Wazanzibar muungano tutaununua...

Wazanzibar muungano tutaununua...

Status
Not open for further replies.
hapa umeichanganya historia.waarabu walianza kuja pwani ya east Africa kabla karne ya 5-7 kwa misingi ya biashara na si kuongoza ni kweli yawezekana kulikuwa na watu Zanzibar ila walikuwa wachache nao walitoka bara(sio Tanganyika pekee).mreno alikanyaga pwani ya kilwa karne ya 15 tena mwishoni na alikuta mwarabu akiendesha biashara ikiwemo utumwa katika ukanda huu.pengine unaweza ukajiuliza jambo dogo kwann mwarabu aliitawala sana Zanzibar tofauti na pwani ya bara? jibu ni dogo nani kama la mchangiaji niliyemnukuu visiwa hivi havikuwa na idadi kubwa ya watu hivyo kuwa summon na kuwa rule likawajambo rahisi.utumwa ulichangia kuweka idadi ya weusi kuongezeka ndani ya visiwa hivi.jamii yote ni moja ila imetenganishwa na mazingira.na wareno hawakutawala kwa miaka 500 hilo ni hapana walitawal kwa takriban karne 2 kisha waarabu mwishoni mwa karne ya 18 wakawatoa kwenye miji ya pwani za Zanzibar,kilwa na Mombasa.kwa wakati huo ukoloni haukuwa unatambulika kwenye maskio ya watu weusi na ile dhana ya kuwa weupe ni watu waliobarikiwa iliganda kweny vichwa vya wazee wetu.bado ukweli ni kama ule aliousema ndugu yangu hapo juu watu wa visiwa hivi ni zao la mchanganyiko wa watu wa bara.kuna wanyamwezi wengi tu Zanzibar na sio rahisi kumtambua mpaka akupe mwenyrwe ukweli

Mkuu naona umechanganya historia hapo..viziwa vya zanzibar hata Vasco Dagama amepita kuweka maji na kununu mali nyengine kwenye safari yake ya India,kuwepo na wenyeji kidogo hakufanyi kuwa hakukuwepo na wenyeji katika hivyo visiwa,wareno walishindwa kuweka makaazi katika hiyo miaka 500 kwasababu wenyeji walikuwa hawasikilizani na wareno tafauti kubwa labda dini,sasa ujiulize hawa wenyeji walikuwa wameshakuwa na dini ya kiislam huu Uislam kauleta nani hapo ,hapo ndio linakuja jibu lako kuwa warabu waliwahi kufika zanzibar kabla wareno lakini wao walikuwa wanafanya biashara zao na kupita.

Mwarabu alianza kutawala Kilwa,makao makuu yake yalikuwa kilwa kabla ya kuitwa kuisaida zanzibar kuwaondoa wareno,Kuhusu Watumwa walikuwa wanapita tu zanzibar baada ya kuuzwa kwa mnanda kwenye soko na mkunazini walisafirishwa na kupelekwa nchi za mbali,sioni hii kama inachangia kuwepo kwa watu wengi weusi hapo zanizibar.

Wanyamwezi, waliletwa na mwarabu kwani wanyamwezi walikuwa wafanyakazi wazuri na waaminifu kwa warabu hasa wakati mwarabu anaenda safari za ndani ya afrika kutafuta meno ya temba na watumwa na vitu vyengine

Wamanyema wameletwa na waraabu hili kabila lilipendwa sana na mwarabu wanawake wa kimanyema ndio waliokuwa wameolewa katika koo za kisulatani na wengi wao ndio waliokuwa wakifanya kazi za ndani katika nyumba za sultan

Sasa kuna kabila kama la kizaramo ambao vile vile wako wengi hapo zanzibar,hili kabila unaweza kwenda nyuma zaidi wakati wa Mwinyi Mkuu ambae mwarabu alimuhamisha kutoka shangani na kumepleka Bambi kama sikosei

Kwa matiki hiyo uataona kuwa wenyeji wa zanzibar kama walikuwa kidogo au wingi walikua ni makabila ya pwani ya afrika mashariki wagunya,wazaramo,wadigo,wasegeju.......haya makabila yalikuwa na utamaduni wakulala "dago" wakati wakienda kuvua sehemu za mbali,makabila mengine kama wanyamwezi,wamanyema na makabila ya mbali ya afrika ndio hao waliokuwa wakitwa wageni ijapokuwa walikuwa ni watu weusi...

Waswahili wa zanzibar walienda bega kwa bega na warabu wa Oman watu kama akina TipTip walikuwa waswahili wanafanya vitu sawa sawa na mwarabu na ndio maana wakathubuti kuwaia wawasaidie kumtoa Mreno na ndio maana wakawachia Warabu watawale nchi hii.

Kutoka na historia ya Zanzibar sioni kama Sultan alikuwa mkoloni kama propaganda za siasa zinavyosema,Ukiangalia picha za Sultani wa zanzibar utaona kuwa hawa jamaa ni warabu waliochanganya na watu wa makabila ya waafrika,yaani hawana tafauti kisura na akina Salim Moh'd Salim,Seif Shariff au Aman karume na hizo ndio sura za Visiwani,lamu,Mombasa,kismayu sura za watu wa pwani ya africa mashariki

source bibi yangu 🙂
 
Ndio Tofauti, Kwani visiwa vya Mafia, Kilwa Kisiwani, Songosongo, Nyuni, Kibaazi na Ukerewe viko Zanzibar au sio? Teh teh teh

Ha Ha Ha , kwa hiyo viko Zanzibar? amka usiote ndoto ya mchana. Mnajidai kuanza kuhaha baada ya kuona tumekazana na kutaka nchi yetu mnaanza kuleta issues nyingine zisizo na msingi. Chamuhimu kilka mmoja awe na nchi yake na wabara warudi bara kwao na wanzanzibari warudi kwao period!
 
Ha Ha Ha , kwa hiyo viko Zanzibar? amka usiote ndoto ya mchana. Mnajidai kuanza kuhaha baada ya kuona tumekazana na kutaka nchi yetu mnaanza kuleta issues nyingine zisizo na msingi. Chamuhimu kilka mmoja awe na nchi yake na wabara warudi bara kwao na wanzanzibari warudi kwao period!

Sasa basi ndio maana tukawadaia katika Rasimu 2 kuwa lazima nchi yenu ya Tanganyika irudi, sio mujibadishe jina eti Tanzania Bara, msituletee misamiati hapa!!!😡
 
hiyo ZNZ unazungumzia ndio ile ya Sultani?unazungumzia bendera ya Sultan?wala usihofu,mutaipata tu na Sultan wenu atarudi,sasa hivi tunahakikisha tunawasaidieni mpate nchi yenu!na hii katiba ya serikali tatu hatutaki,tunataka serikali moja ya Tanganyika!Suala la uraia wa nchi mbili pia hatulitaki!ngoja kura ya maoni ije,tutawasaidia mpate nchi yenu mpumuwee!

Msichukie Waarabu waliokuwa hawakuwadharau kama hao mabwana.zenu wazungu mnaowapapatikia hebu soma hapa:

Bristol & Transatlantiska
Itikadi ya ubaguzi wa Rangi

Kadiri biashara ya watumwa ilivyoendelea, Wazungu walianzisha itikadi ya ubaguzi wa rangi ambayo inaweza kutumika kuhalalisha hiyo biashara.
Waafrika walikuwa walidhaniwa kuwa daraja la chini ya binadamu, wasio na ustaarabu, na watu duni mbele ya Wazungu katika kila hali. Na kuwa wao watu weusi walikuwa yaani 'si miongoni mwao' (wakisema "not one of us"), walikuwa ni kama bidhaa wanaweza kununuliwa na kuuzwa. Maendeleo ya ubaguzi wa rangi yanahusishwa na biashara ya watumwa.

