Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,124
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!
Ng`wanakidiku,
Propaganda kama hizi ziliwahadaa watanzania mwaka 1995.Hii digital generation haiwezi kudanganyika kirahisi kiasi hiki.Sasa hivi watanzania wanajua ni nini wanachotaka,wanajua ni kitu gani wanakosa ukilinganisha na wenzao wa nchi nyingine.Kipindi kile utandawazi ulikuwa haujapata nguvu,sasa tunashuhudia hadi popular uprising ikiwa catalysed vizuri kwa kutumia social networks like Twitter,Facebook,Orkut na kwa hapa kwetu tunashuhudia jinsi mitandao kama Jamii Forums inavyowapa headache watawala,
Tafadhali unapoleta upotoshaji hapa ujiandae vizuri,Mbona hutoi mfano wa demokrasia iliyokomaa kutoka Ghana ambayo imebadilisha serikali mara kadhaa? Mbona hutoi mfano mzuri wa Zambia ingawa MMD kilikua chama cha upinzani kilichondolewa na chama kingine?Unapopotosha katika mazingira kama haya kwa mfano kuhusu ishu ya Zambia,ni lazima uwaeleze watu ukweli kwamba MMD waligeuka kuwa chama-mabavu (dictatorial Party) dhidi ya upinzani.Chama cha Patriotic Front cha Comrade Sata kinafanya vizuri so far.
Badala ya kuwakataza vijana wa Tanzania ambao kwa hali ilivyo sasa hawazuiliki,washauri CCM muda utakapofika waachie madaraka kwa amani.Washauri wafuate njia ya rupia Banda na chama cha MMD,washauri wafuate njia ya John Kuffour na Nana Addo-Akufo wa Ghana alivyompisha mpinzani Prof.John Evans Atta-Mills.Ghana is rocking.Usiwashauri CCM kufuata njia ya Laurent Gbagbo
CCM imekaa madarakani muda wote huo,nakushangaa unatumia nguvu nyingi kuwashawishi watu wasiichague chadema.kama CCM ni chama kizuri na chenye sera nzuri dhidi ya umaskini,ujinga, Maradhi na sasa kuna adui mwingine Ufisadi ni kwa nini watumie nguvu nyingi kiasi hiki?Si watanzania tayari wangekuwa wameshajua uzuri wa chama hicho?
Jumuiya za chama cha mapinduzi si zile tulizozoea tena yaani jumuiya za vijana (UVCCM) ,Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) nk. Jumuiya halisi ni CCM-EPA,CCM-MEREMETA,CCM-RICHMOND,CCM-IPTL,CCM-DOWANS,CCM-KAGODA,CCM-UDA,CCM-RADA nk, Hizi ndizo jumuiya halisi zilizoko kazini ndani ya CCM.Kama jumuiya hizi zitakisaidia chama na kushinikiza sera zitakazoijenga nchi dhidi ya CHADEMA basi hilo kundi la watu unaowapa ulichokiita 'Nasaha' lina tatizo.Kama ujumbe wako ulikuwa umelenga Audiance ya watu wa Mirembe then JF is not the right place.
Kwa hiyo tuchukulie kwamba ni ujumbe uliotumwa sehemu kwa makosa,ume-land kwenye wrong Audiance !pole......