Waziri Mbarawa: Kuna haja ya kuongeza magati bandari. Watanzania kwenda Misri kujifunza jinsi ya uendeshaji wa Treni ya SGR

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Tanzania imepata ugeni kutoka Misri ukiongozwa na Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Luteni Jenerali Kamel Alwazeer kwa lengo la kujifunza fursa za uwekezaji zilizopo Nchini
20240220_023822.jpg

Akizungumza wakati wa kuwakaribisha wageni hao, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema “Sekta ya Uchukuzi, Serikali ya Tanzania imeweka fedha nyingi kwa ajili ya kuhakikisha sekta inakua.

“Sekta hiyo ikikua na Uchumi wa Nchi yetu utakua, kwani wenzetu wameendelea sana na tumewaeleza miradi mbalimbali wanayoweza kuwekeza, mfano pale Bandari ya Dar, tuna mradi wa ujenzi wa bandari katika namba 13, 14 na 15 katika mfumo wa PPP.”

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema pamoja na maboresho yaliyofanywa katika bandari ya Dar es Salaam, kuna haja ya kuongezwa gati namba 13 hadi 15.

Profesa Mbarawa amesema tayari, Serikali imefanya maboresho makubwa katika bandari hiyo lakini bado kuna msongamano wa meli bandari hapo.
20240220_023810.jpg

Akizungumza katika kikao cha Wizara ya Uchukuzi ya Tanzania na Misri kilichohusu ushirikiano wa uwekezaji katika sekta ya uchukuzi Profesa Mbarawa amesema kuna haja ya kuongeza magati katika bandari hiyo, ili kupunguza msongamano wa meli zinazohudumiwa.

"Pamoja na maboresho ya bandari yaliyofanywa na Serikali hivi karibuni bado kuna meli 18 zinasubiri kuhudumiwa,"amesema Profesa Mbarawa.

Ameongeza "Kule Misri wana reli iliyojengewa katika Mfumo wa SGR, wana reli ya kawaida na nyingine ya ‘express’. Tumewaomba vijana wetu kutoka TRC watembelee wajifunze jinsi ya kuendesha Reli ya SGR na Waziri (wa Misri) amekubali bila tatizo, kilichobaki ni wataalam kukaa pamoja kuangali jinsi inavyoweza kutekelezwa."

Kuhusu ushirikiano kati ya Misri na Tanzania, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema utawezesha watu wa Tanzania na Misri kubalilishana ujuzi na hatimaye kukuza uchumi huku akieleza manufaa katika ajira.

Katika maombi yake Profesa Mbarawa amemuomba Waziri wa Uchukuzi wa Misri kuridhia kuwapokea watanzania watakaokwenda kujifunza uendeshaji wa Mradi wa Reli ya Kisiasa (SGR).

Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa amezikaribisha kampuni za Misri kuwekeza katika miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), maboresho ya bandari za Tanzania.
20240220_023814.jpg

Upande wake Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Luteni Jenerali Kamel Alwazeer ameeleza kuridhishwa na fursa za uwekezaji katika sekta ya uchukuzi nchini na kwamba wapo tayari kuwekeza.

Amesema hatua ya mwendelezo wa kikao hicho, amemkaribisha Profesa Mbarawa kwenda Misri kwa mazungumzo na kujifunza zaidi.

"Sisi tupo tayari kuwekeza na kubadilishana uzoefu tulionao kwa watendaji wa Tanzania ili kuongeza ushirikiano," amesema.
 
Last edited:
Mkandarasi wa SGR ni Mturuki, anayesupply train zenyewe ni Mkorea Kusini na Watanzania wanakoenda kujiunza jinsi ya kusimamia na kuendesha SGR ni Misri.....hakika Tanzania inapaswa kuingizwa kwenye ajabu la 9 la dunia
 
Tanzania imepata ugeni kutoka Misri ukiongozwa na Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Luteni Jenerali Kamel Alwazeer kwa lengo la kujifunza fursa za uwekezaji zilizopo Nchini

Akizungumza wakati wa kuwakaribisha wageni hao, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema “Sekta ya Uchukuzi, Serikali ya Tanzania imeweka fedha nyingi kwa ajili ya kuhakikisha sekta inakua.

“Sekta hiyo ikikua na Uchumi wa Nchi yetu utakua, kwani wenzetu wameendelea sana na tumewaeleza miradi mbalimbali wanayoweza kuwekeza, mfano pale Bandari ya Dar, tuna mradi wa ujenzi wa bandari katika namba 13, 14 na 15 katika mfumo wa PPP.”

Ameongeza "Kule Misri wana reli iliyojengewa katika Mfumo wa SGR, wana reli ya kawaida na nyingine ya ‘express’. Tumewaomba vijana wetu kutoka TRC watembelee wajifunze jinsi ya kuendesha Reli ya SGR na Waziri (wa Misri) amekubali bila tatizo, kilichobaki ni wataalam kukaa pamoja kuangali jinsi inavyoweza kutekelezwa."

Kuhusu ushirikiano kati ya Misri na Tanzania, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema utawezesha watu wa Tanzania na Misri kubalilishana ujuzi na hatimaye kukuza uchumi huku akieleza manufaa katika ajira.

Katika maombi yake Profesa Mbarawa amemuomba Waziri wa Uchukuzi wa Misri kuridhia kuwapokea watanzania watakaokwenda kujifunza uendeshaji wa Mradi wa Reli ya Kisiasa (SGR).

Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa amezikaribisha kampuni za Misri kuwekeza katika miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), maboresho ya bandari za Tanzania.

Upande wake Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Luteni Jenerali Kamel Alwazeer ameeleza kuridhishwa na fursa za uwekezaji katika sekta ya uchukuzi nchini na kwamba wapo tayari kuwekeza.

Amesema hatua ya mwendelezo wa kikao hicho, amemkaribisha Profesa Mbarawa kwenda Misri kwa mazungumzo na kujifunza zaidi.

"Sisi tupo tayari kuwekeza na kubadilishana uzoefu tulionao kwa watendaji wa Tanzania ili kuongeza ushirikiano," amesema.
Haujawahi kuwa na SGR sasa huo uzoefu wakubadilishana umeupata lini! Badala ya kushukuru kufundishwa na wewe unajifanya mjuvi! Uongouongo tu mpaka basi.
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Tanzania imepata ugeni kutoka Misri ukiongozwa na Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Luteni Jenerali Kamel Alwazeer kwa lengo la kujifunza fursa za uwekezaji zilizopo Nchini

Akizungumza wakati wa kuwakaribisha wageni hao, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema “Sekta ya Uchukuzi, Serikali ya Tanzania imeweka fedha nyingi kwa ajili ya kuhakikisha sekta inakua.

“Sekta hiyo ikikua na Uchumi wa Nchi yetu utakua, kwani wenzetu wameendelea sana na tumewaeleza miradi mbalimbali wanayoweza kuwekeza, mfano pale Bandari ya Dar, tuna mradi wa ujenzi wa bandari katika namba 13, 14 na 15 katika mfumo wa PPP.”

Ameongeza "Kule Misri wana reli iliyojengewa katika Mfumo wa SGR, wana reli ya kawaida na nyingine ya ‘express’. Tumewaomba vijana wetu kutoka TRC watembelee wajifunze jinsi ya kuendesha Reli ya SGR na Waziri (wa Misri) amekubali bila tatizo, kilichobaki ni wataalam kukaa pamoja kuangali jinsi inavyoweza kutekelezwa."

Kuhusu ushirikiano kati ya Misri na Tanzania, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema utawezesha watu wa Tanzania na Misri kubalilishana ujuzi na hatimaye kukuza uchumi huku akieleza manufaa katika ajira.

Katika maombi yake Profesa Mbarawa amemuomba Waziri wa Uchukuzi wa Misri kuridhia kuwapokea watanzania watakaokwenda kujifunza uendeshaji wa Mradi wa Reli ya Kisiasa (SGR).

Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa amezikaribisha kampuni za Misri kuwekeza katika miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), maboresho ya bandari za Tanzania.

Upande wake Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Luteni Jenerali Kamel Alwazeer ameeleza kuridhishwa na fursa za uwekezaji katika sekta ya uchukuzi nchini na kwamba wapo tayari kuwekeza.

Amesema hatua ya mwendelezo wa kikao hicho, amemkaribisha Profesa Mbarawa kwenda Misri kwa mazungumzo na kujifunza zaidi.

"Sisi tupo tayari kuwekeza na kubadilishana uzoefu tulionao kwa watendaji wa Tanzania ili kuongeza ushirikiano," amesema.
Sgr mpaka ikamilike, nchi tele zitakuwa zimeweka utaalamu wao, sasa sijui wapi wanavifaa na utaalamu bora, na utunzaji wa reli utatumia njia ya mtaalamu yupi?!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom