Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Afrika (OAU) Dk. Salim Ahmed Salim amewataka wazanzibari kushikamana katika kudai haki zao na kuacha kutumia visingizio visivyokuwa na msingi ambavyo vinaweza kuongeza joto la kisiasa na kukwamisha maendeleo ya Zanzibar.
Dk. Salim ameyasema hayo muda mfupi baada ya kuzindua kitabu kilichotungwa na Professa Thomas Burgess, Ali Sultan Issa na Maalim Seif Sharif Hamad kiitwacho Race Revolution and the Struggle for Human Rights in Zanzibar katika hafla iliyofanyika katika ukumbi mpya wa Al- Yamin Funguni Mjini Zanzibar.
Alisema tofauti za kisiasa hazina budi kuwachwa kwani zinaweza kuchangia migogoro katika nchi hali ambayo inaweza kusababisha machafuko kama nchi nyingi za Afrika ambazo zimeingia katika vita bila ya kutarajia kutokana na kushindwa kuvumiliana na kuendekeza mambo madogo madogo ambayo hayana faida kwa taifa.
Dk. Salim alisema njia moja iliyo sahihi kwa wazanzibari kabla ya kushugulikia mambo mengine ni kuungana kwa lengo la kudai haki katika muungano na kuacha kuleta visingizio ambavyo havina msingi wala nia ya kujenga mustakabali mzuri katika nchi na wananchi wake.
Kabla ya kushughulikia mambo ya msingi kwanza tuungane kwani watu wanataka haki zaidi katika muungano na tusiwasingizie watu wengine ni mambo yetu wenyewe kama hili la upemba na uunguja, tumejiingiza katika mambo ya kijinga kabisa yasiyo na msingi, wewe CCM wewe CUF hayana maana yoyote alisema Dk Salim huku akiungwa mkono na washiriki kwa kupigiwa makofi.
Dk. Salim ambaye kwa kiasi kikubwa alizungumzia umuhimu wa mshikamano miongoni mwa jamii alisema wapo baadhi ya viongozi wa Tanzania Bara ambao hawautaki muungano kama ilivyo kwa baadhi ya wazanzibari lakini alitahadharisha hali hiyo na kusema ni hatari katika dunia ya sasa.
Tufahamu katika dunia ya leo watu wanapenda tuweke mshikamano hata katika nchi kubwa tunaona wenzetu wan chi za ulaya wanavyoungana na kuunda European Union Alisema kiongozi huyo.
Alisema licha ya kuwepo dosari za msingi za hapa na pale katika muungano lakini hakuna mtu mwenye akili timamu atakayeukataa muungano kwa sasa ambapo umetimiza zaidi ya miaka 45 ambapo alisema dosari hizo zinapaswa kuzungumzwa na kupatiwa ufumbuzi ili kuwa na hali ya usalama nchini.
Katika muungano kila mtu anasema kuna kasoro lakini hilo sio kama haliwezi kuzungumzwa ni jambo la busara kwanza tuungane wenyewe na baadae tukae kulizungumza alisisitiza Dk. Salim.
Awali katika hafla hiyo washiriki walisema kumekuwepo na unafiki mkubwa kwa baadhi ya viongozi Zanzibar waliopo madarakani hali inayochangia kwa kiasi kikubwa kukosekana haki ya wazanzibari katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Washiriki hao wamesema mbali ya kuwepo usiri, woga na unafiki lakini pia baadhi ya lawama zimetupwa kwa viongozi wa Tanzania bara ambao wanaikandamiza Zanzibar kwa makusudi jambo ambalo Dk Salim alisema kwa sasa hakuna haja ya kumtafuta mchawi kwani wachawi ni wazanzibari wenyewe ambao hawataki kuleta umoja na mshikamano katika nchi yao.
Mimi ni CCM ni Seif Sharif ni CUF lakini mchango wake ni mkubwa katika nchi hii mbona tunakaa pamoja kwa nini isiwezekane kwa wengine mimi nadhani tuanzie hapa alisema Dk. Salim huku akipongezwa na washiriki.
Akizungumzia suala la uandishi wa vitabu Dk. Salim aliwapongeza walioandika kitabu hicho na kusema kwamba wakati umefika wazanzibari wenyewe kuandika historia ya nchi yao kwani baadhi ya watu wamekuwa mahodari wa kuiandika historia ya Zanzibar lakini mara nyingi wamekuwa wakipotosha baadhi ya ukweli.
Katika hatua nyengine Msaidizi wa Maalim Seif, Ismail Jussa amelelemikia kitendo kilichofanywa na mawaziri wa serikali ya mapinduzi Zanzibar na viongozi wa CCM kukataa kuhudhuria katika hafla hiyo licha ya kupewa mwaliko.
Mara nyingi mawaziri wa SMZ na CCM huwa hawataki kuhudhuria shughuli tunazowaalika wakati sisi wanapotualika tunakwenda lakini hili wanajua kabisa kuwa kitabu hiki kitazinduliwa na Dk. Salim wamekataa kuja kwa makusudi pamoja na kuwa ni kiongozi wao ndiye tuliyemualika kuwa mgeni rasmi alisema Jussa.
Katika hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi na watu mbali mbali mashuhuri wakiwemo viongozi wa vya upinzani, watu waliopigania uhuru wa Zanzibar pamoja na Nassor Hassan Moyo ambaye ana ushawishi mkubwa wa kisiasa visiwani Zanzibar.
Viongozi ambao hawakuhudhuria katika hafla hiyo ni pamoja na Naibu Waziri Kiongozi, Ali Juma Shamhuna, Waziri wa Maji, Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Saleh Ramadhan Ferouz, Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi Ali Mzee Ali, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Machano Othman Said na wengineo.
SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG
Dk. Salim ameyasema hayo muda mfupi baada ya kuzindua kitabu kilichotungwa na Professa Thomas Burgess, Ali Sultan Issa na Maalim Seif Sharif Hamad kiitwacho Race Revolution and the Struggle for Human Rights in Zanzibar katika hafla iliyofanyika katika ukumbi mpya wa Al- Yamin Funguni Mjini Zanzibar.
Alisema tofauti za kisiasa hazina budi kuwachwa kwani zinaweza kuchangia migogoro katika nchi hali ambayo inaweza kusababisha machafuko kama nchi nyingi za Afrika ambazo zimeingia katika vita bila ya kutarajia kutokana na kushindwa kuvumiliana na kuendekeza mambo madogo madogo ambayo hayana faida kwa taifa.
Dk. Salim alisema njia moja iliyo sahihi kwa wazanzibari kabla ya kushugulikia mambo mengine ni kuungana kwa lengo la kudai haki katika muungano na kuacha kuleta visingizio ambavyo havina msingi wala nia ya kujenga mustakabali mzuri katika nchi na wananchi wake.
Kabla ya kushughulikia mambo ya msingi kwanza tuungane kwani watu wanataka haki zaidi katika muungano na tusiwasingizie watu wengine ni mambo yetu wenyewe kama hili la upemba na uunguja, tumejiingiza katika mambo ya kijinga kabisa yasiyo na msingi, wewe CCM wewe CUF hayana maana yoyote alisema Dk Salim huku akiungwa mkono na washiriki kwa kupigiwa makofi.
Dk. Salim ambaye kwa kiasi kikubwa alizungumzia umuhimu wa mshikamano miongoni mwa jamii alisema wapo baadhi ya viongozi wa Tanzania Bara ambao hawautaki muungano kama ilivyo kwa baadhi ya wazanzibari lakini alitahadharisha hali hiyo na kusema ni hatari katika dunia ya sasa.
Tufahamu katika dunia ya leo watu wanapenda tuweke mshikamano hata katika nchi kubwa tunaona wenzetu wan chi za ulaya wanavyoungana na kuunda European Union Alisema kiongozi huyo.
Alisema licha ya kuwepo dosari za msingi za hapa na pale katika muungano lakini hakuna mtu mwenye akili timamu atakayeukataa muungano kwa sasa ambapo umetimiza zaidi ya miaka 45 ambapo alisema dosari hizo zinapaswa kuzungumzwa na kupatiwa ufumbuzi ili kuwa na hali ya usalama nchini.
Katika muungano kila mtu anasema kuna kasoro lakini hilo sio kama haliwezi kuzungumzwa ni jambo la busara kwanza tuungane wenyewe na baadae tukae kulizungumza alisisitiza Dk. Salim.
Awali katika hafla hiyo washiriki walisema kumekuwepo na unafiki mkubwa kwa baadhi ya viongozi Zanzibar waliopo madarakani hali inayochangia kwa kiasi kikubwa kukosekana haki ya wazanzibari katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Washiriki hao wamesema mbali ya kuwepo usiri, woga na unafiki lakini pia baadhi ya lawama zimetupwa kwa viongozi wa Tanzania bara ambao wanaikandamiza Zanzibar kwa makusudi jambo ambalo Dk Salim alisema kwa sasa hakuna haja ya kumtafuta mchawi kwani wachawi ni wazanzibari wenyewe ambao hawataki kuleta umoja na mshikamano katika nchi yao.
Mimi ni CCM ni Seif Sharif ni CUF lakini mchango wake ni mkubwa katika nchi hii mbona tunakaa pamoja kwa nini isiwezekane kwa wengine mimi nadhani tuanzie hapa alisema Dk. Salim huku akipongezwa na washiriki.
Akizungumzia suala la uandishi wa vitabu Dk. Salim aliwapongeza walioandika kitabu hicho na kusema kwamba wakati umefika wazanzibari wenyewe kuandika historia ya nchi yao kwani baadhi ya watu wamekuwa mahodari wa kuiandika historia ya Zanzibar lakini mara nyingi wamekuwa wakipotosha baadhi ya ukweli.
Katika hatua nyengine Msaidizi wa Maalim Seif, Ismail Jussa amelelemikia kitendo kilichofanywa na mawaziri wa serikali ya mapinduzi Zanzibar na viongozi wa CCM kukataa kuhudhuria katika hafla hiyo licha ya kupewa mwaliko.
Mara nyingi mawaziri wa SMZ na CCM huwa hawataki kuhudhuria shughuli tunazowaalika wakati sisi wanapotualika tunakwenda lakini hili wanajua kabisa kuwa kitabu hiki kitazinduliwa na Dk. Salim wamekataa kuja kwa makusudi pamoja na kuwa ni kiongozi wao ndiye tuliyemualika kuwa mgeni rasmi alisema Jussa.
Katika hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi na watu mbali mbali mashuhuri wakiwemo viongozi wa vya upinzani, watu waliopigania uhuru wa Zanzibar pamoja na Nassor Hassan Moyo ambaye ana ushawishi mkubwa wa kisiasa visiwani Zanzibar.
Viongozi ambao hawakuhudhuria katika hafla hiyo ni pamoja na Naibu Waziri Kiongozi, Ali Juma Shamhuna, Waziri wa Maji, Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Saleh Ramadhan Ferouz, Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi Ali Mzee Ali, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Machano Othman Said na wengineo.
SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG