Watoto kumsikiliza zaidi mama yao kuliko baba ni machungu

Kweli na hasa sisi wanawake. Tunapenda sana kujihesabia haki jamani.
True kabisa tena na mnavyowafundisha watoto kujenga chuki dhidi ya baba kisa tu ugomvi wenu, kimsingi hilo jambo sio zuri aidha litawaathiri kisaikolojia au baadae na pia utawapandikiza roho ya kisasi na chuki jambo ambalo kwa watoto sio vizuri...

Mkigombana yamalizeni kiutu uzima na sio kuwahusisha watoto kwa kuwa haileti taswira nzuri kifamilia na hata mbele ya jamii inayokuzungukeni..

Kesi za namna hii husababisha watoto kumsikiliza Mama tu na hata wakati mwingine kumpuuza/kumdharau Baba mzazi kisa tu, Mama aliwaambia watoto wamchukie Baba..

Hili jambo hupelekea mmomonyoko wa maadili(heshima/ustaarabu) kutokea kwenye jamii yetu kutokana na kuwa watoto wamekosa malezi ya upande wa mzazi wa kiume kitu ambacho sio kizuri..

Kiuhalisia mtoto anahitaji malezi ya wazazi wote wawili na pia sio vyema kujenga mazingira ya kumchukia Baba au kuchukiana miongoni mwa wanafamilia.. Tuboreshe mahusiano yetu ya kifamilia tuishi vyema...Migogoro iwe sehemu ya kujifunza na tusiiendekeze,tuonyane na turekebishane kwa ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla hasa kwenye suala la Maadili mema
 
ili familia iende vizuri lazima baba awe mkali, matokeo yake watoto humchukia baba, ikitokea mama hajielewi ni rahisi sana watoto kuside na mama na kumtenga baba, watoto wanaweza wapenda wote baba na mama kila mtu ananafasi yake.
Hapa issue ni mama anatakiwa awe rational na kuwa na busara katika kujua maamuzi anayofanya baba ni kwa manufaa na ustawi wa familia na hivyo ampe support ili watoto wasione ni uamuzi tu wa baba.
Mama akiwa na hofu ya Mungu na busara hata baba akitoa adhabu ikimuuma mama hukimbilia chumbani na akirudi anamwambia mtoto usirudie tena . akifanya hivyo na watoto watajua kuwa hilo ni kosa kwa baba na kwa mama na hivyo hawatakuwa wana base upande mmoja
 
Mama ndiye mlezi mkuu wa familia na hata jamii kwa ujumla hili linafahamika...lakini baba ana nafasi yake kubwa katika kuimarisha malezi yawe mazuri na yenye tija ikiwa ni pamoja na kutimiza majukumu na wajibu wake kama baba,hivyo inampasa kuwa na muda maalum kwa ajili ya familia yake,kama kazi zake ni za ubize sana.
Ikiwa wewe ni mama na unatambua u mlezi mkuu wa familia, basi migogoro yako na mumeo usiwashirikishe watoto wala kuongea mapungufu yake ikiwa ni pamoja na maneno ya kumshusha thamani baba yao.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umemlinda na kumtunzia heshima mumeo kwa watoto.
 
Ni kwa sababu 100% mtoto kama hawajambadilisha hospital ana uakika huyu ndo mama yake.

Mnachapiwa kisa muitwe baba, mtoto unajua kabisa sio wako ila kwa kuwa ulishawaambia ndugu kuwa ni wako unakufa kiume.mwanangu, mwanangu....

Kitanda hakizai halamu, kwenye uwezo wa kutoa matumizi ndo baba.

Mama ni mama, nani kama mama.

Baba ni baba ila sometimes sio baba.

Wenye janga kubwa hilo ni wale ambao hawana ndoa rasmi, ila na kwenye ndoa linawakumba ila kwa asilimia ndogo.

NOTE: sio wote jamani naomba munielewe.
nimekusamehe kwa kuwa umejitetea mapema
 
True kabisa tena na mnavyowafundisha watoto kujenga chuki dhidi ya baba kisa tu ugomvi wenu, kimsingi hilo jambo sio zuri aidha litawaathiri kisaikolojia au baadae na pia utawapandikiza roho ya kisasi na chuki jambo ambalo kwa watoto sio vizuri...

Mkigombana yamalizeni kiutu uzima na sio kuwahusisha watoto kwa kuwa haileti taswira nzuri kifamilia na hata mbele ya jamii inayokuzungukeni..

Kesi za namna hii husababisha watoto kumsikiliza Mama tu na hata wakati mwingine kumpuuza/kumdharau Baba mzazi kisa tu, Mama aliwaambia watoto wamchukie Baba..

Hili jambo hupelekea mmomonyoko wa maadili(heshima/ustaarabu) kutokea kwenye jamii yetu kutokana na kuwa watoto wamekosa malezi ya upande wa mzazi wa kiume kitu ambacho sio kizuri..

