Wazanzibar muungano tutaununua...

Wazanzibar muungano tutaununua...

Status
Not open for further replies.
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi tafiti zinaonyesha kuwa baada ya miaka hamsini ijayo visiwa vya Pemba na Unguja vitakuwa vimemezwa na bahari. Hii pia haihitaji wageni wa nje waje wawaonyeshe bali ni nyie kufanya juhudi kidogo tu kuwauliza wazee wenu wa miaka ile na kuangalia kingo za bahari mtakuwa mmepata majibu kwa wepesi zaidi. Wanasiasa ni wajuvi wakuongea majukwaani na kusimulia uwepo wa nchi ya ahadi, msipumbazwe na masimuliza ya Singapore au Dubai angaliehistoriayenu kama taifa mtagundua ghiriba ya watawala. Katika kadhia hii ya kuitana majina yasiyo na staha je mlisha jaribu kuongelea suala la ardhi na uwiano wa watu!!!!(jinsi mnavyo zaliana), je mlisha jaribu kutafiti hisia za watanganyika juu ya maneno ya dharau na kashfa mnayo toa dhidi yao na mustakabali wa nchi hizi mara baada ya kujitenga!!!. Madai mnayoyataka ni kweli yana msingi na ni haki yenu kama taifa like kujiunga na OIC kuwa na mafungamana na nchi zingine nje ya mwamvuli wa Tanzania lakini ni nchi ngapi ni wanachama wa hizo jumuiya na wamepata hayo maendeleo mnayoyatamani?, je si kweli kwamba wanasiasa wanataka kufanya ukuwadi wa rasilimali mlizo nazo kwa hawa they so called wawekezaji!!
Tahadhari yangu kwenu ni kuwa historia haiongopi mjihadhari na kuanza kutafuta mzanzibari halisi maana mlisha anza kwenye mijadali katika mitandao ya kijamii - ref balozi Karume na comments zake - Nalikumbuka sana soko la utumwa zanzibar ila utumwa wa kifikra kwa karne hii ndo mbaya zaidi maana huyo unaye mwabudu naye anakwake na vipaumbele vyake katika suala la maendeleo na siku zote jaribu kuwa na amani na majirani zako wa karibu kuliko rafiki wa mbali kupata msaada wakati wa shida (kwa uharaka) itakuwa ni ngumu. TUZIRUHUSU FIKRA ZETU ZIFIKIRI MBALI ZAIDI KULIKO MAHITAJI YETU YA SASA maana kunawenzenu walishindwa uchaguzi na sababu walizotoa ni kwamba uwingi wa watanganyika eneo lile ndo sababu ya wao kushindwa na ndio hawa wanaopiga ngoma hii ambayo wengi tunaicheza bila kujua ni nani kamlipa mpiga zumali

So Muungano utazuia Mwenyezi asivizamishe au vipi? Hii inaonyesha wazi kuwa imani yenu kuwa kama hamuvipati kuvimeza ndani ya Muungano basi na vizame almuradi vinawakereketa matumbo yanawauma au sio? 😀😀😀
 
Tofauti ya hizo nchi ulizozitaja na Zanzibar ni kwamba Zanzibar haina cha kuhofia kuhusu kile kinachoitwa 'protection of infant industries'

Kwa hiyo hizo nchi nyingine zitabakiwa na karata ya kutumia kodi kama kinga lakini Zanzibar haitakuwa na cha kupoteza kiuchumi zaidi ya gains.
Senksi.
Lakini free port itasababisha Zanzibar kuupoteza utamaduni wake wa Kiislamu kwa kiasi kikubwa (mfano Dubai na Indonesia🙂 kitu kile kile ambacho tunakipigania sasa kwenye muungano.
 
Dunia azima ifikie mwisho kama ambavyo muumba alishapanga. Kiama ili kije ni lazima dalili zote zitime. 'laa yasta akhiruuna ssaa, walaa yastaqdimuun'
 
So Muungano utazuia Mwenyezi asivizamishe au vipi? Hii inaonyesha wazi kuwa imani yenu kuwa kama hamuvipati kuvimeza ndani ya Muungano basi na vizame almuradi vinawakereketa matumbo yanawauma au sio? 😀😀😀
Nilitarajia utajibu hoja alizotoa na sio kutoa jibu la blabla kama hili ulilotoa. Hebu jiulize mmejiandaaje kwenye suala la ardhi kama nchi ya Zanzibar.

