Watu kuoga hadharani ni utamaduni au imani ya kishirikina?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Sijui kama na mikoa mingine ina watu wa wenye ujasiri huo!. Nimeshaona hayo zaidi ya mara moja Kanda ya Ziwa.

Wakati fulani, nilikuwa nikienda sehemu fulani jijini Mwanza kwa gari la taasisi fulani. Hilo gari lilikuwa na watu wazima pamoja na wanafunzi wa shule fulani ya huko huko jijini Mwanza. Moja ya njia gari letu lilikopita ni kando kando ya Ziwa Victoria. Ilikuwa ni majira ya Mchana.

Ghafla, wanafunzi waliokuwemo kwenye hilo gari walianza kupiga kelele zilizoashiria wameona kitu kisichokuwa cha kawaida. Na ndivyo ilivyokuwa. Waliwaona wanaume watu wazima wakioga ziwani jirani na gari letu lilikokuwa likipita. Kumbe walikuwa wanaoneshana hayo "maajabu".

Niliwakemea na wakatulia, lakini hata mimi binafsi nilishangazwa na ujasiri wa hao watu kuthubutu kuoga hadharani majira ya Mchana.

Wakati mwingine tena, nilienda maeneo ya machimbo ya dhahabu wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Kutokana na shughuli iliyonipeleka huko kunihitaji kuwepo huko muda mrefu, nililazimika kutafuta makazi ya muda. Nilipangisha kwenye gesti iliyo huko huko machimboni.

Wateja wengi wa hiyo gesti walikuwa ni watu wanaojishughulisha na shughuli za madini(dhahabu).

Siku moja, majira ya saa tisa Alasiri, nilishtushwa na niliyoyashuhudia . Nilikuwa naenda bafuni kuoga, ndipo nikamkuta mmoja wa wapangaji wa hiyo gesti akioga huku mlango ukiwa wazi.

Siku nyingine tena, majira kama hayo hayo, saa tisa Alasiri, nilimkuta mpangaji mwingine akioga huku mlango wa bafuni ukiwa wazi kabisa

Matukio hayo mawili yalinisukuma kuwauliza wenyeji niliozoeana nao maana ya hayo mambo. Mmoja wa niliowauliza aliniambia kuwa kuwa inawezekana ni masharti ya dawa alizopewa na mganga wa Kienyeji, eti ili zimsaidie kufanikiwa kwenye shughuli ya dhahabu.

Hivi karibuni tena, nimeyaona matukio kama hayo mara mbili. Safari hii, ni mwanaume mtu mzima kuoga kwenye mto ulio pembezoni mwa barabara, Mchana, tena akiwa ametazama upande wa barabarani, kwa hiyo watu wanaopita, wakiwemo watoto, wanawaona wakiwa kama walivyozaliwa. Hayo yametokea Geita Vijijini.

Inahitaji ujasiri wa ziada kuweza kufanya hivyo.

Kuuliza si ujinga! Je! Kuoga hadharani ni sehemu ya utamaduni wa baadhi ya watu?
 
Sasa mtu anaogea bafuni ndo unakuja kufunguka Uzi
Je ungeona anaoga balazani si ungeita waandishi wa habari
Mkuu, labda ningewaita madaktari wa magonjwa ya akili. Kuwaita waandishi wa habari ni udhalilishaji.

Kwani wewe kiongozi unaona ni sawa mtu kuoga bafu
likiwa wazi kabisa na huku bafu lina mlango?

Sidhani kama hilo ni jambo la kawaida.
 
Kwa wakazi wanaozunguka ziwa Victoria na visiwa vyake kuoga ziwani hadharani ni kawaida kabisa tena ziko sehemu maalumu za wanaume na wanawake na zinaribiana mno ni kawaida kabisa.Wa kule guest kuacha mlango wazi pengine ni mambo mengine kama uliyoyasema.
 
IMG_4269.jpg

Mwamba huyu kaoga kariakoo leo na kavunja nazi.hatariii
 
Sijui kama na mikoa mingine ina watu wa wenye ujasiri huo!. Nimeshaona hayo zaidi ya mara moja Kanda ya Ziwa.

Wakati fulani, nilikuwa nikienda sehemu fulani jijini Mwanza kwa gari la taasisi fulani. Hilo gari lilikuwa na watu wazima pamoja na wanafunzi wa shule fulani ya huko huko jijini Mwanza. Moja ya njia gari letu lilikopita ni kando kando ya Ziwa Victoria. Ilikuwa ni majira ya Mchana.

Ghafla, wanafunzi waliokuwemo kwenye hilo gari walianza kupiga kelele zilizoashiria wameona kitu kisichokuwa cha kawaida. Na ndivyo ilivyokuwa. Waliwaona wanaume watu wazima wakioga ziwani jirani na gari letu lilikokuwa likipita. Kumbe walikuwa wanaoneshana hayo "maajabu".

Niliwakemea na wakatulia, lakini hata mimi binafsi nilishangazwa na ujasiri wa hao watu kuthubutu kuoga hadharani majira ya Mchana.

Wakati mwingine tena, nilienda maeneo ya machimbo ya dhahabu wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Kutokana na shughuli iliyonipeleka huko kunihitaji kuwepo huko muda mrefu, nililazimika kutafuta makazi ya muda. Nilipangisha kwenye gesti iliyo huko huko machimboni.

Wateja wengi wa hiyo gesti walikuwa ni watu wanaojishughulisha na shughuli za madini(dhahabu).

