Wazanzibar muungano tutaununua...

Wazanzibar muungano tutaununua...

Status
Not open for further replies.
Ina maana wazungu ndio waliowaita weusi washenzi na sio waarabu?.hebu rudia ukweli shenzi ilitumiwa na waarabu katika minajili yakuonyesha ujinga wa zanj people(weusi)

Eti waarabu hawakuwatesa weusi je umepata kusikia habari za zenj rebellion? Ikiwa ilitokea mnamo karne ya 8 au9 hao weusi waliokuwa kwenye mabonde ya Iraq ya sasa walizaa wapi na wameishia wapi? Washenzi walikuwa ni wa zanj ambao ni babu zetu regardless anatoka wapi.ikiwa babu yako ni mwarabu basi hakuwa mshenzi ila kama ni mweusi alikuwa mshenzi kama babu yangu mimi.

Unaishia kusema tu wapo weusi walioenda uarabuni kisha majina hakuna.mbona America inafahamika more than 14% ni blacks weusi wa uarabuni waliyeyuka?

Unapoongelea swala la shule hakuna wazee wa Tanganyika waliosoma? Shule kama ya mwambao primary school iliyokuwa inajulikana kama marien schule iliyojengwa na wajerumani huko bagamoyo haikuwafunza waafrica?


kwanza hili neno Mshenzi si la Kiarabu nitolee ushahidi mmoja kama hilo neno ni la Kiarabu.
Pili kwa mujibu wa huyo huyo W. Ingrams katika kitabu chake amesema kuwa hili neno Mshenzi ni la kiswahili na walikuwa wakiitwa watu kama wao hasa wao wazungu na mwanzo liliwakera ila baadae liliwafurahisha kwani maana yake halisi ni sifa ya mtu mweledi aliebobea (Expartriate) so sio tusi.

Ila kwa fikira za watu wengine wa zamani nilowauliza wanasema hili neno linatokana na hao wakoloni wa Kijerumani kuwaita Waafrika Schwainz yaani Nguruwe na badala yake Waafrika wakalitohoa kilahaja na kulitamka Shenzi na pengine hao hao Waafrika waliwageuzia wazungu kibao na kuwaita wao Shenzi na walipoulizwa maana wakajibu kuwa ni Ubingwa ( kwa ile kawaida ya asiejuwa maana haambiwi maana na ukila na kipofu usiumshike mkono) teh teh teh

Wakush ( Cushites) ndio wametawanyika kila upande hasa baada ya gharika Nuhu Safina ilipotua na wengine bado wako huko huko Iraq ndio wanajulikana kama Zang na ndio wengine kule Iran wanaishi katika jimbo la Shiraz na Waliokuja kusini wakafika katika bara la Africa ndio hao Afariks (Afars wa Djibouti) na Amonites (Wa Amu walisambaa katika visiwa na ukanda wa Afrika Mashariki).

Hawa Afars ndio chimbuko la wasomali, wahabeshi, wasudani, wanubi, wamasai, wapare, wachaga na watutsi na wengineo.
 
Kwanza hizo takwimu sio za wamisionary hizo ni takwimu rasmi za maofisa wa Serikali ya Himaya Uingereza-Zanzibar.

Basi hao Waafrika 300 wafungwe miyororo na waarabu 3 yaani kila mwarabau ana uwezo wa kukamata watu mia kwa pamoja na kuwafunga mmoja mmoja wengine wamekaa watoa macho wasiweze kumzidi nguvu wasubiri kungoja kufungwa minyororo na wao, hata mnyama hakubali, kweli hao waafrika walikuwa mazezeta kiasi gani hata wafae kufanywa watumwa ina maana wewe unakubali huo utafiti wa kisayansi feki waliotumia wazungu kuwa waafrika are so inferior kiasi hawakuwa na fikra hata ya kutoroka wacha kupigana na adui yao?

kuhusu waarabu imeshakueleza mmoja ni huyo ex PM wa Kuwait. Sheikh Saad Al Sabah na Mwengine ni Prince Bandar bin Sultan wa Saudia na hao wamekaa na utajiri kuliko akina Bush, Clinton na Blair. Waarabu sio kawaida yao kuanika.mambo yao uwani kama wazungu lakini hao wawili wanakutosha kwa sasa.

