Watawala wetu mmerogwa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Na. M. M. Mwanakijiji

Naomba niandikie kutoka kwenye hisia kidogo; Naomba niandike toka kwenye vionjo vyangu vilivyojeruhiwa; Naomba niandikie kutoka kwenye moyo uliojawa na hasira, kero na ambao unajihisi kinyaa!; Naomba niandike kama mtu ambaye akili zake hazijakaa sawasawa na ambaye anaweza kuitwa "fyatu"! Naomba niandike kuhusu haya ya Shirika letu la ndege la ATCL ambalo limekuwa kituko cha taifa na aibu ya nchi yetu!

Watawala wetu mmerogwa? Tumefikaje hapa, je hili limefika kama kwa ghafla na kwamba hakukuwa na dalili zozote? Kwamba leo bila haya mnaitisha vikao vya dharura na kutoa "siku saba" za kupata maelezo toka kwa wazembe na waliofuja mali za shirika hili kana kwamba hamkuliona hili? Ati leo mnathubutu kuelezea kilichofanyika ATCL kuwa ni uzembe wakati kwa mwaka mzima vumbi lake mlishaliona toka mbali? Mmerogwa nyinyi?

Nauliza kama mmerogwa kwa sababu hakuna maelezo yoyote ya kiakili ambayo yana ushawishi wa kimantiki na yenye uzito wa ushahidi wa kisayansi yanaweza kuelezea ubutu wa matendo yenu na ukimya wa maneno yenu kwa mwaka mzima tangu king'ora cha tahadhari tulipokipuliza mwezi Disemba mwaka jana! Ni watu waliopumbazwa na dawa za mitishamba au waliorogwa 'kisayansi' ndio pekee wanaweza kufafanua ni kitu gani kiliwakumba. Mmepitiwa na jini gani lililowafanya mduwae na kuangusha midomo yenu ya chini na denda zikidondoka kama wale wasemwao "washangaao feri"?

Tuliimba na kupaza sauti, makoo yetu yakakauka. Tukawaambia tena bila kuuma uma maneno kuwa ATCL kuna uozo; tena uozo mkubwa wa kiuongozi. Tukaweza mipango yao ya kukodisha dege lenye matatizo ya kiufundi zaidi ya 100 tena kwa bei mbaya; tukawawekea na mikataba yao waliyoingia kuhusu dege hilo hilo, lakini muda wote huo nyinyi mkaendelea kukaa kimya na kuacha ATCL ijiendeshe kama kikaragosi kinachoenda kwa kupiga ufunguo!

Tukawawekea na ushahidi jinsi gani watendaji wa ATCL wamefuja mali zetu huku wakikinga mikono yao kuyupa zaidi; tukawaonesha jinsi mikakati yao ilivyokuwa mibaya na mibovu; tukawaonesha ni jinsi gani David Mattaka na genge lake la makuwadi wa ufisadi wameshindwa kuliongoza shirika hilo. Kwa mwaka mzima tumefanya hivyo pasipo mafanikio.

Tumefanya kama kile tulichokifanya kwenye suala la Ukraine miaka miwili iliyopita ambapo tulionesha upungufu na uozo wa bodi ya mikopo. Mkasimama mkatubeza, mkatucheka kwa sababu ati tunawaonea wivu; kwamba hatupendi maendeleo yenu; kwamba tunajifanya tunajua sana; kwamba ati kama tuna uchungu basi turudi nyumbani kusaidia nchi yetu; kwamba tukae kimya kwa sababu sisi ni wakimbizi! Hivi nyinyi mmerogwa?

Mkadharau sauti za tahadhari zilizopigwa kama kengele kwenye Jamiiforums; mkanyamaza tulipoandika kwenye magazeti yetu; mkawa mnatafuta kujua ni nani anavujisha "siri za serikali". Mkawatimua watu kazi ATCL mkidhania kuwa mmeziba uozo wenu! Sasa leo mnashtuka kana kwamba mmegutushwa na mpiga mbiu!? Mnabeba shuka kupeleka hospitali wakati mgonjwa keshakufa? Mmerogwa nyinyi?

