DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,152
Katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Jawadu Mohamed, amesema kauli zinazotolewa na baadhi ya wanachama wa chama hicho, wakiwemo aliyekuwa Mbunge wa Kawe (CCM) ,Askofu Josephat Gwajima, na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, hazina mashiko ya hoja, bali zimejawa na chuki, ubinafsi, na kukosa ushahidi wa msingi dhidi ya uongozi uliopo madarakani.
Jawadu ametoa kauli hiyo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa baadhi ya wanachama wa CCM waliotoa matamko ya ukosoaji dhidi ya serikali.
“Mimi natofautiana na kauli za baadhi ya wanasiasa wenzetu, hasa ndugu Polepole na Gwajima. Kauli zao zimejikita zaidi katika mtazamo wa chuki binafsi kuliko uhalisia wa mambo. Unapodai kuwa kuna kuyumba kwa mifumo ya kiuongozi pasipo ushahidi wa wazi, wakati huo huo serikali hiyo hiyo inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kitaifa – hoja hiyo haiwezi kusimama,” amesema Jawadu.
Jawadu ametoa kauli hiyo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa baadhi ya wanachama wa CCM waliotoa matamko ya ukosoaji dhidi ya serikali.
“Mimi natofautiana na kauli za baadhi ya wanasiasa wenzetu, hasa ndugu Polepole na Gwajima. Kauli zao zimejikita zaidi katika mtazamo wa chuki binafsi kuliko uhalisia wa mambo. Unapodai kuwa kuna kuyumba kwa mifumo ya kiuongozi pasipo ushahidi wa wazi, wakati huo huo serikali hiyo hiyo inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kitaifa – hoja hiyo haiwezi kusimama,” amesema Jawadu.