Watoto wa vigogo na ajira BoT

Watoto wa vigogo na ajira BoT


Ndio maana nawaunga mkono masela wa vjiweni kwa kauli yao kuwa "bora vita ije nchi hii kila mtu achukue chake.....!" Si unaona watoto wa gadafi now, wako ndani ikiwa ni pamoja na kujilundikia mali huku watu vijijini hawana maji safi ya kunywa.

Kibanga Msese
 
Maskin atazidi kuwa maskin naye tajiri atajirike zaid*2 nawapigia makofi eeh
 
Gazeti la Jamuhuri la October 23, 2012 Limewataja vijana wafuatao kuwa ni watoto wa vigogo waliojazana BOT: Kweli Tanzania ina wenyewe


Salama Ali Hassan Mwinyi
Filbert Tluway Sumaye
Zaria Rashid Kawawa
Blasia William Mkapa
Herriet Marten Lumbanga
Pamela Edward Lowassa
Rachel Muganda
Salma Omary Mahita
Justine Mungai
Kenneth Nchimbi
Violet Philemon Luhanjo
Liku Kate Kamba
Thomas Mongela
Jabir Abdallah Kigoda......

Hujaeleweka mkuu. Issue siyo kufanyia kazi BOT, je wana sifa? Kama wana sifa mie sioni tatizo wana haki kama mtu mwingine yeyote.
 
Ni mwendo wa vimemo tu mkuu! ukija majira ya joto mwakani utalikuta jina la Mwanaisha wa jeikei. Hapo hakuna kitu kama merit ama competence bali Mungu tu anajua.
 
Hii ni nchi ya chukua chako mapema, nashangaa sana watu wanaoishabikia ccm hii labda ya 1977. Si Bot au ndani ya ccm yenyewe ni watoto wa wakubwa kwa kwenda mbele si nape wala january!
 
Sijui ni kwanini baba yangu hakutafuta kiwanja kigogo. Ungekuta na mimi ni mtoto wa kigogo sasa.
 
Sio kila mtu alioko BOT kaingia kwa kubebwa wengine wanasifa za vyeti vya baba zao na CV za dada zao.
Tanzania ni zaidi nchi...
 
Kwa wingi wa majina hayo ipo wazi hawajaingia kwa kufuata kanuni na taratibu za ajira. Haiwezekani kuwa coincidence hata siku moja.
Mimi nilidhani ni kwenye siasa tu ndo wanapachikana. Kwa mtindo huu nchi imekwisha. Lazima tufanye mabadiliko. La sivyo hatutafika mahali.
 
2594_60951381103_513551103_1983304_8013546_n.jpg


Huyo hapo mwenye miwani anaitwa JABIR OMARI KIGODA. Ni mtoto wa fisadi Bw. Abdallah Omari Kigoda. Nasikia jamaa alipata DIVISION FOUR kidato cha nne lakini hivi sasa ana kazi nzuri tu katika benki (YAO) ya biiiiooootiii BOT(BANGAIZA ONGA TOKOMEA) kwa vyeti feki.
Kuna kitu kimoja ambacho mimi binafsi naamini ya kwamba huwezi zuia mvua. Lakini tunaweza zuia watu kama hawa wasiendelee na tabia kama hii YA KUDHOROTESHA UCHUMI WETU. Ningemwomba Mh. JK awaamuru wakaguzi wake wapitie waajiriwa wote na kufukuza watu kama hawa ambao wamejazana tu kwenye ofisi ambazo zina watu wanaostahiri(WASOMI WENYE VYETI VISIVYO BANDIA)
Kuwekana ndugu kwa ndugu kwenye ofisi bila kwalifikesheni huitwa(NEPOTISM), kitu ambacho always huaribu ufanisi wa kazi.
BABA yake mzee Kigoda mwenyewe ni fisadi mkubwa, na nimesikia amenunua hoteli mbili huko mkoani Tanga kwa pesa ya walalahoi. Je mambo haya yataisha lini ndugu wadau?
Source:ZEUCHUNGU : VIONGOZI TUGAWANE UMASKINI: KUJIACHIA TUUUUUUU

 
KAKA ACHA MAPEPE,UNAJITUNGIA HABARI TU HAPA,KAMA HUNA KIPYA KAA PEMBENI.KWANZA SUMAYE HANA MTOTO ANAEITWA ROGERS,BALI ANA WATOTO WAWILI AMBAO NI FILBERT NA FRANK,PILI FILBERT ALIRUDI NCHINI BAADA YA KUMALIZA MASTERS YAKE YA COMPUTER SCIENCE.NA ALIPORUDI ALIKAA MIEZI NANE AKIFANYA KAZI KTK KAMPUNI BINAFSI NDIO AKAAJILIWA.HUO UZUSHI UMETOA WAPI KAKA?ATA UKIULIZA WATU ALIOSOMA NAO TOSAMAGANGA F 5&6 WATAKWAMBIA JINSI ALIVYO MTU SIMPLE NA WAKUJITUMA.KAZINI KWAKE WANAMTEGEMEA MTAFUTE BOSI WAKE MZEE MASAWE ATAKWAMBIA.PIA WAPO WENYE CPA NA
NK.WIVUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU MBAYA JAMANI
Ndo maana unajiita fisadi mtoto
 