Na wacha kuniita mwongo nimekutolea data na taarehe na majina. Toa zako za kupinga hoja zangu.

Na nimeshakujibu sababu nikuogope nini mimi ni Muungwana nina akili timamu sina matusi kama wewe. Tafuta data za kupinga haya.

Ahsanta kwa kunisoma

watumwa wengi waliochukuliwa walikuwa ni wakiume hao wamewaoa kina nani?. wanawake wakizenj ni wengi tu walichukuliwa na waarabu na kuwaoa tena wengine hata kwa nguvu.mbona wakiume hatuwasikii? au wao hawakiwa na uwezo wakuoa?

waarabu walianza biashara ya utumwa tangu karne ya 1 kabla haijashamiri karne ya 9 had 12 hao waliobebwa zama hizo wako wapi?
 
Zanzibar kote nimetembea watanganyika wanachowanyonya wao ni kipi haswaa, waaachieni waende jamani tumechoka kero, waacheni wakapigane wenyewe kwa wenyewe, ni kipi kinachotushinda ss kukendesha kama tanganyika? naunga mkono serikali tatu na sisi tanganyika tuwe na rais, wao wana rais sisi hatuna na tuwe na bendera ya tanganyika, visiwa visiwa kitu gani kwani si tuna mbudya na bongoyo?
 
Zanzibar imehifadhiwa au umehujumiwa? Unazungumza nini iwapo kila kifanywacho na Zanzibar inakuwa tishio kwenu hivyo mnakipiga vita?

Si unataka ukweli? Kuna lazima gani ya kuwapangia Wazanzibar lazima wafuate mnachotaka nyie. Miaka 12 nyuma hivi Zanzibar ilikuwa soko la bidhaa kwa nchi zote za Afrika Mashariki. Nini mlifanya? Mliweka kila aina ya vikwazo kuzuiia jitihada zetu hadi mkafanikiwa na kuwafanya wafanyabiashara wa Zanzibar kuhamisha biashara zao Tanganyika (huku mkilalama eti ooh wameweka mitaji kwetu).
Ni mara ngapi wawekezaji wa aina mbalimbali wametaka kuwekeza Zanzibar mnapinga eti uwekezaji huo utakuathirini nyie. Mifano ni mingi kama saruji, uwanja wa ndege na mashirika ya anga.

Sasa huku unakuuita kufadhili au kudhalili?

Si uende kwenu bwana kama una nguvu pigana uikomboe nchi yako
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

Ivi all hasani mwinyi ni ametokea bara au zanzibar jibu lipo ndie alieanza kuibadilisha tanzani au mmesahau unga wa njano baada ya mwinyi kila mtu alifurai wapeni zanbr yao nyerere kawamaliza kina karume kisa nn kwa nn aliing'ang'ani zanzibar acheni ubaguzi jitu eti kina makame ...kani ndo mzanzbr peke yake ubaguzi tu na mara nyingi ni dini
 
Zanzibar imehifadhiwa au umehujumiwa? Unazungumza nini iwapo kila kifanywacho na Zanzibar inakuwa tishio kwenu hivyo mnakipiga vita?

Si unataka ukweli? Kuna lazima gani ya kuwapangia Wazanzibar lazima wafuate mnachotaka nyie. Miaka 12 nyuma hivi Zanzibar ilikuwa soko la bidhaa kwa nchi zote za Afrika Mashariki. Nini mlifanya? Mliweka kila aina ya vikwazo kuzuiia jitihada zetu hadi mkafanikiwa na kuwafanya wafanyabiashara wa Zanzibar kuhamisha biashara zao Tanganyika (huku mkilalama eti ooh wameweka mitaji kwetu).
Ni mara ngapi wawekezaji wa aina mbalimbali wametaka kuwekeza Zanzibar mnapinga eti uwekezaji huo utakuathirini nyie. Mifano ni mingi kama saruji, uwanja wa ndege na mashirika ya anga.

Sasa huku unakuuita kufadhili au kudhalili?

Ni ukosefu wa kufikiri kudhania kuwa watu milioni moja na ushee wanaweza kuwa tishio kwa watu milioni 43.
Kujilisha na kujilinda tu hamuwezi !
Try thinking better.
 
Ni ukosefu wa kufikiri kudhania kuwa watu milioni moja na ushee wanaweza kuwa tishio kwa watu milioni 43.
Kujilisha na kujilinda tu hamuwezi !
Try thinking better.

Naam iwapo muhusika ni wa kawaida lakini kwa Mtanganyika hilo si ajabu. Sasa kwanini mmebaki kinya mpaka hao 1.5 wanakukumbusheni nyie 43 kuwa kulikuwa na nchi inaitwa Tanganyika na mnalazimika kuifufua sasa?
 
Naam iwapo muhusika ni wa kawaida lakini kwa Mtanganyika hilo si ajabu. Sasa kwanini mmebaki kinya mpaka hao 1.5 wanakukumbusheni nyie 43 kuwa kulikuwa na nchi inaitwa Tanganyika na mnalazimika kuifufua sasa?
Tumevavalisha hadi nepi na sasa mna miaka 50 lakini hamkui mmedumaa.
 
Tumevavalisha hadi nepi na sasa mna miaka 50 lakini hamkui mmedumaa.

Wacha bwana, sisi tukivaa nepi wakati nyie mkivaa masulumbwete sasa nani amekuwa fundi. Hivyo huna watoto nyumbani wanaokushinda kwa mambo ya kisasa?
 
watumwa wengi waliochukuliwa walikuwa ni wakiume hao wamewaoa kina nani?. wanawake wakizenj ni wengi tu walichukuliwa na waarabu na kuwaoa tena wengine hata kwa nguvu.mbona wakiume hatuwasikii? au wao hawakiwa na uwezo wakuoa?

waarabu walianza biashara ya utumwa tangu karne ya 1 kabla haijashamiri karne ya 9 had 12 hao waliobebwa zama hizo wako wapi?

Ni ushahidi gani huo ulionao kiwa ni wanaume peke yao ndio waliochukuliwa utumwani?

Nipe reference kama waarabu walifanya utumwa kuanzia karne ya 1

Umeshindwa kuniletea data kama zangu usilete hadithi za vijiweni pls.
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

Wewe huna uzanzibari wowote!
Kwanza maneno yako na Pasco hayana tofauti!
Msukuma toka lini akajiita Makame !
 
Last edited by a moderator:
watumwa wengi waliochukuliwa walikuwa ni wakiume hao wamewaoa kina nani?. wanawake wakizenj ni wengi tu walichukuliwa na waarabu na kuwaoa tena wengine hata kwa nguvu.mbona wakiume hatuwasikii? au wao hawakiwa na uwezo wakuoa?

waarabu walianza biashara ya utumwa tangu karne ya 1 kabla haijashamiri karne ya 9 had 12 hao waliobebwa zama hizo wako wapi?

Hebu mdau tusaidie huo ushahidi wa kuwa WAARABU WALIANZA UTUMWA TOKA KARNE YA KWANZA!

Manake mi nna ushahidi kuwa walioanzisha utumwa SI WAARABU HATA KIDOGO!

Nasubiri jibu.
 
watumwa wengi waliochukuliwa walikuwa ni wakiume hao wamewaoa kina nani?. wanawake wakizenj ni wengi tu walichukuliwa na waarabu na kuwaoa tena wengine hata kwa nguvu.mbona wakiume hatuwasikii? au wao hawakiwa na uwezo wakuoa?

waarabu walianza biashara ya utumwa tangu karne ya 1 kabla haijashamiri karne ya 9 had 12 hao waliobebwa zama hizo wako wapi?


mzungu kabebwa na MTUMWA WAKE WA KIAFRIKA
attachment.php


mzungu akiwa amebebwa na mwafrika na huku kavaliswa pembe za ngombe...

 
watumwa wengi waliochukuliwa walikuwa ni wakiume hao wamewaoa kina nani?. wanawake wakizenj ni wengi tu walichukuliwa na waarabu na kuwaoa tena wengine hata kwa nguvu.mbona wakiume hatuwasikii? au wao hawakiwa na uwezo wakuoa?

waarabu walianza biashara ya utumwa tangu karne ya 1 kabla haijashamiri karne ya 9 had 12 hao waliobebwa zama hizo wako wapi?
Uzuri wa JF ukitaka kuja na kitu weka na reference siyo kutoa maneno mdomoni bila facts wala data za kutosa.

