Wazanzibari kuwasilisha petition UN

Wazanzibari kuwasilisha petition UN

Tujiulize nini? Wao si wanataka kiti, kwanini wasianzie ndani
Wana VP mzanzibar, wajumbe wa NEC-CCM, Bunge n.k. mbona hawafikishi madai yao
Lini umewasikia wakijadili ndani ya baraza la wawakilishi
Kwanza mimi ni Mtanganyika, ninachokifahamu ni hiki kupitia historia niliyosoma kwenye makala mbalimbali na kama sipo sahihi tafadhali nirekebishe. Suala lenyewe linahusu uhusiano wa Zanzibar na Tanganyika kwenye suala linalounda dhana nzima ya Muungano wetu. Ningependa tusafiri na historia pengine inaweza ikatupa mwangaza.

Kipindi cha Abdu Jumbe Jaji Bashir Swanzy kupitia serikali ya Jumbe iliandaa hati ya mashtaka kuhoji muundo na uhalali wa Muungano kwenye mahakama maalum ya katiba ya JMT ya 1977. Lakini kwa ghafla hati hiyo ilipotea mezani kwa Abdu Jumbe na kwa kipindi hicho alikuwa ni Rais wa Znz na ilipotea kwa mazingira ya kutatanisha lakini ilionekana mikononi mwa Mwl. Nyerere. Mwalimu aliitisha kikao cha halmashauri kuu ya Taifa Dodoma, 1984 January Jumbe akabanwa kwa madai ya kutaka kuvunja Muungano. Kilichotokea ni kazi ya historia, wote tunafahamu kilichomtokea.

Mara nyingi tunaona masuala ya namna haya yakizungumzwa au kuitishwa mjadala yanayotokea yanakuwa ni historia. Sifahamu mengi ila hayo ndiyo ninayoyafahamu na pengine hiyo ndiyo imekuwa ni sababu kwa Wazanzibari kufanya hivyo, na kwa nini sisi tukose kiti UN kwa sababu Uhuru tumepata 1961 na Muungano ni 1964. Kwa nini? Au kuna kitu nakikosa juu ya hili?

Ndiyo maana swali ulilouliza juu ya Zanzibar nikakukoti na kuandika nasi tujiulize vivyo hivyo, kwa nini wamechupa kote huko na kurukia huko majuu?
 
Ndiyo maana swali ulilouliza juu ya Zanzibar nikakuti na kuandika nasi tujiulize vivyo hivyo, kwa nini wamechupa kote huko na kurukia huko majuu?
Tujiulize kitu gani ? Wangeanza hapa nyumbani tungejiuliza

Haya mambo ya hati ya muungano ni sababu zao za kila siku. Kesho utasikia wanapunjwa BoT, keshokutwa utasikia kwanini hawana Vodacom, siku nyingine kwanini hawaingizi bidhaa za uchochoro bure huku bara n.k.

Hoja yao ya kwanza ilikuwa kudhulumiwa uchumi. Hapa JF kwa miaka mingi tumeifanyinga finyanga hoja hiyo siku hizi kimyaa! Husikii maana kwa uchumi wa znz halafu uambiwe wanaibiwa , ni kicheko

Tatizo la wznz ni moja, adui yao ni Tanganyika, lakini hawajui kuwa Tanganyika ndiyo inawaweka pamoja
Ukiitoa Tanganyika katika matatizo yao, utasikia huyu kazaliwa Dodoma, huyu baba yake ni Mkuranga n.k.

Hebu jiulize kwanini walimkataa Dr Salim Ahmed Salim?
Huyu angekuwa Rais pengine angeelewa concern zao, lakini walimpiga chini
Jiulize kwanini walikataa serikali 3 bunge la katiba? Hizo ndizo zingewasaidia na leo wasingeenda UN

Jiulize kwanini Baraza la wawakilishi ni lao peke yao hawawezi kujadili hoja hadi wapeleke UN, why?
 
Mkuu mbona weshaamua zamani lakini hawasikilizwi. Watawala wao wanasema Zanzibar ikiachiliwa ni tishio kiuchumi na kiusalama. Na hili wanalisema mchana kweupe!
Nafikili nimejieleza vizuri.. Wao walisha amua ila ndio hivo watawala

mwanza kwetu
 
Imekaa poa hii nitafurahi kuona wazanzibari wakijiamulia mambo yao wenyewe

'HOW MUCH IS TOO MUCH?'
 
Tujiulize kitu gani ? Wangeanza hapa nyumbani tungejiuliza

Haya mambo ya hati ya muungano ni sababu zao za kila siku. Kesho utasikia wanapunjwa BoT, keshokutwa utasikia kwanini hawana Vodacom, siku nyingine kwanini hawaingizi bidhaa za uchochoro bure huku bara n.k.

Hoja yao ya kwanza ilikuwa kudhulumiwa uchumi. Hapa JF kwa miaka mingi tumeifanyinga finyanga hoja hiyo siku hizi kimyaa! Husikii maana kwa uchumi wa znz halafu uambiwe wanaibiwa , ni kicheko

Tatizo la wznz ni moja, adui yao ni Tanganyika, lakini hawajui kuwa Tanganyika ndiyo inawaweka pamoja
Ukiitoa Tanganyika katika matatizo yao, utasikia huyu kazaliwa Dodoma, huyu baba yake ni Mkuranga n.k.

