johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,958
- 141,951
Waziri wa TAMISEMI Mh. Jaffo amesema hatashangaa endapo mkuu wa wilaya ya Kisarawe mh Joketi atapandishwa cheo kwa sababu ndiye DC anayeongoza kwa kuchapa kazi kuliko wakuu wa wilaya wote Tanzania.
Mh Jaffo amesema ameamua kuyasema hayo kwa sababu yeye siyo mnafiki kwani wanafiki wana tabia ya kumsifia mtu akishakufa.
Jaffo amesisitiza kuwa yeye ndio Boss wa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wote hivyo pongezi anazotoa kwa DC Joketi ni za dhati kabisa kwa sababu anaujua vizuri utendaji wa watendaji wote katika wizara yake akiwa kama msaidizi wa Rais Magufuli pale TAMISEMI.
Source Ayo tv!
Maendeleo hayana vyama!
Mh Jaffo amesema ameamua kuyasema hayo kwa sababu yeye siyo mnafiki kwani wanafiki wana tabia ya kumsifia mtu akishakufa.
Jaffo amesisitiza kuwa yeye ndio Boss wa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wote hivyo pongezi anazotoa kwa DC Joketi ni za dhati kabisa kwa sababu anaujua vizuri utendaji wa watendaji wote katika wizara yake akiwa kama msaidizi wa Rais Magufuli pale TAMISEMI.
Source Ayo tv!
Maendeleo hayana vyama!