Wazanzibari kuwasilisha petition UN

Wazanzibari kuwasilisha petition UN

Kuna wakati unabidi ukubali kumuachia aende,Zanzibar haijawahi kuwa muhimu kwa Tanzania bara kwa kitu chochote kile.
Wana bahar na nyinyi mnayo, hamtafuti madini, mafuta, chakula sasa si muwaache watibuane wenyewe kati ya Unguja na Pemba?
Hizi hoja sijui wanabanwa na Muungano zijibiwe kwa kuwaacha kivyao kama Sudani Kusini walivyoachwa wenyewe na hata yanayoendelea huko hayawaumizi Khartoum kabisa ila wale waliowatuma na kuwapa kiti chao UN.
Wapeni Zanzibar kisiwa chao na waambieni wafungashe kurud kwao wakajenge nchi yao huko kwani nyinyi bara mna kila kitu sasa woga wa nini? Kama mnahofia usalama hawa watu ni wepesi sana na hawawezi kuwa tishio kwa namna yoyote ile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu huu mjadala haitatokea ufanyike ,,,,,
....viapo vya marais vinawabana
" Kuulinda na kuutetea Muungano"
Pengine labda tutafsiri dhana ya kuulinda na kuutetea. Maana kilugha na maana kisheria.

Wanasheria wanaweza wakatusaidia hili.
 
Mi nawaacha na porojo zenu, kwanza ngojeni niwatafune wenye vyura nikiishiwa nguvu za kiume ndo nidai kuvunjika kwa muungano.

**Mpemba halisi**
 
Udini unawasumbua

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama Lukuvi hakuwaita wazanzibari ni maharamia kwasababu wanamini dini ya Kiislam yasingelifikia haya,Mdini ni Lukuvi na serikali yake,wazanzibar na wakristo wameishi pamoja miaka na miaka bila ya matatizo yoyote..

Ukristo umeanzia Zanzibar ndio ukafika Tanganyika,Kanisa la mwanzo kujegwa Tanzania limejengwa Zanzibar Mbweni Zanzibar
 
  1. Muungano wetu sio wa merger, yaani sio wa kuunganisha, kiasi utasema tutaumega, muungano wetu ni wa fussing, kama chemical reaction ya two chemical zika undergoes a chemical reaction na kuunda a new compound, hakuna tena process ya kuirudisha into its original forms
.

Safi sana, kumbe unakumbuka chemistry vizuri kabisa, sasa uwe unadondoshea mambo kama haya unapomuuliza mzee wetu maswali.

Tujiulize nini? Wao si wanataka kiti, kwanini wasianzie ndani
Wana VP mzanzibar, wajumbe wa NEC-CCM, Bunge n.k. mbona hawafikishi madai yao
Lini umewasikia wakijadili ndani ya baraza la wawakilishi
Ni kwasababu wanaowashwa sio "wazanzibara" bali ni wale wengine.
 
cuf bhana imetoka kwa uchaguzi haukuwa halali sasa kuna petition
Ikimalizika petition,Zanzibar inaelekea kwenye kura ya maoni kuhusu kuutaka au kuukubali Muungano chini ya usimamizi wa UN,sio ZEC,mwendo mdundo,mbele kwa mbele mpaka Zanzibar ijitoe katika makucha ya mkoloni mweusi
 
Kung'ang'ania huu muungano ni sawa na biashara kichaa. Gharama nyingi lkn mapato sifuri!
 
Achana na maneno ya kipuuzi ya lukuvi, wapewe nchi yao tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Lukuvi kawaita waislam wote wa Zanzibar ni maharamia,Lukuvi mdini,unafikiri Wazanzibar watajisikiaje,Lukuvi hajui kuwa Zanzibar kuna wakiristo ambao wengine hawana uhusiano na Tanganyika na wanaishi bila ya matatizo yoyote na Wazanzibari walio waislam

Hizi siasa za maji taka zinatengeza chuki baina ya yetu..
 
Lukuvi kawaita waislam wote wa Zanzibar ni maharamia,Lukuvi mdini,unafikiri Wazanzibar watajisikiaje,Lukuvi hajua kuwa Zanzibar kuna wakiristo ambao wengine hawana uhusuiano na Tanganyika na wananishi bila ya matatizo yoyote na Wazanzibari walio waislam

Hizi siasa za maji taka zinatengeza chuki baina ya yetu..
Kuna viongozi wengine hawajielew kabisa, kwenye hili na huyu ni mmoja wapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lukuvi kawaita waislam wote wa Zanzibar ni maharamia,Lukuvi mdini,unafikiri Wazanzibar watajisikiaje,Lukuvi hajua kuwa Zanzibar kuna wakiristo ambao wengine hawana uhusuiano na Tanganyika na wananishi bila ya matatizo yoyote na Wazanzibari walio waislam

Hizi siasa za maji taka zinatengeza chuki baina ya yetu..
Kama ni kweli basi mpuuzi
 
Wazanzibar wangeachiwa waamue wenyewe hatma ya mambo yao,wapewe Uhuru wautakao wajiendeshe wenyewe tuungane kwenye mengine,
Sent using Jamii Forums mobile app

Mama Asha Bakari (RIP) aliwahi kusema serikali ya Zanzibar ni ya mapinduzi na mapinduzi hayaondelewi kwa karatasi.
 
Hivi kwenye huu Muungano anayefaidi ni nani? Zanzibar au tanganyika? Mtoto akililuia wembe mpe.

Tuna Mambo ya kujadili kwasasa lakini sio Muungano
 
Kama ni kweli basi mpuuzi
Video iko youtube,cha kusikitisha zaidi kayaongea hayo kanisani kuwahamisha wakristo wazidi kuuangalia huu Mungano kwa jicho jingine,nafikiri kutokana na yale aliyoyasema Liukuvi angekuwa kasema mwengine kama vile kutoka vyama vya upinzani angeliambiwa mchochezi..

Chakusangaza zaidi wazanzibari wamekaa kimya na ile kauli,nasikia Lukuvi aliulizwa swali kwanini kasema maneno yale alipokwenda Oman akakataa,lakini kasau hii ni karne ya IT(Information Technology) video imezagaa youtube na na mitandao mengine ya kijamii

 
Back
Top Bottom