Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Mkuu wa India kuanza ziara Tanzania Alhamisi
(FikraPevu) Waziri Mkuu wa India Bw. Manmohan Singh anatarajiwa kuwasili nchini siku ya Alhamisi wiki hii kuanza ziara rasmi ya kiserikali kwa muda wa siku tatu akiwa mgeni wa Rais Jakaya Kikwete. Bw. Singh atakuwa anaingia nchini akitokea Ethiopia ambako atashirikia Mkutano wa pamoja wa Biashara kati ya India na Afrika. Ziara yake ya Ethiopia anaifanya kwa mara ya kwanza tangu ashike madaraka. Ziara yake katika Afrika itachukua siku sita.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Dar-es-Salaam Bw. Singh anakuja nchini kuitikia mwaliko ambao ulitolewa na Rais Kikwete kwa Waziri Mkuu huyo wa taifa ambalo linapiga kasi zaidi ya maendeleo na ambalo lina nguvu ya Nyuklia. Mheshimiwa Singh amekubali mwaliko huo katika barua yake aliyomwandikia Rais Kikwete na iliyokabidhiwa kwake na Balozi wa India katika Tanzania, Mheshimiwa K.V. Bhagirah wakati Balozi huyo alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Kikwete leo, Alhamisi, Mei 19, 2011, Ikulu, Dar es Salaam. imeseta taarifa hiyo iliyosainiwa na Ikulu bila kusainiwa na mtu yeyote.
Akijibu mwaliko huo Bw. Sing amesema kuwa Nakushukuru kwa barua ya kunilialika kuitembelea nchi yako nzuri. Itakuwa ni heshima kwangu kuitembelea Tanzania na naukubali mwaliko huo kwa furaha kubwa na kuwa Nina ari kubwa kukutana nawe na marafiki wengine wa Tanzania wakati wa ziara hiyo na kujadili njia ya kuuinua uhusiano kati ya nchi zetu kwenye ngazi mpya kwa manufaa ya wananchi wa nchi zetu mbili
Ziara ya Bw. Singh nchini imekuja wakati ambapo taifa hilo la India likizidi kututumua nguvu zake za kiuchumi na ushawishi hasa katika eneo la Afrika na kuonekana ikiingia katika ushindani wa ushawishi kati ya na China pamoja na nchi za Magharibi ambazo zimekuwa na nafasi ya pekee katika bara la Afrika kwa muda mrefu.
Kabla hajaanza ziara yake hiyo ndefu leo Jumatatu Bw. Singh alielezea siku ya Jumapili mwelekeo wa ziara yake hiyo kuwa uhusiano kati ya India na Afrika utahusisha zaidi ni kuipa uwezo Afrika na kubadilishana ujuzi, biashara na ujenzi wa miundombinu. Bw. Singh amesema kuwa uwepo wa watu wengi wenye asili ya India katika kila kona ya Afrika ni ushahidi wa wazi wa mahusiano yetu ya kihistoria.
Soma Zaidi tovuti Dada ya JamiiForums -Fikrapevu.com
(FikraPevu) Waziri Mkuu wa India Bw. Manmohan Singh anatarajiwa kuwasili nchini siku ya Alhamisi wiki hii kuanza ziara rasmi ya kiserikali kwa muda wa siku tatu akiwa mgeni wa Rais Jakaya Kikwete. Bw. Singh atakuwa anaingia nchini akitokea Ethiopia ambako atashirikia Mkutano wa pamoja wa Biashara kati ya India na Afrika. Ziara yake ya Ethiopia anaifanya kwa mara ya kwanza tangu ashike madaraka. Ziara yake katika Afrika itachukua siku sita.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Dar-es-Salaam Bw. Singh anakuja nchini kuitikia mwaliko ambao ulitolewa na Rais Kikwete kwa Waziri Mkuu huyo wa taifa ambalo linapiga kasi zaidi ya maendeleo na ambalo lina nguvu ya Nyuklia. Mheshimiwa Singh amekubali mwaliko huo katika barua yake aliyomwandikia Rais Kikwete na iliyokabidhiwa kwake na Balozi wa India katika Tanzania, Mheshimiwa K.V. Bhagirah wakati Balozi huyo alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Kikwete leo, Alhamisi, Mei 19, 2011, Ikulu, Dar es Salaam. imeseta taarifa hiyo iliyosainiwa na Ikulu bila kusainiwa na mtu yeyote.
Akijibu mwaliko huo Bw. Sing amesema kuwa Nakushukuru kwa barua ya kunilialika kuitembelea nchi yako nzuri. Itakuwa ni heshima kwangu kuitembelea Tanzania na naukubali mwaliko huo kwa furaha kubwa na kuwa Nina ari kubwa kukutana nawe na marafiki wengine wa Tanzania wakati wa ziara hiyo na kujadili njia ya kuuinua uhusiano kati ya nchi zetu kwenye ngazi mpya kwa manufaa ya wananchi wa nchi zetu mbili
Ziara ya Bw. Singh nchini imekuja wakati ambapo taifa hilo la India likizidi kututumua nguvu zake za kiuchumi na ushawishi hasa katika eneo la Afrika na kuonekana ikiingia katika ushindani wa ushawishi kati ya na China pamoja na nchi za Magharibi ambazo zimekuwa na nafasi ya pekee katika bara la Afrika kwa muda mrefu.
Kabla hajaanza ziara yake hiyo ndefu leo Jumatatu Bw. Singh alielezea siku ya Jumapili mwelekeo wa ziara yake hiyo kuwa uhusiano kati ya India na Afrika utahusisha zaidi ni kuipa uwezo Afrika na kubadilishana ujuzi, biashara na ujenzi wa miundombinu. Bw. Singh amesema kuwa uwepo wa watu wengi wenye asili ya India katika kila kona ya Afrika ni ushahidi wa wazi wa mahusiano yetu ya kihistoria.
Soma Zaidi tovuti Dada ya JamiiForums -Fikrapevu.com