Analogia Malenga
Platinum Member
- Feb 24, 2012
- 5,292
- 10,842
Musoma. Naibu Waziri wa Nishati, Stephen Byabato amewataka watumishi wa umma wasiopenda ilani ya Chama cha Mapinduzi kuacha kazi mara moja kwakuwa kufanyakazi ya umma huku wakichukia ilani hiyo ni kupoteza muda.
Byabato ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Februari 26, 2021 wakati akizungumza na watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoa wa Mara juu ya mikakati ya kufanikisha majukumu ya watumishi hao.
Amesema kuwa mtumishi wa umma anayechukia ilani ya CCM na chama chenyewe anajidanganya kwakuwa anatakiwa kutekeleza ilani hiyo ambayo ndiyo dira ya kufanya kazi yake kwa ufanisi.
Amesema kuwa hata yeye kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa mtumishi wa umma na alikuwa akipenda ilani ya CCM pamoja na chama chenyewe baada ya kubaini kuwa haiwezekani kutenganisha ilani hiyo na utumishi wa umma.
"Kama kuna mtumishi haipendi ilani ya CCM anajidanganya na niwatake tu waache kazi kwavile watatukwamisha kwenye utekelezaji wa ilani hiyo tuliyoinadi kwa nguvu zote na kukubaliwa kisha ikapokelewa na hatimaye ikapigiwa kura na wananchi" amesema Byabato.
Ametolea mfano wa mwanafunzi mwenye imani tofauti ambaye anasoma shule ambayo sio ya imani yake lakini ni lazima afuate sheria na taratibu za shule anayosoma huku akisema kuwa hakuna sababu ya kukwamisha kazi kwasababu ya kuchukia ilani hiyo ambayo ndiyo dira yao.
"Haiwezekani usiende msikitini wakati unasoma shule ya Kiislamu eti kwasababu wewe sio Muislam kama hauwezi ni vema ukahama kwenye shule hiyo tofauti na hapo lazima ufuate sheria na taratibu za pale" amesema.
Ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuboresha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kujamii ili kufanikisha hilo ni lazima ilani ya CCM ifuatwe na Serikali haitakuwa na huruma kwa atakayejaribu kukwamisha utekelezaji huo.
Amesema kuwa ili kufanikiwa kutekeleza majukumu ya kiutumishi wafanyakazi hao hawanabudi kupenda kazi zao huku akifafanua kuwa ni vigumu kufanikiwa kwenye utumishi kama mtumishi atakuwa hapendi kazi yake.
Chanzo: Mwananchi
Byabato ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Februari 26, 2021 wakati akizungumza na watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoa wa Mara juu ya mikakati ya kufanikisha majukumu ya watumishi hao.
Amesema kuwa mtumishi wa umma anayechukia ilani ya CCM na chama chenyewe anajidanganya kwakuwa anatakiwa kutekeleza ilani hiyo ambayo ndiyo dira ya kufanya kazi yake kwa ufanisi.
Amesema kuwa hata yeye kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa mtumishi wa umma na alikuwa akipenda ilani ya CCM pamoja na chama chenyewe baada ya kubaini kuwa haiwezekani kutenganisha ilani hiyo na utumishi wa umma.
"Kama kuna mtumishi haipendi ilani ya CCM anajidanganya na niwatake tu waache kazi kwavile watatukwamisha kwenye utekelezaji wa ilani hiyo tuliyoinadi kwa nguvu zote na kukubaliwa kisha ikapokelewa na hatimaye ikapigiwa kura na wananchi" amesema Byabato.
Ametolea mfano wa mwanafunzi mwenye imani tofauti ambaye anasoma shule ambayo sio ya imani yake lakini ni lazima afuate sheria na taratibu za shule anayosoma huku akisema kuwa hakuna sababu ya kukwamisha kazi kwasababu ya kuchukia ilani hiyo ambayo ndiyo dira yao.
"Haiwezekani usiende msikitini wakati unasoma shule ya Kiislamu eti kwasababu wewe sio Muislam kama hauwezi ni vema ukahama kwenye shule hiyo tofauti na hapo lazima ufuate sheria na taratibu za pale" amesema.
Ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuboresha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kujamii ili kufanikisha hilo ni lazima ilani ya CCM ifuatwe na Serikali haitakuwa na huruma kwa atakayejaribu kukwamisha utekelezaji huo.
Amesema kuwa ili kufanikiwa kutekeleza majukumu ya kiutumishi wafanyakazi hao hawanabudi kupenda kazi zao huku akifafanua kuwa ni vigumu kufanikiwa kwenye utumishi kama mtumishi atakuwa hapendi kazi yake.
Chanzo: Mwananchi