Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
huyo mtoto wa marehemu wa kwanza baada ya mizengo namfahamu nilisoma nae tunduru secondary ni bandidu kinoma anaitwa Geofrey chonanga
Vipi, alikuwa anawaibia vitu vyenu?
huyo mtoto wa marehemu wa kwanza baada ya mizengo namfahamu nilisoma nae tunduru secondary ni bandidu kinoma anaitwa Geofrey chonanga
Huyo alikuwa tu diwani au kuna kazi maalum za chama alizokuwa anafanya??? It's very interesting news.....
Ila kwa ushiriki wa Pinda hapo nadhani huyo marehemu alikuwa hatari kwa Taifa.
Naomba viongozi woote ws CCM wafe...shetani endelea kuua haya maccm maana ni mashetani wenzako.hizi ni habari njema kusikia maccm yanakufa!
Halafu ni wachafu wavuta bangi Hilo ni somo kwa Mwigulu
Naomba viongozi woote ws CCM wafe...shetani endelea kuua haya maccm maana ni mashetani wenzako.hizi ni habari njema kusikia maccm yanakufa!
WAZIRI mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda ambae ni mlezi wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa jioni ya leo amewasili mkoani Iringa na kufika nyumbani kwa aliyekuwa diwani wa kata ya marehemu Idd Chonanga na kuungana na waombolezaji katika kuifariji familia ya diwani huyo.
Waziri Pinda ambae aliongoza na mkewe mama Tunu Pinda na viongozi wengine wa CCM mkoa wa Iringa pamoja na viongozi wa serikali ya mkoa wa Iringa wakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma walifika nyumbani kwa marehe mu Chonanga eneo la Nduli majira ya saa 10.56 na kutumia muda wa zaidi ya dakika 10 kuifariji familia hiyo.
Akiwa nyumbani kwa marehemu Chonanga waziri Pinda na mkewe wametoa pore kwa familia hiyo ya Chonanga na kuwaomba kuendelea kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo na kuwa wao katika chama wapo pamoja na familia hiyo katika maombolezo hayo .
Waziri Pinda amesema kuwa binafsi kama mlezi wa CCM mkoa wa Iringa ameguswa na kifo cha diwani Chonanga na kuwa kutokana na kuwa katika ziara ya kichama mkoa wa Iringa ameona ni vema kabla ya kuanza shughuli za chama kufika kuhani msiba huo .
Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu alisema kuwa CCM wilaya ya Iringa mjini na mkoa kwa ujumla wamepata pigo kubwa kwa kifo cha diwani huyo na kusema kuwa CCM itashiriki kwa asilimia 100 mazishi hayo yatakayofanyika mapema kesho katika kijiji hicho cha Nduli.
Kwa upande wake Greyson Chonanga ambae ni mtoto wa marehemu Chonanga ameeleza kufurahishwa na hatua ya waziri mkuu kufika kuhani msiba huo na kuwa wao kama familia hawakutambua kuwa msafara mkubwa kama huo wa kitaifa ungefika kuhani msiba huo.
Huku wakazi wa eneo hilo la Nduli wameelezwa kufurahishwa na umoja wa kweli uliopo ndani ya serikali ya CCM kutokana na viongozi wake kuwajali watu wa chini wanaowaongoza na kuwa utu ambao waziri mkuu ameonyesha ni upendo tosha kwa wana Nduli kwa serikali ya CCM.
Alisema Adam Kalinga mkazi wa kata hiyo ya Nduli ambae alikuwepo msibani hapo kuwa katika kuenzi kazi za marehemu Chonanga wao wataendelea kutambua mchango wake .
![]()
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu wa pili kulia akitoa akiitambulisha familia ya marehemu diwani Idd Chonanga aliyekuwa diwani wa kata ya Nduli aliyefariki dunia jana
![]()
Mtoto mkubwa wa marehemu Idd Chonanga Bw Greyson Chonanga akipewa mkono wa pole na waziri mkuu Mizengo Pinda aliyefika nyumbani kwao eneo la kijiji cha Nduli kuhani msiba huo jioni ya leo. Anayeshuhudia ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu
![]()
Viongozi mbali mbali wa CCM na serikali mkoa wa Iringa wakiwa na waziri mkuu Mizengo Pinda pamoja na waombolezaji wa msiba wa aliyekuwa diwani wa kata ya Nduli Idd Chonanga aliyefariki jana
![]()
![]()
Mtoto mkubwa wa diwani Chonanga akitoa maelezo kwa waziri mkuu Pinda juu ya kifo cha baba yake
![]()
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiomboleza msiba wa diwani Chonanga leo katika kijiji cha Nduli Iringa mjini
![]()
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akiwaaga waombolezaji leo
Waziri mkuu akiaganga na familia ya marehemu Chonaga leo kijiji cha Nduli Iringa mjini
![]()
![]()
Mtoto mkubwa wa marehemu Chonanga akimuongoza waziri mkuu na msafara wake kuondoka eneo hilo
![]()
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa akiwapa pore wafiwa
![]()
Ndugu wa diwani Chonanga wakiangana na waziri mkuu Pinda
![]()
Waziri Pinda akiagana na famili ya marehemu Chonanga leo
![]()
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma kushoto akiwa na mke wa waziri mkuu mama Tunu Pinda na viongozi wengine wa CCM mjini Iringa
![]()
Mwenyekiti wa CCM mjini Iringa Abed Kiponza akimng'ata sikio mama Tunu Pinda
![]()
Familia ya marehemu Chonanga akifurahia baada ya kutembelewa na waziri mkuu
![]()
Msafara wa waziri mkuu Mizengo Pinda ukitoka kuhani msiba wa diwani wa kata ya Nduli Idd Chonanga aliyefariki jana na kuzikwa kesho kijijini hapo.
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
Jembe la manispaa ya Iringa mkurugenzi wa Halmashauri ya manispaa Teresia Mahongo akimpokea waziri mkuu Mizengo Pinda kwa tabasamu kali ![]()
![]()
![]()
Meneja wa Tanroads mkoa wa Iringa ambae anafanya makubwa katika barabara ya Iringa - Dodoma Paul Lwakurwa akipongezwa na waziri mkuu kwa kazi nzuri ![]()
![]()
![]()
![]()
Wadau wa masuala ya utalii mkoa wa Iringa ambao wanapigania kuitangaza hifadhi ya Ruaha na hifadhi za kusini
![]()
![]()
Hawa watoto wa Marehemu walio kulia kwa Waziri Mkuu Pinda ndio waliokwenda kuwakata mapanga wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CHADEMA na ambao kesi yao iko mahakamani?
Mkuu hebu tizama viatu alivyovaa mizengo pinda vinachekesha hahaha! !!
![]()
Full vumbi halafu kisigino kirefu mtindo ambao siku za leo kutembea ni karaha. Anajisikiaje kutembelea kiatu cha kisigino hivyo, kwa vile ameshazoea basi.
Cha kushangaza aliongozana na mkewe, hakuweza kukumbuka hata papertowel kupanguza kidogo vumbi lile, labda alitokea shambani kuvuna mahindi maana kipindi hiki mavuno yameanza. Lakini kama aliteremka toka kwenye ndege kama mlolongo wa pic zinavyoonyesha duh! Hii kali.