Je, ikitokea, Serikali ya Tanganyika ikiamuru Wazenj walioko huku Bara warejee Visiwani Zanzibar, maandalizi yakoje? Mnauchumi kwa kuhimili kishindo chao hao wageni kwa muda wa walau wiki moja?

Muungano ukivunjwa, je mtawaweza kuhimili vishindo vya msongamano wa wananchi hapo visiwani? kumbuka Wazenj fecundity yenu iko juu sana!!!. Je suala la ubaguzi umeliweka vipi huko, maana isije ikawa muungano kufa zanzibar ikawa haipo ila Unguja na Pemba
 
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi tafiti zinaonyesha kuwa baada ya miaka hamsini ijayo visiwa vya Pemba na Unguja vitakuwa vimemezwa na bahari. Hii pia haihitaji wageni wa nje waje wawaonyeshe bali ni nyie kufanya juhudi kidogo tu kuwauliza wazee wenu wa miaka ile na kuangalia kingo za bahari mtakuwa mmepata majibu kwa wepesi zaidi. Wanasiasa ni wajuvi wakuongea majukwaani na kusimulia uwepo wa nchi ya ahadi, msipumbazwe na masimuliza ya Singapore au Dubai angaliehistoriayenu kama taifa mtagundua ghiriba ya watawala. Katika kadhia hii ya kuitana majina yasiyo na staha je mlisha jaribu kuongelea suala la ardhi na uwiano wa watu!!!!(jinsi mnavyo zaliana), je mlisha jaribu kutafiti hisia za watanganyika juu ya maneno ya dharau na kashfa mnayo toa dhidi yao na mustakabali wa nchi hizi mara baada ya kujitenga!!!. Madai mnayoyataka ni kweli yana msingi na ni haki yenu kama taifa like kujiunga na OIC kuwa na mafungamana na nchi zingine nje ya mwamvuli wa Tanzania lakini ni nchi ngapi ni wanachama wa hizo jumuiya na wamepata hayo maendeleo mnayoyatamani?, je si kweli kwamba wanasiasa wanataka kufanya ukuwadi wa rasilimali mlizo nazo kwa hawa they so called wawekezaji!!
Tahadhari yangu kwenu ni kuwa historia haiongopi mjihadhari na kuanza kutafuta mzanzibari halisi maana mlisha anza kwenye mijadali katika mitandao ya kijamii - ref balozi Karume na comments zake - Nalikumbuka sana soko la utumwa zanzibar ila utumwa wa kifikra kwa karne hii ndo mbaya zaidi maana huyo unaye mwabudu naye anakwake na vipaumbele vyake katika suala la maendeleo na siku zote jaribu kuwa na amani na majirani zako wa karibu kuliko rafiki wa mbali kupata msaada wakati wa shida (kwa uharaka) itakuwa ni ngumu. TUZIRUHUSU FIKRA ZETU ZIFIKIRI MBALI ZAIDI KULIKO MAHITAJI YETU YA SASA maana kunawenzenu walishindwa uchaguzi na sababu walizotoa ni kwamba uwingi wa watanganyika eneo lile ndo sababu ya wao kushindwa na ndio hawa wanaopiga ngoma hii ambayo wengi tunaicheza bila kujua ni nani kamlipa mpiga zumali

Ahsante mkuu kwa tafiti yako, ila sisi Wazanzibar hatuogopi kufaa tukifa kwenye bahari yetu wenyewe.....na kwa Wazanzibar bora tumezwe na Bahari kuliko kumezwa kwenye tumbo chafu lilojaa husda na ghilba za Watangamyika (wavimba macho) na wala hatuna wasi kwa hiloo tutafutie menginee
 