Biashara ya watumwa isingaliendela bila ya itikadi hii kutumika ili kuihalalisha.

Ubaguzi wa rangi hauwezi kupuuzwa katika utafiti wowote biashara ya utumwa.

Wa Anglikana kwao rangi nyeusi ilishabihishwa na mauti na uovu kwa karne na dahari, kabla ya kukutana watu wowote weusi. Hivyo muonyo wao wa kwanza kwa watu wenye ngozi nyeusi ilikuwa kudhani kwamba walikuwa baadhi aina ya shetani au mnyama wa kutisha. Kutokana na dhana hii mbovu, na kutokana na hadithi za wasafiri ', ukazuka ubaguzi wa wa-Afrika, kama washenzi, kuwa ni wepesi kwa mifadhaiko ya ngono, wavivu, wasioaminika na walaji nyama nyama (cannibalistic). Kulikuwa na watu wachache ambao walipinga mtazamo huu wa kibaguzi. Richard Ligon, katika kitabu Chake Historia ya Kweli na Halisi ya Kisiwa cha Barbados, kilicho chapishwa katika 1657, aliandika dhidi ya dhana hiyo mashuhuri. Yeye aliamini 'kwamba waaminifu, wenye imani (faithfull) na miongoni mwao kuna watu wenye utambuzi, kama miongoni mwa wale wa Ulaya.

Na kutoka mwaka 1600, na maendeleo ya kisayansi kuzidi katika Ulaya, ubaguzi wa rangi nao 'ulithibitishwa' (kuhalalishwa) kisayansi. Wanasayansi na wana falsafa kama David Hume alidiriki kusema ya kuwa Waafrika walikuwa 'kijinsia ni watu duni kwa wazungu'. Iliaminika zaidi kwamba Waafrika na Wazungu walikuwa na Maendeleo tofauti.
Wengi, kama Sir Thomas Herbert, kuandika katika 1634, waliamini kuwa Waafrika lazima wanahusiana na nyani na walikuwa tofauti na kabila duni. Hii ilikuwa muda mrefu kabla nadharia ya Charles Darwin ya Mageuzi (Evolution), ambayo ilionyesha kuwa binadamu wote asili yao ni moja (Nyani). Katika kipindi cha karne ya 18 na 19, watu wengi weupe walipiga kampeni kwa ajili ya kusitisha biashara ya watumwa na Uhuru wa watumwa. Lakini ni watu weupe wachache tu waliamini katika usawa watu wote, kwamba ni usawa kati ya Jamii ya weusi na weupe.

Katika karne ya 19, itikadi ya ubaguzi wa rangi ilipewa nguvu sayansi 'fake' kama hii phrenology. Iliaminika kwamba sura na umbo la fuvu ndio linaashiria tabia ya mtu. Phrenologists walitumia nadharia yao juu fuvu la Mwafrika na kujumuisha Waafrika Wote kama ni Duni kwa Jamii nyeupe kielimu, kiutamaduni na kimaadili. Phrenology ilionyesha Waafrika kuwa unsuited kufanya Kazi Nyingine Zaidi ya kwamba inasimamiwa na watu weupe. Katika Mawazo ya wengi wao, hii iliwapa haki ya kuwafanya Waafrika kuwa watumwa.

Utafiti wa teleology unalenga katika Ubunifu Asilia (design in nature). Hii iliwapa wazungu haki ya kusema kuwa Waafrika walikuwa, kiasili, wanafaa kwa kufanya Kazi za nguvu lakini si za kufikiri na za ujuzi. Walikuwa, wameumbwa kuwatumikia watu weupe. "Negro kama (wanavyowaita) kwa ujumla alizaliwa awe Mtumwa" aliandika Sir Harry Johnston, Mkoloni wa Kiingereza katika Afrika katika miaka ya 1890.

Anthropology, utafiti wa watu, katika mambo mengine ulikita katika uchunguzi wa ukubwa wa ubongo na maumbile ya kimwili ya watu. Anthropologists nao walithubutu kuhitimisha kwamba wa Afrika walikuwa ni watu Duni kuliko Wazungu, Aina tofauti ya watu yenye ukaribu zaidi kuhusiana nyani kuliko wazungu.

Naturalist wa Kiingereza, Charles Darwin, akaanzisha ya nadharia ya Mageuzi [Evolution] Nadharia yake alipendekeza kuwa Wazungu walikuwa wanahusiana na Waafrika na kwamba binadamu Wote walikuwa wanahusiana na nyani. Wakati hii ilitoa kero kwa ile anthropological theory kuhusu aina tofauti na anwaa za maumbile, Mambo mengine ya nadharia ya mabadiliko bado 'yalithibitisha' ubora wa Jamii nyeupe Juu ya Jamii za wengine Wote. Nadharia yake aliona kuwa Anglo-Saxon, yaani, British, wako daraja ya juu katika kipimo cha mabadiliko [Evolutionary Scale]. Yaani Waingereza walikuwa Juu ya Mti wa Familia ya Wanadamu, zaidi 'kistaarabu' [Most Civilized Race]. Wafrika, as 'primitive' race, wailionekana kuwa kama watoto wachanga na unintelligent. Jamii 'Duni' waliokuwa wamepotea aidha ili watawaliwe au kuangamizwa na Jamii 'Bora'. Maisha ya Mwenye Nguvu Mpishe (Survival of fittest theory) ilikuwa ni sheria katika nadharia ya Darwin ya Mageuzi.

Imani katika Ubwanyenye wa Jamii ya watu Weupe Uingereza na Ulaya ndio ulihuisha upanuzi wa himaya (Empire). Himaya ya Uingereza iliongezeka wa Kutoka Wazo 'kwamba Uingereza walikuwa Kabila Bora la Utawala wa Dunia', maoni yaliyotolewa na Cecil Rhodes, mtawala wa kikoloni ambaye alianzisha koloni ya Uingereza
ya Rhodesia, katika Afrika (Sasa Zimbabwe).

Hizi nadharia za 'kisayansi' nadharia za duni wa Muafrika kwa ujumla ulikubalika na wananchi wa Uingereza. Ubaguzi wa rangi ilikuwa kuchukuliwa kirahisi kama jambo la.kawaida. Kwa mfano, vitabu vya GA Henty vilikuwa vikionekana kama vya umuhimu mkubwa kwa ajili wavulana. Kitabu chake "By Sheer Pluck": Hadithi ya. Vita vya Ashanti kiliandikwa Mwaka 1884 na pengine bado inapatikana katika Maktaba za SHULE Hadi katikati ya karne ya 20 wavulana wanasoma hicho kitabu hujifunza kuwa watu weusi ni 'KAMA Watoto tu. Wao Siku zote ama wanacheka tu au kufanya kugombana. Wao naturally ni wazuri wenye shauku (passionate), goigoi, lakini wenye juhudi ya kazi ngumu kwa muda tu; wajanja hadi hatua fulani, wajinga sana kupita maelezo... Wao hawana uhalisi, kabisa hawana uwezo wa Uvumbuzi (they are absolutely without originality, absolutely without inventive power)

Watu weusi wanaoishi nchini Uingereza, pamoja na wale wanaoishi katika nchi zao wenyewe Chini ya tawala za Ukoloni wa Ulaya, walikuwa lazima wakabiliane na ubaguzi huu. Ubaguzi wa rangi imekuwa ni kitovu cha mazoea kwa watu weusi katika Uingereza, kwa karne nyingi zilizopita.