Leo ati kwa ujasiri mnasimama; macho meupe tena makavu, mnasema ati mnataka maelezo ya kina kuwa nini kimetokea ATCL! Ati mnaomba maelezo kutoka kwa watu wale wale ambao wanatakiwa wawe Keko wakiwa na pingu katika miguu na mikono yao. Leo mnakaa meza moja na mafisadi mliowaweka hapo, mkitumaini watawaambia kitu kingine zaidi ya kutaka fedha zaidi! Ati mmewapa siku saba za kujieleza! Maelezo gani zaidi ya kuangalia ndege zenu zisizoruka kama tai aliyekatwa mbawa!

Kama vile wasio na akili timamu wanakuja mbele yenu na suti zao za bei mbaya na kuomba fedha zaidi kuwa kinachohitajika ni fedha zaidi! Katika hali yenu ya kurogwa (bewitched state) mnakaa na kufikiria kuwapa fedha zaidi ili kulinasua shirika. Tutawapeleka hospitali gani nyinyi maana hata walioko Mirembe wanaweza wakawakimbia baada ya kuwauliza "ukichaa wenu umeanza lini"?

Badala ya kuamua kuchukua hatua za kushughulikia tatizo hili mnafanya kile ambacho ni kitendo cha woga kabisa; kwamba mnataka wachina waingie mkataba wa kuliendesha! kwamba ya Afrika ya Kusini hayakuwa funzo, ya Tanesco hayakuwa funzo, mnataka na ATCL mjaribu tena! Hivi katika taifa letu hakuna watu wenye uwezo kweli wa kuliendesha shirika hilo? Kweli mmekuwa waoga kushughulikia matatizo hadi tatizo likija mnakimbilia kwa "mjomba" Uchina, mmerogwa nyinyi?

Mnataka kutuambia kuwa mmeshindwa kukaa chini na kugonganisha vichwa vyenu kutafuta suluhisho la kitanzania kwenye tatizo la kitanzania? Hivi mnaogopa nini kufanya maamuzi magumu na kutoa nafasi kwa WAtanzania wazalendo wa kweli kuliendesha? NI ninyi wenyewe mlimrudisha David Mattaka licha ya kuwekwa nje ya utumishi, mlikuwa mnafikiria nini? Kwamba ATCL ni mahali pa mafunzo?

Katika wazimu wangu, nina uhakika tukitafuta watu wawili wa watatu wenye akili za biashara wanaweza kulitengeneza shirika hili na wenyewe wakatengeneza pesa vile vile. Tumeshindwa kuwaita wafanyabiashara wa Kitanzania, wasomi, na watalaamu wa mambo ya anga na kusema "tunaomba msaada tufanye nini"?

Kama mlivyokuwa goigoi kwenye wizi wa Benki Kuu, kama mlivyo goi goi kwenye suala la Elimu ya Juu (mmeunda kamati kuchunguza matatizo ya vyuo vikuu wakati mwaka mmoja mliopita mliunda kamati kama hiyo hiyo au hamkumbuki mlifanya hivyo?), kama mlivyo goi goi kwenye Jeshi la Polisi; kama mlivyo goi goi kwenye Usalama wa Taifa, mmekaa na kusubiri hadi vinuke kabisa ndiyo mnyanyuke! Mmerogwa na nani? Na ni kitu gani tunaweza kuwapa kikawazimua toka katika hali yenu ya bumbuwazi la ulozi?

Mnataka tuombe Bunge liunde Kamati Teule ichunguze ATCL? Msituambie kuwa sasa nchi yetu ianze kuongozwa na Kamati za Bunge maana hata la Dowans nusura mliingize Taifa mkenge licha ya kuwaambia tangu mwaka jana kuwa Dowans haikustahili kuchukua mkataba wa Richmond lakini katika kiburi chenu mkafanya hivyo.

Sasa hili la ATCL limedhihirisha tatizo liliopo. Mmezoea kubebana sana, mmezoea kuoneana haya sana, mmezoea kukenuliana meno kama fisi wanapoona mifupa!! Mmebakia kupigiana makofi!

Zindukeni katika usingizi wenu! Amkeni kutoka katika dimbwi la mshangao wenu, kwani hakuna hirizi itakayowazindua, hakuna ramli itakayowaamsha, hakuna mganga atakayeinua zindiko mlilojipigia wenyewe katika ufisadi wa matendo yenu. Na msitegemee kuchanjwa chale za kinga ya pingu zilizopo mbele zenu!

