Waziri Masauni ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.

==
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni ametoa onyo kali kwa watu wanaotumia uhuru wa kutoa maoni vibaya kwa lengo la kuhatarisha usalama na kuleta mpasuko kwa taifa.

Kauli hiyo imekuja baada ya kuibuka baadhi ya watu hususani wanasiasa kutumia majukwaa yao kutoa kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani vyenye kuleta mgawanyiko nchini.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masaun ameyasema hayo wakati akizungumza na Wananchama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kindondoni Shamba iliyopo Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa tawi katika kata hiyo lililopo Chuo Kikuu Huria.

"Ninalielekeza jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama kuhakikisha havimfumbii macho mtu yeyote au kikundi chochote kitakachopelekea kwa vitendo au kwa kauli katika kuvunja sheria za nchi yetu na kuhatarisha usalama wa nchi hii"_ Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni

"Katika nchi hii kama kuna chama kinachosifika katika ujenzi na misingi ya umoja na mshikamano na amani ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ndiyo kina dhamana ya kuiongoza Serikali, na Serikali hii inayo jukumu la kuhakikisha nchi inabaki kuwa salama na kuwa moja kwa kudumisha umoja na mshikamano, vyama vingine havina jukumu hilo"_Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni
 
Aanze na Faiza fox huyu mchochezi wa kidini .,

Pia Jussa huyu na wapemba wenzake kila siku kututukana watanganyika wanataka kuvunja muungano

,sunday manara huyu anabagua watu wa bara ,anadai bandari Ni ya waarabu na ya watu wa pwani, watu wa mikoani wafunge mdomo

Bunge la tanzania kwa kumtukana mbowe kwa kejeli wengi wao ni wabunge wa Zanzibar walimwita ana mdomo na masikio Kama chakubanga

Mashekhe wa bakwata kwa kuwakebehi na kuwadhalilisha wachungaji wakristo, wanasema wanataka kumpindua rais

Sheikh mwaipopo kwa kumbagua na kumtuka pro shivdi ,anadai si mtanzania Ni mwindi

...kwa ujumla wapo wengi wa kupita nao, ndugu masaudini
 
..Wazanzibari kama Othman Masoud, Juma Duni, Ismail Jussa,.wakiukosoa muungano hatusikii wakitishiwa na Bwana Masauni.

..Watanganyika wakikosoa muungano ndipo Bwana Masauni anajitokeza kuelekeza vyombo vya dola dhidi yao.
Awatishe Wazanzibari wenzie haogopi?Watamtolea macho na maneno hadi aombe "yeesheeee"/pooh!
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
View attachment 2682444
Mpuuzi huyu. Watanganyika wanatetea mali asili zao. Za kwa hazikugawiwa kwa waarabu. The so called muungano uvunjike kila mmoja ajue lake.
 
Back
Top Bottom