mawazo hasi kama haya ndiyo yanayojenga makundi na mifarakano ndani ya chadema.
Kuna watu wengine kama wewe wanafikiri chadema ni yao na ndiyo nyumba yao wakiwa ndiyo baba na mama huku wale wengine wakiwa ni watu wa kuja, kujileta au kuletwa.
Hebu fikiria mtu anayedhani chadema ni yake halafu wewe wa 'kuja' umwambie kuwa anachokifanya hakifai na kiko nje ya taratibu, kanuni, itifaki na katiba. Kwanza hawezi hata kukusikiliza na ukizidisha kelele atakachofanya ni kukufukuza kwenye chama "chake" katika misingi hiyo hiyo ya uvunjifu wa taratibu, kanuni, itifaki na katiba na huwezi kupata nafasi ya rufaa wala msamaha. Rufaa na msamaha utatoka wapi wakati hukumu ni batili.
Mentality kama hizi haziwezi kukifanya chama kikawa na demokrasia pana inayowafikia wale wenye inferiority na mtazamo huu.
Chama ambacho kina misingi ya demokrasia, wanachama ndiyo wenye chama na katika wanachama hao, hakuna anayejulikana kama niwa kuja, kujileta na kuletwa kwa sababu kila mwanachama ana haki na uwezo uliosawa. Hakuna kura za veto ndani ya vyama vya demokrasia. Hakuna kura inayoyoizidi kura ya mwingine na hata maamuzi lazima yafanyike kwa kura au makubaliano ya wanachama.
Hii uliyoleta hapa ni pumba kisiasa hasa pale unaposimama kwenye majukwaa na kudai chadema ni chama cha demokrasia na maendeleo.