ATCL haihitaji kubinafsishwa, ATCL haina sababu ya kuitiwa wajomba zetu wachina kuja kuiokoa; ATCL haitaji wataalamu kutoka mbinguni na mabingwa wa utawala kutoka mbingu ya saba. Wamarekani wana msemo "you messed it up, you clean it up" kwamba "mmechafua wenyewe, safisheni wenyewe!". Hili mmelivundisha wenyewe, sasa linanuka mnauliza "kwanini linanuka"?

Labda mnahitaji kuombewa nyinyi; mnahitaji kupepewa; au kufukizwa kwa harufu ya maji yaliyochemshwa ya mwarobaini! au tumwombe Kakobe awawekee mikono! au Shehe aliyebobea katika mambo ya roho awasomee!

Au mwataka tuite mashehe waje wawasomee dua ya kuondoa majini mliyoyakumbatia, na tukawaombe wachungaji waje wakemee mapepo yenu ya ufisadi yaliyowapanda katika vichwa vyenu, labda...... labda... mtarudi kwenye akili timamu!

au mnatuonaje sisi Watanzania, tumerogwa?

labda nyinyi na sisi sote tumerogwa na hakuna wa kutusaidia!
 
Kile kikombe cha maovu kimejaa 3/4.
Kikifurika tutawanywesha Ghadhabu na hasira ya maovu yao kutoka katika kikombe walokijaza wenyewe.
Nchi yetu ni changa sana katika viwanja wa Ufisadi.
Kuna matokeo mengi yasiyokusudiwa yatokanayao na ufisadi bado hayajaja. Lakini Dalili za mwanzo za matokeo ya Ufisadi zinajonyesha dhahiri miitaani.

Dalili moja kubwa yenye matokeo mabaya kwa kila mtu na hasa wale wenye hali njema, ni kushuka kwa maadili ya kijamii kwa ujumla na imani iliyojengeka miongoni mwa vijana wengi kwamba utajiri katika jamii hupatikana kwa dhurma bila kujali matokeo.

Mambo haya mawili yaashiria kwamba unyama unachukua nafasi katika maisha ya kila siku ya watanzania.

Kuna mtu atapona?
 
MMKJJ hawa watu naona hawana uzalendo, yaani kila siku wanawaza ni jinsi gani ya kuiba na naona hawatosheki, yaani wanashindwa hata kutumia njia nyingine ambayo ni kufanya kampuni/ATCL ifanye vizuri yaani ipate faida kubwa na wachukue marupurupu mazuri. Yaani kama ulivyosemwa wamelogwa na aliyewaloga bahati mbaya alishafariki kwa hiyo hawawezi kupona haoo, dawa yao ni kuwaweka keko na kutowatoa/ kuchukua kila walichoiba na kutowapa hata genge la kuuza matunda kwa sababu wamelogwa. Na mengine ni matatizo ya the so called UUNGWANA wetu, yaani mtu mzembe aliyeshindwa bado mnamuweka aongoze kitu?! Mhmm!! Sijui lini tutafika na sijui lini tutajifunza. Kwa sababu umeshasema mwaka mzima umepita toka wameambiwa kuhusu hili suala, lakini waapi, ndio maana nakuambia aliyewaloga kashafariki kwa hiyo hawana dawa na ndio maana labda wanataka wachina kwa sababu wao hawana dawa.
 
Kawambwa, wakati anapokea wizara ya miundombinu, alisema kuwa sasa ameletwa kwenye fani yake maana yeye ni mhandisi, na kwamba hatadanganywa! Takriban mwaka mmoja umepita tangu aseme maneno hayo. Minongóno ya ufisadi ATCL ilikuwepo muda mrefu. Binafsi nakiri kusoma makala kadhaa za mwanakijiji akifunua uozo ATCL takriban mwaka mmoja uliopita. Bado hakuna kilichofanyika zaidi ya ATCL kuendelea kuhujumiwa. Matokeo ni hayo sasa - it is grouded! what a shame? what a loss? Mhandisi wetu Kawambwa ameweza kudanganywa na mtangazaji wa Radio Tanzania zamani kipindi cha Mbiu ya Mikoa - Bwana Nyangányi!! Amedaganywa na Mattaka aliyefukuzwa utumishi wa umma na Mkapa!! Kama hawa kina Mattaka na Nyangányi wameweza kumdanganya, sumbuse hao wakandarasi wa barabara! Bado namuheshimu Kawambwa. Nasubiri hatua zaidi atakazochukua dhidi ya menejimenti ya ATCL wakiwemo Nyangányi na Mattaka. Hatua zozote za kulindana kitoto atakazochukua, zitanifanya niondoe heshima yangu kwake (Kawambwa) and count down another failure in the muungwana's cabinet.
 