Ahsante mkuu kwa tafiti yako, ila sisi Wazanzibar hatuogopi kufaa tukifa kwenye bahari yetu wenyewe.....na kwa Wazanzibar bora tumezwe na Bahari kuliko kumezwa kwenye tumbo chafu lilojaa husda na ghilba za Watangamyika (wavimba macho) na wala hatuna wasi kwa hiloo tutafutie menginee
Wastaarabu hujenga hoja, hawatukana. Kwani ukitukana Watanganyika unapata nini cha maana katika maisha yako
 
Ningefurahi sana kama zanzibar ikiwa nchi yake inayojitegemea yenyewe bila kufungamana na tanganyika ili kila mmoja aijenge nchi yake na watu wake.sababu zanzibar awataki na aina aja yakulazimisha muungano usiyo na tija kwa zanzibar na tanganyika coz sijaona manufaa yoyote yatokanayo na muungano huhu cyo maisha kuwa bora zanzibar wala tanganyika.
 
Mapinduzi yalikuwa, kwa kiasi fulani ni kisasi dhidi ya utumwa, yaliofanywa na watu na kufanyiwa watu ambao hawahusiki na utumwa. Yasmin Alibhai-Brown
Fikra ya uzalendo ya Pan-Africanism ambayo ilikuwa ikiongozwa na hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilikuwa kila asiye Muafrika ni mgeni Afrika na kwa hiyo asiyekuwa na asili yenye kutoka bara la Afrika basi ni mgeni Zanzibar hata kama alizaliwa na alikuwa na mizizi mirefu ndani ya nchi hiyo. Na aliyekuwa ana asili ya Kiafrika na hata kama hakuzaliwa na wala hana mizizi mirefu Zanzibar basi ana haki zaidi juu ya kuitawala Zanzibar kwa sababu ni Muafrika.
Neno Afrika linatokana na neno Ifriqiya, ambayo kihistoria ilikuwa ni jimbo la Kaskazini ya Afrika katika nchi ambayo leo inajulikana kwa jina la Tunisia. Ibn Khaldun, mwanafalsafa wa historia maarufu duniani na baba wa sayansi ya jamii (sociology) aliyeishi miaka 676 nyuma, anamtaja katika kitabu chake Mfalme wa zamani wa Yemen Afriqus b. Qays b. Sayfi, ambaye aliishi wakati wa [Nabii] Musa au labda kidogo kabla yake na kuwa wanahistoria wanajisemea kuwa ndie alieivamia Ifriqiyah.1 Ibn Khaldun hakuwa anashuku kuwepo kwa mfalme kutoka Yemen ambaye akijulikana kwa jina la Afriqus ambalo inawezekana sana likawa moja wapo wa asili ya jina la Afrika. Wako wenye kusema neno Afrika linatokana na lugha ya kienyeji ya Afrika ya Kaskazini iitwayo Berber.2 Lini bara la Afrika lilianza kujulikana kwa jina la Afrika ni jambo liloanzishwa na wakoloni wa kizungu na ni suala linahohitajia kuthibitishwa kwa ushahidi wa kiutafiti.
Fikra zilizozagaa ni kwamba Zanzibar ni ya Muafrika mweusi mwenye asili ya bara peke yake kuliko Muafrika mwingine yeyote hata kama amezalika huko Zanzibar kwa daraja nyingi. Fikra hii inatokana na fikra nyengine iliyokalishwa kwenye fikra za wengi yakuwa Bara la Waafrika ni Bara la watu weusi tu, na labda tuseme la Mungu Mweusi. Na watu weusi wenyewe ni wanaotokana na asili ya Kibantu na Wabantu wenyewe wawe hawana asili au uhusiano wa karibu na Waarabu.
Na mizizi ya Waafrika ni Wabantu peke yao inalitenga kundi kubwa la Waafrika wa Afrika ya Kaskazani, Ethiopia, Somalia, Djibouti, Eritrea, Mauritius, wazungu wa Afrika Kusini, au Zimbabwe, Kenya, pamoja na Mayahudi na Wahindi wazalendo wa Afrika, na makabila yote ya kibinaadamu ambayo yana chimbuko lao Afrika.
Hapana shaka yoyote kuwa Afrika imedhulumiwa na Waafrika weusi bado hawajachukuwa dhamana ya kushiriki kwa machifu na makabila yaliyoshiriki kuwatia utumwani Waafrika wenzao. Haya yameelezwa kwa ufasaha ndani ya kitabu Zanzibar: Kinyangayiro na Utumwa na mwaka 2009 kimetoka kitabu muhimu chenye kichwa cha maneno Its Our Turn to Eat (Sasa ni Zamu Yetu Kula) ambacho kinaelezea kwa undani namna ufisadi ulivyokumbatiana na ukabila nchini Kenya.3
Historia yote na kharita (ramani) zenye kulionyesha bara la Afrika kabla halikupewa jina la Afrika huonekana kuwa haina maana. Kwa hiyo kharita za miaka ya 1860 na za nyuma sana kabla ya hapo, zenye kuonyesha eneo la Afrika Mashariki kuwa likijulikana kama ni Ethiopia au mwambao wa Azania au Sudan au Zinjibar huonekana ni dalili tosha za ushahidi wa ubeberu kabla ya Waafrika kujitawala baada ya Wazungu kulipa bara lote jina la Afrika.
