Watanzania msiipigie kura CHADEMA 2015

Kwa mm siwez kukupinga kwan uwezo wako wa kufikir hapo ndo kikomo! Zaid chakukusadia nenda kajipange uweunakuja na maada zenye kuleta maana
 
Kwanza mtoa mada nimeipenda sana signature yako. You are believer!!!!!!! Common features za believers ni kwamba kwanza ni waoga wa mabadiliko, pili wanachokiamini ndio hicho hicho hata kama kina upungufu fulani...
CCM si bwana Yesu, ni chama cha wanadamu na chaweza kushikwa na wezi, majangili, wala rushwa, wauza mihadarati na mafioso. CCM ya leo ni pango la wanyang'anyi wake up ndugu yangu.

Mundali huyu kiduku ni uzembe wake wa kufikiri, waumini wa kikristo ni wachambuzi wazuri wa mambo labda kama unasemea wale wa Mohammed, wenyewe huwa hawafikiri mara mbili ndo maana kwao kujitoa muhanga ni kama jambo dogo!
 
Mundali huyu kiduku ni uzembe wake wa kufikiri, waumini wa kikristo ni wachambuzi wazuri wa mambo labda kama unasemea wale wa Mohammed, wenyewe huwa hawafikiri mara mbili ndo maana kwao kujitoa muhanga ni kama jambo dogo!

Mmh hapa naona mada inahama taratiiibu. Nikirudi kwenye mada Mi naona Tz hatuna ufahamu wa juu kuhusu upinzani. Yanini kuwa na vyama pinzani kwa chama tawala ikiwa wenyewe nao wanapingana. Wazo langu, utamu wa upinzani utaonekana pale tutapobaki na chama kimoja au viwili vya upinzani hapa hata CCM watapata hofu na watajitahidi kusafisha nchi. Otherwise itabaki Siasa=Biashara
 
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!

Pole sana ndugu yangu.....mbinu nzuri ni kuua tu viongozi wa upinzani na kujapora ushindi wao haya mengine mnajitia aibu tu watu wanelewa kuwa Zambia iko imara ktk nyanja nyingi kwa kuruhusu chama chochote kile kuongoza nchi...sio upuuzi wako huu.
 
Historia ya kenya ni ya uhuru kwa damu kama huijui rudi darasani, umeona ubaya wa kenya uzuri zambia mbona huusemi? Kwa masikitiko sana umenilazimisha kukuita una wazimu na unatakiwa ukapimwe akili, taabu zote tunazopata wewe huzioni au uko ikulu?
 
Nimesoma mara nyingi lakini sijaelewa........wadau aliyeelewa anieleweshe kwa maneno rahisi tafadhali. ..........
 
Ni ukweli usiopingika kuwa CCM ni chama kongwe na hawakurupuki ktk maamuzi. We angalia mchakao wa kusuluhisha hili suala la madakitari, ni suala ambalo limefanywa kwa umakini na linaendelea kutatuliwa kwa umakini. Sasa hao kenya tangu waweke upinzani;
  1. Mwaikibaki na Raila waligombana
  2. Raila alijilimbikizia mali kwa kuchukua mikataba ya mafuta toka Arabuni,
  3. Mwaka 2007 wakenya wakachinjana kwa sababu ya uchu wa madaraka wa hao wapinzani
  4. Na sasa hawataki kuwasikiliza wanachi wanyonge waliowapatia kura na wameamua kuwafukuza kazi!
Je kumfukuza mtu au kumfuta mtu kazi ni suluhisho? si ni ujinga? Kwani serikali ya CCM wasingeweza kuwafukuza ma Dr? Mbona wameamua kutumia njia ya mahakama wakati huo wanaendelea na mazungumuzo! Msiniite kiduku, naomba mtafakari!!

Napata hofu na uwezo wako wa kuelewa na namna ambavyo unatumia mifano. Jaribu kufikiria nchi nyingine ya Afrika ambayo imeweka upinzani na kukatokea machafuko kama ya Kenya. Mimi sitaki kuangalia Kenya walifanya nini hadi wakafika hapo walipo kwa sababu hakuna ambacho tunawazidi Wkenya zaidi ya Ardhi.
1. Elimu wanatuzidi sana, tena siyo kidogo, ni wakenya wangapi wanafundisha shule na vyuo Tz?
2. Ni watz wangapi wanafundisha Kenya?
3. Tz tunabenk ambazo wawekezaji wake ni Wkenya, ngapi Kenya zimewekezwa na Wtz?
4. Uchumi wa Kenya hauwezi kulingalisha na kwetu, tupo mbali sana.
5. Elimu ya uraia Kenya ni kubwa kuliko kwetu, ndio maana bado tunauza viparata vya kura kwa buku.