Kawambwa, wakati anapokea wizara ya miundombinu, alisema kuwa sasa ameletwa kwenye fani yake maana yeye ni mhandisi, na kwamba hatadanganywa! Takriban mwaka mmoja umepita tangu aseme maneno hayo. Minongóno ya ufisadi ATCL ilikuwepo muda mrefu. Binafsi nakiri kusoma makala kadhaa za mwanakijiji akifunua uozo ATCL takriban mwaka mmoja uliopita. Bado hakuna kilichofanyika zaidi ya ATCL kuendelea kuhujumiwa. Matokeo ni hayo sasa - it is grouded! what a shame? what a loss? Mhandisi wetu Kawambwa ameweza kudanganywa na mtangazaji wa Radio Tanzania zamani kipindi cha Mbiu ya Mikoa - Bwana Nyangányi!! Amedaganywa na Mattaka aliyefukuzwa utumishi wa umma na Mkapa!! Kama hawa kina Mattaka na Nyangányi wameweza kumdanganya, sumbuse hao wakandarasi wa barabara! Bado namuheshimu Kawambwa. Nasubiri hatua zaidi atakazochukua dhidi ya menejimenti ya ATCL wakiwemo Nyangányi na Mattaka. Hatua zozote za kulindana kitoto atakazochukua, zitanifanya niondoe heshima yangu kwake (Kawambwa) and count down another failure in the muungwana's cabinet.

sasa kuna mtu yeyote anayeweza kukisia sababu itakayotolewa baada ya siku saba..
 
sasa kuna mtu yeyote anayeweza kukisia sababu itakayotolewa baada ya siku saba..

...yap, itakuwa kama hivi;

"Nchi hii siku hizi inaendesha mambo yake kwa kufuata utawala wa sheria. Ingekuwa enzi za zamani…watu wanachukuliwa wanapelekwa pasipojulikana miaka mitatu, minne au mitano hawasikiki, lakini leo utaanzia wapi…huwezi," -Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Bunge mjini Dodoma 9/4/2008.

...halafu kuna watu wataandamana kumuunga mkono.
 
hawa dawa yo ni sanduku la KURA. Lakini sheria za uchaguzi bado zinawasaidia, ila kila kitu kina muda. Hawawezi kutufanya wajinga wakati wote, bali wanatufanya wajinga kwa muda fulani.
 
Na. M. M. Mwanakijiji
Kama vile wasio na akili timamu wanakuja mbele yenu na kuomba fedha zaidi kuwa kinachohitajika ni fedha zaidi! Katika hali yenu ya kurogwa (bewitched state) mnakaa na kufikiria kuwapa fedha zaidi ili kulinasua shirika. Tutawapeleka hospitali gani nyinyi maana hata walioko Mirembe wanaweza wakawakimbia baada ya kuwauliza "ukichaa wenu umeanza lini"?


Kutoka katika Biblia (Matthew 25 : 14-30) kuna somo kuwa mtu mmoja tajiri aliwapa watumishi wake watatu pesa, halafu yeye mwenyewe akaenda safari ya mbali: mtumishi mmoja alipata talanta 5, wa pili akapata talanta mbili na yule wa tatu akapata talanta moja. Tajiri aliporudi kutoka safari yake, akawakauta watumishi wake wakiwa wanamsubiri: aliyekuwa amepewa talanta tano alirudisha talanta kumi, na aliyekuwa na talanta mbili akarudisha talanta nne. Lakini yule wa tatu aliyekuwa amepewa talanta moja alirudisha ile ile talanta moja kama alivyopewa. Tajiri yule alimwadhibu huyu ambaye hakuzalisha ingawa hakupoteza pesa zake. Sasa hata mimi nashidwa kuelewa hawa ambao siyo tu hakuzalisha bali pia wamepoteza tulizowapa, iweje waje kutuomba pesa zaidi?.
 
Mkuu Mwanakijiji, Hii ni kati ya hoja zako nyingi zenye ukweli wa kusisimua na inatutia nguvu mpya pale ambapo tunakuwa mioyo yetu inakuwa imefifia kwa kukata tamaa... Tafadhali itoe ktk kijarida chetu tukufu CHECHE ili niweze ku-usambaza ujumbe huu kwa wadau wengi hasa wasiokuwa na ufahamu/upeo wa kile kinachowapelekea wao kuwa ktk lindi la umasikini. Wanabodi pls tushirikiane kuwafikishia ujumbe vijana hasa walioko masokoni, migodini, vitu vya mabasi na na hata mashuleni!!! amin amin nawaambia; mabadiliko ya kweli yatatokana kwa kuwaelimisha na kuwahamasisha haya makundi ya vijana! enough is enough!!! Tanzania ni yetu sote...
 
Mkuu Mwanakijiji, Hii ni kati ya hoja zako nyingi zenye ukweli wa kusisimua na inatutia nguvu mpya pale ambapo tunakuwa mioyo yetu inakuwa imefifia kwa kukata tamaa... Tafadhali itoe ktk kijarida chetu tukufu CHECHE ili niweze ku-usambaza ujumbe huu kwa wadau wengi hasa wasiokuwa na ufahamu/upeo wa kile kinachowapelekea wao kuwa ktk lindi la umasikini. Wanabodi pls tushirikiane kuwafikishia ujumbe vijana hasa walioko masokoni, migodini, vitu vya mabasi na na hata mashuleni!!! amin amin nawaambia; mabadiliko ya kweli yatatokana kwa kuwaelimisha na kuwahamasisha haya makundi ya vijana! enough is enough!!! Tanzania ni yetu sote...

Hii haitasubiri wiki ijayo.. wasomaji wa "Cheche" wataipata kwenye email zao katika "pdf"... (na mabadiliko kidogo).
 
MZee Mwanakijiji,

Mie huwa sielewi ila nahisi hawa viongozi kama Ma waziri ,Wakurugenzi huwa wanamroga Mhe. Rais ili wanedelee kukaaa katika Madaraka..Haiingii Akilini mtu kama Mataka anaendelea kuwapo madarakani wakti alishafukuzwa kipindi cha Mkapa kwa matumizi mabaya ya ofisi ya Umma.

Sasa sijui tatizo ni haw watu wa idara wanaofanya vetting au ni nani.Mie nahisi wamemroga Mkwere!

We need a serious Solution na jambo jema ni kufanya maombi ya kitaifa na Rais Inabidili ahudhulie na apate maombi.

I have a feeling Mkulu hajui kinachoendelea kwa kuwa wanamtafutia sana safari na vikao vingi iliasijue chochote
 
Mgonjwa anapokuwa na hali tete huwa anapelekwa ICU ili kuokoa maisha yake lakini mgonjwa wetu ATCL wala hakupelekwa ICU walimwacha wodini ajifiee!!!!! shame
 
hivi ni watawala au viongozi? kama ni watawala wako sahihi kwa chochote wanachofanya!!!!
 
Tatizo ni kule juu, hatuna Uongozi bora, right tungekuwa na viongozi wa juu waadilifu, wangeteua wasaidizi waadilifu. Mtu akiteuliwa anaanza kujaza rafiki zake tu ili waendeleze ushikaji na upuuzi wao kwa maslahi binafsi.

Hakika suluhisho la haya yote ni kuiondoa CCM na viongozi wake madarakani, imeoza, viongozi wetu wamerogwa wakarogeka na mchawi aliyewaroga amekufa.

Inatia uchungu mkubwa, vizazi vyetu vijavyo vya waTZ wanaviweka wapi? Hatari!


Piga vita CCM piga Vita ufisadi.
 
Mzee MKJJ

Mwenye MASIKIO NA ASIKIE

You just can not say more - You have just said it ALL

= = =
 
Najua wanene wenyewe wanapitia hapa JF, si ajabu nao wanajiuliza hivi hawa watu humu JF wanapiga sana kelele kuhusu uozo wa serikali na watendaji wake bila kuchoka WAMELOGWA?
 
Unajua wakati mwingine nafikiri we "a selfish bunch of self-proclaimed non-governmental watchdog"... Yawezekana tumezidi kutafuta mabaya, labda tujiulize mazuri ya ATCL ni yapi na tumpe Mattaka Udaktari wa Falsafa...

At least waliweza kubadilisha ATCL rangi zake!!! that is something to be proud of!
 
Back
Top Bottom