Tawi la uafrika ni mtu mweusi lina mzizi mrefu katika kuyakana makabila mengine ya Kiafrika ambayo yaliwasili mwambao wa Afrika hata kabla ya kuwasili Wabantu Pwani ya Afrika ya Mashariki. Anaelezea Profesa Ibrahim Noor Shariff:
Kuna baadhi ya watu wanafikiri kuwa Waafrika wote ni Wabantu na kuwa kila asiyekuwa Mbantu ni mgeni Afrika Mashariki. Ukweli ni kuwa Wabantu ndio katika waliofika Afrika Mashariki, khasa sehemu za Pwani karibuni kabisa. Kwa mfano, Wabantu Wagiriama wamewasili Giriama Kenya kama miaka mia tatu iliyopita. (Soma kitabu cha chifu wao R. G. Ngala kiitwacho Nchi na Desturi za Wagiriama. E. A Literature Bureau. 1949. Ukurasa wa 2).4
Mohamed Said ni msomi wa kwanza kabisa aliyeweza kuweka mkono wake juu ya mpigo wa moyo wa propaganda ya TANU kuhusu suala la Ubantu na wasio Wabantu, yaani, Waislamu. Kwa mujibu wa Mohamed Said:
Katika mwaka 1955, kikundi cha TANU Bantu kiliundwa makhsusi kukabiliana na tatizo la udini kutokana na hisia za baadhi ya Waislam ndani ya TANU. Tangu kuundwa kwa TANU, kulikuwa na hisia ya kupinga Ukristo ndani ya chama. Tatizo hili la udini lilikuwa likichemka pole pole na chini kwa chini ndani ya TANU.
Ilikuwa kazi ya kikundi cha TANU Bantu kuwafichua na kuwapiga vita wanachama wa TANU waliokuwa na hisia kama hizo. Bantu ilifanikiwa sana katika hili hadi kudiriki kupiga marufuku mamkuzi ya Waislam ya Asalaam Alaikum (Amani iwe juu yako) baina ya Waislam kwa msingi kuwa ilikuwa inawabagua Wakristo na hivyo inawatengaMamkuzi yale ya Kiislam yalionekana kama yanakwenda kinyume na imani ya TANU na ilishauriwa kuwa salaam aleikum ipigwe marufuku isitumike. Ikiwa mathalan kwa kusahau Muislam mmoja atatoa salaam kwa Muislam mwenzake, kwa kawaida angejibiwa Alaikum salaam maana yake Amani iwe juu yako pia. Badala ya majibu haya mazuri, majibu yaliyobuniwa na Bantu yalikuwaAhlan tabu maana yakeah tabu tu!5
Lengo la Bantu Pan-Africanism si kuutumikiya uhakika wa historia au kuwapenda Waafrika na kuwachukiya Waarabu, bali ni kulipuuza suala zima la makabila, tamaduni, na staarabu na dini ya Kiisilamu zilizokuwepo Afrika ya Mashariki kabla ya kuwasili kwa Wabantu na khasa kwa Ukristo kutoka Ulaya. Mgeni mmoja kutoka Umoja wa Mataifa aliyekwenda kuitembeleya taasisi ya kihistoria ya kitaifa iliopo Dar es Salaam, alisikitishwa sana kuona historia ya Waarabu Tanzania imeshirikishwa na kitu kimoja tu: utumwa. Wanahistoria na wataalamu wa ilimu ya athari (archaeology) wanashindana na kuukiuka au kuuficha ukweli wowote ule wenye kuonyesha kuwa hakujakuwepo makabila yasiyo ya Kibantu Afrika ya Mashariki kabla ya kuwasili kwa Wabantu.
Ile historia ndefu ya Bahari ya Hindi yenye kuiunganisha Afrika ya Mashariki na ya Kati na Bara Arabu, Uajemi, Bara Hindi, Uchina, Misri, n.k, huwa inaonekana haina maana kwa sababu haikidhi haja na hoja za kisiasa. Au kama itatambulikana itakuwa kujengea hoja kuwa ilikuwa historia ya kibeberu iliyokuwa na kituo chake Zanzibar. Marejeo ya historia ya Afrika ya Mashariki yaliyoandikwa na akina Ibn Battuta, au Muruj al-Dhahab wa Maadin al Jawhar cha Al-Masudi, au Kilwa Chronicles iliopo jumba la makumbusho la Uingereza, hayapitiwi na wasomi wengi wa Tanganyika waliojazwa na kujaa chuki dhidi ya makabila mengine yasiyo ya Kibantu ya Afrika ya Mashariki.
Katika utangulizi wa kitabu chao Mapambano ya Ukombozi Zanzibar, B.F. Mrina na W.T. Matokke wa Chuo Kikuu cha Chama, Kivukoni, wanafafanuwa kuwa: Madhumuni ya kuandika kitabu hiki ni kujaribu kukusanya pamoja data kwa ajili ya kuweza kufundishia. Jitihada zilizofanywa zilikuwa na lengo la kupata maandishi ambayo yanaweza kutumiwa na walimu na wanafunzi katika Vyuo vya Chama Cha Mapinduzi.6
Pia katika sifa iliyopewa kitabu na kampuni ya uchapaji, Tanzania Publishing House, ni hii propaganda bila ya kizoro ambayo nainukuu kwa urefu:
CC: gombesugu Khawarizm wabara Bill Cosby
 