Huyo hapo mwenye miwani anaitwa JABIR OMARI KIGODA. Ni mtoto wa fisadi Bw. Abdallah Omari Kigoda. Nasikia jamaa alipata DIVISION FOUR kidato cha nne lakini hivi sasa ana kazi nzuri tu katika benki (YAO) ya biiiiooootiii BOT(BANGAIZA ONGA TOKOMEA) kwa vyeti feki.
Kuna kitu kimoja ambacho mimi binafsi naamini ya kwamba huwezi zuia mvua. Lakini tunaweza zuia watu kama hawa wasiendelee na tabia kama hii YA KUDHOROTESHA UCHUMI WETU. Ningemwomba Mh. JK awaamuru wakaguzi wake wapitie waajiriwa wote na kufukuza watu kama hawa ambao wamejazana tu kwenye ofisi ambazo zina watu wanaostahiri(WASOMI WENYE VYETI VISIVYO BANDIA)
Kuwekana ndugu kwa ndugu kwenye ofisi bila kwalifikesheni huitwa(NEPOTISM), kitu ambacho always huaribu ufanisi wa kazi.
BABA yake mzee Kigoda mwenyewe ni fisadi mkubwa, na nimesikia amenunua hoteli mbili huko mkoani Tanga kwa pesa ya walalahoi. Je mambo haya yataisha lini ndugu wadau?
Source:ZEUCHUNGU : VIONGOZI TUGAWANE UMASKINI: KUJIACHIA TUUUUUUU


hapo umechemka
 

Siku chache baada ya kuibuka mjadala wa kuwapo watoto wengi wa vigogo ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), hali kama hiyo imejitokeza tena kwenye Idara ya Afya katika Jiji la Dar es Salaam na manispaa zake tatu za Temeke, Ilala na Kinondoni, JAMHURI imebaini.

Baadhi ya wafanyakazi wa Idara hiyo, wametoa waraka wakihoji namna watoto hao wa vigogo walivyoweza kushika nyadhifa kubwa katika manispaa hizo, ilhali watumishi wengine wenye sifa, ama wakiachwa au wakipelekwa mbali na Jiji la Dar es Salaam.

Katika waraka huo, ambao JAMHURI imepata nakala yake, wanatajwa baadhi ya watoto wa vigogo na nyadhifa zao kuwa ni Janeth George Kahama, ambaye ni Mganga Mkuu wa Jiji.


Huyu anatoka katika familia ya Mzee George Kahama, mmoja wa mawaziri wawili walio hai wa kwanza katika Baraza la Kwanza la Mawaziri la Tanganyika huru. Mwingine aliye hai ni Job Lusinde.

Waraka huo pia unasema nafasi ya Mganga Mkuu Msaidizi wa Jiji la Dar es Salaam inashikwa na Dkt. Hawa Rashidi Kawawa. Huyu ni mtoto wa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Tanganyika, Waziri Mkuu wa Tanzania, na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Hivi ni kweli watoto hawa wa wakubwa ndiyo wenye sifa tu za kushika nyadhifa hizi? Kweli, wanaweza kuwa na sifa, lakini iweje wasipelekwe Tandahimba, Kibondo au Karagwe? Kwanini Dar es Salaam tu?” Wamehoji waandishi wa waraka huo.

Wameendelea kusema kuwa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni ni Dkt. Gunini Kate Kamba. Huyu ni mtoto wa Kamba aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza na ndani ya CCM. Wadhifa wa karibuni kabisa aliokuwa nao ni wa ubunge katika Bunge la Afrika Mashariki.

Kwa upande wa Manispaa ya Ilala, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo ni Dkt. Asha Omar Mahita. Dkt. Asha ni mtoto wa aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) mstaafu Omar Mahita.

Mtoto mwingine wa kigogo ni Dkt. Amani Kighoma Malima ambaye ni Mganga Mfadhiwi wa Hospitali ya Temeke. Huyu ni ndugu yake na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima.

Dkt. Amani ni mtoto wa marehemu Kighoma Malima, ambaye alishika nyadhifa mbalimbali serikalini. Mara ya mwisho kabla ya kufikwa na mauti alikuwa Waziri wa Fedha.

Aidha, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Temeke, Dkt. Sylvia Mamkwe, ingawa si mmoja wa watoto wa vigogo, lakini alikuwa na uhusiano wa karibu mno wa kikazi na aliyekuwa Mganga Watoto wengine wa vigogo waliojazwa Idara ya Afya.
Watoto wa vigogo wameshika nafasi zote za Jiji - Ilala, Temeke, Kinondoni

Mkuu wa Serikali, Dkt. Deo Mtasiwa; aliyeondolewa kwenye nafasi hiyo mwaka huu kutokana na shinikizo la madaktari waliogoma.

“Haya ni majina ya baadhi tu ya watoto wa vigogo katika Idara ya Afya katika Jiji la Dar es Salaam na Manispaa zake. Tunauliza, iweje watoto wa wakubwa tu ndiyo washike nyadhifa hizi kwa Dar es Salaam na si mikoani?” Umehoji waraka huo.

Wiki iliyopita, JAMHURI iliandika taarifa ya kuwapo watoto wengi wa vigogo ndani ya BoT.

-----------------------------------------------------------
Hadi sasa, majina yanayovuma ya watoto hao ni:

1. Pamela Edward Lowassa,
2. Filbert Tluway Sumaye,
3. Zaria Rashidi Kawawa,
4. Harriet Matern Lumbanga,
5. Salama Ali Hassan Mwinyi,
6. Rachel Muganda,
7. Salma Omar Mahita,
8. Justina Joseph Mungai,
9. Kenneth Nchimbi,
10. Blasia William Mkapa,
11. Violet Philemon Luhanjo,
12. Liku Kate Kamba,
13. Thomas Mongella na
14. Jabir Abdallah Kigoda.
------------------------------------------------------------------
Kuwapo kwa watoto wa wakubwa katika sehemu nyeti na nzuri kumeanza kuzua minong’ono ya upendeleo miongoni mwa wananchi.

Mmoja wa wananchi amehoji hali hiyo kwa kusema, “Ninachojiuliza na sipati majibu mpaka sasa ni hiki, kama imetokea coincidence (bila kutarajia) BoT ikaajiri watoto 14 wa vigogo; je, coincidence hiyo hiyo inaweza kutokea kwenye Wizara ya Elimu watoto wenye majina kama hayo hayo wakapangwa kwenda kufundisha shule za kata vijijini, ambako hakuna maji wala umeme na wakaendelea kuifanya kazi hiyo kwa moyo wa kizalendo bila kujali kuwa mishahara imechelewa na hawajapandishwa vyeo; na wakati huo huo wakiidai serikali sikivu malikimbizo?
 
huu ujinga wa kuwasema watoto wa viongozi kana kwamba wao hawana haki ya kuajiriwa mi sikubalianai nao kabisa, nafikiri hoja ingekuwa:
wana sifa za kushika nafasi hizo au hawana sifa?
wana uwezo wa kuendesha nafasi walizo nazo au hawana uwezo?
walizipata kwa upendeleo au walishindanishwa na wengine katika usaili kisha wakapata?
elimu yao inaruhusu kushika nafasi hizo au hapana?

haya mengine ni ubaguzi kama ulivyo ubaguzi mwingine, kuwa mtoto wa waziri au wa nani sijui hakukuzuii kupata haki zingine kama mtanzania ikiwa pamoja na kuajiriwa
jamani muwaache wapumue,
msiwe kama uamsho ambao kazi yao ni kulalamika tu
unahusika binafsi kuwa katika hali uliyo nayo leo, never blame someone for the situation you are in
 
naona umesahau
aliyenacho ataongezewa na asiyenacho atanyang'anywa hata kidogo alichonacho
 
huu ujinga wa kuwasema watoto wa viongozi kana kwamba wao hawana haki ya kuajiriwa mi sikubalianai nao kabisa, nafikiri hoja ingekuwa:
wana sifa za kushika nafasi hizo au hawana sifa?
wana uwezo wa kuendesha nafasi walizo nazo au hawana uwezo?
walizipata kwa upendeleo au walishindanishwa na wengine katika usaili kisha wakapata?
elimu yao inaruhusu kushika nafasi hizo au hapana?

haya mengine ni ubaguzi kama ulivyo ubaguzi mwingine, kuwa mtoto wa waziri au wa nani sijui hakukuzuii kupata haki zingine kama mtanzania ikiwa pamoja na kuajiriwa
jamani muwaache wapumue,
msiwe kama uamsho ambao kazi yao ni kulalamika tu
unahusika binafsi kuwa katika hali uliyo nayo leo, never blame someone for the situation you are in

utakuwa mtt wa kigogo ww
 
huu ujinga wa kuwasema watoto wa viongozi kana kwamba wao hawana haki ya kuajiriwa mi sikubalianai nao kabisa, nafikiri hoja ingekuwa:
wana sifa za kushika nafasi hizo au hawana sifa?
wana uwezo wa kuendesha nafasi walizo nazo au hawana uwezo?
walizipata kwa upendeleo au walishindanishwa na wengine katika usaili kisha wakapata?
elimu yao inaruhusu kushika nafasi hizo au hapana?

haya mengine ni ubaguzi kama ulivyo ubaguzi mwingine, kuwa mtoto wa waziri au wa nani sijui hakukuzuii kupata haki zingine kama mtanzania ikiwa pamoja na kuajiriwa
jamani muwaache wapumue,
msiwe kama uamsho ambao kazi yao ni kulalamika tu
unahusika binafsi kuwa katika hali uliyo nayo leo, never blame someone for the situation you are in

Una vested interests na hawa watoto. haiwezekani wote wakawekwa sehemu "nzuri" as if watoto wa maskini ambao baba na mama zao hawana majina wasiwemo. wangapi wapo mitaani hawana ajira na wana sifa nzuri, LAKINI WA VIGOGO WOTE WANA KAZI. hakuna haki kabisa. Unasema kama hujafikiri !
 
Back
Top Bottom