Hebu jiulize kwanini walimkataa Dr Salim Ahmed Salim?
Huyu angekuwa Rais pengine angeelewa concern zao, lakini walimpiga chini
Jiulize kwanini walikataa serikali 3 bunge la katiba? Hizo ndizo zingewasaidia na leo wasingeenda UN

Jiulize kwanini Baraza la wawakilishi ni lao peke yao hawawezi kujadili hoja hadi wapeleke UN, why?
Brother, tusijitie upofu ilhali historia ipo wazi juu ya hili,Mara ngapi hata huku bara tukihoji Muungano kwa kupaza sauti unaingia kwenye matatizo.

Tusijitie upofu, kama madai yao ni ya msingi tuwape, kama madai yao si ya msingi tuwajibu tena kwa hoja tena huu mjadala unabidi ufanyike kwa wazi RAIA wote tuhushudie. Kwa nini tunakilazimisha hiki kisiwa? Kwa nini? Au mnaajenda ya siri? Tuambieni kama mnaajenda ya siri ili na sisi tufahamu.

Na kwa nini sisi tumekosa kiti UN mpaka tunatumia cha kwao? Tulipata Uhuru 1961 muungano ni 1964, kwa nini sisi tumekosa kiti? Nataka jawabu juu ya hili.
 
Ifike hatua tukaachie kanchi kaende kwani tuna hasara gani? Badala ya kujadili mambo ya msingi tunakaa mara oo bara wa Airtel Tigo,na Voda, sisi tuna zantel tu, ni upumbavu
Wakishinda hapa wataanza kuidai Dar es salaam, Tanga, Kilwa, na Mombasa zote zilikuwa kwao

'HOW MUCH IS TOO MUCH?'
 
Pasco umesema kweli kwa maneno. Lakini najiuliza haya uliyoyapendekeza yanawezekanaje Tanzania ya sasa na iliyopita? Hakuna BLW litakalojadiliwa kwani hii ni ajenda ya CCM. Hakutaundwa mahakama ya katiba kwani inajulikana wazi matokeo ya kuundwa kwa mahakama hiyo. Hili la kuwa Tanzania pekee ndie mwamuzi wa mwishi ndio hasa moja ya sababu kwanini Wazanzibari wanaenda UN.[

Huyo mayala ni mwongo anadanganya. Historia inatufundisha kuwa senegali na Gambia waliwahi kuwa na muungano kama wa Tz. ikafika wakti upande mmoja wakaona wanaonewa na mwsho muungano ukavunjika.

Mfano mwengine ni Kesi ya East Timor iliyokuwa sehemu ya Indonesia. Baada kelele nyingi East timor waliweza kujiondoa ktk himaya ya Indonesia kupitia UN. Na sisi tunapoleta issue za kutafuta haki na kuachnaa ukoloni wa Tanganyika tunaona uko mwanga na uchochoro wa kutokea. Hakika tutafanikiwa na njia pekee ni hiyo ya UN. Ukoloni wa tanganyika kwa znz una mwsho.
 

Huyo mayala ni mwongo anadanganya. Historia inatufundisha kuwa senegali na Gambia waliwahi kuwa na muungano kama wa Tz. ikafika wakti upande mmoja wakaona wanaonewa na mwsho muungano ukavunjika.

Mfano mwengine ni Kesi ya East Timor iliyokuwa sehemu ya Indonesia. Baada kelele nyingi East timor waliweza kujiondoa ktk himaya ya Indonesia kupitia UN. Na sisi tunapoleta issue za kutafuta haki na kuachnaa ukoloni wa Tanganyika tunaona uko mwanga na uchochoro wa kutokea. Hakika tutafanikiwa na njia pekee ni hiyo ya UN. Ukoloni wa tanganyika kwa znz una mwsho.
 
Wakishinda hapa wataanza kuidai Dar es salaam, Tanga, Kilwa, na Mombasa zote zilikuwa kwao

'HOW MUCH IS TOO MUCH?'
Hoja uliyoileta hapo juu haina mashiko na haitatokea na ikitokea ni kama wanataka kufanya kitendo cha kuvamia mipaka ya nchi huru. Kwani hii mipaka tayari ilishagawanywa na wakoloni na hiyohiyo mipaka ndiyo tuliyoipigania mpaka ikawa huru.

In short hoja yako ni mufilis.

Halafu umeandika waidai na Mombasa?! Unatania au? Hii asubuhi umeianzaje?
 
Kwanini UN na siyo Dodoma?
Iko wapi petition ya Wazanzibar iliyowakilishwa Dodoma, tukijua wana wabunge wao
Iko wapi petition iliyowasilishwa baraza la wawakilishi ikiwa ndani ya baraza ni wao peke yao

JokaKuu Mag3

Wabunge wa CCM bungeni ni vibraka wa Tanganyika. Hawana gutt ya kuitetea znz. huwaoni kuke bungeni wanatoa macho makubwa kama kuku malaya inapozungumzwa issue ya uonevu wa tanganyika dhidi ya znz? Bora CUF wanaonesha umahiri wa kiwango cha juu. Hao wabunge wa CCM wa kutoka znz wakiambiwa sasa tuwe na nchi moja wataunga mkono.
 
sioni umuhimu wa muungano zaidi ya kuibana tanganyika isipumue,wapeni kinchi chao tubaki na tanganyika yetu..ajenda za kijinga za kuimeza zbar kama hazikutimia kipindi cha giza miaka 54 iliyopita haziwezi kutimia sasa

Kwanini mnang'ang'ania?
 
Suala la Wazanzibari kuwasilisha petition kwa katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kutaka kurejeshewa kiti chake na mamlaka yake yaliyoporwa na Taifa la Tanganyika kwa kisingizio cha kuwepo kwa Muungano uliokosa misingi ya kisheria katika kuanzishwa kwake, ambapo hivi sasa suala hilo liko Mahakamani kwa kuhojiwa kisheria. petition hiyo, itawasilishwa kwa utaratibu maalumu wa kisheria za kimataifa mbele ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) ili nae aiwasilishe mbele ya baraza kuu la Umoja wa Mataifa iweze kujadiliwa kwa mujibu wa utaratibu wa baraza hilo.

Hata hivyo, wasimamizi wa suala hili wanawaomba Wazanzibari walio ndani na nje ya Zanzibar waendelee kufuatilia hatua zinazoendelea kuchukuliwa kwa misingi ya sheria za kitaifa na kimataifa ili kwa muda mfupi ujao nchi yetu irejee kuitumia haki yake ya uhuru,uwanachama wake wa kudumu UN na mamlaka yake kitaifa na kimataifa, na kuwa na ushirikiano wa kirafiki na watu na Mataifa ya jirani Tanganyika, Kenya, Uganda, Burundi, Ruwanda, Sudani na nchi zote za Umoja wa Afrika na ulimwengu mzima.

Kwa heshima ya sheria za kimataifa za ushirikiano bila ya ubaguzi wa aina yoyote, kazi hii inaendelea kufanywa na viongozi wetu wanao simamia hizi kesi, na baadhi ya wanasheria wa ndani ya Zanzibar na nje ya Zanzibar kwa manufaa ya Wazanzibari wote.
# AjendaYaZanzibar
Mmmmmhh,,,nan aliwasilisha yaan najaribu kufikiri upinzani ,serikali au nan???
 
toka zako.... huu muungano wabara ndio tunaforce utake usitake na inaonekana wazenj hawajawah ridhia huu ushenz from day 1

Paskali Mayalla wewe ni mwongo. Waambie wanajamvi East Timor ilijiondoa vipi ktk uonevu wa Indonesia kama si kupitia UN?
 
kwani lazima upinzani wafanye kila kitu?!..upinzani kazi yao kula ruzuku
Kwa ikili ya kawaida serikali inaweza Fanya kitu kama hicho ,,kiapo mojawapo cha marais wa pande zote ni kuulinda na kuuteatea muungano ,ni rais yupi atakubari jambo hilo lifanyike chini ya utawala wake ,,,,sipingi hoja ila najaribu kufir tu
 
Kwanini UN na siyo Dodoma?
Iko wapi petition ya Wazanzibar iliyowakilishwa Dodoma, tukijua wana wabunge wao
Iko wapi petition iliyowasilishwa baraza la wawakilishi ikiwa ndani ya baraza ni wao peke yao

JokaKuu Mag3
Mkuu,nafikiri unakumbuka sakata ya rasimu ya Katiba mpya nini kilitokea Dodoma,nafikiri unakumbuka uchaguzi wa raisi Zanzibar 2015,nafikiri unaona nini kinatokea katika chaguzi ndogo zinazoendelea kila siku kukicha

Dodoma hakuaminiki mkuu,Hilo kubwa lao huko Dodoma ameshasema CCM itatawala milele ....acha wazanzibari wafanye wanachofanya Mungu atawasaidia,.

Dodoma unakaribishwa wewe kashangalie Jumba la Bunge
 
Brother, tusijitie upofu ilhali historia ipo wazi juu ya hili,Mara ngapi hata huku bara tukihoji Muungano kwa kupaza sauti unaingia kwenye matatizo.

Tusijitie upofu, kama madai yao ni ya msingi tuwape, kama madai yao si ya msingi tuwajibu tena kwa hoja tena huu mjadala unabidi ufanyike kwa wazi RAIA wote tuhushudie. Kwa nini tunakilazimisha hiki kisiwa? Kwa nini? Au mnaajenda ya siri? Tuambieni kama mnaajenda ya siri ili na sisi tufahamu.

Na kwa nini sisi tumekosa kiti UN mpaka tunatumia cha kwao? Tulipata Uhuru 1961 muungano ni 1964, kwa nini sisi tumekosa kiti? Nataka jawabu juu ya hili.
Mkuu huu mjadala haitatokea ufanyike ,,,,,
....viapo vya marais vinawabana
 
Back
Top Bottom