Inawezekana kweli CCM ni chama kizuri, sina uhakika sana, labda kikipakwa rangi kinaweza kuonekana. Lakini Muonekano wake Tangu alipokiacha Mwl JK 1985 ni tofauti sana na vile ambavyo wengi tulidhani kuwa kingelikuwa. Kifupi serikali na CCM imeshindwa na ili tutoke hapa tulipo tunahitaji chama Mbadala ambacho kitakuwa na maono na mtazamo mpya utakaoendana na hali ya maisha ya sasa. Hizi ni baadhi tu ya sababu ambazo zinaonesha kuwa serikali ya JK imeshindwa...
1. Angalia hali ya uchumi wa nchi ilivyo mbaya. Rejea malalamiko ya wafanyakazi kucheleweshewa mishahara, angalia ukosefu wa fedha za kigeni na kuporomoka kwa shilingi dhidi ya dola
2.Angalia upatikanaji wa UMEME ulivyo wa kusua sua. Hakuna nchi ambayo imeendelea ikiwa na nishati ya umeme ya kipuuzi kama Tz
3. Angalia Rais wa serikali na CCM yake anavyouza sura kwenye TV akisisitiza watu kuomba risiti punde wanaponunua bidhaa.Hii inaonesha ni kiasi gani serikali ya JK inavyotegemea mapato yake ya ndani kutoka kwenye kodi za walalahoi huku wamiliki wa migodi, viwanda, vitalu vya hifadhi, makampuni ya cm na wawekezaji wengine wasivyolipa kodi na wakiongezewa muda wa majaribio bila kulipa kodi.
4. Hakuna serikali ambayo iliwahi kuwaendeleza wananchi wake kwa kutegemea kodi za kununua na kuuza bidhaa, maendeleo huletwa kwa kutegemea raslimali za nchi. Sisi dhahabu, almasi, tanzanite, gas, misitu, wanayama, samaki na vingine vingi tumeuza kwa wazungu bila kupata lolote.
5. Rais ameshindwa mara nyingi kuwawajibisha aliowateua kumuwakilisha kwenye wizara mbalimbali. Rejea mabomu mbagala, mauaji ya Arusha, mauaji ya Tarime (Nyamongo), kukosekana kwa Umeme na mengine mengi.
6. Kikwete na kabineti yake wameshindwa kukaa na kuelewana ni kipi cha kuongea na wakati gani. rais amegeuka kuwa machinga wa kutembea kila anakosikia kuna kusanyiko la viongozi bila kushughulikia matatizo ya nchi. rejea safari za KIkwete za hivi Karibuni nje ya nchi huku Wtz wakifa kwa mgomo wa mdk.
7.......................................
8.......................................
8.......................................

Siku tukiwa na akili za kuona kuwa tatizo ni CCM na vilaza wake, ndipo tutafahamu ni namna gani ya kujitoa hapa tulipo. vinginevyo, hakuna ambacho kitafanyika kama CCM itaendelea kutawala nchi hii.
 
Mtoboasiri, sikiliza! Ukilinganisha upiznani wa hizo nchi ni stable, hwezi kulinganisha na upinzani wa TZ ambao wamejaa njaa (mfano David Kafulila alikuwa na haja gani ya kupiga magoti na kulia ili asamehewe?) na CHADEMA ni chama kilicho jaa migogoro ya hapa na pale, labda kikiundwa chama kingine chenye mlengo na dhamira ya dhati ya kusikiliza matatizo ya watanzania walio wengi na kisiwe na migogoro

Labda kijana nikufundishe tu kidogo ili nikusaidie..Chama chochote kna nafasi kubwa ya kushika hatamu ya uongozi kama kinakidhi yafuatayo;
i)Kimejengwa ktk misingi inayoonesha uendelevu
ii)Kina sera na itikadi zinazotekelezeka
iii)Kinatekeleza yale yote kinachoahidi kupitia viongoz wake..
Iv)Kina dira ya kukiongoza
v)Kina viongoz bora,imara na wasio na kashfa
vi)Kipo mstari wa mbele kumkomboa mwananchi...Haya,heb nikumbushe hiki Chama Chetu cha Magamba kina sifa ipi hapo?
 
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!
M`A`VI Yako
 
Kajipange zaid ndo ujekukampen hapa huku mda bado haujafika! Mpendwa na vimaada vyako visivyo na miguu wala mikono
 
CCM ni chama ambacho kimelaaniwa tangia kuanzishwa kwake,ni heri kife hata leo mana kinatesa wananchi.
 
Mtoa thread inaonekana ni mtu wa kufikiria leo pekeyake ya kesho NA HATA MILELE la hasha ndio maana anaifananisha Tz na Ke. Hivi ameifikiria na kuiangalia ZAMBIA chini ya MICHAEL SATA? KWELI MWANDIKA THREAD HATUFAI KWENYE MCHAKATO WA KUIANDAA TANZANIA YA KESHO !
EE MUNGU MPE HUYU MTOA UZI HUU HEKIMA NA BUSARA ILI AWE NA FIKRA ZA KESHO NA HATA MILELE SIO LEO TU!
 
Ukitaka kujipima masumbwi huendi kuchokoza wagonjwa Mwaisela au Kibasila unakwenda mitaa ya wagumu na kuwaambia wamelegea kama mrenda hapo ni kweli unajima kimasumbwi.
Wakenya ni wenzetu hawa wote tuko behewa moja la third class, nafuu yao ni kwamba akipita mzungu na pipi wanajitahidi kuomba kwa broken English kwa ujinga wetu tunawaona wajanja.

Utulivu siku zote huwepo ukizungukwa na watu wenye mawazo tegemezi.

Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!
 
Back
Top Bottom