Makala-Kwa hisani ya Peter Fryer na uchunguzi Juu ya Historia ya watu weusi nchini Uingereza katika kitabu chake "Staying in Power" (Kubaki Madarakani)
 
Msichukie Waarabu waliokuwa hawakuwadharau kama hao mabwana.zenu wazungu mnaowapapatikia hebu soma hapa:

Bristol & Transatlantiska
Itikadi ya ubaguzi wa Rangi

Kadiri biashara ya watumwa ilivyoendelea, Wazungu walianzisha itikadi ya ubaguzi wa rangi ambayo inaweza kutumika kuhalalisha hiyo biashara.
Waafrika walikuwa walidhaniwa kuwa daraja la chini ya binadamu, wasio na ustaarabu, na watu duni mbele ya Wazungu katika kila hali. Na kuwa wao watu weusi walikuwa yaani 'si miongoni mwao' (wakisema "not one of us"), walikuwa ni kama bidhaa wanaweza kununuliwa na kuuzwa. Maendeleo ya ubaguzi wa rangi yanahusishwa na biashara ya watumwa.

Biashara ya watumwa isingaliendela bila ya itikadi hii kutumika ili kuihalalisha.

Ubaguzi wa rangi hauwezi kupuuzwa katika utafiti wowote biashara ya utumwa.

Wa Anglikana kwao rangi nyeusi ilishabihishwa na mauti na uovu kwa karne na dahari, kabla ya kukutana watu wowote weusi. Hivyo muonyo wao wa kwanza kwa watu wenye ngozi nyeusi ilikuwa kudhani kwamba walikuwa baadhi aina ya shetani au mnyama wa kutisha. Kutokana na dhana hii mbovu, na kutokana na hadithi za wasafiri ', ukazuka ubaguzi wa wa-Afrika, kama washenzi, kuwa ni wepesi kwa mifadhaiko ya ngono, wavivu, wasioaminika na walaji nyama nyama (cannibalistic). Kulikuwa na watu wachache ambao walipinga mtazamo huu wa kibaguzi. Richard Ligon, katika kitabu Chake Historia ya Kweli na Halisi ya Kisiwa cha Barbados, kilicho chapishwa katika 1657, aliandika dhidi ya dhana hiyo mashuhuri. Yeye aliamini 'kwamba waaminifu, wenye imani (faithfull) na miongoni mwao kuna watu wenye utambuzi, kama miongoni mwa wale wa Ulaya.

Na kutoka mwaka 1600, na maendeleo ya kisayansi kuzidi katika Ulaya, ubaguzi wa rangi nao 'ulithibitishwa' (kuhalalishwa) kisayansi. Wanasayansi na wana falsafa kama David Hume alidiriki kusema ya kuwa Waafrika walikuwa 'kijinsia ni watu duni kwa wazungu'. Iliaminika zaidi kwamba Waafrika na Wazungu walikuwa na Maendeleo tofauti.
Wengi, kama Sir Thomas Herbert, kuandika katika 1634, waliamini kuwa Waafrika lazima wanahusiana na nyani na walikuwa tofauti na kabila duni. Hii ilikuwa muda mrefu kabla nadharia ya Charles Darwin ya Mageuzi (Evolution), ambayo ilionyesha kuwa binadamu wote asili yao ni moja (Nyani). Katika kipindi cha karne ya 18 na 19, watu wengi weupe walipiga kampeni kwa ajili ya kusitisha biashara ya watumwa na Uhuru wa watumwa. Lakini ni watu weupe wachache tu waliamini katika usawa watu wote, kwamba ni usawa kati ya Jamii ya weusi na weupe.

Katika karne ya 19, itikadi ya ubaguzi wa rangi ilipewa nguvu sayansi 'fake' kama hii phrenology. Iliaminika kwamba sura na umbo la fuvu ndio linaashiria tabia ya mtu. Phrenologists walitumia nadharia yao juu fuvu la Mwafrika na kujumuisha Waafrika Wote kama ni Duni kwa Jamii nyeupe kielimu, kiutamaduni na kimaadili. Phrenology ilionyesha Waafrika kuwa unsuited kufanya Kazi Nyingine Zaidi ya kwamba inasimamiwa na watu weupe. Katika Mawazo ya wengi wao, hii iliwapa haki ya kuwafanya Waafrika kuwa watumwa.

Utafiti wa teleology unalenga katika Ubunifu Asilia (design in nature). Hii iliwapa wazungu haki ya kusema kuwa Waafrika walikuwa, kiasili, wanafaa kwa kufanya Kazi za nguvu lakini si za kufikiri na za ujuzi. Walikuwa, wameumbwa kuwatumikia watu weupe. "Negro kama (wanavyowaita) kwa ujumla alizaliwa awe Mtumwa" aliandika Sir Harry Johnston, Mkoloni wa Kiingereza katika Afrika katika miaka ya 1890.

Anthropology, utafiti wa watu, katika mambo mengine ulikita katika uchunguzi wa ukubwa wa ubongo na maumbile ya kimwili ya watu. Anthropologists nao walithubutu kuhitimisha kwamba wa Afrika walikuwa ni watu Duni kuliko Wazungu, Aina tofauti ya watu yenye ukaribu zaidi kuhusiana nyani kuliko wazungu.

Naturalist wa Kiingereza, Charles Darwin, akaanzisha ya nadharia ya Mageuzi [Evolution] Nadharia yake alipendekeza kuwa Wazungu walikuwa wanahusiana na Waafrika na kwamba binadamu Wote walikuwa wanahusiana na nyani. Wakati hii ilitoa kero kwa ile anthropological theory kuhusu aina tofauti na anwaa za maumbile, Mambo mengine ya nadharia ya mabadiliko bado 'yalithibitisha' ubora wa Jamii nyeupe Juu ya Jamii za wengine Wote. Nadharia yake aliona kuwa Anglo-Saxon, yaani, British, wako daraja ya juu katika kipimo cha mabadiliko [Evolutionary Scale]. Yaani Waingereza walikuwa Juu ya Mti wa Familia ya Wanadamu, zaidi 'kistaarabu' [Most Civilized Race]. Wafrika, as 'primitive' race, wailionekana kuwa kama watoto wachanga na unintelligent. Jamii 'Duni' waliokuwa wamepotea aidha ili watawaliwe au kuangamizwa Jamii 'Bora'. Maisha ya Mwenye Nguvu Mpishe (Survival of fittest theory) ilikuwa ni sheria katika nadharia ya Darwin ya Mageuzi.

Imani katika Ubwanyenye wa Jamii ya watu Weupe Uingereza na Ulaya ndio ulihuisha upanuzi wa himaya (Empire). Himaya ya Uingereza iliongezeka wa Kutoka Wazo 'kwamba Uingereza walikuwa Kabila Bora la Utawala wa Dunia', maoni yaliyotolewa na Cecil Rhodes, mtawala wa kikoloni ambaye alianzisha koloni ya Uingereza
ya Rhodesia, katika Afrika (Sasa Zimbabwe).

