mkuu wahidas kwa sasa si lolote si chochote mbele ya yutong, zhongtong, higer za hamanju,maning nice, machinga, najma na buti la zungu. wahdas alitamba zamani akiwa na scania zake matata kama vile DUME JEURI na UNAKATAA UGALI
iyo al saedy kuna siku nilipanda nilifika dar saa tano tumetoka mbeya stend tunafika mwanjelwa dereva anasema gari haina mafuta tukarudi tena stend kuu wakaweka mafuta tunafika mikumi katikati mafuta yakaisha tena
Happy nation ana bus moja inaenda mwanza mwisho wa reli hamna cha yutong wala nn!!inakupita uko kwenye SUV kama unatembea kwa miguu vile!!niliogopa sana
Kuna mashine moja ya Happy Nation nyuma imeandikwa "Voice of Manka". Hicho ni kisu, mwisho wa maneno. Sijajua hiyo scania engine yake ilifanywa nini. Hiyo ndo kiboko ya gari zote za Mbeya, iringa na Songea.
Juzi nimepanda hili hili Nganga la kwenye picha, dereva akasema hili scandal lilimkosa kwa bahati mbaya tu, cause na yeye alikuwa anataka afanye over-taking bahati tu akasita wenzake wote wakapita, kumbe kuna jamaa ana camera.
Aliishia kula ujiko na sifa kibao kumbe ndio wale wale
hapa yu tong ni NEW FORCE. imepitwa NGANGA nayo itaachwa. TWIGA siku hizi amefulia ana basi moja safari si kila siku. sasa hivi ABOOD anaongoza iliyokuwa inaenda Tunduma sasa imepelekwa Mbeya kukazia ligi namba zake ni 297 ATH. then linafuata TWIGA ndo HAPPY. na NGANGA. YUTONG haziwezi ligi na SCANIA hasa kwa MARCOPOLO