Last edited by a moderator:
Wastaarabu hujenga hoja, hawatukana. Kwani ukitukana Watanganyika unapata nini cha maana katika maisha yako

Kama unajali ustaarabu anza kuwafunza hao jamaa zako maana hao ndio wakuu wa matusi na kejeli kwa Wazanzibar.....sis twaendeleza
 
Kama unajali ustaarabu anza kuwafunza hao jamaa zako maana hao ndio wakuu wa matusi na kejeli kwa Wazanzibar.....sis twaendeleza

usijali wa nyumbani.wanyika wanajifanya wana wide horizon ya kuongelea mambo hata kama hajenda shule.mimi nakushauri uwaambie sentesi moja tu.wanasema zanzibar itazamishwa na maji,wewe wajibu hivi!bora zanzibar izamishwe na maji kuliko kuzamishwa na muungano.halas!
 
Ndugu makamee, usiwe na wasiwasi. Siku muungano utapovunjika ndio siku tuaiona zanzibar mpya kabisa. Kama wao walivojipanga na sisi pia tumejipanga. Mauritius, Sechelles, reunion, comoros, mauritius etc ni visiwa wenzetu ambao tumo katika bahari moja. C humi za mataifa haya ni bora kuliko uchumi wetu wakati sisi tuna rasilimali kuwaliko wao. Ha kiliopo ni ubadhirifu unao fanywa na hao wanaotetea serikali mbili. Hata pesa (fedha) zikiletwa za misaada, wao ndio wenye kuzifanyia mipango wakijenga makasri tunguuu nk.
Zanzibar iliweza kuendesha mambo yake kabla na inaweza pia kujiendeleza vizuri sana ikawa ni kioo kwa AFRIKA MASHARIKI,
 