Hizi nadharia za 'kisayansi' nadharia za duni wa Muafrika kwa ujumla ulikubalika na wananchi wa Uingereza. Ubaguzi wa rangi ilikuwa kuchukuliwa kirahisi kama jambo la.kawaida. Kwa mfano, vitabu vya GA Henty vilikuwa vikionekana kama vya umuhimu mkubwa kwa ajili wavulana. Kitabu chake "By Sheer Pluck": Hadithi ya. Vita vya Ashanti kiliandikwa Mwaka 1884 na pengine bado inapatikana katika Maktaba za SHULE Hadi katikati ya karne ya 20. wavulana wanasoma hicho hujifunza kuwa watu weusi ni 'KAMA Watoto tu. Wao Siku zote ama wanacheka tu au kufanya kugombana. Wao naturally ni wazuri wenye shauku (passionate), goigoi, lakini wenye juhudi ya kazi ngumu kwa muda; wajanja hadi hatua fulani, wajinga sana kupita maelezo ya ... Wao hawana uhalisi, kabisa hawana uwezo wa Uvumbuzi (they are absolutely without originality, absolutely without inventive power)

Watu weusi wanaoishi nchini Uingereza, pamoja na wale wanaoishi katika nchi zao wenyewe Chini ya tawala za Ukoloni wa Ulaya, walikuwa lazima wakabiliane na ubaguzi huu. Ubaguzi wa rangi imekuwa ni kitovu cha mazoea kwa watu weusi katika Uingereza, kwa karne nyingi zilizopita.

Makala-Kwa hisani ya Peter Fryer na uchunguzi Juu ya Historia ya watu weusi nchini Uingereza katika kitabu chake "Staying in Power" (Kubaki Madarakani)

Mkuu,

Naamini kabisa yanayosemwa hapo juu,na si tu Uingereza hata marekani na maeneo mengine ya America ya kusini ubaguzi wa rangi ulikuwa wa kiwango cha juu!

Lakini huwa najiuliza pamoja na waarabu kuwa ni namba moja katika biashara ya utumwa mbona hatuwaoni idadi ya watu weusi wengi huko nchini mwao kama Oman Saudia Arabia na nchi nyingine za kiarabu kulinganisha na washiriki wengine wa biashara hiyo kama Uingereza n.k.?

Au unataka tuamini kuwa zile tuhuma za kuwang'oa mbu.pu watu weusi ili wasizaliane nchini mwao zilikuwa ni za kweli?

Na pia mbona hao wazungu wamejenga mashule,barabara,reli,vyuo,na kuleta maendeleo kwa hao watu weusi unaosema wanawabagua wakati hao waarabu wamewarithisha 'kitabu kitukufu' tu!

Nitashukuru ukinipa jibu!
 
Mi mwenyewe kwa upande wangu hata sielewo pros and cons za muungano. Sielewi ikabisaaaaaaa
 
Mkuu,

Naamini kabisa yanayosemwa hapo juu,na si tu Uingereza hata marekani na maeneo mengine ya America ya kusini ubaguzi wa rangi ulikuwa wa kiwango cha juu!

Lakini huwa najiuliza pamoja na waarabu kuwa ni namba moja katika biashara ya utumwa mbona hatuwaoni idadi ya watu weusi wengi huko nchini mwao kama Oman Saudia Arabia na nchi nyingine za kiarabu kulinganisha na washiriki wengine wa biashara hiyo kama Uingereza n.k.?

Au unataka tuamini kuwa zile tuhuma za kuwang'oa mbu.pu watu weusi ili wasizaliane nchini mwao zilikuwa ni za kweli?

Na pia mbona hao wazungu wamejenga mashule,barabara,reli,vyuo,na kuleta maendeleo kwa hao watu weusi unaosema wanawabagua wakati hao waarabu wamewarithisha 'kitabu kitukufu' tu!

Nitashukuru ukinipa jibu!

sasa nakujibu kwa statistics:

Katika kitabu cha W.Ingrams Zanzibar its History and Its People -1919 anasema population ya Zanzibar 1902 haikuwa na uhakika mwana takwimuu mmoja alomnukuu anasema walikuwapo watu 400,000 na mwengine anasema kasoro ya hao ila ametoa takwimu kuwa Waarbu walikuwa 5000, na hiyo ni pamoja na wnawake, vizee na watoto.

Katika ripoti ya maendeleo ya British Resident (Waziri Mkuu) wa Zanzibar katika Legislative Council 1959 akitoa takiwimu kwa sensa ilofanywa 1958 Zanzibar ilikuwa na population ya 260,000+ ni.akatoa details za mgawanyo wa makabila na humo alitaja Waarabu ni 15,000 pamoja na wanawake na watoto na vizee.

Sasa tirudi huko nyuma ikiwa katika mwaka 1902 Zanzibar ilikuwa na Waarabu 5000 na Utumwa ulifutwa kabisa 1897 yaana miaka mitano nyuma, jee waarabu hao walikuwa na nguvu gani wa kuwatia utumwani mamilioni ya Waafrika?

Hii ndio sababu ya kuwa Arabuni hakuna watu wengi weusi sababu historia ya kweli imefichwa na Wamisionary kwa ajenda ya kidini ili kuonyesha dunia kuwa Kanisa limewaokoa wa Afrika kutoka utumwani na baadae Wakoloni Wazungu wakaitumia kuwagawa watu kwa matabaka baina yao ili wawatawale.

Na kwa taarifa yako Waafrika wanaotokana na vizazi vya watumwa waliokuwa Arabuni hawataki kabisa kujinasibisha na Afrika na utagombana.nao vikali sana ukiwauliza kwao Afrika ni wapi. Teh teh teh.

Baadhi yao ni matajiri sana na wake zao ni waarabu. Baadhi yao niaofisa wakubwa.serikalini hasa katika vyombo vya usalama na Jeshi.

Barabara ya Kilwa mpaka Mtwara na Daraja la Mkapa juu ya Mto Rufiji ni.msaada wa Kuwait.sababu marehem alokuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo mama yake ni Mmakonde wa Nachingwea. Upooo?
 
Hatujawahi kuwa wategemezi kwani hadi sasa hakuna uhakika wa mapato yanayodaiwa kuwa yanakusanywa na Muungano kweli yanahalalisha matumizi mnayotubebsha kwa shughuli ambazo hazituhusu> Gharama kama za majeshi hazituhusu sisi hata kidogo, tunahitaji kiwango kidogo cha mapolisi kwani tayari tuna askari wetu, elimu ya juu sanasana tutatowa wanafunzi 500 kwa mwaka kwenye jumuia ya wanafunzi 70,000. Ukienda mambo ya nje Wazanzibari wote ni 12 kati ya zaidi ya 1000 wa Tanganyika. Umeme mpaka sasa unabidi ujiulize ni wa nani, iwapo Tanganyika haipo?
Angalia sasa makusanyo,TRA hukusanya mapato yote ya Bandarini, viwanja vya ndege na kila sehemu itayotowa mapato. Ukija bahari kuu, Tanganyika haina eneo kubwa lakini wanakusanya rasilimali za sehemu ya Zanzibar,

Ukifika hapo ndio unapoweza kujuwa kuwa Zanzibar inaweza kujiendeleza wenyewe bila matatizo yoyote.
Wakati huu si wa kuongea mambo yasiyo ukweli au au usiuokuwa na uhakika nayo.

Zanzibar yenye watu karibu milioni moja na nusu imefadhiliwa sana na muungano hilo halina ubishi.

Kama mtoa mada alivyosema , makelele mengi na ya muda mrefu kujitoa katika muungani yametokea visiwani.

Pamoja na maudhi mengi Watanganyika washasema liwalo na liwe, muungani basi.
Sababu zisizo na msingi za watu milioni 43 kugawana sawa mapato na watu milioni moja na nusu ni ujinga uliokithiri

Zanzibar ijitawale isiwe tegemezi.
 
sasa nakujibu kwa statistics:

Katika kitabu cha W.Ingrams Zanzibar its History and Its People -1919 anasema population ya Zanzibar 1902 haikuwa na uhakika mwana takwimuu mmoja alomnukuu anasema walikuwapo watu 400,000 na mwengine anasema kasoro ya hao ila ametoa takwimu kuwa Waarbu walikuwa 5000, na hiyo ni pamoja na wnawake, vizee na watoto.