Siku moja, majira ya saa tisa Alasiri, nilishtushwa na niliyoyashuhudia . Nilikuwa naenda bafuni kuoga, ndipo nikamkuta mmoja wa wapangaji wa hiyo gesti akioga huku mlango ukiwa wazi.

Siku nyingine tena, majira kama hayo hayo, saa tisa Alasiri, nilimkuta mpangaji mwingine akioga huku mlango wa bafuni ukiwa wazi kabisa

Matukio hayo mawili yalinisukuma kuwauliza wenyeji niliozoeana nao maana ya hayo mambo. Mmoja wa niliowauliza aliniambia kuwa kuwa inawezekana ni masharti ya dawa alizopewa na mganga wa Kienyeji, eti ili zimsaidie kufanikiwa kwenye shughuli ya dhahabu.

Hivi karibuni tena, nimeyaona matukio kama hayo mara mbili. Safari hii, ni mwanaume mtu mzima kuoga kwenye mto ulio pembezoni mwa barabara, Mchana, tena akiwa ametazama upande wa barabarani, kwa hiyo watu wanaopita, wakiwemo watoto, wanawaona wakiwa kama walivyozaliwa. Hayo yametokea Geita Vijijini.

Inahitaji ujasiri wa ziada kuweza kufanya hivyo.

Kuuliza si ujinga! Je! Kuoga hadharani ni sehemu ya utamaduni wa baadhi ya watu?
Nipo kanda ya ziwa

Kwa watu wanaoishi karibu na ziwa(jamii ya wavuvi) hili la kuogea mwaloni ni jambo la kawaida sana

Ila hao wa migodini itakuwa ni madawa maana kuwa bafuni na usifunge mlango ni jambo la ajabu kidogo
 
kuna mwamba nimetoka kumrudisha home wakati tupo njiani nikawa namuelekeza kusu hizi njia panda huwa nakuta chupa sana mida ya asubui sasa kwenye pita pita mbele tukakutana na chupa mida ya night haina hata mdaa kuwekwa
 
Sijui kama na mikoa mingine ina watu wa wenye ujasiri huo!. Nimeshaona hayo zaidi ya mara moja Kanda ya Ziwa.

Wakati fulani, nilikuwa nikienda sehemu fulani jijini Mwanza kwa gari la taasisi fulani. Hilo gari lilikuwa na watu wazima pamoja na wanafunzi wa shule fulani ya huko huko jijini Mwanza. Moja ya njia gari letu lilikopita ni kando kando ya Ziwa Victoria. Ilikuwa ni majira ya Mchana.

Ghafla, wanafunzi waliokuwemo kwenye hilo gari walianza kupiga kelele zilizoashiria wameona kitu kisichokuwa cha kawaida. Na ndivyo ilivyokuwa. Waliwaona wanaume watu wazima wakioga ziwani jirani na gari letu lilikokuwa likipita. Kumbe walikuwa wanaoneshana hayo "maajabu".

Niliwakemea na wakatulia, lakini hata mimi binafsi nilishangazwa na ujasiri wa hao watu kuthubutu kuoga hadharani majira ya Mchana.

Wakati mwingine tena, nilienda maeneo ya machimbo ya dhahabu wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Kutokana na shughuli iliyonipeleka huko kunihitaji kuwepo huko muda mrefu, nililazimika kutafuta makazi ya muda. Nilipangisha kwenye gesti iliyo huko huko machimboni.

Wateja wengi wa hiyo gesti walikuwa ni watu wanaojishughulisha na shughuli za madini(dhahabu).

Siku moja, majira ya saa tisa Alasiri, nilishtushwa na niliyoyashuhudia . Nilikuwa naenda bafuni kuoga, ndipo nikamkuta mmoja wa wapangaji wa hiyo gesti akioga huku mlango ukiwa wazi.

Siku nyingine tena, majira kama hayo hayo, saa tisa Alasiri, nilimkuta mpangaji mwingine akioga huku mlango wa bafuni ukiwa wazi kabisa

Matukio hayo mawili yalinisukuma kuwauliza wenyeji niliozoeana nao maana ya hayo mambo. Mmoja wa niliowauliza aliniambia kuwa kuwa inawezekana ni masharti ya dawa alizopewa na mganga wa Kienyeji, eti ili zimsaidie kufanikiwa kwenye shughuli ya dhahabu.

Hivi karibuni tena, nimeyaona matukio kama hayo mara mbili. Safari hii, ni mwanaume mtu mzima kuoga kwenye mto ulio pembezoni mwa barabara, Mchana, tena akiwa ametazama upande wa barabarani, kwa hiyo watu wanaopita, wakiwemo watoto, wanawaona wakiwa kama walivyozaliwa. Hayo yametokea Geita Vijijini.

Inahitaji ujasiri wa ziada kuweza kufanya hivyo.

Kuuliza si ujinga! Je! Kuoga hadharani ni sehemu ya utamaduni wa baadhi ya watu?
Ukiwa na muda Usiku wa Saa 8 jitegeshe mahala pale Mbezi Beach Makonde utamuoa Mzee Mmoja anatoka Kwake na Ndoo kisha anaoga haraka katikati ya Barabara na Kunya ( Kuukweka ) kidogo kisha anarejea Kwake Geti Kali Jirani na Chuo cha Taasisi ya Kiislamu kilichoungua mapema mwaka huu.
 
Back
Top Bottom