Waziri Mhagama Apokea Muongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathimini katika Taasisi za Umma

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,902
944

WAZIRI MHAGAMA APOKEA MWONGOZO WA KITAIFA WA UFUATILIAJI NA TATHMINI KATIKA TAASISI ZA UMMA.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu nayeshugulika na Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama, Amepokea Rasimu ya kwanza ya Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali katika Taasisi za Umma.

Akipokea Rasimu hiyo, tarehe 24/08/2023 Jijini Dodoma, Waziri Mhagama alisema Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali Nchini, Utasaidia kuwa na matokeo ambayo yanaendana na programu na Miradi iliyopangwa kutekelezeka ndani ya Taifa, na Itasaidia Serikali kujipangia Programu zenye matokeo chanya.

“Tunaweza tukawa na matokeo yakawa hasi, ama mradi usifanye vizuri, ila tukiwa na Mwongozo mzuri basi utatusaidia ndani ta Taifa kuwa na matokeo mazuri yaliyowekwa kutokana na Utekelezaji wa mradi Husika” alibainisha.

Sambamba na hilo, alisema kuwa, mwongozo huu utafikisha Taifa mahali ambapo dhana ya uwajibikaji wa hiari na uratibu wa Pamoja itafikiwa na kujifanyia tathmini katika usimamizi na utekelezaji wa programu, zilizopo nchini na Usimamizi mzuri wa Rasilimali watu na Rasilimali fedha kwenye Serikali kuu, Taasisi na Serikali za Mitaa.

Aidha, Mhe. Waziri Mhagama Alisema ana Imani kuwa Muongozo huu, utasaidia kuimarisha Utawala Bora na kuendelea kusema kuwa, bila Utawala bora hakuna kizuri kitakachofanyika, katika dhana nzima ya kutelekeza kazi za kila siku akitolea mfano dhana ya uwajibikaji na mapambano dhidi ya rushwa.

“Tunatarajia kuwa Mwongozo huu Utatusaidia kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala na Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu na muda Mfupi.” Alihimiza.

Aliongeza kusema kuwa Mwongozo huu utasaidia kukamilisha programu na miradi Pamoja na kufikisha huduma kwa wananchi kwa wakati na viwango vinavyotarajiwa na kuokoa Rasilimali fedha kwa kiasi kikubwa.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.10.jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.10.jpeg
    64.7 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.11(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.11(1).jpeg
    66.9 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.10(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.10(1).jpeg
    57.2 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.11.jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.11.jpeg
    63.1 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.11(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-08-27 at 01.59.11(2).jpeg
    49.2 KB · Views: 1

WAZIRI MHAGAMA APOKEA MWONGOZO WA KITAIFA WA UFUATILIAJI NA TATHMINI KATIKA TAASISI ZA UMMA.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu nayeshugulika na Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama, Amepokea Rasimu ya kwanza ya Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali katika Taasisi za Umma.

Akipokea Rasimu hiyo, tarehe 24/08/2023 Jijini Dodoma, Waziri Mhagama alisema Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali Nchini, Utasaidia kuwa na matokeo ambayo yanaendana na programu na Miradi iliyopangwa kutekelezeka ndani ya Taifa, na Itasaidia Serikali kujipangia Programu zenye matokeo chanya.

“Tunaweza tukawa na matokeo yakawa hasi, ama mradi usifanye vizuri, ila tukiwa na Mwongozo mzuri basi utatusaidia ndani ta Taifa kuwa na matokeo mazuri yaliyowekwa kutokana na Utekelezaji wa mradi Husika” alibainisha.

Sambamba na hilo, alisema kuwa, mwongozo huu utafikisha Taifa mahali ambapo dhana ya uwajibikaji wa hiari na uratibu wa Pamoja itafikiwa na kujifanyia tathmini katika usimamizi na utekelezaji wa programu, zilizopo nchini na Usimamizi mzuri wa Rasilimali watu na Rasilimali fedha kwenye Serikali kuu, Taasisi na Serikali za Mitaa.

Aidha, Mhe. Waziri Mhagama Alisema ana Imani kuwa Muongozo huu, utasaidia kuimarisha Utawala Bora na kuendelea kusema kuwa, bila Utawala bora hakuna kizuri kitakachofanyika, katika dhana nzima ya kutelekeza kazi za kila siku akitolea mfano dhana ya uwajibikaji na mapambano dhidi ya rushwa.

“Tunatarajia kuwa Mwongozo huu Utatusaidia kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala na Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu na muda Mfupi.” Alihimiza.

Aliongeza kusema kuwa Mwongozo huu utasaidia kukamilisha programu na miradi Pamoja na kufikisha huduma kwa wananchi kwa wakati na viwango vinavyotarajiwa na kuokoa Rasilimali fedha kwa kiasi kikubwa.
Mama wa vitenge sana output 0
 
Back
Top Bottom