Watoto!!

Nikikumbuka nilivyoteswa na shangazi yangu nakosa cha kusema nimebaki na huzuni tu

Huzuni yako huzuni yetu...pole ndugu!Ila sasa hivi umechana na adha hiyo kwahiyo tuliza moyo wako wala usihuzunike!
 
Kila siku tunaongelea mapenzi tunasahau watoto....embu leo tuwe kifamilia zaidi.

Leo kuna kipindi nlikua naangalia kikanisikitisha sana.Kuna mwanamke yeye anamwadhibu mtoto wake kwa kumnywesha pilipili na kumuogesha maji baridi kabisa...wakati mwingine eti anamlisha sabuni.

Nikakumbuka wakati nakua kuna mtoto wa jirani yetu yeye alikua naishi na babu yake, siku moja aliachwa nyumbani alafu akaenda kucheza....babu yake alivyorudi alichofanya ni kumchapa alafu akamweka kwenye gunia lenye yale majani yanayowasha alafu akamtundika wakati chini moto unawaka.Yule mtoto alitoka mwekundu kama nini sijui....sikumbuki kama kuna jirani aliyethubutu kumkemea yule mzee.Nyingine tuliwahi kua na msichana wa kazi ambae alikua na mtoto wa zaidi ya mwaka mmoja.....ilikua tukiwa shule yule dada anamfunga mtoto wake kwenye mguu wa kitanda ili eti asimsumbue.Yule mtoto analia na kukojoa pale pale mpaka analala...tukirudi basi tunakakuta kamelala uvunguni.Anagombezwaaa ila tukiwa hatupo tu anafanya vile vile.
Bila kusahau wale watu wanaoishi na watoto wa wenzao pamoja na wa kwao alafu wanawatreat fofauti.Kuna baadhi ya ndugu zangu nimewahi kuishi nao wa aina hiyo.....unakuta wale watoto wasio na mtu wa kumlilia wananyanyaswa ila wale wakwao na wale wenye ndugu au wazazi wao wenye uwezo wanalelewa vizuri tu.
Na yule aliyevutwa nyusi na mwalimu mpaka macho yakageuka!!

Kusema kweli hizi hali zote zinasikitisha.Kuona mtu mzima anamnyanyasa mtoto kwa sababu yoyote ile na kwa kisingizo chochote kile haifai.Wengi wao hawana wa kumlilia na kushtaki sio kitu ambacho kinaweza kufanyika kirahisi kwasababu kitendo cha kumpeleka mzazi au ndugu anaekulea kwenye vyombo vya sheria mara nyingi itaongeza matatizo zaidi ya kupunguza..

Naomba niwaombeni wanajamii tuwe na huruma jamani.Awe mtoto wako...wa ndugu au jirani jaribu kutokua mnyanyasaji.Kama mzazi kua na ukaribu na mwanao ili hata kama kuna mtu mwingine anaemnyanyasa iwe shuleni, mtaani au nyumbani iwe rahisi kukwambia.Na kwa wale ambao wanaishi na watu ambao sio wazazi halisi wa wanao (mama na baba wa kambo) kua na tabia ya kuongea na mwanao kujua mambo yanayoendelea nyumbani ukiwa haupo.
Mateso ya utotoni hua yanaacha makovu mabaya sana....JALI NA KUA NA HURUMA huo ndo ubinadamu!
Lizzy nilipata bahati ya kuona picha za huyo mtoto aliyevutwa nyusi na mwalimu mpaka macho yakavimba in short ni kwamba hizo picha zilikuwa zinahuzunisha sana na zinatisha ni kama vile macho ya huyo mtoto yalikuwa yameliwa na wadudu tuwe na huruma na watoto jamani.
 
Kila siku tunaongelea mapenzi tunasahau watoto....embu leo tuwe kifamilia zaidi.

Leo kuna kipindi nlikua naangalia kikanisikitisha sana.Kuna mwanamke yeye anamwadhibu mtoto wake kwa kumnywesha pilipili na kumuogesha maji baridi kabisa...wakati mwingine eti anamlisha sabuni.

