BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata watuhumiwa saba kwa tuhuma za kupanga njama, kumtishia kwa silaha, na baadaye kumteka mwanamke aliyefahamika kwa jina la Hani Hussein (29) Mkazi wa Masaki, Dar es Salaam.
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashilia watuhumiwa saba kwa madai ya kupanga njama, kumtishia kwa silaha na kumteka mwanamke aaliyefahamika kwa jina la Hani Hussein (29), mkazi wa Masaki.
Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro leo Oktoba 30, 2023 amesema tukio la kumteka binti huyo lilitokea Oktoba 16, 2023.
“Tukio hili limetokea Oktoba 16, 2023 saa nne asubuhi wakati Hani Hussein akiwa anaendesha gari lake aina ya Toyota Rav4, ghafla akiwa eneo la Msasani Village alisimamishwa na sehemu ya kundi la watuhumiwa hao na kuingia ndani ya gari, kumtishia kwa silaha, kumteka na kuelekea maeneo ya Mbezi Beach mtaa wa ujirani ambako walimshikilia kwa nguvu kwa siku nne huku wakidai fedha kwa vitisho kwa baba wa mtekwaji kuwa asipotoa kiasi cha Dola za Marekani 3.5 milioni mtoto wake angepoteza maisha.
"Baada ya kupata taarifa ya tukio hilo, Jeshi la Polisi lilianza ufuatiliaji wa na Oktoba 19 tulifanikiwa kumuokoa na kuwakamata watekaji wote wakiwa na gari walilomteka, pamoja na silaha ilyotumika Pistol Glock 19 iliyotengenezwa Austria ikiwa na risasi 4," amesema Kamanda Muliro.
Amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Hassan AbusherNur (39) raia wa Canada mwenye asili ya Somalia na mkazi wa Msasani, Nathan Lungumisa (27), Fredick Chahonza (49), Assad Abdurasur (43), Fahad Mussa (32), Ilfan Saleh (41) na Nicolas Nilay (39).
Aidha ameeleza kuwa tayari upelelezi na watuhumiwa wote watafikishwa Mahakama ya Kisutu kwa hatua zaidi za kisheria.
MWANANCHI
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashilia watuhumiwa saba kwa madai ya kupanga njama, kumtishia kwa silaha na kumteka mwanamke aaliyefahamika kwa jina la Hani Hussein (29), mkazi wa Masaki.
Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro leo Oktoba 30, 2023 amesema tukio la kumteka binti huyo lilitokea Oktoba 16, 2023.
“Tukio hili limetokea Oktoba 16, 2023 saa nne asubuhi wakati Hani Hussein akiwa anaendesha gari lake aina ya Toyota Rav4, ghafla akiwa eneo la Msasani Village alisimamishwa na sehemu ya kundi la watuhumiwa hao na kuingia ndani ya gari, kumtishia kwa silaha, kumteka na kuelekea maeneo ya Mbezi Beach mtaa wa ujirani ambako walimshikilia kwa nguvu kwa siku nne huku wakidai fedha kwa vitisho kwa baba wa mtekwaji kuwa asipotoa kiasi cha Dola za Marekani 3.5 milioni mtoto wake angepoteza maisha.
"Baada ya kupata taarifa ya tukio hilo, Jeshi la Polisi lilianza ufuatiliaji wa na Oktoba 19 tulifanikiwa kumuokoa na kuwakamata watekaji wote wakiwa na gari walilomteka, pamoja na silaha ilyotumika Pistol Glock 19 iliyotengenezwa Austria ikiwa na risasi 4," amesema Kamanda Muliro.
Amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Hassan AbusherNur (39) raia wa Canada mwenye asili ya Somalia na mkazi wa Msasani, Nathan Lungumisa (27), Fredick Chahonza (49), Assad Abdurasur (43), Fahad Mussa (32), Ilfan Saleh (41) na Nicolas Nilay (39).
Aidha ameeleza kuwa tayari upelelezi na watuhumiwa wote watafikishwa Mahakama ya Kisutu kwa hatua zaidi za kisheria.
MWANANCHI