Watu huona nini wanapokaribia kufa?

Watu huona nini wanapokaribia kufa?

mshana jr ulishawahi kwenda kuzimu??maana pale juu nimesoma soma michango nimekuta umedokeza jambo hilo unaweza kutusaidia kastory hako kidogo kama hutajali mpendwa
 
....ngoja nami nichangie kidogo experience yangu....kama kufa kuna hatua 5 nadhani nimefika mbili! na kama ni 3 nimekanyaga moja....nilikuwa nafanya kazi ya umeme kiwanda fulani....nikanaswa na umeme....within a second niliyaona maisha yangu yote niliyoishi kwa spidi ya ajabu....nikahuzunika nikatamani ningepata muda niishi ili niwe bora zaidi....here I am n still sijawa bora!!! Yesu nirehemu, nisaidie....nadhani moja ya kitu kilichonisaidia kufa sikuwaza kukubali mauti....mtu kabla ya kufa nadhani roho ya mauti inashinda maana mimi kama niliishinda....inakuwa inakuita we unakataa.
 
Nimeogopa sana ila ngoja namimi nichangie.kuna jamaa yangu alipata ajali na gari ilimlalia kutoka kiunoni hadi miguuni.Jamaa anasema aliona giza.......
 
Baaadae aliona mwanga uliokua unamzunguka,alisikia sauti ikimwuliza 'umetenda dhambi'akajibu mbona sijatenda dhambi......
 
....ngoja nami nichangie kidogo experience yangu....kama kufa kuna hatua 5 nadhani nimefika mbili! na kama ni 3 nimekanyaga moja....nilikuwa nafanya kazi ya umeme kiwanda fulani....nikanaswa na umeme....within a second niliyaona maisha yangu yote niliyoishi kwa spidi ya ajabu....nikahuzunika nikatamani ningepata muda niishi ili niwe bora zaidi....here I am n still sijawa bora!!! Yesu nirehemu, nisaidie....nadhani moja ya kitu kilichonisaidia kufa sikuwaza k
hahahaha hakunaga mwili utakao itwa na kifo ukakubali lazima mabishano yatokee mpaka kifo kitakapo uweza huo mwili
 
Ghafla alifika sehemu iliyokuwa na geti kubwa,walisimama wadada wawali warefu sana.Wakamwambia 'karibu kwenye sehemu hii ya kwanza ya mateso'Jamaa aligoma kuingia.....
 
Elimu nzuri inatoka kwenye biblia,ukitaka kusema kuhusu kitu unasema na kitabu habari inapopatikana na aliyeandika ila kukaa na kutoka imagination zetu ni tatizo maana umesema kuzimu sidhani kama wote lazima waende huko nashauri jua dini yako hautapata shida kuhusu uzushi wowote
 
Akaanza kuomba na kumlilia Mungu sana.Alikuwa akisema tu Yesu niokoe.Alipozidi kusema hivyo ndipo akawa anaenda mbali nao na mwisho akazinduka,baada ya watu kuliondoa gari.
 
naogopa kufa......... Naogopa
sipendi hata kuwazia mambo ya Kifo ingawa najua nitakufa
Looh! Bibie wakiogopa kivuli chako? pole,anyway kuogopa kitakacho kusibu haisadii cha msingi "JIFANYIE MAANDALIZI" ili uweze kuvuka kwa salama,ni ushauri tu.
 
Mshana Jr. Jamani umenikumbusha mbali sana yaani baba yangu, Alipotaka kufa aliniaga kabisa akasema leo birthday ya mtoto wako ila nasubiria hiyo keki alafu siku zangu hapa duniani zimeisha kabisa sitakula kingine zaidi ya keki ya mtoto wako. Kweli tumamaliza birthday saa 12.30 jioni akasema naenda kuswali Magharib kwa waislam wanajua, baadaye akaswali na akamwambia mama napumzika kidogo hapa kitandani, jamani wanajamvi chakula kimeiva mama anaenda kumuamsha ndio ameshaenda zake kama kalala. R.I.P baba yangu iliniumiza sana na sina sherehe ya birthday ya mtoto wangu kwa kuwa kila mwaka ndio kumbukumbu yake ya kuzaliwa na baba yangu kufa. Naumia sana mwenzenu jamani. Umenikumbusha sana Mshana. Kwahiyo mwengine huona kifo chao.
Even my mom kabla hajafariki alituagaga kabisa nakutoa maelezo. Wengine huona kabisa ila one day tutakuja kuonana na wapendwa wetu
 
Mtu anapokuwa katika hali ya kufa macho yake haya ya nyama hufunga hata kama akiyakodoa vipi haoni mambo ya hapa Duniani tena na badala yake macho yake ya rohoni hufunguka na kuwaona malaika wanaompokea ili kumpeleka kule anakostahili kama alikuwa ameokoka atawaona malaika watakatifu wakija kwa shangwe na kumlaki ndio pale utaona mtu wa namna hii yeye kufa ni kama kalala tu wala hasumbui na kama mtu huyu alikuwa hajaokoka basi huwaona malaika waovu wakimlaki nao kwa asili hawavutii hata kidogo ili kumpeleka kule anakostahili sasa hapa ndipo seleka huwa lipo kwani alipokuwa na wakati mzuri wa kutengeneza na Mungu au alipohubiriwa juu ya wokovu alipinga na kujifariji kwa kuona yupo sahihi sana na akaaminishwa pia kuwa yupo sawa na mbinguni wote huingia tu kwa taratibu na kanuni fulani fulani sasa anapoona wanaokuja kumlaki ni kinyume na matarajio hapo ndipo maumivu, majuto, kilio, kelele za kuomba msaada hutokea akiamini mliopembeni mnaweza kumsaidia kukwepa au kukabiliana kumbe asijue kipindi kile ni cha muda mchache sana na ni cha mhusika na aliowatumikia kwa kujua au kutokujua, ndugu tambua hakuna njia fupi ya kwenda mbinguni lkn pia kwenda mbinguni ni mchakato hivyo anza sasa acha mazoea na kuyarahisisha mambo kama ufanyavyo sasa Wokovu ndio njia pekee ya kuingia Mbinguni yawezekana umesikia sana maneno haya japo unajitia moyo kwa kusema kufa ni kufa tu na Mungu mwenyewe ataamua nikuambie rafiki umechelewa kabla hujaanza tambua hivi Dunia yote inaendeshwa na kanuni ili kutekeleza mambo mbalimbali, Je Mungu yeye hana kanuni? Kama kupanda tu basi kuna kanuni vp mbele za Mungu! Amka leo Yesu anakuhitajj pamoja na faida zote utakazopata kupitia kumwani Bwana Yesu pia hicho ulichonacho sasa ambacho baadhi yenu nimeona baada ya kusoma Uzi wa mleta mada mmepatwa 'Hofu' Yesu atakuondolea na hiyo inaitwa "Hofu ya mauti" na inatesa watu wengi na imemaliza wengi chukua hatua sasa. Ameeen
 
Mmmh! Wengine tunalala wenyewe mkuu.. Kuna siku nilishuhudia nyoka mkubwa akiwa ndani ya kaburi watu tukachangukana na kumuacha marehemu.. Cha Ajabu tuliporudi tukakuta nyuki ndani ya kaburi badala ya nyoka... Ilitokea HANDENI hili tukio lilinifanya niwe mtu wa kushtuka kwa miaka kadhaa
Huyo.mtu alikua sio mwema kabisaa dahh
 
.... Usiwe mtu wa kuzini, usiwe mchawi, usiwe mlevi, usiwe mwizi, usiwe msengenyaji, usitukane watu Hapa JF,usitongoze watu hapa JF kwa lengo la uzinzi, usiwe mwongo, usiwe......... .....
Usiwe mwoga, usiwe mfirraji au mwenyewe tabia za mbwa
 
Back
Top Bottom