Nikakumbuka wakati nakua kuna mtoto wa jirani yetu yeye alikua naishi na babu yake, siku moja aliachwa nyumbani alafu akaenda kucheza....babu yake alivyorudi alichofanya ni kumchapa alafu akamweka kwenye gunia lenye yale majani yanayowasha alafu akamtundika wakati chini moto unawaka.Yule mtoto alitoka mwekundu kama nini sijui....sikumbuki kama kuna jirani aliyethubutu kumkemea yule mzee.Nyingine tuliwahi kua na msichana wa kazi ambae alikua na mtoto wa zaidi ya mwaka mmoja.....ilikua tukiwa shule yule dada anamfunga mtoto wake kwenye mguu wa kitanda ili eti asimsumbue.Yule mtoto analia na kukojoa pale pale mpaka analala...tukirudi basi tunakakuta kamelala uvunguni.Anagombezwaaa ila tukiwa hatupo tu anafanya vile vile.
Bila kusahau wale watu wanaoishi na watoto wa wenzao pamoja na wa kwao alafu wanawatreat fofauti.Kuna baadhi ya ndugu zangu nimewahi kuishi nao wa aina hiyo.....unakuta wale watoto wasio na mtu wa kumlilia wananyanyaswa ila wale wakwao na wale wenye ndugu au wazazi wao wenye uwezo wanalelewa vizuri tu.
Na yule aliyevutwa nyusi na mwalimu mpaka macho yakageuka!!

Kusema kweli hizi hali zote zinasikitisha.Kuona mtu mzima anamnyanyasa mtoto kwa sababu yoyote ile na kwa kisingizo chochote kile haifai.Wengi wao hawana wa kumlilia na kushtaki sio kitu ambacho kinaweza kufanyika kirahisi kwasababu kitendo cha kumpeleka mzazi au ndugu anaekulea kwenye vyombo vya sheria mara nyingi itaongeza matatizo zaidi ya kupunguza..

Naomba niwaombeni wanajamii tuwe na huruma jamani.Awe mtoto wako...wa ndugu au jirani jaribu kutokua mnyanyasaji.Kama mzazi kua na ukaribu na mwanao ili hata kama kuna mtu mwingine anaemnyanyasa iwe shuleni, mtaani au nyumbani iwe rahisi kukwambia.Na kwa wale ambao wanaishi na watu ambao sio wazazi halisi wa wanao (mama na baba wa kambo) kua na tabia ya kuongea na mwanao kujua mambo yanayoendelea nyumbani ukiwa haupo.
Mateso ya utotoni hua yanaacha makovu mabaya sana....JALI NA KUA NA HURUMA huo ndo ubinadamu!
Lizzy hapa ndipo napokupendea
Be blessed
 
Lizzy nilipata bahati ya kuona picha za huyo mtoto aliyevutwa nyusi na mwalimu mpaka macho yakavimba in short ni kwamba hizo picha zilikuwa zinahuzunisha sana na zinatisha ni kama vile macho ya huyo mtoto yalikuwa yameliwa na wadudu tuwe na huruma na watoto jamani.

Fynest bwana!Kisa chakunipa picha asubuhi yote hii?Tena digito!Sijui aliyefanya hivyo aliionaje kazi ya mikono yaketa afterwards!
 
Nakumbuka shuleni(msingi) tulikuwa tunafanyishwa kazi za bustani, kusomba tofali na nyingine nyingi eti elimu ya kujitegemea walimu wanakula mshiko usipofanya unakula SSS... Enzi hizo utasikia watoto wa walimu, afisa elimu, mtendaji walikuwa ni wagonjwa wa kudumu hivyo hawatakiwi kufanya kazi ngumu
 
Lizzy hapa ndipo napokupendea
Be blessed

Hata mi nakupenda pia Marytina sema na wewe kuhusiana na ile thread, ishu nzima inaweza kugeuka aina ya unyanyasaji mkamwachia mtoto makovu ya ajabu!Kuweni waangalifu na msijifikirie wenyewe tu!Nwy ubarikiwe mpendwa!
 
Matesha wangu ana miaka kumi sasa. Sikumbuki kama nlishawahi kumchapa japo kwenzi. Na tabia yae ni njema hakuna mfano. Kupiga si kufunza tabia njema. Zungumzeni na watoto wenu, sikilizeni shida na matatizo yao. Wasaidieni kupata suluhisho. Waongozeni njia kwa upendo wanapokosea. Kuweni mfano kwa kutenda yaliyo mema.

Napenda sana watoto.

Alaaniwe anayetesa na kuwapiga watoto na wanawake.

Mungu na amrehemu.
 
Lizy umenikumbusha kipindi wazazi wangu walipofariki!!! jina langu lilibadilika na kuwa mbwa, nguruwe, masikini, fisi, paka mweusi ila namshukuru Mungu aliyejuu leo niliyekuwa paka mweusi nimekuwa dhahabu kwao wao!!

Nampenda Mungu Jehovah aliyenitoa chini na kuniketisha kitini na Wafalme, ama kweli yy huviinua vinyonge!!!

Ni vibaya sana kumfanyia mtu vibaya kwakuwa ww huijui kesho yake!!!
 
Nakumbuka shuleni(msingi) tulikuwa tunafanyishwa kazi za bustani, kusomba tofali na nyingine nyingi eti elimu ya kujitegemea walimu wanakula mshiko usipofanya unakula SSS... Enzi hizo utasikia watoto wa walimu, afisa elimu, mtendaji walikuwa ni wagonjwa wa kudumu hivyo hawatakiwi kufanya kazi ngumu

Hahahaha walimu wengine hua wanawatumia wanafunzi kama kitega uchumi!Hovyo kweli!
 
Lizy umenikumbusha kipindi wazazi wangu walipofariki!!! jina langu lilibadilika na kuwa mbwa, nguruwe, masikini, fisi, paka mweusi ila namshukuru Mungu aliyejuu leo niliyekuwa paka mweusi nimekuwa dhahabu kwao wao!!

Nampenda Mungu Jehovah aliyenitoa chini na kuniketisha kitini na Wafalme, ama kweli yy huviinua vinyonge!!!

Ni vibaya sana kumfanyia mtu vibaya kwakuwa ww huijui kesho yake!!!

Pole sana dear!Dah wanadamu sie tuna mambo!Ila uzuri Mungu hamtupi mja wake!
 
Lizy umenikumbusha kipindi wazazi wangu walipofariki!!! jina langu lilibadilika na kuwa mbwa, nguruwe, masikini, fisi, paka mweusi ila namshukuru Mungu aliyejuu leo niliyekuwa paka mweusi nimekuwa dhahabu kwao wao!!

Nampenda Mungu Jehovah aliyenitoa chini na kuniketisha kitini na Wafalme, ama kweli yy huviinua vinyonge!!!

Ni vibaya sana kumfanyia mtu vibaya kwakuwa ww huijui kesho yake!!!
pole sana dear
 
Asante sana Lizzy,

Huwa mara nyingi nashindwa kuelewa unavyoafikiria hadi kupata topic zenye mvuto wa aina yake kama hii hapa.

Nashindwa pa kuanzia kwani hadithi zangu katika haya mambo ya kunyanyasa watoto ni za kutisha....Naomba nijizuie kueleza zaidi ya hapo.

Hata hivyo wanangu nawachapa inapobidi, nawapenda sana, nawajali na ustawi wao ni kipaumbele changu cha kwanza. Sitaki wapate maisha ya ajabu na mateso kama niliyopata mimi!

Hata hivyo baadhi ya watoto wanakuwa na vitu vya ajabu ajabu..mfano, wengine anajifunza uongo bado wadogo sana. Jambo la muhimu ni kwa wazazi kuwasaidia na pia kujitahidi kuwa mfano bora kwao.

Ila kuna wazazi wengine wanalea watoto wao kama vitu visivyo na thamani yoyote...Kwa ni kama magunia ya takataka, na hali inakuwa mbaya waki wengi sana!
 
Aisee Susy hapo juu.

Nimesikitika sana wakati naisoma posti yako lakini mwisho wa posti nimefarijika sana.

Hatupaswi kulipa visasi...na kuitwa kwako mbwa, nguruwe nk labda niyo vimekufikisha hapo ulipo. Samehe na chapa mwendo.

Pole kwa kuwapoteza wazazi wako, na Mungu aendelee kukupa nguvu.

Babu Asprin amekupenda ghafla.
 
Aisee Susy hapo juu.

Nimesikitika sana wakati naisoma posti yako lakini mwisho wa posti nimefarijika sana.

Hatupaswi kulipa visasi...na kuitwa kwako mbwa, nguruwe nk labda niyo vimekufikisha hapo ulipo. Samehe na chapa mwendo.

