dubu
JF-Expert Member
- Oct 18, 2011
- 3,496
- 3,461
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, ameonya watu au vikundi vya watu ambavyo vinatumia uhuru wa kutoa maoni kutoa kauli za uchochezi na zenye mrengo wa kutaka kuligawa taifa, ambapo amesema serikali haitavumilia vitendo hivyo.
==
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni ametoa onyo kali kwa watu wanaotumia uhuru wa kutoa maoni vibaya kwa lengo la kuhatarisha usalama na kuleta mpasuko kwa taifa.
Kauli hiyo imekuja baada ya kuibuka baadhi ya watu hususani wanasiasa kutumia majukwaa yao kutoa kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani vyenye kuleta mgawanyiko nchini.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masaun ameyasema hayo wakati akizungumza na Wananchama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kindondoni Shamba iliyopo Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa tawi katika kata hiyo lililopo Chuo Kikuu Huria.
"Ninalielekeza jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama kuhakikisha havimfumbii macho mtu yeyote au kikundi chochote kitakachopelekea kwa vitendo au kwa kauli katika kuvunja sheria za nchi yetu na kuhatarisha usalama wa nchi hii"_ Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni
"Katika nchi hii kama kuna chama kinachosifika katika ujenzi na misingi ya umoja na mshikamano na amani ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ndiyo kina dhamana ya kuiongoza Serikali, na Serikali hii inayo jukumu la kuhakikisha nchi inabaki kuwa salama na kuwa moja kwa kudumisha umoja na mshikamano, vyama vingine havina jukumu hilo"_Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni
==
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni ametoa onyo kali kwa watu wanaotumia uhuru wa kutoa maoni vibaya kwa lengo la kuhatarisha usalama na kuleta mpasuko kwa taifa.
Kauli hiyo imekuja baada ya kuibuka baadhi ya watu hususani wanasiasa kutumia majukwaa yao kutoa kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani vyenye kuleta mgawanyiko nchini.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masaun ameyasema hayo wakati akizungumza na Wananchama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kindondoni Shamba iliyopo Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa tawi katika kata hiyo lililopo Chuo Kikuu Huria.
"Ninalielekeza jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama kuhakikisha havimfumbii macho mtu yeyote au kikundi chochote kitakachopelekea kwa vitendo au kwa kauli katika kuvunja sheria za nchi yetu na kuhatarisha usalama wa nchi hii"_ Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni
"Katika nchi hii kama kuna chama kinachosifika katika ujenzi na misingi ya umoja na mshikamano na amani ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ndiyo kina dhamana ya kuiongoza Serikali, na Serikali hii inayo jukumu la kuhakikisha nchi inabaki kuwa salama na kuwa moja kwa kudumisha umoja na mshikamano, vyama vingine havina jukumu hilo"_Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni