Watanzania wengi wanashindwa kumiliki Magari mapya kwasababu ya Utitiri wa Kodi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Kama ni mfuatiliaji wa aina za Magari yanayomilikiwa na Watanzania walio wengi, utagundua kuwa asilimia kubwa wananunua Magari ambayo ni "Used" tena kwa miaka 10 au 15 nyuma, na yote ni sababu ya wingi wa Kodi za ajabu ajabu kutoka Mamlaka za nchi hii.

Tofauti na ukienda nchi za wenzetu mfano Afrika Kusini, Kenya au Rwanda, Watu wanaendesha Matoleo mapya ya Magari kwasababu Serikali zao zimeweka kodi rafiki za uagizaji Magari ili kuepuka kuwa dampo la Magari chakavu.

Hapa kwetu Tanzania kuwa na gari jipya ni kama anasa au unaonekana fisadi. Wakati ni jambo la kawaida kwa wenzetu. Ifike hatua nchi iwe na mipango ya maana kwa raia wake. Iweke kodi rafiki ili kuvutia Watu kumiliki Magari mapya sio vyuma chakavu.

Lakini pia, kodi rafiki zitavutia hata Watu kununua magari kutoka nchi nyingine kwa wingi sio Tanzania inaonekana soko la magari ya Japan tu tena hasa Toyota.
 
Wimbo wa uzalendo ni ngumu kueleweka iwapo hizo kodi zinatumika vibaya na watawala na ripoti ya CAG inapuuzwa.

Ulaya na Asia kodi zinatumiwa vizuri na serikali ndio maana wananchi wanalipa kodi bila shuruti.
 
Used hazina Kodi ?!!!

Tatizo la watanzania Hatuna Buying Power; Hivi unaweza kuniambia gari mpya (Cheapest) hata kabla ya Kodi ni Bei gani alafu niambie ni Watanzania wangapi wana hizo pesa...
 
Hatari sana hii nchi yaani kodi ya gari Mpya ni unaagiza gari tena nyingine kwa nchi seriously!

CCM ni kirusi hatari tena takataka na laana kwa hili Taifa!
 
Used hazina Kodi ?!!!

Tatizo la watanzania Hatuna Buying Power; Hivi unaweza kuniambia gari mpya (Cheapest) hata kabla ya Kodi ni Bei gani alafu niambie ni Watanzania wangapi wana hizo pesa...
Gari new model
bei rahisi sana mzigo ikitokea kiwandani ila gharama za kodi kwa nchi inakofika ni problem,
Angalia kama Botswana kodi ni rafiki watu wanamiliki chuma kali na ana nyumba ya Slop!
 
Gari new model
bei rahisi sana mzigo ikitokea kiwandani ila gharama za kodi kwa nchi inakofika ni problem,
Angalia kama Botswana kodi ni rafiki watu wanamiliki chuma kali na ana nyumba ya Slop!
Unaongelea New Model au Unaongelea Gari Mpya ? Sababu kuna tofauti Kubwa...
 
Back
Top Bottom