Pole kwa kuwapoteza wazazi wako, na Mungu aendelee kukupa nguvu.

Babu Asprin amekupenda ghafla.

Kweli mkuu,

Hii thread imenipa wakati mgumu. Huwa nikikumbuka hayo mambo hatima yake ni kumwaga machozi mbele za watu.. Ngoja nijaribu kuzuia kwani umri huu kuanza kuangua kilio si jamboo dogo!

Maj Gen DC!
 
Fynest bwana!Kisa chakunipa picha asubuhi yote hii?Tena digito!Sijui aliyefanya hivyo aliionaje kazi ya mikono yaketa afterwards!
Umenikumbusha sababu nilijaribu kufuatilia kwa karibu hicho kisa, you can imagine huyo mtoto after that incident baada ya kupelekwa CCBRT ambao ndio wataalamu wa macho baada ya kumfanyia uchunguzi akaambiwa harusiwi kukaa kwenye jua inabidi pia akae sehemu ambayo hakuna mwanga mpaka apone sasa na huyu mtoto alikuwa anasoma atakuwa amekosa mambo mangapi
 
Hehe babu DC ntakwambia siri yangu siku nyingine!Pole kwa yaliyokukuta na hongera kwa kuwapenda wanao na kutaka kuwafunza kabla ya dunia!Kumchapa mtoto kama kunaendana na kiasi ni sawa kabisa!Mi nakumbuka marehemu bibi yangu aliwahi kunichapa mara moja tu tena kwasababu nilidanganya.Siku hiyo nilikasirika nikajiambia namchukia ila tangu siku hiyo nilichukia uongo!Sasa hivi hua nashukuru Mungu alinipa vile viboko maana vilinijenga na nnampenda sana kwa hilo!Kwahiyo babu tembeza viboko inapobidi!
 
Lizy umenikumbusha kipindi wazazi wangu walipofariki!!! jina langu lilibadilika na kuwa mbwa, nguruwe, masikini, fisi, paka mweusi ila namshukuru Mungu aliyejuu leo niliyekuwa paka mweusi nimekuwa dhahabu kwao wao!!

Nampenda Mungu Jehovah aliyenitoa chini na kuniketisha kitini na Wafalme, ama kweli yy huviinua vinyonge!!!

Ni vibaya sana kumfanyia mtu vibaya kwakuwa ww huijui kesho yake!!!
Pole sana Susy
 
Umenikumbusha sababu nilijaribu kufuatilia kwa karibu hicho kisa, you can imagine huyo mtoto after that incident baada ya kupelekwa CCBRT ambao ndio wataalamu wa macho baada ya kumfanyia uchunguzi akaambiwa harusiwi kukaa kwenye jua inabidi pia akae sehemu ambayo hakuna mwanga mpaka apone sasa na huyu mtoto alikuwa anasoma atakuwa amekosa mambo mangapi

So unfair!Sijui watu huruma ya kibinaadamu wameuza kwa bei gani!
 
Hehe babu DC ntakwambia siri yangu siku nyingine!Pole kwa yaliyokukuta na hongera kwa kuwapenda wanao na kutaka kuwafunza kabla ya dunia!Kumchapa mtoto kama kunaendana na kiasi ni sawa kabisa!Mi nakumbuka marehemu bibi yangu aliwahi kunichapa mara moja tu tena kwasababu nilidanganya.Siku hiyo nilikasirika nikajiambia namchukia ila tangu siku hiyo nilichukia uongo!Sasa hivi hua nashukuru Mungu alinipa vile viboko maana vilinijenga na nnampenda sana kwa hilo!Kwahiyo babu tembeza viboko inapobidi!

Lizzy please...hilo jina la babu lilikufa ili kumwachia mzee wa Liliondo na kikombe chake!

Nakushukuru sana kwa kunielewa linapokuja suala la kumchapa mtoto pale anapokosea na kama kuna sababu ya msingi ya kufanya hivyo. Na pia adhabu ilingane na kosa na umri wa mtoto. Kwa hiyo mimi ni muumini wa kiboko cha ulezi ili mtoto ajue kuwa akikosea ataadhibiwa na kurekebishwa! Hata hivyo napinga sana adhabu za kuumiza na kuharibu watoto kwani mimi ni muhanga wa hayo mambo!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom