Watanzania wameyakataa kabisa majiko ya umeme, hivi ni ujinga au ushamba?

Watanzania wameyakataa kabisa majiko ya umeme, hivi ni ujinga au ushamba?

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
8,091
Reaction score
23,624
Gas ikiisha unasikia Watanzania wajinga wakisema "sijui kwa nini gesi lazima iishe usiku."

Sawa gas imeisha usiku kwa nini usingekuwa na backup ya jiko la umeme?

Utamsikia Mtanzania anakwambia jiko la umeme linatumia umeme mwingi, ok well mbona ndani una vyombo vingi sana vya umeme na haulalamiki?

Kwani jiko la umeme unalitumia siku nzima?

Mtu ana flat screen ya milioni lakini jiko la umeme hata la plate 2 linamshinda.

Kuna ujinga mwingi sana kwenye jamii ya Watanzania, pesa ya kufanya au kununua vitu vya kijinga wanazo ila kuongeza units za umeme awe anatumia jiko la umeme hana.


Kuna majiko ya single burner yana 1000 watt

1000 watt ni sawa na 1kWh kwa saa

Tuseme kwa kadirio la juu unatumia jiko kwa masaa 2 kila siku yaani 2kWh

Kwa siku 30 za mwezi utakuwa umetumia 60kWh


Kwa sasa Tanesco wanachaji 1kWh kwa Tshs 100-290 kwa wateja wa kawaida

60kWh×Tshs 290 unapata 18,000/=

Kwa mwezi unaweza kutumia gesi ya shilingi ngapi?

Pia siku hizi kuna majiko janja ya umeme ya induction haya kwenye matumizi ya nishati ya umeme ni rafiki sana na ni teknolojia ya kisasa. Ukinunua induction cooker hautajuta
 
Na siku hizi majiko ya umeme simple na ambayo matumizi yake ya umeme sio makubwa yako mengi tu. Bei iko reasonable

Watanzania wanathamini sana flat screens sijui wamerogwa
Mambo au vitu ambavyo Watanzania wengi wamekataa kabisa kuwa navyo katika nyumba zao

Washing machine, A.C, reading room, solar panels hasa wa mjini, heater n.k

Ongezea
 
Na siku hizi majiko ya umeme simple na ambayo matumizi yake ya umeme sio makubwa yako mengi tu. Bei iko reasonable

Watanzania wanathamini sana flat screens sijui wamerogwa
Kwahyo hii hela yangu nlipokua naenda kununua inch 65" Kesho niache, duh! Kwel uchawi upo Bora nisingeingia JF Leo 😆😆
 
Moja umeme ni cheaper kuliko gesi hususan kwa vyombo vyembe ufanisi vya sasa (Hapa Elimu inahitajika)


Mbili ni Serikali hii ambayo haina mapenzi na watu wake kushindwa kupunguza gharama ya umeme ili kila mtu atumie umeme sababu kama taifa tutasave pesa tunazotumia kuagiza gesi ughaibuni


Mwisho kabisa kama viongozi wangekuwa na mapenzi mema na wananchi badala ya kutoa ruzuku kwenye gesi wangetoa kwenye induction cooker

 
Gharama ya umeme ipo juu kidogo Tanzania ingawaje ukitumia kama backup sio mbaya maana umeme huo huo unalipia kiwanja chako pia una VAT na wanatamani waweke Import duty ingawaje umeme ni wa kwetu wao wataweka tu na kusema unatoka Ethiopia maana wa Mtera una gharama sana Wabongo wakishapata madaraka sio watu kabisaa.
 
Back
Top Bottom