Waziri Mulugo aumbuliwa na Sugu

Waziri Mulugo aumbuliwa na Sugu

Aibu kubwa kwa JK na serikali ya CCM kwa kutokuwa makini na teule zake
 
madai ya mh sugu yanahitaji majibu yakinifu kutoka serikali,tukianzia na baraza la elimu, RITA, uhamiaji+wizara ya ambo ya ndani wao ndio watoa passport nk, we need to know his real name.
 
Waziri wa Elimu kuwa alichakacua Elimu yake duuu Mungu aepushie mbali na kuinusuru Elimu za watoto wetu
 
Ila kazi kweli kweli, hata mimi siku nyingi nimekuwa namfahamu kwajina la Mlungu nashangaa mara baada ya unaibu waziri anaitwa Mlugo. Serikali yetu iko makini sana hata tuhuma hizi itajifanya haioni wala haisikiiiiiii.
 
Tanzania RAHA!

Hii siyo raha ni tatizo kubwa. Ni tatizo kubwa la kimaadili na kitaasisi. Mathalan:

1. Msemaji mkuu wa serikali anasema nini juu ya tuhuma ya Mhemishiwa kujinufaisha kwa kutumia cheti cha mtu mwingine ?
2. Chuo Kikuu Huria wanasemaje au jambo hili haliwahusu ! A whole University !!
3. Baraza la Mitihani wanasemaje au nao jambo hili haliwahusu !! Hawana kitengo cha uchunguzi au uhakiki ?
4. Polisi wanasemaje ? Au uchunguzi wa maswala kama haya siyo dili !
5. Ningekuwa mojawapo waliogombea jimbo la Mheshimiwa huyu ninge petition taasisi zote husika kuanzisha uchunguzi kwa lengo la kuhakiki vyeti vya Mheshiwa huyu kwa sababu uadilifu wake kama kiongozi wa serikali na mbunge umetiliwa shaka kutokana na tuhuma ya udanganyifu na kujinufaisha kwa kutumia cheti cha mtu mwingine.

Yote au baadhi ya hayo yasipofanyika tunapaswa kutambua kwamba taasisi zetu, utendaji wake na uadilifu wa viongozi wa taasisi hizo una mashaka makubwa, na kama taifa hili siyo jambo la kufurahia. Kama hao ndiyo viongozi wetu tutarajie nini kutoka kwa wananchi wa kawaida ?
 
Sugu amejaribu kusema machache sana kuhusu huyu Amini,ni kweli hilo ndiyo jina lake kamili,tunamfahamu vizuri sana huyu Amini hasa jinsi alivyopata kumiliki ile shule ya southern highland.alichomfanya yule mmliki halisi wa ile shule nadhani anakumbuka.ili awe salama inabidi akae kimya sana,tuyajua madudu yake mengi mno.tunajua kuwa huo unaibu waziri ni fadhira kupitia kwa Riz 1.kutokana na mlugo alivyomhost alipokwenda mby kufanya kampain ya banayake .mlugo aligharamia kila kitu wakati wa ziara ya Rz1Huyu Mlugo ni,mtupu,jamani .
Teh,teh,teh,teh we nawe umeifanya jioni yangu iwe safiiiiii acha nifuate ka wine kangu dukani hilo nalo neno.
 
Mwehhhh!!!!!Bujibuji umenichekeshajeeeee !!!!!!umenikumbusha mbali kweli NA hivyo VIBAMA!!!!!tulivilajeee wakati tupo Loleza.....hahahahaaaa!!!!!!kweli JF is a stress free zone....LOL!!!

mama takwenya?
 
Vituko vya serikali ya J.K waziri wa elimu hana elimu ya kutosha hiyo kidogo aliyonayo ameungaunga mara AMINI mara PHILIPO kweli hawa watu ndio wa kuongoza nchi?Mungu jalia tufike 2015 tuondoe mizigo na wababaishaji wanaogawa madaraka kama pipi au karanga bila vigezo. Mulugo ovyo
 
Nadhani kwa sasa kama kuna mawaziri vituko hapa TZ ni waziri wa elimu na naibu wake hawa jamaa nina wasiwasi mkubwa sana na uwezo wao
 
Hawezi kubisha huyu kiazi, wote hawa wamesoma chini yangu, na hata mwalimu wao Mpesya (former mbunge wa Mbeya aliyepigwa chini na Sugu) anawajua vizuri wote. Huyu tena alikuwa zuzu kweli, na bingwa wa kuiba mahindi ya kuchoma ya wamama wake wa FFU (shule ipo jirani kabisa na kambi ya FFU)... Sema tu nchi yenyewe inaongozwa na mchovu ...yeye analetewa majina na vishtobe wake na anawapa vyeo bureee (kama yule DC wa Korogwe alivyotoboa siri...)

Madai mazito haya ya Mbilinyi na vyeti bandia vya Mulugo@Amim
 
Sugu ongea kaka,watanzania wengi tunashindwa kujua wasifu wa huyo mshikaji:glasses-nerdy:
 
Hivi nchi hii tunakwenda wapi jamani? Naibu waziri wa elimu ni kihiyo!!! Balaa kubwa. Anyway, napita tu. Nitarudi baadae.
 
Kweli kuunga unga sio vibaya ila inakuwa mbaya zaidi unapounga unga kwa kutumia jina la mtu mwingine halafu bado unateuliwa kuwa waziri tena wa wizara nyeti ya elimu?
Ina maana hakuna vetting kabla mtu hajateuliwa? Huko tunakoelekea tunaweza kuongozwa na jambazi au mtu asiye raia wa tz kwenye wizara ya mambo ya ndani
 
Loleza enzi gani? Za Mama Mosha, Machibya na Msyani? Mlinzi akiwa Kayange na Lori lenu la blue?

Lol!!!!I missed this...!!!Bujibuji lazima ulikuwa Iyunga au MTC.....enzi za hao wote uliowataja hapo juu....tena usinikumbushe Kajange...!!!hahahaa..Yule babu alikuwa hakubali tukatize lile geti....!!but tulikuwa tunakula kona vilevile...usicheze NA adolescence bwana....!!Lol
 
Mwanamuziki V/s Mwalimu wapi na wapi? Mwalimu ataendelea kuwa mwalimu ilihali mwanamuziki akiendelea kutunga nyimbo nyingi kuendeleza muziki.
 
Duu!! hata hapo mbeya mjini walijua kuvitengeneza hata mimi amenikumbusha mbali nilivila sana malawi karonga wakati wa likizo 1981-1984-Tosamaganga.

Hahahaaa!!!walijua kuvitengeneza haswaa...vikiwa Vya motomoto unakula hadi basi...halafu uzuri no artificial additions...just ndizi kisukari na unga wa mahindi baaasi....
 
Back
Top Bottom