JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Hayo yameelezwa na baadhi ya wazazi wakati Shirika la World Vision Tanzania kupitia mradi wa Buhoma likitoa madawati 150 katika shule hizo ili kusaidia kuboresha miundombinu ya kufundishia na kujifunza na kukuza taaluma kwa wanafunzi.
Kwa upande wake Meneja wa Shirika la World Vision Tanzania Kanda ya Kigoma Mkama Nangu, amesema wataendelea kuunga juhudi za Serikali katika kusaidia watoto, ikiwemo masuala ya elimu na afya na kwamba katika bajeti ijayo wamejipanga kutoa madawati zaidi ya 700.
Awali, akipokea madawati hayo Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanal Izack Mwakisu ameagiza madawati hayo kuleta mabadiliko katika taaluma na kuhakikisha yanatunzwa ili kuhudumia Wanafunzi kwa kipindi kirefu na kuwasihi wadau wengine kuwekeza maendeleo kwa jamii ya wahitaji.
Chanzo: EATV