Kiuhalisia mtoto anahitaji malezi ya wazazi wote wawili na pia sio vyema kujenga mazingira ya kumchukia Baba au kuchukiana miongoni mwa wanafamilia.. Tuboreshe mahusiano yetu ya kifamilia tuishi vyema...Migogoro iwe sehemu ya kujifunza na tusiiendekeze,tuonyane na turekebishane kwa ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla hasa kwenye suala la Maadili mema
Asante jose
 
Pengine watoto wadogo, lakini wakishakuwa wakubwa huwa wanaona ukweli uko wapi, "You can fool some people sometimes, but you can`t fool all of the people all the time".

Mzazi yeyote anayewaingiza watoto kwenye magonvi yake na mzazi mwenzake, hana mapenzi ya dhati kwa watoto wake.
 
Ikiwa wewe ni mama na unatambua u mlezi mkuu wa familia, basi migogoro yako na mumeo usiwashirikishe watoto wala kuongea mapungufu yake ikiwa ni pamoja na maneno ya kumshusha thamani baba yao.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umemlinda na kumtunzia heshima mumeo kwa watoto.
Sasa hapo ndipo hekima na maarifa yanapotumika,.mwanamke aliye mpumbavu na mjinga ataharibu nyumba yake kwa mikono yake yeye mwenyewe.
 
Pia kumbuka baba wakati mwingine anakuwa bize sana kutokana na aina ya kazi yake hivyo mama anao muda mwingi wa kuwa na watoto. Hapo ndipo shida inapoanzia.
Samahani kama wewe ni mzazi na mimi nini mzazi, mtoto anapotoka tumboni harufu ya kwanza ni ya mama. Mtoto asiponyonya titi la mama anapata mapungufu ingawa wenzetu wana formula ya maziwa kubalance. Maneno ya mama na ile kumbatia ni tosha kumpa mtoto ukaribu kwake. Kazi ya baba ni kuleta ingawa siyo wote na kufoka.
Mapenzi ya mtoto yanatoka kwamama ndo maaana watoto amboa mama zao waliwaterekeza kuwa hamnazo, huwa wanaishia mitaani na ikitokea mama akafariki, mara nyingi watoto wanapata shida. Baba yeye ni kuuliza watoto wameshindaje, hawaoshi kuona kama wana makovu, mabaka wala hawajala wiki. Yeye anategemea neema za watu wengine kuambiwa yanayotokea kwenye familia yake.
 
Wababa watimize wajibu wao! Sidhani kama watoto ni wajinga kiasi hicho, amuone baba anamuhudumia, na anamuonesha upendo na bado amchukie!!
 
Ni kweli kabisa na ukichunguza kwa umakini jambo hili linashika kasi sana katika familia nyingi, na kama hujaambiwa na wanafamilia huwezi gundua.

Tatizo kubwa naona ni sisi kina mama tunajisahau na kuona kuwa tuna haki zaidi ya waume zetu.
Watoto pia tumeshindwa kusimamia nafasi zetu na kuegemea upande mmoja bila kutafakari madhara ya baadae.

Ni kweli hakuna kama mama, lakini hata baba pia ana mchango wake katika maisha yetu haijalishi mapungufu aliyonayo.
Ukiangalia familia nyingi za namna hii watoto wa kiume ndiyo humchukia zaidi na kumtenga baba kutokana na sababu mbalimbali za kifamili, bila kujali na wao watakuwa na familia na mambo kama haya yaweza tokea.
Na yanapokuja kutokea kwao ndipo huanza kulalama kuwa wanawake hawafai, mara hivi mara vile.
Tuweni na mioyo ya kuwasamehe wazazi wetu pale wanapoenda ndivyo sivyo na kusimamia nafasi zetu bila kujali.

Kwani sisi sote ni binadamu hatutakuja kuoa au kuolewa na malaika.

NB: Hii si kwaliotelekezwa na baba zao toka ujauzito, kuzaliwa hadi kuwa mtu mzima.
Nimefurahi umeandika kwa hisia kali...nina wazo.
Unajua wazazi wengi wa kiume wamekuwa wakali sana haswa kwa watoto wao,hakuna ukaribu,unakuta mtoto anakimbilia kwa mama kama kimbilio lake...hii tabia inavyoendelea unakuta Baba anakuwa anafoka,au kumpiga mama au kumtukana Mama mbele ya watoto huku wanaona hii inajengea hisia za chuki toka kwa watoto kwenda kwa Baba yao,hata ile tabia ya kufoka kila wakati,kukosa muda wa kufurahia na watoto wote,ukaribu na familia...Mwisho wa siku watoto wakikua wakubwa wanakuwa wanamtenga baba yao au wanampendelea zaidi Mama kwasababu hawavutiwi na Baba,na wababa wanakuwa wanaumia bila kujua chanzo haswa ni nini?
Unaweza kuta Mtoto akipiga simu nyumbani anweza kuongea na mama yake hata dakika 30,lakini akiongea na baba dakika 5,10 tuu hivyo baba anakuta anaumia kuwa "hivi muda wooote huo mlikuwa mnaongea nini na mtoto wako?etc etc
so vijana,kina Baba tubadilike tuwe karibu na watoto wetu na kuwapenda/kuwachukulia kama rafiki zetu angali wadogo.
 
Mtasingizia maneno bureeee, wanaume mnajitenga sana malezi ya watoto.
Busy na simu mkisogelewa wakaliii muda wote yupo na mama ataachaje kumpenda na kumsilikiza mama.
 
Back
Top Bottom