usijali wa nyumbani.wanyika wanajifanya wana wide horizon ya kuongelea mambo hata kama hajenda shule.mimi nakushauri uwaambie sentesi moja tu.wanasema zanzibar itazamishwa na maji,wewe wajibu hivi!bora zanzibar izamishwe na maji kuliko kuzamishwa na muungano.halas!
umemaliza darasa la ngapi mpaka unapata ujasiri wa kuwaponda wenzako kuwa hawajasoma, umewahi rudi chuoni wewe baada ya kumaliza. Na kama umewahi kwenda shule/chuo basi ulienda kwenye shule ambayo walimu walikubeba kama boga, hawakukupa chakula sawasawa kama sio basi ulikuwa kiazi kisichoiva au yai viza. Maana walimu ambao ni mahili watakufundisha kuwa mstaarabu, usitukane wenzako, hata vitabu vya dini vinakataza. Soma hata hivyo upate maarifa.

Mmejiandaaje kiuchumi kuwapokea watu wakati wa exodus from Tanganyika. ardhi ipo kuhimili huo msongamano? jiulize maswali magumu, kubali majibu mazito hata kama ni machungu just take them. MSITUKANE WATANGANYIKA
 
Ngo'mbe huona thamani ya mkia wake,pale unapokatika,natamani kuona tukiuza nyanya nchi jirani ya zanzibar ,tukiuza umeme nchi jirani ya zanzibar ,tukiuza mahindi,viazi,nchi jirani ya zanzibar .
 
Kama unajali ustaarabu anza kuwafunza hao jamaa zako maana hao ndio wakuu wa matusi na kejeli kwa Wazanzibar.....sis twaendeleza
wataje walio tukana hapa, acha visingizio. Hata kama wametukana, je hilo linajustify wewe kutukana?
 
wataje walio tukana hapa, acha visingizio. Hata kama wametukana, je hilo linajustify wewe kutukana?


Vyema hivyo ulivyonena...lakini yalazim nawe pia ujiulize/uchangie objectively...kwanini wakemea tu hayo uitayo weye ati ndo "matusi" kutoka upande mmoja tu!?

Sasa hapo ndo watuonyehsa nini!?...yaani hayo matusi mangine toka kwa hao jamaa zako ndo halali na yanakubalika!?

Kama huwezi kukemea matusi kutoka pande zote...nakhis kiungwana ni bora tu ujinyamazie,au vipi Mkuu!?

Ahsanta.
 
Vyema hivyo ulivyonena...lakini yalazim nawe pia ujiulize/uchangie objectively...kwanini wakemea tu hayo uitayo weye ati ndo "matusi" kutoka upande mmoja tu!?

Sasa hapo ndo watuonyehsa nini!?...yaani hayo matusi mangine toka kwa hao jamaa zako ndo halali na yanakubalika!?

Kama huwezi kukemea matusi kutoka pande zote...nakhis kiungwana ni bora tu ujinyamazie,au vipi Mkuu!?

Ahsanta.
Kumbe mna lugha za kiungwana na staha hivi; sasa kwani kule tulikotoka mlikuwa mnaporomosha matusi. Kama lengo ni kuvunja Muungano Wazenj vunjeni tu haina shida lakini fanyeni hivyo baada ya kuhesabu gharama. Vinginevyo mtalia na kujutia sana.

TANGANYIKA YETU IRUDI TU, ILI TUHESHIMIANE MAANA NAONA ITAONDOA DHARAU ZA WATU WA ZANZIBAR ZA KUWAITA WATANGANYIKA WAKOLONI WAKATI WAO NDIYO WANAOFAIDIKA NA HUU MUUNGANO
 
Ngo'mbe huona thamani ya mkia wake,pale unapokatika,natamani kuona tukiuza nyanya nchi jirani ya zanzibar ,tukiuza umeme nchi jirani ya zanzibar ,tukiuza mahindi,viazi,nchi jirani ya zanzibar .

Sasa hapo huyo ng'ombe ndo nani!?...tartib Yakhe na lugha yako kali,fanza staha japo kiduchu!

Sie wala hatuli nyanya...twatumia tungule!

Sie hatuli wala hatuna asili ya kutumia mahindi...labda tu kwa dharura!!