Katika ripoti ya maendeleo ya British Resident (Waziri Mkuu) wa Zanzibar katika Legislative Council 1959 akitoa takiwimu kwa sensa ilofanywa 1958 Zanzibar ilikuwa na population ya 260,000+ ni.akatoa details za mgawanyo wa makabila na humo alitaja Waarabu ni 15,000 pamoja na wanawake na watoto na vizee.

Sasa tirudi huko nyuma ikiwa katika mwaka 1902 Zanzibar ilikuwa na Waarabu 5000 na Utumwa ulifutwa kabisa 1897 yaana miaka mitano nyuma, jee waarabu hao walikuwa na nguvu gani wa kuwatia utumwani mamilioni ya Waafrika?

Hii ndio sababu ya kuwa Arabuni hakuna watu wengi weusi sababu historia ya kweli imefichwa na Wamisionary kwa ajenda ya kidini ili kuonyesha dunia kuwa Kanisa limewaokoa wa Afrika kutoka utumwani na baadae Wakoloni Wazungu wakaitumia kuwagawa watu kwa matabaka baina yao ili wawatawale.

Na kwa taarifa yako Waafrika wanaotokana na vizazi vya watumwa waliokuwa Arabuni hawataki kabisa kujinasibisha na Afrika na utagombana.nao vikali sana ukiwauliza kwao Afrika ni wapi. Teh teh teh.

Baadhi yao ni matajiri sana na wake zao ni waarabu. Baadhi yao niaofisa wakubwa.serikalini hasa katika vyombo vya usalama na Jeshi.

Barabara ya Kilwa mpaka Mtwara na Daraja la Mkapa juu ya Mto Rufiji ni.msaada wa Kuwait.sababu marehem alokuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo mama yake ni Mmakonde wa Nachingwea. Upooo?

Kwani weusi(washenzi kama walivyoitwa na mwarabu waliwaoa waarabu?) Ikiwa ndio ile rai ya baada ya mapinduzi ya kujichagulia mabinti wa kiarabu ilitokana na nini.hebu kuwa muwazi kwa mwarabu mweusi alikuwa mjinga tu na mpaka leo bado mjinga mbele ya macho yake.madada zenu wangapi huenda kuwa wafanyakazi wa ndani uarabuni umewauliza wanayofanyiwa?
 
Mkuu naona umechanganya historia hapo..viziwa vya zanzibar hata Vasco Dagama amepita kuweka maji na kununu mali nyengine kwenye safari yake ya India,kuwepo na wenyeji kidogo hakufanyi kuwa hakukuwepo na wenyeji katika hivyo visiwa,wareno walishindwa kuweka makaazi katika hiyo miaka 500 kwasababu wenyeji walikuwa hawasikilizani na wareno tafauti kubwa labda dini,sasa ujiulize hawa wenyeji walikuwa wameshakuwa na dini ya kiislam huu Uislam kauleta nani hapo ,hapo ndio linakuja jibu lako kuwa warabu waliwahi kufika zanzibar kabla wareno lakini wao walikuwa wanafanya biashara zao na kupita.

Mwarabu alianza kutawala Kilwa,makao makuu yake yalikuwa kilwa kabla ya kuitwa kuisaida zanzibar kuwaondoa wareno,Kuhusu Watumwa walikuwa wanapita tu zanzibar baada ya kuuzwa kwa mnanda kwenye soko na mkunazini walisafirishwa na kupelekwa nchi za mbali,sioni hii kama inachangia kuwepo kwa watu wengi weusi hapo zanizibar.

Wanyamwezi, waliletwa na mwarabu kwani wanyamwezi walikuwa wafanyakazi wazuri na waaminifu kwa warabu hasa wakati mwarabu anaenda safari za ndani ya afrika kutafuta meno ya temba na watumwa na vitu vyengine

Wamanyema wameletwa na waraabu hili kabila lilipendwa sana na mwarabu wanawake wa kimanyema ndio waliokuwa wameolewa katika koo za kisulatani na wengi wao ndio waliokuwa wakifanya kazi za ndani katika nyumba za sultan

Sasa kuna kabila kama la kizaramo ambao vile vile wako wengi hapo zanzibar,hili kabila unaweza kwenda nyuma zaidi wakati wa Mwinyi Mkuu ambae mwarabu alimuhamisha kutoka shangani na kumepleka Bambi kama sikosei

Kwa matiki hiyo uataona kuwa wenyeji wa zanzibar kama walikuwa kidogo au wingi walikua ni makabila ya pwani ya afrika mashariki wagunya,wazaramo,wadigo,wasegeju.......haya makabila yalikuwa na utamaduni wakulala "dago" wakati wakienda kuvua sehemu za mbali,makabila mengine kama wanyamwezi,wamanyema na makabila ya mbali ya afrika ndio hao waliokuwa wakitwa wageni ijapokuwa walikuwa ni watu weusi...

Waswahili wa zanzibar walienda bega kwa bega na warabu wa Oman watu kama akina TipTip walikuwa waswahili wanafanya vitu sawa sawa na mwarabu na ndio maana wakathubuti kuwaia wawasaidie kumtoa Mreno na ndio maana wakawachia Warabu watawale nchi hii.

Kutoka na historia ya Zanzibar sioni kama Sultan alikuwa mkoloni kama propaganda za siasa zinavyosema,Ukiangalia picha za Sultani wa zanzibar utaona kuwa hawa jamaa ni warabu waliochanganya na watu wa makabila ya waafrika,yaani hawana tafauti kisura na akina Salim Moh'd Salim,Seif Shariff au Aman karume na hizo ndio sura za Visiwani,lamu,Mombasa,kismayu sura za watu wa pwani ya africa mashariki

source bibi yangu 🙂

Vasco da gama aliingia pwani ya Africa mashariki 1497 ama 98 miaka 500 baadae ni mwaka 1998 hivyo ndivyo ukweli ulivyo?

Tukumbuke baada yakudondoka kwa fort Jesus ureno habari yao iliisha kweny ukanda wetu.na swala la dini kumbuka kilwa ilijengwa na waarabu na kuwa chini ya misingi ya kdini haswa.nadhani wafahamu jinsi mreno alivyouteketeza mji ule uliokuwa unavutia.kama Zanzibar alishindwa kuelewana na wenyeji kilwa aliwezaje?
 
sasa nakujibu kwa statistics:

Katika kitabu cha W.Ingrams Zanzibar its History and Its People -1919 anasema population ya Zanzibar 1902 haikuwa na uhakika mwana takwimuu mmoja alomnukuu anasema walikuwapo watu 400,000 na mwengine anasema kasoro ya hao ila ametoa takwimu kuwa Waarbu walikuwa 5000, na hiyo ni pamoja na wnawake, vizee na watoto.

Katika ripoti ya maendeleo ya British Resident (Waziri Mkuu) wa Zanzibar katika Legislative Council 1959 akitoa takiwimu kwa sensa ilofanywa 1958 Zanzibar ilikuwa na population ya 260,000+ ni.akatoa details za mgawanyo wa makabila na humo alitaja Waarabu ni 15,000 pamoja na wanawake na watoto na vizee.

Sasa tirudi huko nyuma ikiwa katika mwaka 1902 Zanzibar ilikuwa na Waarabu 5000 na Utumwa ulifutwa kabisa 1897 yaana miaka mitano nyuma, jee waarabu hao walikuwa na nguvu gani wa kuwatia utumwani mamilioni ya Waafrika?

Hii ndio sababu ya kuwa Arabuni hakuna watu wengi weusi sababu historia ya kweli imefichwa na Wamisionary kwa ajenda ya kidini ili kuonyesha dunia kuwa Kanisa limewaokoa wa Afrika kutoka utumwani na baadae Wakoloni Wazungu wakaitumia kuwagawa watu kwa matabaka baina yao ili wawatawale.

