Watanzania tunapandikizwa chuki

Watanzania tunapandikizwa chuki

Hasa hasa hawa watekaji wanapandikiza chuki. Bahati mbaya si serikali wala polisi wanaoonekana kukerwa. Hata ccm haijakerwa na matukio haya.
Kujenga ni kazi ngumu sana ila kubomoa ni kazi rahisi sana. Kazi ngumu ya jasho na gharama kubwa iliyojengwa na Nyerere ya amani na mshikamano wa taifa inabomolewa na wajinga wachache wanaotumia usalama wa taifa bila kukemewa na yeyote.

hao wanaotekwa wakitekwa amani itapatikana trust me
 
Mapungufu ya serikali hii ya kidikteta yamezidi na hakuna hata dalili ya kuyarekebisha. Kwa mfano badala ya kujisahihisha katika utendaji, usimamizi na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kimaendeleo, wanatumia TISS kuwateka na kuwatesa wakosoaji. Huu ni upuuzi ambao watanzania hatuwezi kuuvumilia hata kidogo.

shughuli za kimaendeleo zipo nyingi na zinaenda vizuri, labda upo bize na vitu visivyo na maana. usalama wataendelea na kazi yao kama kawaida. nchi yetu kwanza.
 
Huna ndugu alie potea wala huna ndugu alie umizwa, ingekuwa una jamaa katika wale maiti walio okotwa mtu ruvu usinge sema haya, bora ukae kimya maana sasa giza linazidiwa na nuru, maovu yote yataonekana tu, eti njia sahihi ni ipi hiyo? kuendelea kuambiwa subiri? mpaka lini wacha watu wapige mayowe bana.
 
Chuki nyingine zinatengenezwa na serikali, mfano kwenye hili suala la vyeti.
Serikalini imefanya uhakiki wa vyeti ambapo waliogundulika Kuwa na vyeti vya kughushi wamefukuzwa kazi na wengine kupandishwa mahakamani.
Daudi bashite yeye pamoja na Utata uliodhahiri kuhusu vyeti vyake haufanyiwi kazi.
Unafikiri hao watumishi wengine waliofukuzwa kazi wanachuki kiasi dhidi ya serikali kutokana na hii double standard.
Chuki za wananchi dhidi ya Serikali inasababishwa na Serikali yenyewe

una ushahidi wa vyeti feki, usifate wanasiasa...
 
Huna ndugu alie potea wala huna ndugu alie umizwa, ingekuwa una jamaa katika wale maiti walio okotwa mtu ruvu usinge sema haya, bora ukae kimya maana sasa giza linazidiwa na nuru, maovu yote yataonekana tu, eti njia sahihi ni ipi hiyo? kuendelea kuambiwa subiri? mpaka lini wacha watu wapige mayowe bana.

piga mayowe ya kisomi mtu aone sio mayowe ya mtu asieenda shule, yenye chuki ndani yake
 
Chuki zinanapandikizwa nayule asiyependa mbunge wa chama A kwenda kumjulia hali mbunge wa chama B pale Kisongo gerezani,wakati wanafanya kazi pamoja na ni wa Tanzania

kweli ndugu, ila fatilia vizuri kuna kitu pale.
 
piga mayowe ya kisomi mtu aone sio mayowe ya mtu asieenda shule, yenye chuki ndani yake
Mayowe ya kisomi yanpigwaje? mtu mwenye maumivu awe msomi awe asie soma kuna tofauti ya kuonesha maumivu? Mayowe ya kisomi yatapigwa na mnafiki asie na maumivu...acha kujidanganya usomi hauzuii hisia.
 
Bashite peke yake amesababisha chuki kwa 60% na chuki zingine zimetokana na Udikteta
Unamchukia sababu alianzisha vita ya dawa za kulevya? Km ni hivyo hongera teja! Au jamia mexco.
 
