Mshana Jr, naomba unijibu haya matatu, nayasubiria hapa asubuhi hii;
1 - Kuna wale kabla ya kufa, anaoza mwili mzima, na siyo kwamba alikuwa na kansa labda ama magonjwa hatari, hapana. Alianza tu kuwa mnyonge, vipimo vyote takribani yupo sawa, ila mwili unamuoza na kunuka, haja zote hapo hapo, ila baadaye kama miezi hivi anakufa.
2 - Kuna wale kabla ya kufa wanakata kauli tu, haongei chochote ila ukimsemesha anasikia, kula kwa shida, zaidi muda wote huwa anatokwa tu na machozi, hadi anapofariki machozi humtoka tu.
3 - Kuna wale ambao anakufa (mwanaume), Uume umemsimama tu muda wote, na mila za kwetu huku (sipataji), haruhusiwi kuzikwa hadi unywee, hivyo kuna vitu vitafanywa (sivisemi).
Hao wote juu hapo, ni mateso ama wanalipwa kabla ya kuzimu.
Ahsante!