Sie wala hatutumii viazi...twatumia mbatata tena kiduchu tu kwenye urojo!? Teeh! Teeh! Teeh!

Nitakurejea tena kuhusu hilo suala lako la ati kutuuzia huo umeme...lakini nakukumbusha tu yakuwa hilo suala/topic ni ndefu mno!

Nakhis Watanganyikwa wengi mno mnaishi kwa hadaa za hao Viongozi wenu...maana nyie mumezoea kuambiwa urongo/kudanganywa kama vile wakti wa enzi za "Mwalimu" aka "Baba wa Taifa"! Dah!

Hivi Mkuu,wewe kwa akili yako yoote na maarifa yako kiduchu ulonayo...yaani unaamini yakuwa ati SMZ/Wazanzibary maisha yao takriban yoote katika huo ati ndo muitao Muungano,yakuwa wanaishi bure mpaka kufikia wasaidiwe Bills za umeme na hiyo Tanganyikwa!? Duh!

Kwanza kwa pesa/senti zipi ilokua nazo hiyo Tanganyikwa mpaka iweze ku-afford zigo loote hilo!? Teeh! Teeh! Teeeh!

Pili,hiyo Tanganyikwa muizungumzayo iwapi,au ndo imebaki nchi tu ya kufikirika kwenye vichwa/bongo zenu kama katika ile Lila na Fila ya Sheikh Shaaban Robert!?

Nyinyi Watanganyikwa...wakti mkila pumba za kulisha farasi/dona la njano,mkifulia na kukogea harita,mkitembea m.a.t.a.k.o nje na wangine wakionyesha tupu zao hadhwarani kwa ukosefu wa mavazi/lebasi,mkivaa mipira michakavu ya motokari/makatambuga...hivi umeshawahi/mmeshawahi kujiuliza ni misaada mingapi mliokua mkipata wakti huo kutoka kwa Serikali ya Zanzibar na hata Wazanzibary wa kawaida tu!?

Wafahamu wakti huo sisi pale Unguja tulikua na aina takriban sabaa za mchele tena kutoka nchi tafauti duniani zenye kusifika kwa kilimo cha mpunga!...na nyie mlikua mkipawa hata pumba za malisho ya farasi kwa ration tena kiduchu mno!! Dah!

Sasa wee kweli una maarifa japo ya kuazima!?...ati kuja hapa hadhwarani kutishia Wazanzibary kwa hayo mahindi yenu machafu/low grade na viazi vilojaa wadudu,na zile nyanya mbovu za pale Ilula na Mkuzi!? Teeh! Teeh! Teeh!

Kadai Tanganyikwa yenu kwanza...khalaf ndo urejee hapa jamvini kwa hizo tashtit zako za kitoto!?

Au Mkuu ulikua tu watakafurahisha hili jamvi kwa mas'khara kiduchu!? Teeh! Teeh! Teeh!

Ahsanta.
 
Kumbe mna lugha za kiungwana na staha hivi; sasa kwani kule tulikotoka mlikuwa mnaporomosha matusi. Kama lengo ni kuvunja Muungano Wazenj vunjeni tu haina shida lakini fanyeni hivyo baada ya kuhesabu gharama. Vinginevyo mtalia na kujutia sana.

TANGANYIKA YETU IRUDI TU, ILI TUHESHIMIANE MAANA NAONA ITAONDOA DHARAU ZA WATU WA ZANZIBAR ZA KUWAITA WATANGANYIKA WAKOLONI WAKATI WAO NDIYO WANAOFAIDIKA NA HUU MUUNGANO


Mkuu,

Tafadhali acha kuijitoa fahamu na maarifa kiduchu ulonayo!

Usianze kunichanganyia mada/Topics...mie huwa sian dasturi ya kupoteza fursa/wakti wangu adilifu kwa malumbano yaso tija!

Mie nalizungumzia kiduchu,kuhusu weye kukemea hayo uloita ati ndo matusi!

Nikakwambia yakuwa je mbona wakemea tu upande mmoja na hao jamaa zako wawaacha huwakanyi asilan!?