Halafu tufahamishe machifu tanganyika walikuwa wanawakusanya vipi watumwa.
 
mzungu kabebwa na MTUMWA WAKE WA KIAFRIKA
attachment.php


mzungu akiwa amebebwa na mwafrika na huku kavaliswa pembe za ngombe...

Hawa wazungu washenzi sana wanamvalisha pembe mwafrika ili aonekane kama mnyama halafu kuna matumwa ya kiakili humu eti yanasema mzungu hakufanya biashara ya utumwa.
 
Hawa wazungu washenzi sana wanamvalisha pembe mwafrika ili aonekane kama mnyama halafu kuna matumwa ya kiakili humu eti yanasema mzungu hakufanya biashara ya utumwa.

Mkuu huyo asemae hivyo basi ujue anaabudu mungu mzungu! Na hakuna kingine cha ziada..

Halafu hao waliowanya babu zetu namna hio hao hao ndio wakatuletea na dini yao!
Masikitiko makubwa sana.
 
Ni ushahidi gani huo ulionao kiwa ni wanaume peke yao ndio waliochukuliwa utumwani?

Nipe reference kama waarabu walifanya utumwa kuanzia karne ya 1

Umeshindwa kuniletea data kama zangu usilete hadithi za vijiweni pls.

Wewe ndo umeng'ang'a na vitabu vya w Ingrams bila kujua yeye anaweza kuwa driven na self emotions na akaupindisha ukweli.

Historians estimate that between
650 and 1900, 10 to 18 million
peoples were enslaved by Arab
slave traders and taken from Africa
across the Red Sea , Indian Ocean ,
and Sahara desert. [4][5][6][7] The
term Arab when used in historical
documents often represented an
ethnic term, as many of the "Arab"
slave traders, such as Tippu Tip
and others, although with distant
patrilineal descent from Arabs,
were physically indistinguishable
from the "Africans" whom they
enslaved and sold. Due to the
nature of the Arab slave trade, it
is impossible to be precise about
actual numbers.hiyo ni kwa mujibu wa vitabu vilivyokusanywa na kuusaka ukweli....

Kuhusu ushahidi juu ya watumwa waliochukuliwa unataka kusema wanaume hawakuwepo? Na ukitaka kujua iwapo waarabu walianza biashara ya utumwa lini rudi kwenye vitabu
 
Ndugu zangu ambao si wazanzibar mnaochangia uzi huu tafadhalini nawaomba kwa lugha laini mnisaidie kuwaelimisha wazanzibar wenzangu umuhimu wa huu Muungano tulionao kwetu sisi kama wazanzibar pia kama nchi.
Ndugu Makame, hilo tumelifanya sana na tunaendelea kutoa elimu tena na tena. Tatizo hao wanasiasa wenu (jamii ya Jussa Ismail) ni wagumu kusema ukweli, wanapotosha wananchi. Leo hii Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi visiwani kwa sababu wanazozijua wao, ila huku bara Mzanzibari anajenga nyumba popote anapojisikia, anamilikia mashamba popote anapojisikia na anamiliki biashara vile anavyotaka. Ingekuwa Watanganyika ni wabinafsi kama Wazanzibari sidhani kama Mpemba angeruhusiwa kumiliki shamba kule Mvomero Morogoro ama Bahi Dodoma. Sasa basi, iwao Muungano huu utafikia mwisho hivi karibuni (baada ya Tanganyika kuwepo), hizi privileges zote huenda zisiwepo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom