Watuhumiwa wenzake na Mbowe yawezekana kweli waliteswa na kupigwa, lakini je hawakupanga kushiriki njama za ugaidi?

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi ya Tanzania kipo wazi kabisa, kuwa mahakama haitakataa kupokea ushahidi wa mtuhumiwa kukubali kutenda kosa hata kama alipata vitisho, mateso na au bakshishi iwapo ni kweli alihusika, ila kama alipigwa na kuteswa na polisi wakageuza uongo uwe kweli hapo ndipo itakataa kupokea huo ushahidi.

Kesi ya Mbowe na wenzake inaendelea naona wafuasi wa CHADEMA wanashupaa sana kudhania kuwa watuhumiwa wenzake na Mbowe kutoa maelezo kuwa walipigwa na kuteswa itakuwa ni sababu ya kutotenda kosa. Ni wazi kuwa mtu anatakiwa akiri kosa kwa hiari kama kifungu cha 27 cha sheria ya ushahidi inavyosema.

Lakini kama akikiri kwa lazima halafu ikawa kweli alitenda kosa basi hapo kuna hatia. Je, wakati hizi kesi ndogo juu ya kesi kubwa zikiendelea na tuhuma za kupigwa na kuteswa zikiibuka, Je hawakushiriki kipanga kulipua vituo vya mafuta?

Factum probandum?
 
Unajua press ya juzi, JWTZ wamebadili gia angani,walichopanga kuongea sicho walichokiongea,unapotaja "Makomandoo" maana yake ni "Highly trained soldiers"Kwa muktadha huu wa kesi ya Mbowe na ushahid unaotolewa na hawa Makomandoo wetu,jua tu hali si shwari. UTANIELEWA MWAKANI.
 
Unajua press ya juzi,JWTZ wamebadili gia angani,walichopanga kuongea sicho walichokiongea,unapotaja "Makomandoo" maana yake ni "Highly trained soldiers".....kwa muktadha huu wa kesi ya Mbowe na ushahid unaotolewa na hawa Makomandoo wetu,jua tu hali si shwari....UTANIELEWA MWAKANI.
Jikite kwenye mada.
 
Uneandika mengi yasiyoeleweka hebu tuanzie hapa, haki ya kumpiga mtuhumiwa hao polisi wameipata toka kwa kifungu gani cha sheria?

Kama unakiri polisi "inawezekana" waliwapiga watuhumiwa hapo watuhumiwa wanastahili kupewa haki yao, nayo ni ku prove kwa mahakama kweli walipigwa ikibidi wapelekwe hospitalini wakachunguzwe na daktari majibu ya vipimo apelekewe jaji kwa maamuzi.

Jaji akijiridhisha aangalie ni sheria zipi zimevunjwa na polisi kwa kujichukulia mamlaka ya kuwapiga watuhumiwa wakiwa mikononi mwao hivyo jaji aamue kwa kutumia sheria husika, na sio kwa maoni yake.
 
Uneandika mengi yasiyoeleweka hebu tuanzie hapa, haki ya kumpiga mtuhumiwa hao polisi wameipata toka kwa kifungu gani cha sheria?

Kama unakiri polisi "inawezekana" waliwapiga watuhumiwa hapo watuhumiwa wanastahili kupewa haki yao, nayo ni ku prove kwa mahakama kweli walipigwa ikibidi wapelekwe hospitalini wakachunguzwe na daktari majibu ya vipimo apelekewe jaji kwa maamuzi.

Jaji akijiridhisha aangalie ni sheria zipi zimevunjwa kwa polisi kujichukulia mamlaka ya kuwapiga watuhumiwa wakiwa mikononi mwao hivyo jaji aamue kwa kutumia sheria husika, na sio kwa maoni yake.
Wapi nimeandika polisi wanayo haki ya kupiga?

Ishu ni kama walikiri kwa kupigwa na kuteswa na kweli walipanga kulipua vituo vya mafuta. Kama ni kweli mahakama itauchukua huo ushahidi.
 
Unajua press ya juzi,JWTZ wamebadili gia angani,walichopanga kuongea sicho walichokiongea,unapotaja "Makomandoo" maana yake ni "Highly trained soldiers".....kwa muktadha huu wa kesi ya Mbowe na ushahid unaotolewa na hawa Makomandoo wetu,jua tu hali si shwari....UTANIELEWA MWAKANI.


Kwamba JWTZ “wamebadiri Gia angani, walichopanga kuongea sio walichokiongea “... Tafadhali unaweza kuthibitisha maneno yako haya?
 
Unajua press ya juzi,JWTZ wamebadili gia angani,walichopanga kuongea sicho walichokiongea,unapotaja "Makomandoo" maana yake ni "Highly trained soldiers".....kwa muktadha huu wa kesi ya Mbowe na ushahid unaotolewa na hawa Makomandoo wetu,jua tu hali si shwari....UTANIELEWA MWAKANI.
Vijana wanahasira mi hadi naogopa sijui na Mabagao anasepa next yr feb/march
 
Wapi nimeandika polisi wanayo haki ya kupiga?

Ishu ni kama walikiri kwa kupigwa na kuteswa na kweli walipanga kulipua vituo vya mafuta. Kama ni kweli mahakama itauchukua huo ushahidi.
Mtuhumiwa hata kama ana hatia, sharti zifuatwe taratibu zinazokubalika kisheria kumkamata na kumfikisha mahakamani, kuvunja taratibu hizo kabla ya kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo anastahili kuachiwa huru, huwezi kuharibu hatua za mwanzo halafu ukarekebishe mbele ya safari, hiyo kitu haipo kisheria ni vile mnabebwa na "maoni" ya jaji.
 
Mtuhumiwa hata kama ana hatia, sharti zifuatwe taratibu zinazokubalika kisheria kumkamata na kumfikisha mahakamani, kuvunja taratibu hizo kabla ya kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo anastahili kuachiwa huru, huwezi kuharibu hatua za mwanzo halafu ukarekebishe mbele ya safari, hiyo kitu haipo kisheria ni vile mnabebwa na "maoni" ya jaji.
Mkuu soma vizuri kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi.

Mfano mtu anatuhumiwa kwa ujambazi wa siraha, anafikishwa kituo cha polisi, anapigwa na kuteswa anakubali na anawapeleka polisi alipoficha siraha na vitu alivyoiba. Ikikifaka mahakamani itakuwaje?
 
Kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi ya Tanzania kipo wazi kabisa, kuwa mahakama haitakataa kupokea ushahidi wa mtuhumiwa kukubali kutenda kosa hata kama alipata vitisho, mateso na au bakshishi iwapo ni kweli alihusika, ila kama alipigwa na kuteswa na polisi wakageuza uongo uwe kweli hapo ndipo itakataa kupokea huo ushahidi.

Kesi ya Mbowe na wenzake inaendelea naona wafuasi waCdm wanashupaa sana kudhania kuwa watuhumiwa wenzake na Mbowe kutoa maelezo kuwa walipigwa na kuteswa itakuwa ni sababu ya kutotenda kosa. Ni wazi kuwa mtu anatakiwa akiri kosa kwa hiari kama kifungu cha 27 cha sheria ya ushahidi inavyosema.

Lakini kama akikiri kwa lazima alafu ikawa kweli alitenda kosa basi hapo kuna hatia. Je, wakati hizi kesi ndogo juu ya kesi kubwa zikiwndelea na tuhuma za kupigwa na kuteswa zikiibuka, Je hawakushiriki kipanga kulipua vituo vya mafuta?

Factum probandum?
Mtakubali tu hatua kwa hatua. Mkishakubali kuwa waliteswa mnakubali kuwa confession zilifanyika kwa mateso hence Trumped up cases😅😅😅

Kazi wanayofanya akina Kibatala et al ni nzuri mnoa. Wala hawana haraka. They lay ground foundation slowly but firmly. Tutakuwa kwenye Ku ruleout tuhuma zenyewe baadae.
 
Mkuu soma vizuri kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi.

Mfano mtu anatuhumiwa kwa ujambazi wa siraha, anafikishwa kituo cha polisi, anapigwa na kuteswa anakubali na anawapeleka polisi alipoficha siraha na vitu alivyoiba. Ikikifaka mahakamani itakuwaje?
Sasa ndio tutaona vituo vya mafuta walivyochoma moto😅😅😅
 
Mtakubali tu hatua kwa hatua. Mkishakubali kuwa waliteswa mnakubali kuwa confession zilifanyika kwa mateso hence Trumped up cases😅😅😅

Kazi wanayofanya akina Kibatala et al ni nzuri mnoa. Wala hawana haraka. They lay ground foundation slowly but firmly. Tutakuwa kwenye Ku ruleout tuhuma zenyewe baadae.
Tunakubali na akina nani? Utarule out tuhuma baadae na nani?
 
Mkuu soma vizuri kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi.

Mfano mtu anatuhumiwa kwa ujambazi wa siraha, anafikishwa kituo cha polisi, anapigwa na kuteswa anakubali na anawapeleka polisi alipoficha siraha na vitu alivyoiba. Ikikifaka mahakamani itakuwaje?
Hiyo siraha yenyewe atakuwa kaikubali kwa sababu ya mateso. Ndio maana unaona Jaji Siyani aliutema mzigo maana ku rule in mateso ya Admoo ilikuwa kesi imeisha.
 
Si ndio maana mahakama zikawepo ili zitafsiri sheria na kuhakikisha haki inatendeka?

Kama wamekiri kwa kupigwa hilo ni jambo moja.

Kuthibitisha kwamba walichokiri kwa kushurutishwa ikiwepo kupigwa ni kweli au sio kweli hiyo ni kazi ya mahakama kuthibitisha kwa ushahidi.

Na hadi sasa kwa mwenendo wa kesi, ni kama bado wamejikita kwenye mazingira ya kukusanya ushahidi wa upelelezi uliohusisha kuteswa kwa watuhumiwa. Bado ngwe ya tuhuma yenyewe haijaanza kikamilifu lakini orodha ya mashahidi inaelekea ukingoni na tafrani zinaendelea kuibuka.

Kuna mahali makosa yalifanyika, hasa kiongozi alipotangazia umma kwamva kuna watu wameshahukumiwa na hata hii kesi ni kama alishaitolea maamuzi.

Ni mtihani mzito sana kwa jaji wa hii kesi.

Tukirudi kwenye swali lako, ikithibitika waliteswa wakatoa ushahidi wa kuhusika kupanga matukio ya ugaidi pasi shaka, watesaji watachukua stahiki yao, hali kadhalika magaidi nao sheria itachukua mkondo wake.

Hakuna utetezi kwamba kupitia utesaji ndio imesaidia taarifa sahihi kupatikana.

(Nakiri kutokusoma hicho kifungu cha 29 umekipendekeza) huenda kinaruhusu kutesa watu ili kupata taarifa sahihi, lakini kwa uelewa wangu, mtuhumiwa ana haki zake za msingi, ikiwepo kutokumtesa. Pua hana hatia hadi itakapothibitika ndio anatakiwa atumikie adhabu kwa mujibu wa sheria.
 
Back
Top Bottom