Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Wajumbe, hali ya siasa kwa Mbunge wa Mtama Nape Moses Nnauye inazidi kuwa mbaya kuelekea 2025 baada ya Wazee wa kabila la Wamwera kuafikiana kuwa kijana huyo hawezi tena kuwa chaguo lao na badala yake wanahitaji mtu kutoka katika familia ya Hayati Bernard Membe kama hatua ya kumuenzi Mwanadiplomasia huyo.
Hatua hiyo imekuja baada ya mwanamke (Binti) anayejulikana kama Siwema Chekanao ambaye alikuwa miongoni mwa wanawake waliolala ardhini na Nape kutembea juu ya migogongo yao kama hatua ya kumliwaza kijana wao (Nape) baada ya kufurushwa uwaziri na Hayati John Magufuli.
Huu ni utamaduni wa kabila la Wamwera kwa mtu wao aliyeumizwa. Lakini katika zoezi hilo Binti Siwema Chekanao anadaiwa Nape alimvunja kiuno na kumuahidi kwamba angemgharamikia matibabu. Siwema amefikisha malalamiko yake kwa wazee hao japo ni wa kutembea na wheel chair Toka alipovunjwa kiuno na Waziri Nape anayedaiwa kublock namba ya simu ya Binti huyo mwenye mateso na maumivu usiku na mchana.
Aidha, habari kutoka jimboni Mtama zinaeleza kwamba hata wazee hao walipomtafuta amtibie Binti yao bado Nape ameonesha kuwadharau jambo ambalo wazee hao kuamua kuandaa "zoezi la laana" litakalofanyika siku ya kuadhimisha 40 ya Membe aliyefariki jijini Dar es salaam mapema mwaka huu.
Haijawekwa wazi kuwa katika familia hiyo ya Membe hasa ni nani analengwa kumrithi marehemu kufuatia watoto wa marehemu Cesilia, Richard na Denis hawaoneshi urithi wa siasa kama baba Yao na pia bado ni wadogo. Mjane wa marehemu Dorcas naye hatajwi sana jambo ambalo inadaiwa mlengwa ni mdogo wa Membe, Stephen K. Membe ambaye ndiye Msemaji wa familia hiyo kwa Sasa.
"Huyu kijana (Nape) ni mpuuzi sana na mjivuni, bila marehemu kutuambia tumpe Ubunge angekuwa wapi? Asubiri 40 atujue Wamwera", anasema Mzee Yasini Hassan katika kikao Cha maandalizi ya 40 ya Membe.
Itakumbukwa kwamba Nape ni miongoni mwa wabunge waliopita bila kupingwa baada ya mpinzani wake kutoka upinzani kutekwa na kuswekwa ndani Hadi muda wa kurejesha fomu kupita.
My take: Nape angetafuta Jimbo lingine analokubalika hasa Ubungo na Singida alikokulia.
NAWASILISHA.
Hatua hiyo imekuja baada ya mwanamke (Binti) anayejulikana kama Siwema Chekanao ambaye alikuwa miongoni mwa wanawake waliolala ardhini na Nape kutembea juu ya migogongo yao kama hatua ya kumliwaza kijana wao (Nape) baada ya kufurushwa uwaziri na Hayati John Magufuli.
Huu ni utamaduni wa kabila la Wamwera kwa mtu wao aliyeumizwa. Lakini katika zoezi hilo Binti Siwema Chekanao anadaiwa Nape alimvunja kiuno na kumuahidi kwamba angemgharamikia matibabu. Siwema amefikisha malalamiko yake kwa wazee hao japo ni wa kutembea na wheel chair Toka alipovunjwa kiuno na Waziri Nape anayedaiwa kublock namba ya simu ya Binti huyo mwenye mateso na maumivu usiku na mchana.
Aidha, habari kutoka jimboni Mtama zinaeleza kwamba hata wazee hao walipomtafuta amtibie Binti yao bado Nape ameonesha kuwadharau jambo ambalo wazee hao kuamua kuandaa "zoezi la laana" litakalofanyika siku ya kuadhimisha 40 ya Membe aliyefariki jijini Dar es salaam mapema mwaka huu.
Haijawekwa wazi kuwa katika familia hiyo ya Membe hasa ni nani analengwa kumrithi marehemu kufuatia watoto wa marehemu Cesilia, Richard na Denis hawaoneshi urithi wa siasa kama baba Yao na pia bado ni wadogo. Mjane wa marehemu Dorcas naye hatajwi sana jambo ambalo inadaiwa mlengwa ni mdogo wa Membe, Stephen K. Membe ambaye ndiye Msemaji wa familia hiyo kwa Sasa.
"Huyu kijana (Nape) ni mpuuzi sana na mjivuni, bila marehemu kutuambia tumpe Ubunge angekuwa wapi? Asubiri 40 atujue Wamwera", anasema Mzee Yasini Hassan katika kikao Cha maandalizi ya 40 ya Membe.
Itakumbukwa kwamba Nape ni miongoni mwa wabunge waliopita bila kupingwa baada ya mpinzani wake kutoka upinzani kutekwa na kuswekwa ndani Hadi muda wa kurejesha fomu kupita.
My take: Nape angetafuta Jimbo lingine analokubalika hasa Ubungo na Singida alikokulia.
NAWASILISHA.