Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa Nduli, Iringa kwenye msiba wa Diwani Chonanga

Hivi ni kweli sura yako ilivyo ndiyo roho yako ilivyo? jinsi sura inavyo kuwa mbaya na roho...sijui mambo ya saikolojia, lakini watu wenye sura mbaya hujihisi inferior, na kuhisi wako less regarded katika jamii, hivyo maamuzi hua ni ya chuki..."WApigeni tu mpaka wakome".

Hapa kuna ukweli mkubwa, wewe nenda tu hospitali ama benki. ukitaka kuhudumiwa haraka mtafute tu dada mwenye sura nzuri, msalimie na umwombe kuwa una haraka halafu utuletee jibu.

Nilishafanya hii kitu karibu mara 4. NMB magomeni mara 2 nilikuwa na haraka, nahitaji kutoa hela kupitia kaunta. Foleni ilikuwa balaa. Sasa nilichofanya ni kumfuata dada mmoja mrembo, japo alikuwa ana pete ya ndoa, nikamwomba anichukulia hela nina haraka, akachukua slip ndani ya dakika 5 nikashika pesa mkononi. Siku nyingine nikapata msaada wa dada mwingine mrembo palepale NMB Magomeni. Pia Ifakara hospitali (ST. FRANCIS) nikiwa natibiwa mimi mwenyewe miaka ya mwaka 1998. Nililazwa, akiingia nesi mmoja mrembo ananihudumia kwa ukarimu wa hali ya juu kweli kweli. Lakini wacha waingie wenye sura za MAGAMBA, utaona mziki wake. Shinyanga Hospitali ya mkoa, nilimpeleka mama yangu yangu. Nikaenda maabara nikakuta foleni kubwa, nikamwita dada mmoja Mrembo, nikamwelezea. Ndani ya nusu saa majibu yakatoka.

Kwa hiyo mkuu kuna ukweli flnai ndani yake
 
Picha hii ya mwisho ndiyo imefanya post ya mwanadiwani isinitapishe, maana nilikuwa naona mazombi tu, karibia na mwasho wa movie ndiyo nikaona binadamu wa kisasa. kama utafanikiwa kumuona huyo wa kwanza, nifikishie salamu zangu kwa huyo wa kati

Nitamtafuta na nitamfikishia salam zake.

Anyway picha hii imebeba msiba wa MAGAMBA.
 
Kifo huwalinganisha wote, CCM na CHADEMA. Kaburi ndo mwisho wa ubabe. Tutende mema tukiwa hai, chama chako hakitakuwepo wakati wa hukumu. Askari wa Tanzania akamuuliza Yesu, na sisi askari tufanye nini? Yesu akamjibu, watendee watanzania wote sawa bila kujali itikadi zao za siasa au dini.

Mungu amsamehe marehemu, nahisi hakujua alipokuwa anatenda. Pole sana Mwanadiwani, bila shaka kwa kuondokewa na baba yako. Mwanadiwani umebaki hai, nakuomba unapotumiwa na CCM hufikirie kesho ya kifo. Diwani sasa anaulizwa kwa nini alimpiga mbunge, CCM hakipo kumtetea. Dunia mapito.

Mkuu Ujumbe MZITO huu, MWENYE MASIKIO NA ASIKIE
 
WAZIRI mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda ambae ni mlezi wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa jioni ya leo amewasili mkoani Iringa na kufika nyumbani kwa aliyekuwa diwani wa kata ya marehemu Idd Chonanga na kuungana na waombolezaji katika kuifariji familia ya diwani huyo.

Waziri Pinda ambae aliongoza na mkewe mama Tunu Pinda na viongozi wengine wa CCM mkoa wa Iringa pamoja na viongozi wa serikali ya mkoa wa Iringa wakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma walifika nyumbani kwa marehe mu Chonanga eneo la Nduli majira ya saa 10.56 na kutumia muda wa zaidi ya dakika 10 kuifariji familia hiyo.

Akiwa nyumbani kwa marehemu Chonanga waziri Pinda na mkewe wametoa pore kwa familia hiyo ya Chonanga na kuwaomba kuendelea kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo na kuwa wao katika chama wapo pamoja na familia hiyo katika maombolezo hayo .

Waziri Pinda amesema kuwa binafsi kama mlezi wa CCM mkoa wa Iringa ameguswa na kifo cha diwani Chonanga na kuwa kutokana na kuwa katika ziara ya kichama mkoa wa Iringa ameona ni vema kabla ya kuanza shughuli za chama kufika kuhani msiba huo .

Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu alisema kuwa CCM wilaya ya Iringa mjini na mkoa kwa ujumla wamepata pigo kubwa kwa kifo cha diwani huyo na kusema kuwa CCM itashiriki kwa asilimia 100 mazishi hayo yatakayofanyika mapema kesho katika kijiji hicho cha Nduli.

Kwa upande wake Greyson Chonanga ambae ni mtoto wa marehemu Chonanga ameeleza kufurahishwa na hatua ya waziri mkuu kufika kuhani msiba huo na kuwa wao kama familia hawakutambua kuwa msafara mkubwa kama huo wa kitaifa ungefika kuhani msiba huo.
Huku wakazi wa eneo hilo la Nduli wameelezwa kufurahishwa na umoja wa kweli uliopo ndani ya serikali ya CCM kutokana na viongozi wake kuwajali watu wa chini wanaowaongoza na kuwa utu ambao waziri mkuu ameonyesha ni upendo tosha kwa wana Nduli kwa serikali ya CCM.
Alisema Adam Kalinga mkazi wa kata hiyo ya Nduli ambae alikuwepo msibani hapo kuwa katika kuenzi kazi za marehemu Chonanga wao wataendelea kutambua mchango wake .


Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu wa pili kulia akitoa akiitambulisha familia ya marehemu diwani Idd Chonanga aliyekuwa diwani wa kata ya Nduli aliyefariki dunia jana



Mtoto mkubwa wa marehemu Idd Chonanga Bw Greyson Chonanga akipewa mkono wa pole na waziri mkuu Mizengo Pinda aliyefika nyumbani kwao eneo la kijiji cha Nduli kuhani msiba huo jioni ya leo. Anayeshuhudia ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu


Viongozi mbali mbali wa CCM na serikali mkoa wa Iringa wakiwa na waziri mkuu Mizengo Pinda pamoja na waombolezaji wa msiba wa aliyekuwa diwani wa kata ya Nduli Idd Chonanga aliyefariki jana




Mtoto mkubwa wa diwani Chonanga akitoa maelezo kwa waziri mkuu Pinda juu ya kifo cha baba yake

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiomboleza msiba wa diwani Chonanga leo katika kijiji cha Nduli Iringa mjini

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akiwaaga waombolezaji leo

Waziri mkuu akiaganga na familia ya marehemu Chonaga leo kijiji cha Nduli Iringa mjini




Mtoto mkubwa wa marehemu Chonanga akimuongoza waziri mkuu na msafara wake kuondoka eneo hilo

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa akiwapa pore wafiwa
Ndugu wa diwani Chonanga wakiangana na waziri mkuu Pinda

Waziri Pinda akiagana na famili ya marehemu Chonanga leo

Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma kushoto akiwa na mke wa waziri mkuu mama Tunu Pinda na viongozi wengine wa CCM mjini Iringa

Mwenyekiti wa CCM mjini Iringa Abed Kiponza akimng'ata sikio mama Tunu Pinda

Familia ya marehemu Chonanga akifurahia baada ya kutembelewa na waziri mkuu

napita tu.....ila leo nina mawili...

1. watu wa iringa siku hizi hawahudhurii misiba kama zamani???

2.picha zinaonyesha huyu mzee aliyetangulia kwa shetani hakufanya juhudi yoyote kutafuta riziki halali kwa maisha bora na maendeleo ya maisha...nakubaliana na mmoja wetu kuwa alikuwa ana tabia za ushirikina....hata watoto hajawasomesha...wamebaki katika lindi la umasikini mkubwa....ametuachia kikundi cha majambazi.....

mytake: - nadhani ifike wakati tusikubali kuchagua majobless kwenye nafasi za kisiasa!
 
Faces of thuggery......all around

E84A0583.JPG

Duh, na hawa jamaa ukikutana nao kwenye chochoro huna bahati, haswa hawa wawili pembeni mwa PM
 
E84A0583.JPG

Duh, na hawa jamaa ukikutana nao kwenye chochoro huna bahati, haswa hawa wawili pembeni mwa PM

bila shaka hapo mkulu anamwambia kijana .... siku hizi ni kuwapiga tu!!!

another ramadhani ighondo aka mg'oa kucha in the making! - THIS IS HOW TISS RECRUITS NOW DAYS! no matter walinzi wa OBAMA kuwashangaa wanausalama wa tanzania kutumia mabavu...........zaidi zaidi wanafundishwa kutumia vitu vizito na vyenye ncha kali....
 
Hivi PM kaenda kama kamanda wa CCM mkoa au kwa sababu huyo bwana alitekeleza wazo lake la kupiga! marehemu alikuwa na same wazo la kupiga!
 
Wazr mkuu wetu et ameguswa sana na kfo bha kiongoz huyu wa ccm. Lakni ktk mauaj ya knyama kule Arusha PM hakuguswa hata kdogo(kaul yake bungen ildhihirisha. Anyway, polen wafiwa.
 
Wazr mkuu wetu et ameguswa sana na kfo cha kiongoz huyu wa ccm. Lakni ktk mauaj ya knyama kule Arusha PM hakuguswa hata kdogo(kaul yake bungen ildhihirisha. Anyway, polen wafiwa.
 
E84A0574.JPG
Hawa watoto wa Marehemu walio kulia kwa Waziri Mkuu Pinda ndio waliokwenda kuwakata mapanga wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CHADEMA na ambao kesi yao iko mahakamani?
huyo mtoto wa marehemu wa kwanza baada ya mizengo namfahamu nilisoma nae tunduru secondary ni bandidu kinoma anaitwa Geofrey chonanga
 
mbona hawa watoto na familia ya marehemu diwani hawafanani na udiwani? jamani watoto ni wachafu wamevaa viatu mabuvu nguo chafu. yaan ndio tusema hawa watoto ndio wamevunja kabati? kwa kweri hawa watoto wa diwani wanasthili kua wafungwa tu, mahakama ifanye haraka kuwapeleka wanapostahili hawa machokoraaa
 
Hivi huyu Maremu diwani hakuwa na majirani? mbona msiba uko na family members tu......inaelekea hakuwa na mahusiano mazuri na jamii inaomzunguka! Halafu nadhani ndo mwisho wa hii familia sioni hata dalili ya mwenye hema kati yao!
Huwa hakuna kiongozi wa CCM mwenye mahusiano na jamii yaliyo mazuri
 
Back
Top Bottom