Watu huona nini wanapokaribia kufa?

Watu huona nini wanapokaribia kufa?

Mshana Jr, naomba unijibu haya matatu, nayasubiria hapa asubuhi hii;

1 - Kuna wale kabla ya kufa, anaoza mwili mzima, na siyo kwamba alikuwa na kansa labda ama magonjwa hatari, hapana. Alianza tu kuwa mnyonge, vipimo vyote takribani yupo sawa, ila mwili unamuoza na kunuka, haja zote hapo hapo, ila baadaye kama miezi hivi anakufa.

2 - Kuna wale kabla ya kufa wanakata kauli tu, haongei chochote ila ukimsemesha anasikia, kula kwa shida, zaidi muda wote huwa anatokwa tu na machozi, hadi anapofariki machozi humtoka tu.

3 - Kuna wale ambao anakufa (mwanaume), Uume umemsimama tu muda wote, na mila za kwetu huku (sipataji), haruhusiwi kuzikwa hadi unywee, hivyo kuna vitu vitafanywa (sivisemi).

Hao wote juu hapo, ni mateso ama wanalipwa kabla ya kuzimu.

Ahsante!
 
Hakuna anayenusurika kufa labda siku haijafika tu,Wakati unakufa huwa unaoneshwa jinsi ulivoishi na huko unapoenda utaishi vipi.(KAMA ULIKUA MWEMA UTAONESHWA NA MAHALA PEMA UENDAPO MARA NYINGI WATU HAWA UFARIKI HALI YA KUWA WANACHEKA NA HAKUNA VURUGU WAKATI ROHO INATOKA...KAMA ULIKUA MUBAYA UTAONESHWA MAHALA PABAYA UENDAPO MARA NYINGI WATU HAWA HUFA KIUBAYA ZAIDI VURUGU NYINGI WENGINE HUTOA ADI MACHO KWA KUSHANGAA SEHEMU MBAYA ANAYOELEKEA)
 
Mshana Jr, tafadhali nimekuita hapo juu Kaka Mkubwa.

Ahsante!
 
Mshana Jr.

Sio rahisi kujua anachoona marehemu kabla ya kifo. Labda kama ulivyoelezea mambo waliyoyaona ambao walikuwa mahututi na baadaye wakaishi.

Mimi naomba kuchepuka ni base na aina ya kifo.

Sijui lakini naamini mtu mwema kabisa ambaye labda Mungu umeshaamua ataenda Mbinguni huyu kwa mategemeo yangu sitarajii afe kifo cha mateso. Kama ajali mbaya ya gari, au kuungua kwa sababu nyumba imeshika moto. Nategemea afe kifo cha amani. Labda tu auwawe kwa imani yake ambapo hapo mpaka Mungu aruhusu.

Kwa mtu katili na ambaye labda hukumu yake ni motoni ningetegemea labda afe kifo cha aibu ambacho hakina maandalizi. Labda tu kama alitubu na kumrudia Mungu wake.

Natumai nimeeleweka japo nimeandika bila mtiririko mzuri.
 
Ukizidi kutenda maovu hata cku ukitaka kufa utahangaika Mpaka basi sijui vinyongo muuaji kuna baba mchawi aliuaga wengi aliteseka huyo mana alianza kuungua kabla ya kifo na kuona vtu vya ajabu. Before MTU kufariki huonyeshwa three month ili atengeneze maisha yake na Mungu duniani
Hiyo imani ya kupewa mienzi3 utengeneze na Mungu wako kabla ya kupita hivi naitaka. Nakuja pm
 
Mshana Jr. Jamani umenikumbusha mbali sana yaani baba yangu, Alipotaka kufa aliniaga kabisa akasema leo birthday ya mtoto wako ila nasubiria hiyo keki alafu siku zangu hapa duniani zimeisha kabisa sitakula kingine zaidi ya keki ya mtoto wako. Kweli tumamaliza birthday saa 12.30 jioni akasema naenda kuswali Magharib kwa waislam wanajua, baadaye akaswali na akamwambia mama napumzika kidogo hapa kitandani, jamani wanajamvi chakula kimeiva mama anaenda kumuamsha ndio ameshaenda zake kama kalala. R.I.P baba yangu iliniumiza sana na sina sherehe ya birthday ya mtoto wangu kwa kuwa kila mwaka ndio kumbukumbu yake ya kuzaliwa na baba yangu kufa. Naumia sana mwenzenu jamani. Umenikumbusha sana Mshana. Kwahiyo mwengine huona kifo chao.
 
"Dini iliyo safi, isiyo na uchafu mbele za Mungu Baba, ndio hii: kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu". Yakobo 1:27
Kumbuka kuwa YESU alikusanya maelfu katika mahubiri yake lakini hakuwa na dhehebu tena yamekuja baadae sana na saidia walio wake wenye kimuabudu kwa haki na kweli ukimpa msaada muhasi ni kazi bure bora ucngejisumbua
 
Mshana Jr. Jamani umenikumbusha mbali sana yaani baba yangu, Alipotaka kufa aliniaga kabisa akasema leo birthday ya mtoto wako ila nasubiria hiyo keki alafu siku zangu hapa duniani zimeisha kabisa sitakula kingine zaidi ya keki ya mtoto wako. Kweli tumamaliza birthday saa 12.30 jioni akasema naenda kuswali Magharib kwa waislam wanajua, baadaye akaswali na akamwambia mama napumzika kidogo hapa kitandani, jamani wanajamvi chakula kimeiva mama anaenda kumuamsha ndio ameshaenda zake kama kalala. R.I.P baba yangu iliniumiza sana na sina sherehe ya birthday ya mtoto wangu kwa kuwa kila mwaka ndio kumbukumbu yake ya kuzaliwa na baba yangu kufa. Naumia sana mwenzenu jamani. Umenikumbusha sana Mshana. Kwahiyo mwengine huona kifo chao.
Daaah!!!!Pole sana "Mauti ni mlango kila mtu/kiumbe lazima aupite"
 
Mshana Jr, naomba unijibu haya matatu, nayasubiria hapa asubuhi hii;

1 - Kuna wale kabla ya kufa, anaoza mwili mzima, na siyo kwamba alikuwa na kansa labda ama magonjwa hatari, hapana. Alianza tu kuwa mnyonge, vipimo vyote takribani yupo sawa, ila mwili unamuoza na kunuka, haja zote hapo hapo, ila baadaye kama miezi hivi anakufa.

2 - Kuna wale kabla ya kufa wanakata kauli tu, haongei chochote ila ukimsemesha anasikia, kula kwa shida, zaidi muda wote huwa anatokwa tu na machozi, hadi anapofariki machozi humtoka tu.

3 - Kuna wale ambao anakufa (mwanaume), Uume umemsimama tu muda wote, na mila za kwetu huku (sipataji), haruhusiwi kuzikwa hadi unywee, hivyo kuna vitu vitafanywa (sivisemi).

Hao wote juu hapo, ni mateso ama wanalipwa kabla ya kuzimu.

Ahsante!
Hao wote wanapitia hari za kifo kutokana na maagano viapo mambo ya giza na laana mbalimbali....na kwakweli hukumu inakuwa bado bali hii ndio inakuwa tamati ya hayo niliyoyataja hapo juu
Kwa kiasi kikubwa ukifuatilia mada zangu nimetahadharisha sana sana kuhusu maagano na viapo
 
Hakuna anayenusurika kufa labda siku haijafika tu,Wakati unakufa huwa unaoneshwa jinsi ulivoishi na huko unapoenda utaishi vipi.(KAMA ULIKUA MWEMA UTAONESHWA NA MAHALA PEMA UENDAPO MARA NYINGI WATU HAWA UFARIKI HALI YA KUWA WANACHEKA NA HAKUNA VURUGU WAKATI ROHO INATOKA...KAMA ULIKUA MUBAYA UTAONESHWA MAHALA PABAYA UENDAPO MARA NYINGI WATU HAWA HUFA KIUBAYA ZAIDI VURUGU NYINGI WENGINE HUTOA ADI MACHO KWA KUSHANGAA SEHEMU MBAYA ANAYOELEKEA)
Umewahi kui-experience hiyo hali?
 
Matola you either don't understand English or uandishia wako umejawa na mhehemko. Nkuba25 did not say/write Gods rather he/she wrote God's - here the exclamation mark and S represent "Possession case" and not plural form of God.

Definitely!!! he doesn't get this language or if he does, very lightly.
In God's hands = Katika mikono ya Mungu, yeye anachukulia kama ni plural ya God i.e trying to say Gods.
 
Niandikapo mistari hii kuna watu wanakufa wengine watakufa baadae wengine usiku mwingi dunia ikiwa tulivu wengine kesho na kuendelea...mbele yao nyuma yetu
f4ced6317175721b54bb48099322a24b.jpg

Kitu cha kushangaza kutoka wale walionusurika kifo ni simulizi zao za yale waliyoyaona au kukutana nayo pale roho zilipokuwa katikati ya kuzimu na dunia
Lakini pia habari nyingine zinasema kuwa watu wanapokuwa katika kipindi hicho,wengi
- huona maisha yao yakipita mbele ya macho yao kama sinema
-wengine mabaya yao hujifunua na kuyasimulia bila kujua
-wengine huomba msamaha
-wengine huomba msaada
-wengine hujiona wakienda mbali sana
Wengine huona moto, malaika au viumbe wa ajabu
Kwa ujumla wake hali hii huelezewa kama hari za kifo...ni kipindi kigumu mno kwa wale wanaokutana na hizi mambo
Lakini kuna wengine hufa wakiwa usingizini kwa amani kabisa wala bila kujitambua kuwa wamekufa , hawa nyuso zao huonekana zimetulia kabisa ni kama wamelala.....!!! Kitu cha ajabu ni wale wafao huku hari za kifo zikiwaandama nyuso hukunjamana na kubaki na maumivu hata baada ya roho kuachana na mwili
Usiwe mtu wa vinyongo Usiwe mtu wa dhuluma Usiwe mtu wa visasi Usiwe mtu wa rohombaya, vitu hivi huzalisha roho zitakazokutesa mpaka kifo....kama una nyongo umezihifadhi tumboni jitahidi kuzitapika usiku huu..ya kesho huyajui
Sasa marehemu anaona tena! Au unamanisha watu huona nini wanapokaribia kuaga dunia?? Kabla ya kufa huwezi mwita mtu marehemu..
 
Back
Top Bottom