Nikakuuliza tena...au hujayaona hayo matusi walotukuna hao jamaa zako pia,tena panapo takriban kila thread humu-JF!

Weye umo na unaonekana kila mara humu-JF...sasa kipi kikufanzacho usikemee japo kiduchu yale matusi na kashfa toka kwa hao jamaa zako!?

Sasa hapo kwenye hiyo bayana yako ati unadai yakuwa...sisi tunaporomosha matusi tangia huko tulipotoka!? Ndo wapi huko!? Au unazungumzia tangia mlipotufanzia yale mauaji ya ile 1964!?

Sasa hapo kweli bado pia watulaumu Mkuu!?...yaani mpaka nyie mmekuja nchini mwetu na kututoa roho tena kwa mahalaiki,si kutukana kiduchu kwa kujitetea ndo iwe kwako/kwenu ati ghadhabu!? Acha hizo weye!

Au weye Mkuu Mwakaboko ni mfuasi wa Chadema...maana nakhis una elemets fulani za hypocricy!? Teeh! Teeh! Teeh!

Shukran kwa kunisikiza japo kiduchu!

Ahsanta.
 
......Au weye Mkuu Mwakaboko ni mfuasi wa Chadema...maana nakhis una elemets fulani za hypocricy!? Teeh! Teeh! Teeh!

Shukran kwa kunisikiza japo kiduchu!

Ahsanta.
Mbona tulikotoka nimekwambia kuwa nimekuelewa, sasa wewe hujaelewa nini? nikueleweshe

Ila naomba usivishe uanachama wa vyama, maana hiyo huwa naiona kama ni auguement ya watu waliofirisika kiakili, kusingizia CHADEMA wakati tatizo liko wazi. Unataka kusema kuwa CDM ndiyo waliowatuma wale Wazenj wawatukane Watanganyika. Usiwe kama wale jamaa ambao wanasema CHADEMA ni tatizo katika nchi wakati matatizo katka nchi hii hayana uhusiano na CHADEMA

acha kusingizia vyama kwa sababu ya kuwa na mtazamo tofauti na wewe. But you are at liberty to remain in the union or take your own way, lakini muhesabu gharama kabla ya kuondoka vinginevyo mtajutia!!!!
 
Mbona tulikotoka nimekwambia kuwa nimekuelewa, sasa wewe hujaelewa nini? nikueleweshe

Ila naomba usivishe uanachama wa vyama, maana hiyo huwa naiona kama ni auguement ya watu waliofirisika kiakili, kusingizia CHADEMA wakati tatizo liko wazi. Unataka kusema kuwa CDM ndiyo waliowatuma wale Wazenj wawatukane Watanganyika. Usiwe kama wale jamaa ambao wanasema CHADEMA ni tatizo katika nchi wakati matatizo katka nchi hii hayana uhusiano na CHADEMA

acha kusingizia vyama kwa sababu ya kuwa na mtazamo tofauti na wewe. But you are at liberty to remain in the union or take your own way, lakini muhesabu gharama kabla ya kuondoka vinginevyo mtajutia!!!!



Duh! Teeh! Teeh! Teeh!

Mkuu,yaani hili povu looote limekutoka na tashtit nyingi mno,sababu ya kutajiwa hiyo Chadema yako tu!? Teeh! Teeh! Teeh!

Kwani mtu kuwa mfuasi/Msukule wa Chadema ni aibu Mkuu!?...mbona unaleta dasturi kama za yule mlevi wa Chang'aa aka Nicholas!? Teeh! Teeh! Teeh!

Acha hizo tishatoto weye! Hivi kweli unaamini hayo uandikayo au unaamua tu kuwafurahisha wenzio!?

Sasa wewe unatishia-nyau Wazanzibary...lakini nasikia majuzi tu Chama chako Chadema ati kimetangaza nafasi ya kazi(ndio! yaani moja tu,kwa Wazanzibary population of over just a million!? Duh!). Chadema bana! Teeh! Teeh!

Sasa mbona mwatuchanganya nyinyi Watanga-nyikwa!? Teeh! Teeh! Teeh!

Ahsanta.

CC;Ritz,Mzito Kabwela
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom