Hapa ndiyo kuna tatizo kubwa kwa Africa ambalo Barack Obama aliliona alipohutubia Bunge la Ghana mwaka 2009 na akasema "Africa doesn't need strongmen, it needs strong institutions."
Ukiwa na strongman akifa na mambo yake YANAKUFA. Lakini Strong Institutions hata Rais akifa zenyewe zinabakia.
Mfano wa strong institutions ni Katiba ya Wananchi, Tume Huru ya Uchaguzi, Mahakama Huru na Bunge Huru. Vile vile TISS inayolinda masilahi ya nchi na siyo ya Rais, Jeshi, Polisi na Magereza.
Kwa Afrika nchi zenye Strong institutions ni Afrika Kusini, Kenya, Egypt.
Maguvu ya Magufuli yalisababisha Bunge liwe butu, Mahakama iwe imamuogopa yeye. Maguvu yakamfanya ajenge kiwanja cha ndege kijijini kwake na kumteua mtoto wa Dada yake Dotto James kuwa Mlipaji Mkuu wa Serikali
Hakuna institutions bila watu!
Institution siyo mashine.
Watu ndo wanatengeneza hizo strong institutions.
Mabadiliko ya kifikra ni ya lazima. Hayaepukiki.
Huwezi kuwa na katiba nzuri, katiba ya ‘wananchi’, bila ya watu kuiandika, kuifuata, kuilinda, kuihifadhi, na kuitetea.
Unaweza kuwa na katiba mpya, ambayo ni nzuri kabisa, lakini huifuati, huilindi, huitetei, na kadhalika.
Hakuna tume huru ya uchaguzi inayojiendesha yenyewe.
Hakuna bunge wala mahakama zinazojiendesha zenyewe.
Na ukitaka mabadiliko ya kweli kwenye hizo taasisi, basi ni lazima pia ubadilike kifikra.
Hakuna mabadiliko yoyote yale ya maana pasipo na mabadiliko ya kifikra.
Mindset lazima ibadilike. Matendo nayo lazima yabadilike.
Ukibadili katiba na ukaacha kubadili fikra, hutoenda popote.
Utaishia kukwama pale pale ulipo.