elimu kinazidi kushuka kwa kasi
 
Bangi kweli noma naona kijana inampa misimamo thabiti ya kukielezea kile anachokiona
 
Now are changing our from KIHIYO to MULUGO.Ni kwa wale wote ambao shule au elimu zao zina utata.MAMULUGO au VIMULUGO ni wengi sana ndani ya CCM na serikali yake.

TE TE TE, WE lupasulwisye MBALI YA KUKUPA LIKE YANGU UMELIPASUA JINA LA MULUGO UNATAKA KULITOHOA LIINGIE KTK MSAMIHATI KUWA NI MTUMIA VYETI VYA KUFOJI, I WISH KUUTUMIA UO MSAMIHATI MAPEMA 2013
 
na Asha Bani

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), amemuumbua Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo, akidai hatishwi na kauli zake kwani ana elimu ya kuungaunga akiwa ametumia jina la mtu mwingine. Kauli ya Mbilinyi maarufu kama Sugu, inakuja siku chache tangu Mulugo atangaze kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kitayarejesha majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani Mbeya, likiwemo la Mbeya Mjini.

Akizungumza jana kwa simu na Tanzania Daima, Mbilinyi alisema anamshangaa Mulugo kwa kauli hiyo wakati akiwa na hali mbaya kisiasa jimboni kwake Songwe, kiasi cha walimu kulalamika kukosa hata chaki shuleni. “Mimi Mulugo hanitishi hata kidogo maana mambo yake yote ni ya kuungaunga, kuanzia elimu yake hadi siasa jimboni. Huyu nimesoma naye Sekondari ya Mbeya Day nikiwa namtangulia, na jina lake alikuwa akiitwa Amim si hili la Philip Mulugo,” alisema.

Mbilinyi aliongeza kuwa amefanya ziara jimboni kwa Mulugo na kuelezwa matatizo mengi yanayowakabili wapiga kura wake, na kwamba alishangazwa na hatua ya kuona walimu wakilalamika kukosa chaki wakati mbunge wao ni naibu waziri wa elimu.
“Haya mambo hatuyasemi kwa sababu ya kuwachukia CCM, bali wanatuletea wenyewe malalamiko wakitaka tuwasaidie kusema. Sasa Mulugo kashindwa kwake anakuja Mbeya Mjini kujitapa kuwa wataning’oa,” alisema.

Aliongeza kuwa, kutokana na ubabaishaji wa Mulugo, kuanzia sasa ataanza kumuita jina lake halali la Amim ili watu wafahamu kuwa hata kweli elimu aliunga licha ya kuteuliwa kuwa naibu waziri. “Kila mtu anakuwa na ndoto, haikataliwi, hata yeye alipotoka hadi kuwa Naibu Waziri wa Elimu ni ndoto pia, hakutegemea kutokana na kusoma kwa kuungaunga kwa kutumia jina na cheti cha mtu, hakuwa na uwezo,” alisema.

Mbilinyi alifafanua kuwa Mulugo amemchokoza mwenyewe na kumtaka atambue kuwa yeye si wa kuchezea wala chama chake cha CHADEMA, na kwamba chama hicho chini yake au mtu mwingine kuliacha Jimbo la Mbeya Mjini ni baada ya miaka 25 ijayo. Alisema kutokana na kupendwa na watu na kuwapa changamoto katika halmashauri licha ya kwamba CCM wana madiwani 22 na CHADEMA 14, anaamini kabisa kwa sasa atajipanga kugombea umeya badala ya ubunge.

“Yaani Mulugo amechemsha, hakuna namna ya kumtoa Sugu wala chama chake, na sasa itafika wakati nitakuwa meya, tena pale ndio wamechemsha kabisa kumweka mwenyekiti asiyekubalika, na sasa wakifanya mikutano yao hawapati watu. “Mulugo ndiyo maana hata historia ya nchi haijui kwa kuwa elimu yake yenyewe ina utata, aanze kuchunguzwa, mtaniambia kafanya jambo la ajabu sana, mwenzake alifaulu, lakini kutokana na kutokuwa na uwezo wa kuendelea na shule yeye akanunua jina lake,” alisema.
Mbilinyi alisema kama Mulugo anahitaji kuendelea na siasa, basi aende Mbeya Mjini ili wamfundishe jinsi ya kuishi na watu jimboni kwake na kujua kero zao.

Hata hivyo, Mulugo alipotafutwa kufafanua madai hayo, alikwepa kulisemea sakata la kutumia jina lingine wakati akisoma sekondari, akisema kuna vitu ni stori, lakini fitina hizo za kisiasa ni majungu ya mtu na mtu. Aliongeza kuwa, Mbilinyi aliwahi kwenda jimboni kwake Songwe na kusema madai hayo pamoja na kumtukana, lakini wananchi walimzomea wakisema wao ndio wanamfahamu mbunge wao kuanzia elimu ya msingi mpaka shahada.

“Matusi yale yalisababisha vurugu mpaka CHADEMA wakapata kura 19 dhidi ya kura 365 za CCM. Nilichokisema kwenye mkutano wa Mbeya ni jambo la kawaida kwa mwanasiasa yeyote aliye makini, tena mjumbe wa NEC. “Nilisema majimbo yote ya CHADEMA Mkoa wa Mbeya tutayarudisha. Sasa kwani mbona wao kila siku wanasema watachukua majimbo yote ya Mkoa wa Mbeya?” alisema Mulugo kupitia ujumbe mfupi wa sms.


Kinanda kinapigwa, sauti taaaaaaaaaaamu inaingia na kuburudisha masikio yangu.
 
Ahaaaaa now I can connect the dots.... Tanzania ni muungano wa Zimbabwe na...... Hahahahahaaaa vihiyo wa Kikwete hawa!
 
Nguvu ya Sugu na Mlugo mkoani Mbeya ni sawa na kutumia kijiko kujazia maji kwenye Pipa. Mlugo Songwe anaabudiwa kama Mungu. Hata kabla hajawa Mbunge. Suala hapo ni busara tu. Sugu yeye CV YAKE YA SHULE IKOJE?

KWANZA POKEA DISLIKE ZANGU ZA KUTOSHA, PIA HACHA KUKUFULU WEWE, USILETE NA KULINGANISHA MAMBO YA MUNGU NA HAWA WASHIRIKINA WA CCM, UTAJISABABISHIA DHAMBI ZA BURe
 
Hakika utawala wa kikwete ni wa kihistoria. Unatakiwa uingie maajabu saba ya dunia. Haitakaa itokee kuwe na viongozi wabovu namna hii then jk anachekacheka tu. Kipofu akiongoza kipofu.... Leo mulugo ni naibu waziri wa elimu Jakaya Mrisho Kikwete shame upon you kwa kumteua wizara ya elimu.
 
Back
Top Bottom