Sisi watanzania roho mbaya na tamaa zinatusumbua, siasa ni biashara km zilivyo biashara nyengne. Tuwaache waliowah kuja mjini wafanye biashara zao na sisi tufanye zetu ilimrad hatuvunji sheria bac. Tutaish kwa aman daima na hatutagombana, lkn tukiwa na roho mbaya za kuoneana wivu ndo yanatukuta sasa Mambo km haya.
 
Unamchukia sababu alianzisha vita ya dawa za kulevya? Km ni hivyo hongera teja! Au jamia mexco.
ww ni mshamba sana upo msitu gani? Vita ya dawa za kulevya alianzisha makonda Bashite? Taasisi ya kuzuia Dawa za kulevya ipo siku nyingi wakati Bashite akiwa Mvuvi na ww ukiwinda sungura kolomije, hakuna cha vita wala nini bali kuna Blackmail ili ww na boss wako Bashite muwachukulie magari, mali na unga kwa watuhumiwa na sasa mmeumbuka kila kitu kipo wazi wale wote mliowabambikia kesi wamekomaa chupi zinawabana mpaka mnakonda viuno na wowo la Bashite limeongezeka.
 
bashite naweza kumsemea kidogo sana, ni jembe sema aliteleza kidogo. na sababu kubwa yy kuteleza ni kuandamwa na jamaa wa madawa.
Bashite kwa sasa ndiyo muuzaji mkubwa wa Unga ana miliki Duka la jumla wateja toka South Africa, china, Brazil mpaka ulaya wanakuja kuchukua Unga kwake kwa kumtumia wakala wake le mutuz kumbuka kwamba kipindi ametangaza List alitumia ile fursa vizuri kwa kukamata Unga kimya kimya akauhifadhi uvunguni kwake, ameanza kuuza kidogo kidogo anapata pesa za kuwalipa nyie kikundi cha Le-mutuz ( kubwa jinga) kuja kumtetea JF na mitandaoni kwa ujumla,
 
Le-mutuz kwa sasa limekuwa jitu hatari sana mlichunge huko mitaani pindi mkiliona, kwanza limekuwa Dalali wa kuuza Unga wa makonda Bashite ambao aliukamata kipindi cha kutaja List, pili linawachunguza wasanii wanaomsema vibaya Bashite kisha linaenda kumwambia ili Bashite awafanyizie umafia kama wa Roma, Tatu linalipwa pesa nyingi kwa kumiliki kikundi cha upelelezi mitaani na kusambaza unga wa bashite huku wengine wakiwa busy kumfanyia kazi kwenye mitandao mbalimbali wakimtetea Bashite. hizo ni mojawapo ya vichochea chuki kwa wananchi wa Tanzania.
 
Huna hoja zaidi ya mikelele.
ww kula pesa za Bashite ulale hapo kwa Le mutuz mda si mrefu watakufukuza kwa kushindwa kumtetea wowo Bashite kwani hawajakutuma kuja kuandika neno mikelele wanataka uwatetee ikibidi useme Bashite ni malaika hana dhambi ili uendelee kulala hapo kwa Le mutuz kinyume na hapo watakufukuza leo leo hii.
 
bashite naweza kumsemea kidogo sana, ni jembe sema aliteleza kidogo. na sababu kubwa yy kuteleza ni kuandamwa na jamaa wa madawa.
Kufoji cheti na jina sio kuteleza kidogo, kuvamia chombi cha habari sio kuteleza kidogo. Nilikuwa namsupport sana Bashite sema daaah sahivi naona I was wrong
 
una ushahidi wa vyeti feki, usifate wanasiasa...
Ushahidi Upo shule aliyosoma Daudi bashite na kupata divisheni ziro huko Mwanza.
Atuambie Ni lini alitengeneza vyeti Kwa jina lake jipya akavitumia kusomea elimu ya juu.
Kwa nini haweki wazi? Anaficha nini?
Acha kutetea ujinga wewe, kuwa makini na watu wanaobadilishabadilisha majina yao wengi want hidden agenda
 
Back
Top Bottom