Na kwa taarifa yako Waafrika wanaotokana na vizazi vya watumwa waliokuwa Arabuni hawataki kabisa kujinasibisha na Afrika na utagombana.nao vikali sana ukiwauliza kwao Afrika ni wapi. Teh teh teh.

Baadhi yao ni matajiri sana na wake zao ni waarabu. Baadhi yao niaofisa wakubwa.serikalini hasa katika vyombo vya usalama na Jeshi.

Barabara ya Kilwa mpaka Mtwara na Daraja la Mkapa juu ya Mto Rufiji ni.msaada wa Kuwait.sababu marehem alokuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo mama yake ni Mmakonde wa Nachingwea. Upooo?

Mkuu,

Nashukuru sana kwa majibu yako mazuri sana,lakini napata ukakasi juu ya mambo kadhaa uliyoyaongelea.

Umesema kuwa historia ya kweli imefichwa na wamisionary kwa ajenda ya kidini lakini hapohapo unatumia rekodi hizo hizo za wamisionary kujenga hoja yako(hebu rejea takwimu zako).

Pia hata hizo takwimu zako hazina mashiko yoyote kwani msafara wa watumwa 300 waliofungwa vizuri chains ulikuwa hautaji hata watu (waarabu) wa3 kuweza kuwasafirisha kutoka bara mpaka visiwani.

Na pia kuniambia kuna matajiri kadhaa weusi uarabuni ambao wana asili ya utumwa huo ni uongo uliokubuhu!Kama sio nitajie wachache tu,maana mie nawajua matajiri wengi tu marekani na uingereza wenye asili ya utumwa na mmojawapo ni first lady wa USA Michelle Obama!Wewe nitajie mmoja tu huko uarabuni,maana baadhiyao umesema ni maafisa wa jeshi,hata sijui nchi gani unaongelea!

Na umeongelea barabara ya kilwa mpaka mtwara imejengwa kwa kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo mama yake ni mmakonde!Hebu nipe jina lake ili niangalie kwenye rank ya uongozi kama yupo,ama utakuwa unaendeleza 'chai' zilezile ambazo mnauziana humu jukwaani!
Japo hujamaliza kunijibu maswali yangu ya msingi lakini usijali najua unahitaji uwe na roho ya mwendawazimu kuyajibu!

Asante!
 
"Haa! hivi kwani kabla ya huu muungano tulikuwa tukijiendeshaje? tumetimiza miaka 50 ya uhuru na mapinduzi, hivi lengo la yote hayo tuyasalimu mamlaka yetu kwa nchi nyengine atuendeshee?

Unavyoongea ni kam Mh Nahodha, kisha anaunyemelea Urais wa Zanzibar wakati tayari hajiamini kiulinzi wala kiuchumi. Wapo wanoweza na ndio tutowaweka madarakani 2015"

1. Mlipata Uhuru lini?! taja,
2. Mkaingia kwenye Muungano lini? taja mwaka,
3.kabla ya mapinduzi na uhuru nani alikuwa anakuendeshea serikali na kwa mtindo upi?
4.Nani anayekuendeshea serikali kwa sasa ?!
5.Je hati za muungano zinasemaje

Jibu la swali la 1,2 na la 3 litakupa swali tena ambalo litajibu hapo kwenye green, JE! hiyo experience ya wazaznbar wao kama wao kujiendesha kama nchi yenye serikali waliipata lini?
 
Vasco da gama aliingia pwani ya Africa mashariki 1497 ama 98 miaka 500 baadae ni mwaka 1998 hivyo ndivyo ukweli ulivyo?

Tukumbuke baada yakudondoka kwa fort Jesus ureno habari yao iliisha kweny ukanda wetu.na swala la dini kumbuka kilwa ilijengwa na waarabu na kuwa chini ya misingi ya kdini haswa.nadhani wafahamu jinsi mreno alivyouteketeza mji ule uliokuwa unavutia.kama Zanzibar alishindwa kuelewana na wenyeji kilwa aliwezaje?

wareno walikuwepo zanzibar kabla ya Vasco dagama kupita zanzibar haimanishi kufika kwa vasco dagama ndio mwanzo wa tarehe ya kuwepo wareno zanizbar,Kilwa ilikuwa chini ya utawala wa kisultan wakati zanzibar ilikuwa ikijitawala wenyewe

ukaaji wa wageni hasa wareno na vitendo vyao vilikwenda kinyume na maadili ya wenyeji ndio kilichowafanya wenyeji kuwaita warabu kumbuka historia inasema wareno walikuwa hapo zanzibar kwa muda miaka mingi zaidi ya mia

Sina ufahamu kama wareno walikaa Kilwa zaidi ya miaka mia mpaka wenyeji wakashidwa kuelewana nao,kwanini wenyeji wa kilwa waliweza kuelewana na wareno inabidi tuwaulize wao mimi nanukuu historia ya zanzibar ambayo inapatikana kwenye google au wikipeadia 😉
 
Hapo kwenye bluu; let's be serious, Muungano ulizaliwa not more than three months baada ya Mapinduzi. Hii inamaanisha kwamba Zanzibar iliwahi kusimama yenyewe kama taifa huru (nje ya Muungano) kwa kipindi kisichozidi miezi mitatu tu! Kabla ya hapo Mamlaka ya Zanzibar yalikuwa chini ya Mkoloni (mwarabu) tangu 1840 - 12th Jan. 1964 yaani kwa miaka 124.

Hivyo, kusema kwamba "kabla ya muungano" Zanzibar iliishije; jibu ni rahisi; YALIKUWA MAISHA YA UKOLONI WA KIARABU, labda ndio aina ya maisha wengine mnayotamani kuishi. Vinginevyo nakubaliana na mleta mada kwamba nje ya Muungano Zanzibar inatakiwa "kuanza upya" kwani kabla ya hapo Zanzibar kama taifa huru "haikuwahi kuwa na chochote" na sio kutuletea majibu mepesi na ya kijinga eti "kabla ya muungano ilikuwaje" kana kwamba Muungano ulikuja muda mrefu baada ya Zanzibar kuwa taifa huru!

Nimekupenda sana mkuu, just a minute ago nimemuuliza huyo kijana maswali ya hayo majibu uliyompa bila kujua kwamba umeshampa majibu tayari, unajua hao hawajiulizi wanakurupuka tuu na sumu walizonyweshwa.

Truly 1964 ndio historia ya zanzbar yenye kujitawala wenyewe ilipoanza na 1964 hiyohiyo ndio Muungano Mtukufu, thus uchumi na maendeleo ya zanzibar baada ya uhuru huwezi kuyazungumzia bila kuitaja Tanzania, otherwise huko nyuma ni vurugu tuu za ukoloni wa waarabu na ufedhuli wao.
 
Kwani weusi(washenzi kama walivyoitwa na mwarabu waliwaoa waarabu?) Ikiwa ndio ile rai ya baada ya mapinduzi ya kujichagulia mabinti wa kiarabu ilitokana na nini.hebu kuwa muwazi kwa mwarabu mweusi alikuwa mjinga tu na mpaka leo bado mjinga mbele ya macho yake.madada zenu wangapi huenda kuwa wafanyakazi wa ndani uarabuni umewauliza wanayofanyiwa?

Wewe unakurupuka umenukuu makala niliyoileta hapo amabayo imeandikwa na wanataaluma wa Kiingereza. Na humo imeeleza kuwa Wazungu wakiwaita waafrika ni washenzi, wapenda ngono, wavivu, machepe na wagomvi sana. Pia wametumia sayansi na hata Biblia kuhalalisha Utumwa.

