Sheria zinazoongoza hizo taasisi zinatungwa na watu, na hao watu ndio huziongoza hizo taasisi wakifuata misingi ya sheria na taratibu iliyowekwa na watangulizi, ukikomalia tu taasisi ni watu, mifumo ni watu, na sijui nini kingine ni watu unakuwa unakosea kwani hao watu huja na kuondoka, na mara nyingi hao watu huja na uwezo na tabia tofauti zinazoweza kuharibu ufanisi wa hizo taasisi.
Hivyo chini ya sheria/taratibu zilizowekwa, hizo taasisi na mifumo mingine hubakia strong regardless ya ni mtu gani anaeziongoza, ndio maana sasa tunataka Katiba Mpya ili chini yake tupate miongozo mahususi ya wapi tunataka taifa letu lielekee, na kila Rais na wengine watakaokuwa madarakani wabanwe na hizo sheria, mengi uliyoandika kwenye uzi wako hayajitoshekezi, bado unatakiwa ujifunze zaidi haya mambo.
Kwa muktadha huo, unaposema Katiba Mpya isubiri mpaka watu wapate elimu hilo halipo, na zaidi unataka kutudumaza kama taifa, haihitajiki kutoa elimu kwa watu, muhimu ni Katiba Mpya (Rasimu ya Warioba) iwekwe pale ituongoze, hao watu unaowataka wapewe elimu wataipata hiyo elimu kwa vitendo pale hiyo Katiba Mpya itakapoanza kutumika.