Sasa wewe unasema waarabu wamewaita waafrika washenzi hali ya kuwa waarabu wameona na waafrika na ndio product ya watu wengi katika ukanda wa Afrika Mashariki wakawa wako mixed race, na hii lugha ya kiswahili ndio faida nyengine.

Wazungu shule zote walizojenga ni za kusomeshea watoto wao. Shule ya Arusha ilijengwa 1933 lakini ikichukuwa watoto wa Kizungu tu.

Shule ya Mbeya imejengwa 1958 nayo ilijengwa kwa ajili ya wazungu tu.

Shule zote zilofuata baadae katika Tanganyika zilikuwa za misionaries.

Kule Zanzibar shule ya mwanzo kabisa ni Shule ya Dole ambayo ndio waliyosoma wazee wetu na.clasmates wao.ndio Kina Mzee A. JUMBE, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Marehwm Mzze. Idriss Abdulwakil na wazee wengi waliokuwa na asili mbali mbali walisoma katika shule hizo na hatimae wengine kuhitimu na kupelekwa scholarship.za nje kama.Makerere na Oxford University UK.

Hao Wazee wote niliowataja hapo walikuwa ni marafiki wazee wenzao.wa makabila mabali mbali lwa kutembeleana na kupendana na wengine kuoleana ndugu zao wa kiarabu kabla ya mapinduzi.

Waliooa kwa nguvu baada ya Mapinduzi mbegu zao ni hizo zinzowaumisha kichwa watu kama Mhe. Mansour Y. Himid, ila wengine wameshindwa kukaa Zanzibar kutokana ya kuwa baada kuunganishwa ASP na TANU kuzaliwa CCM imeshindwa kuwaenzi wao hasa baba zao walipofariki na mifano iko.katika.mitandao ya jamii wanaweka.profile.zao picha zao pia na wengine wameolewa na hao hao maadui za baba zao.

Ama hao Waafrika walioko Arabuni.na.hizo.status zao ni kuwa kule Arabuni ulikwisha tokea karne ya kumi na nane na hao watu wameowana na wenyeji kama.huko unakosikia Salalah Oman na Kuwait na Saudia na wote hao ni waafrika ambao.wamekuwa intergrated katika jamii sawa na waarabu na wana enjoi uraia wao wala hakuna chuki baina ya jamii ndio.maana wanaowa na kuolewa na waarabu weupe na weusi.

Mapichq uneyaona huko kwenye post nyengine.
 
wareno walikuwepo zanzibar kabla ya Vasco dagama kupita zanzibar haimanishi kufika kwa vasco dagama ndio mwanzo wa tarehe ya kuwepo wareno zanizbar,Kilwa ilikuwa chini ya utawala wa kisultan wakati zanzibar ilikuwa ikijitawala wenyewe

ukaaji wa wageni hasa wareno na vitendo vyao vilikwenda kinyume na maadili ya wenyeji ndio kilichowafanya wenyeji kuwaita warabu kumbuka historia inasema wareno walikuwa hapo zanzibar kwa muda miaka mingi zaidi ya mia

Sina ufahamu kama wareno walikaa Kilwa zaidi ya miaka mia mpaka wenyeji wakashidwa kuelewana nao,kwanini wenyeji wa kilwa waliweza kuelewana na wareno inabidi tuwaulize wao mimi nanukuu historia ya zanzibar ambayo inapatikana kwenye google au wikipeadia 😉

Hiyo historia imedukuliwa.rudi nyuma tafuta chanzo cha wareno kuja upande huu wa kusini.kumbuka wareno wameitumia route hii baada ya Christopher Columbus kudai amegundua njia ya karibu zaidi ya kwenda kwa the great Khan.hiyo ilikuwa 1492 na baada ya wareno kuona msafara uliotumwa na hasimu wao mhispania(ambao ni wa Columbus) umeigundua subroute to india ndipo akatumwa Diaz aliyeishia cape of good hope na kushindwa kuendelea.mwaka 1497 da gama alifAnikiwa kuivuka rasi ya tumaini jema na msafara wake na kuifikia pwani ya kilwa baadae mwaka huo ama mwaka uliofuata.

Hao wareno waliokuwa Zanzibar kabla ya da gama ni kina nan? Walipita wapi? Na kwa nn da gama alisema amekuta eneo la watu weusi wanaofanya biashara? Hilo ndilo liliwavuta wareno wengi zaidi kuja huku na kutaka kuweka miji hii chini yao.

Ikiwa wareno walikuwepo kwann waliongezeka baada yA da gama? Walioshi maeneo yapi na waliishi kama kina nani?
 
Ni kweli, miezi miwili na nusu ya uhuru ilikuwa ngumu sana kwa marehemu Karume kushikilia dola ya visiwa viwili kama nchi moja - alishalemewa sana na hatari ya vita vya wenyewe kwa wenyewe - kama historia inavyoonesha. Lakini kwa sasa mazingira ni tofauti na wakati ule tulipohitaji msaada wa Watanganyika ili kuepuka balaa baada ya Mapinduzi matukufu. Sasa tunaweza kabisa kujisimamia kama nchi. Historia imebadilika, watu wamebadilika, mazingira ya ki-dunia yamebadilika. Tunawashukuru Wabara kwa kupita nasi kipindi kile kigumu, lakini shukrani na heshima hii itapungua na kubadilika iwapo mtaendelea kufikiri mtoto akishakua anahitaji tena kutunzwa na kusimamiwa na mzazi. Mzazi mwenye busara humpa mtoto heshima na uhuru wa kujitawala muda unapofika kufanya hivyo!

Hujasema cha tofaouti na wazenji wenzio, Kwasababu wote mnaamini kwamba maendeleo yenu yatakuja baada ya kujitenga na muungano, kwahiyo mnaamini kwamba watanganyika au wabara wanawabana mnoo. Ni upuuzi mtupu kufananisha Muungano na baba anaye mlea mwanae.

Muungano wetu ni udugu kwasababu cc ni watu wa asili moja, Pia Ni kukusanya nguvu ili twende pamoja kimaendeleo ili kujikomboa na sio msaada ili baadae mmoja ajitegemee.

We unafikiri kwanini now dayz kuna Regional Economic integrations na federations kama hii EAC?! Kwani Zambia, Botwsana, Gambia ,Nigeria,Uganda na wakenya hawana maendeleo au hawajaweza kujitegemea kwanini zinaungana? Angalia United Kingdom (UK) ,USA n.k

Inchi kubwakubwa zinafight kuungana nyinyi viduchu mnajifanya mna ubavu
 
Wewe unakurupuka umenukuu makala niliyoileta hapo amabayo imeandikwa na wanataaluma wa Kiingereza. Na humo imeeleza kuwa Wazungu wakiwaita waafrika ni washenzi, wapenda ngono, wavivu, machepe na wagomvi sana. Pia wametumia sayansi na hata Biblia kuhalalisha Utumwa.

Sasa wewe unasema waarabu wamewaita waafrika washenzi hali ya kuwa waarabu wameona na waafrika na ndio product ya watu wengi katika ukanda wa Afrika Mashariki wakawa wako mixed race, na hii lugha ya kiswahili ndio faida nyengine.

Wazungu shule zote walizojenga ni za kusomeshea watoto wao. Shule ya Arusha ilijengwa 1933 lakini ikichukuwa watoto wa Kizungu tu.

Shule ya Mbeya imejengwa 1958 nayo ilijengwa kwa ajili ya wazungu tu.

Shule zote zilofuata baadae katika Tanganyika zilikuwa za misionaries.

Kule Zanzibar shule ya mwanzo kabisa ni Shule ya Dole ambayo ndio waliyosoma wazee wetu na.clasmates wao.ndio Kina Mzee A. JUMBE, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Marehwm Mzze. Idriss Abdulwakil na wazee wengi waliokuwa na asili mbali mbali walisoma katika shule hizo na hatimae wengine kuhitimu na kupelekwa scholarship.za nje kama.Makerere na Oxford University UK.

Hao Wazee wote niliowataja hapo walikuwa ni marafiki wazee wenzao.wa makabila mabali mbali lwa kutembeleana na kupendana na wengine kuoleana ndugu zao wa kiarabu kabla ya mapinduzi.

Waliooa kwa nguvu baada ya Mapinduzi mbegu zao ni hizo zinzowaumisha kichwa watu kama Mhe. Mansour Y. Himid, ila wengine wameshindwa kukaa Zanzibar kutokana ya kuwa baada kuunganishwa ASP na TANU kuzaliwa CCM imeshindwa kuwaenzi wao hasa baba zao walipofariki na mifano iko.katika.mitandao ya jamii wanaweka.profile.zao picha zao pia na wengine wameolewa na hao hao maadui za baba zao.

Ama hao Waafrika walioko Arabuni.na.hizo.status zao ni kuwa kule Arabuni ulikwisha tokea karne ya kumi na nane na hao watu wameowana na wenyeji kama.huko unakosikia Salalah Oman na Kuwait na Saudia na wote hao ni waafrika ambao.wamekuwa intergrated katika jamii sawa na waarabu na wana enjoi uraia wao wala hakuna chuki baina ya jamii ndio.maana wanaowa na kuolewa na waarabu weupe na weusi.

Mapichq uneyaona huko kwenye post nyengine.

Ina maana wazungu ndio waliowaita weusi washenzi na sio waarabu?.hebu rudia ukweli shenzi ilitumiwa na waarabu katika minajili yakuonyesha ujinga wa zanj people(weusi)

Eti waarabu hawakuwatesa weusi je umepata kusikia habari za zenj rebellion? Ikiwa ilitokea mnamo karne ya 8 au9 hao weusi waliokuwa kwenye mabonde ya Iraq ya sasa walizaa wapi na wameishia wapi? Washenzi walikuwa ni wa zanj ambao ni babu zetu regardless anatoka wapi.ikiwa babu yako ni mwarabu basi hakuwa mshenzi ila kama ni mweusi alikuwa mshenzi kama babu yangu mimi.

Unaishia kusema tu wapo weusi walioenda uarabuni kisha majina hakuna.mbona America inafahamika more than 14% ni blacks weusi wa uarabuni waliyeyuka?

Unapoongelea swala la shule hakuna wazee wa Tanganyika waliosoma? Shule kama ya mwambao primary school iliyokuwa inajulikana kama marien schule iliyojengwa na wajerumani huko bagamoyo haikuwafunza waafrica?
 
Mkuu,

Nashukuru sana kwa majibu yako mazuri sana,lakini napata ukakasi juu ya mambo kadhaa uliyoyaongelea.

Umesema kuwa historia ya kweli imefichwa na wamisionary kwa ajenda ya kidini lakini hapohapo unatumia rekodi hizo hizo za wamisionary kujenga hoja yako(hebu rejea takwimu zako).

Pia hata hizo takwimu zako hazina mashiko yoyote kwani msafara wa watumwa 300 waliofungwa vizuri chains ulikuwa hautaji hata watu (waarabu) wa3 kuweza kuwasafirisha kutoka bara mpaka visiwani.

Na pia kuniambia kuna matajiri kadhaa weusi uarabuni ambao wana asili ya utumwa huo ni uongo uliokubuhu!Kama sio nitajie wachache tu,maana mie nawajua matajiri wengi tu marekani na uingereza wenye asili ya utumwa na mmojawapo ni first lady wa USA Michelle Obama!Wewe nitajie mmoja tu huko uarabuni,maana baadhiyao umesema ni maafisa wa jeshi,hata sijui nchi gani unaongelea!

Na umeongelea barabara ya kilwa mpaka mtwara imejengwa kwa kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo mama yake ni mmakonde!Hebu nipe jina lake ili niangalie kwenye rank ya uongozi kama yupo,ama utakuwa unaendeleza 'chai' zilezile ambazo mnauziana humu jukwaani!
Japo hujamaliza kunijibu maswali yangu ya msingi lakini usijali najua unahitaji uwe na roho ya mwendawazimu kuyajibu!

Asante!

Kwanza hizo takwimu sio za wamisionary hizo ni takwimu rasmi za maofisa wa Serikali ya Himaya Uingereza-Zanzibar.

Basi hao Waafrika 300 wafungwe miyororo na waarabu 3 yaani kila mwarabau ana uwezo wa kukamata watu mia kwa pamoja na kuwafunga mmoja mmoja wengine wamekaa watoa macho wasiweze kumzidi nguvu wasubiri kungoja kufungwa minyororo na wao, hata mnyama hakubali, kweli hao waafrika walikuwa mazezeta kiasi gani hata wafae kufanywa watumwa ina maana wewe unakubali huo utafiti wa kisayansi feki waliotumia wazungu kuwa waafrika are so inferior kiasi hawakuwa na fikra hata ya kutoroka wacha kupigana na adui yao?

kuhusu waarabu imeshakueleza mmoja ni huyo ex PM wa Kuwait. Sheikh Saad Al Sabah na Mwengine ni Prince Bandar bin Sultan wa Saudia na hao wamekaa na utajiri kuliko akina Bush, Clinton na Blair. Waarabu sio kawaida yao kuanika.mambo yao uwani kama wazungu lakini hao wawili wanakutosha kwa sasa.

Na wacha kuniita mwongo nimekutolea data na taarehe na majina. Toa zako za kupinga hoja zangu.

Na nimeshakujibu sababu nikuogope nini mimi ni Muungwana nina akili timamu sina matusi kama wewe. Tafuta data za kupinga haya.

Ahsanta kwa kunisoma
 
Wakati huu si wa kuongea mambo yasiyo ukweli au au usiuokuwa na uhakika nayo.

Zanzibar yenye watu karibu milioni moja na nusu imefadhiliwa sana na muungano hilo halina ubishi.

Kama mtoa mada alivyosema , makelele mengi na ya muda mrefu kujitoa katika muungani yametokea visiwani.

Pamoja na maudhi mengi Watanganyika washasema liwalo na liwe, muungani basi.
Sababu zisizo na msingi za watu milioni 43 kugawana sawa mapato na watu milioni moja na nusu ni ujinga uliokithiri

Zanzibar ijitawale isiwe tegemezi.

Zanzibar imehifadhiwa au umehujumiwa? Unazungumza nini iwapo kila kifanywacho na Zanzibar inakuwa tishio kwenu hivyo mnakipiga vita?

Si unataka ukweli? Kuna lazima gani ya kuwapangia Wazanzibar lazima wafuate mnachotaka nyie. Miaka 12 nyuma hivi Zanzibar ilikuwa soko la bidhaa kwa nchi zote za Afrika Mashariki. Nini mlifanya? Mliweka kila aina ya vikwazo kuzuiia jitihada zetu hadi mkafanikiwa na kuwafanya wafanyabiashara wa Zanzibar kuhamisha biashara zao Tanganyika (huku mkilalama eti ooh wameweka mitaji kwetu).
Ni mara ngapi wawekezaji wa aina mbalimbali wametaka kuwekeza Zanzibar mnapinga eti uwekezaji huo utakuathirini nyie. Mifano ni mingi kama saruji, uwanja wa ndege na mashirika ya anga.

Sasa huku unakuuita kufadhili au kudhalili?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom